Hivi Lazaro aliyefufuliwa na Yesu, alitoa ushuhuda gani kuhusu kuzimu baada ya kufufuka?

Hivi Lazaro aliyefufuliwa na Yesu, alitoa ushuhuda gani kuhusu kuzimu baada ya kufufuka?

Huyu Lazaro anatuchanganya, niliwahi kuuliza hapa makuhani na manabii wote wa humu walikwepa kujibu
  1. Tunaambiwa Lazaro alikufa akaenda kustarehe mikononi na kifuani kwa Ibrahimu, je aliyemuona yuko na Ibrahimu ni nani? Alifikishaje hizo taarifa duniani?
  2. Lazaro alipokufa akafufuliwa na Yesu alikuwa amerudi lini toka kwa Ibrahimu?
  3. Tunaambiwa tajiri aliyemtesa Lazaro alimuomba Mungu amtume Lazaro duniani kuwaambia ndugu zake na tajiri watende mema, je hayo maneno yalishuhudiwa na nani?
Huyu Lazaro wa kwa Ibrahimu ni mfano tu, si Lazaro halisi. Ni tofauti na Lazaro aliyefufuliwa na rafiki wa Yesu.
 
Mimi sio msomaji mzuri wa Bibilia, ila nimesikia habari ya Lazoro kufa na baadae kufufuliwa na Yesu wakati Yesu bado yuko hapa duniani na tena tunaambiwa alikuwa anatoa harufu.

Swali ni je, Lazaro alihadithia nini kuhusu kifio au hakusema chochote?

Kwa mfano, wakati anakata roho, nini hasa kilitokea?

Na je, alikufa mara ya pili au ilikuwaje?

Mwenye majibu tafadhali.
Inawezekana una nia ya kutaka kujua lakini amini au usiamini uzi huu utachafua hali ya hewa humu kwa wale wenye kawaida ya kudharau imani za wengine wakiamini kuwa wasiokuwa wa imani yao ni makafir.
 
Luka 16 (Biblia Takatifu)
¯¯¯¯¯¯¯¯¯¯
¹⁹ Akasema, Palikuwa na mtu mmoja, tajiri, aliyevaa nguo za rangi ya zambarau na kitani safi, na kula sikuzote kwa anasa.
²⁰ Na maskini mmoja, jina lake Lazaro, huwekwa mlangoni pake, ana vidonda vingi,
²¹ naye alikuwa akitamani kushibishwa kwa makombo yaliyoanguka katika meza ya yule tajiri; hata mbwa wakaja wakamramba vidonda vyake.
²² Ikawa yule maskini alikufa, akachukuliwa na malaika mpaka kifuani kwa Ibrahimu. Yule tajiri naye akafa, akazikwa.
²³ Basi, kule kuzimu aliyainua macho yake, alipokuwa katika mateso, akamwona Ibrahimu kwa mbali, na Lazaro kifuani mwake.
²⁴ Akalia, akasema, Ee baba Ibrahimu, nihurumie, umtume Lazaro achovye ncha ya kidole chake majini, auburudishe ulimi wangu; kwa sababu ninateswa katika moto huu.
²⁵ Ibrahimu akasema, Mwanangu, kumbuka ya kwamba wewe uliyapokea mambo mema yako katika maisha yako, na Lazaro vivyo alipata mabaya; na sasa yeye yupo hapa anafarijiwa, na wewe unaumizwa.
²⁶ Na zaidi ya hayo, kati yetu sisi na ninyi kumewekwa shimo kubwa, ili wale watakao kutoka huku kwenda kwenu wasiweze; wala watu wa kwenu wasivuke kuja kwetu.
²⁷ Akasema, Basi, baba, nakuomba, umtume nyumbani kwa baba yangu,
²⁸ kwa kuwa ninao ndugu watano, ili awashuhudie, wasije wao pia wakafika mahali hapa pa mateso.
²⁹ Ibrahimu akasema, Wanao Musa na manabii; na wawasikilize wao.
³⁰ Akasema, La, baba Ibrahimu, lakini kama akiwaendea mtu atokaye kwa wafu, watatubu.
³¹ Akamwambia, Wasipowasikia Musa na manabii, hawatashawishwa hata mtu akifufuka katika wafu.


Hapa panaelezea mtu akifa nini hutokea.
 
Ndio maana ya ,imani

Unapaswa kuamini(kusadiki) au usiamini.

Maana kufufua mtu tu ni issue ngumu sana.

Lakini kuna watu wanaamini kwamba hawa wachungaji na maaskofu uchwara na manabii feki wanaweza kuponya cancer, kuponya magonjwa sugu nk

Hili libaki kuwa sehemu ya imani.
 
Luka 16 (Biblia Takatifu)
¯¯¯¯¯¯¯¯¯¯
¹⁹ Akasema, Palikuwa na mtu mmoja, tajiri, aliyevaa nguo za rangi ya zambarau na kitani safi, na kula sikuzote kwa anasa.
²⁰ Na maskini mmoja, jina lake Lazaro, huwekwa mlangoni pake, ana vidonda vingi,
²¹ naye alikuwa akitamani kushibishwa kwa makombo yaliyoanguka katika meza ya yule tajiri; hata mbwa wakaja wakamramba vidonda vyake.
²² Ikawa yule maskini alikufa, akachukuliwa na malaika mpaka kifuani kwa Ibrahimu. Yule tajiri naye akafa, akazikwa.
²³ Basi, kule kuzimu aliyainua macho yake, alipokuwa katika mateso, akamwona Ibrahimu kwa mbali, na Lazaro kifuani mwake.
²⁴ Akalia, akasema, Ee baba Ibrahimu, nihurumie, umtume Lazaro achovye ncha ya kidole chake majini, auburudishe ulimi wangu; kwa sababu ninateswa katika moto huu.
²⁵ Ibrahimu akasema, Mwanangu, kumbuka ya kwamba wewe uliyapokea mambo mema yako katika maisha yako, na Lazaro vivyo alipata mabaya; na sasa yeye yupo hapa anafarijiwa, na wewe unaumizwa.
²⁶ Na zaidi ya hayo, kati yetu sisi na ninyi kumewekwa shimo kubwa, ili wale watakao kutoka huku kwenda kwenu wasiweze; wala watu wa kwenu wasivuke kuja kwetu.
²⁷ Akasema, Basi, baba, nakuomba, umtume nyumbani kwa baba yangu,
²⁸ kwa kuwa ninao ndugu watano, ili awashuhudie, wasije wao pia wakafika mahali hapa pa mateso.
²⁹ Ibrahimu akasema, Wanao Musa na manabii; na wawasikilize wao.
³⁰ Akasema, La, baba Ibrahimu, lakini kama akiwaendea mtu atokaye kwa wafu, watatubu.
³¹ Akamwambia, Wasipowasikia Musa na manabii, hawatashawishwa hata mtu akifufuka katika wafu.


Hapa panaelezea mtu akifa nini hutokea.
Ila binadamu wanajua kutunga hadithi za kuhuzunisha..!!
[emoji2][emoji2][emoji2][emoji2][emoji2][emoji2].....
Duh..!
 
Yule aliyekula makombo je? Biblia inasema alikufa wakakutana na tajiri mbinguni
Ni mifano tu alikuwa anatoa bwana Yesu...
Ila tukio la kufufuliwa lazaro kwa mujibu wa bibilia takatifu ni tukio ambalo lilitokea. Na lazaro aliyekufa na kufufuliwa na Yesu alikuwa rafiki yake Yesu.

Hivyo haya mambo mawili tofauti.
 
Ni mifano tu alikuwa anatoa bwana Yesu...
Ila tukio la kufufuliwa lazaro kwa mujibu wa bibilia takatifu ni tukio ambalo lilitokea. Na lazaro aliyekufa na kufufuliwa na Yesu alikuwa rafiki yake Yesu.

Hivyo haya mambo mawili tofauti.
Ok
 

Mhubiri 9:5, 10​

Biblia Habari Njema (BHN)​

5. Maana, walio hai hujua ya kwamba watakufa, lakini wafu hawajui chochote. Hawana tuzo tena; hata kumbukumbu lao limesahauliwa kabisa

10. Kila unachotaka kufanya kifanye kwa nguvu zako zote, maana, hakuna kazi, wala wazo, wala maarifa, wala hekima huko kuzimu unakokwenda.
 
Back
Top Bottom