Hivi kwanini ujenzi wa makanisa mengi ya KKKT huwa hauishi?

Hivi kwanini ujenzi wa makanisa mengi ya KKKT huwa hauishi?

Tangu nakua kule Keko Magulumbasi, kunapokuwa na ujenzi wa Kanisa la KKKT huwa miaka na miaka ujenzi haukamiliki.

Mifano ipo Mingi tu. Tangu mwaka 1998 Kanisa la pale Korogwe Kimara KKKT ujenzi haujaisha.

Segerea mwisho hadi kesho bado ujenzi haujaisha.

Kibamba shule njia ya Kibwegere ujenzi haujaisha.

Kumara Suka karibu na Temboni ujenzi haujaisha.

Hii ni baadhi ya mifano michache tu, hivi shida nini?
Kwa sababu yanajengwa kwa sadaka na harambee,lakini pia sehemu ya fedha zinazochangwa zinaweza kusaidia masuala mengine ndani ya shirika nyingine kukua.
Hata hivyo kupanda Kwa gharama za vifaa vya Ujenzi nayo ni sababu mojawapo.
Nyingine ni kuhama kwa Washarika watoaji.
Lakini pia kuhamishwa kwa Wachungaji kunapopelekea anayekuja kuwa mtizamo tofauti.
Mwisho,kuwa na wasimamizi wasio waaminifu katika utunzaji na matumizi mabaya ya fedha,ingawa hii si sababu muhimu sana.
 
Hayo waliyotaja ni mangapi kati ya makanisa yote ya KKKT?

Ni asilimia ngapi ya makanisa yote ya KKKT?
Wizi na ubadhilifu wa hata kanisa moja, it's to many!,acha kuhalalisha wizi mkubwa ndani ya KKKT, why kanisa la KKKT kinondoni (karibu na mahakama),halijaisha more than 25 yrs toka lianzwe ujenzi??hawa ni wezi lazima waambie ukweli, lile kanisa angedumu mchungaji Dimwaya(rip),ujenzi ungeshakamilika,ila akasukumwa pembeni na mafisadi yakatake over
 
Uongo .Mchungaji hanunui kiwanja,hachori ramani ya jengo ,hatafuti contractor wa kujenga ,hatafuti Hela za ujenzi Wala kuusimamia sababu sio eneo lake la utaalamu Hilo ni uongo

Nenda kimara korogwe ndio utapata jibu sahihi la icho ulichoongelea
 
KKKT lina waumini wengi sana. Ila wachaga ndio wengi zaidi kwenye nafasi za juu juu kwenye kila usharika.

Sehemu yoyote mchaga akiwepo ujenzi huwa hauishii.. hata nyumba za kuishi za wachaga huwa zinarekebishwa kila mara.

Mchaga na ujenzi ni ndugu
[emoji1787][emoji1787][emoji1787]
 
Du mkuu salute,mada hii imekata kwenye mfupa,KKKT Kinondoni karibu na mahakama pale,ujenzi ule toka mimi nipo secondary school haujaisha, nakumbuka hata PM Lowassa amewahi kufanya harambee za uchangiaji pale, yaani ni wezi..wezi..wezi
Umenikumbusha mbali. Make ile harambee ilileta patashika kwasababu alialikwa Rostam ikawa nongwa kwamba yule alikuwa fisadi ikapelekea mchungaji aliyekuwepo kuondolewa kama sijakosea. So ujenzi wa kanisa nisawasawa na mti kandokando ya mto. Majani ya huo mto hauishi ukijani.
 
Umenikumbusha mbali. Make ile harambee ilileta patashika kwasababu alialikwa Rostam ikawa nongwa kwamba yule alikuwa fisadi ikapelekea mchungaji aliyekuwepo kuondolewa kama sijakosea. So ujenzi wa kanisa nisawasawa na mti kandokando ya mto. Majani ya huo mto hauishi ukijani.
Ahaaaaa mkuu lile kanisa Lina mizengwe sana,but ninaipenda mno kwaya zao za Amkeni na Zayuni, yes ujenzi unaendelea more than 30 yrs !!!!!
 
Wewe unazungumzia ujenzi wa majengo ya kuabudia au miradi mingine ya usharika? Nenda kimara korogwe uone kazi inayofanywa na washarika.
Hiyo miradi inajengwa kwa fedha za waamini/washirika but ikikamilika hao washirika hawanufaiki nayo kutokana na gharama kubwa za huduma za hospital au shule,huu ni unyonyaji mamboleo.
 
KKKT lina waumini wengi sana. Ila wachaga ndio wengi zaidi kwenye nafasi za juu juu kwenye kila usharika.

Sehemu yoyote mchaga akiwepo ujenzi huwa hauishii.. hata nyumba za kuishi za wachaga huwa zinarekebishwa kila mara.

Mchaga na ujenzi ni ndugu
Ni ujinga, chuki na ulimbukeni ndio unakusumbua!
Wachaga ndio wachangiaji wakubwa ktk makanisa ya madhehebu yote makubwa. (Roman &KKKT)
Mfano, DSM makanisa ya Roman wachangiaji wakuu ni wachaga na yanakwisha kwa wakati.
Huyu nyau anaelaumu wachaga sidhani kama ni mchangiaji, yeye kazi kusifia michango ya wenzie!
 
Back
Top Bottom