Hivi, nani anatakiwa kuchinja nyama?

Hivi, nani anatakiwa kuchinja nyama?

usungilo

JF-Expert Member
Joined
Aug 9, 2012
Posts
522
Reaction score
332
Hii ishu ina migogo baadhi ya maeneo na watu wanataka kuanza kugoma kununua nyama. Niliwahi kutana nayo na kwenye maoni ya katiba mpya. Kisheria na kijamii nani wanaruhusiwa kuchinja mifugo machinjioni? Tumezoea mashehe ndo wanachinja, je wachungaji/wainjilisti na mapadre/makatekista wanaruhusiwa kuchinja? Kama ndio kwa nini haikuwekwa zamu? Kama hapana kwa nini iwe hivyo? Kuna ndugu zangu wauza nyama na wengine ni walokole wamenifuata na kuniuliza kuhusu hilo, ukichukulia nina kaelimu ka kukariri wakajua najua kila kitu. Naomba wanasheria, wanajamii, mabwana mifugo na wengine wenye ujuzi wa hili jambo mnijuze ili nisitoe ufafanuzi wa kimgogoro.
 
Hii kitu mkuu falsafa yake ni "complex". Waislam wamewekewa utaratibu wa namna ya kuchinja mnyama ili awe halali
kwao kula, wakristu nahisi hawana kikwazo kinachowazuiya kula nyama kwa namna yeyote alivyochinjwa!
Kwahiyo ni bora tufuate utaratibu ambao hauna shida kwa jamii yote ili kuepusha usumbufu na pia ni ajira kwa wengine!
Mungu ibariki Tanzania.
 
Ntarudi mwishoni wacha waje wachangie wengine kwanza!
Najua una kaudini kiasi ila umesahau kuuliza kwanini J,pili iwe siku ya mapumziko na isiwe Ijumaa na J,pili?
 
Ntarudi mwishoni wacha waje wachangie wengine kwanza!
Najua una kaudini kiasi ila umesahau kuuliza kwanini J,pili iwe siku ya mapumziko na isiwe Ijumaa na J,pili?

Sidhani kama kaelekea huko zaidi, may be! ila mimi nimeliona la kijamii zaidi !!
 
Sidhani kama kaelekea huko zaidi, may be! ila mimi nimeliona la kijamii zaidi !!

Soma vizuri post yake utaona muelekeo wake,ndio kataja wachungaji na mapasta,kwanini asingetaja mtu yyte tu bila kuhusisha dini?ndio namwaambia ukitaka kutazama udini utazame kotekote
 
Hii kitu mkuu falsafa yake ni "complex". Waislam wamewekewa utaratibu wa namna ya kuchinja mnyama ili awe halali
kwao kula, wakristu nahisi hawana kikwazo kinachowazuiya kula nyama kwa namna yeyote alivyochinjwa!
Kwahiyo ni bora tufuate utaratibu ambao hauna shida kwa jamii yote ili kuepusha usumbufu na pia ni ajira kwa wengine!
Mungu ibariki Tanzania.
Hili ndilo jibu haswaa!!
 
Ntarudi mwishoni wacha waje wachangie wengine kwanza!
Najua una kaudini kiasi ila umesahau kuuliza kwanini J,pili iwe siku ya mapumziko na isiwe Ijumaa na J,pili?

mkuu nimesema ni mambo yanayoongelewa mtaani na yaliongelewa kwenye utoaji wa maoni ya katiba. Unajua kuna mambo yalikuwepo inabidi tupate ufafanuzi, je na nchi zingine wanafanya hivyo?
 
Sidhani kama kaelekea huko zaidi, may be! ila mimi nimeliona la kijamii zaidi !!

mkuu nadhani umenielewa. Tangu kuasisiwa kwa udini na jk sasa hivi watu wamefikia kuhoji kila jambo la kijamii linalofanywa na upande mmoja kwa kwa nini na wengine hawahusishwi? Ndo maana nimeuliza wanasheria, wanajamii na watu wa mifugo. Vinginevyo ningeuliza tu kwa ni waislamu ndo wachinjaji? Au ningesema nachukia nyama inayochinjwa na waislamu!
 
Yeyote anaweza kuchinja hasa ikizingatiwa kuwa hizi dini nyemelezi zimemkuta mswahili akijua kuchinja kupika na kula. Nadhani anayeweza kuchinja ni suala la mwenye mnyama. By the way, nani anastahili kuchinja samaki, nyati, Swala, Nyumbu na wengine wengi? Sijui hawa walioweka masharti ya kuchinja mfano ng'ombe kama wanao kwao zaidi ya kuwafaidi toka kwetu.
 
Soma vizuri post yake utaona muelekeo wake,ndio kataja wachungaji na mapasta,kwanini asingetaja mtu yyte tu bila kuhusisha dini?ndio namwaambia ukitaka kutazama udini utazame kotekote

kwani na waislamu ni yeyote anaruhusiwa kuchinja? Mi nachujua ni shehe ndo maana nikataja na viongozi wa imani zingine kwani najua kuna kuhusisha maombi wakati wa uchinjaji! Wewe ndo unaonekana hujasoma vizuri kwani mwanzo nimetaja mashehe na sijasema kila muislamu. Tafadhali sana nahitaji ufafanuzi wa kisheria, kijamii au kiafya. Mambo ya dini weka huko.
 
Hili ndilo jibu haswaa!!

ni jibu sahihi lakini kutokana na waislamu( wao wanawaita wahuni) kuhoji kila kinachoendelea na wa upande mwingine uvumilivu umeanza kuwashinda. Kuna post moja niliiweka humu nikiwa makete wakati wa utoaji wa maoni ya katiba, kuna maoni yalitolewa kila watu wawe na bucha zao na wachinje wao wenyewe.! Nimeulizwa tena na ndugu zangu niwape ufafanuzi nikawaambia ngoja ntalifuatilia. Mambo yanayojitokeza kwenye jamii yanahitaji kutolewa ufafanuzi kama la necta lilivyofafanuliwa
 
Wakatiwingine nahisi kama hizi issue za udini ni syndicate ya kutupoteza mwelekeo kuhusu katiba mpya. Tukae kujadili siku za mapumziko na jinsi ya kuchinja vitoweo halafu tuache kuangalia mambo ya msingi.
 
Yeyote anaweza chinja tu kwetu sisi wakristo hatuna shida hata kama kanyongwa sisi twala. You know what we do initially chakula ni cha mpishi baada ya mimi kupewa na kibadili na kuwa chakula cha Mungu wa Israeli, Ibrahim, Isaka, n.k. Ukiamin tu hata kama kina sumu ya kufisha hakitakudhuru. Hivyo mimi nawashauri wakristo whatever atakayechinja kikubwa ni wewe kumshirikisha Mungu wako ili akipe baraka na nguvu ili kikupe afya. Tuachane na urgument za kidini hili halitatusaidia zaidi utakuta wachinjaji wanakula bila kufuata kanuni za afya na mwisho wanakufa na hypertension. Tuwe wavumilivu kama kristo alivyovumilia mpaka kufa msalabani.
 
Yeyote anaweza chinja tu ..... Tuwe wavumilivu kama kristo alivyovumilia mpaka kufa msalabani.

Kwanza nakugongea "LIKE" halafu naunga mkono hoja 100%. Asiye na kazi, ajadili "kuua", ingawa najua Mkristo wa kweli, hawezi kujadili apewe mamlaka na uwezo wa kuua, na Mwisilamu wa kweli, hawezi kujadili siku ya mapumziko. Wengi wa wanaojadili, wana majina ya Kikristo au ya Kiislamu, wakati hawajui hata makanisa au Misikiti ilipo.
Sitegemei mjadala wowote kati ya waislamu wa kweli na wakristo wa kweli, ila nategemea watakao jadili ni wale mashabiki wa waislamu na mashabiki wa wakristo.
 
Hii ishu ina migogo baadhi ya maeneo na watu wanataka kuanza kugoma kununua nyama. Niliwahi kutana nayo na kwenye maoni ya katiba mpya. Kisheria na kijamii nani wanaruhusiwa kuchinja mifugo machinjioni? Tumezoea mashehe ndo wanachinja, je wachungaji/wainjilisti na mapadre/makatekista wanaruhusiwa kuchinja? Kama ndio kwa nini haikuwekwa zamu? Kama hapana kwa nini iwe hivyo? Kuna ndugu zangu wauza nyama na wengine ni walokole wamenifuata na kuniuliza kuhusu hilo, ukichukulia nina kaelimu ka kukariri wakajua najua kila kitu. Naomba wanasheria, wanajamii, mabwana mifugo na wengine wenye ujuzi wa hili jambo mnijuze ili nisitoe ufafanuzi wa kimgogoro.


Yeyote mwenye kisu anaweza kuchinja. Mi mbona mke wangu anachinja kuku, bata na hata mbuzi kama siko nyumbani. Visingizio vingine hivi ni vya kujiletea wenyewe kutokana na uroho wetu. Eti jirani akikuchinjia sharti umpelekee shingo,si upuuzi huu? Mi nimempa ruhusa mke wangu kuchinja kile akitakacho. In short, anybody mwenye kushika kisu anaruhusa ya kuchinja, hii haina miiko. Ulaya mashine ndizo zinazochinja mbona utamu wa nyama ni ule ule?
 
Hii ishu ina migogo baadhi ya maeneo na watu wanataka kuanza kugoma kununua nyama. Niliwahi kutana nayo na kwenye maoni ya katiba mpya. Kisheria na kijamii nani wanaruhusiwa kuchinja mifugo machinjioni? Tumezoea mashehe ndo wanachinja, je wachungaji/wainjilisti na mapadre/makatekista wanaruhusiwa kuchinja? Kama ndio kwa nini haikuwekwa zamu? Kama hapana kwa nini iwe hivyo? Kuna ndugu zangu wauza nyama na wengine ni walokole wamenifuata na kuniuliza kuhusu hilo, ukichukulia nina kaelimu ka kukariri wakajua najua kila kitu. Naomba wanasheria, wanajamii, mabwana mifugo na wengine wenye ujuzi wa hili jambo mnijuze ili nisitoe ufafanuzi wa kimgogoro.

Hebu tupe ushahidi wa mashehe wanaochinja huko machinjioni, mimi napita pita sana vingunguti kununuwa nyama, sijakutana na shehe anaechinja huko bali nimekuta vijana ndio wanachinja huko.

Au una maana ipi unaposema "mashehe"?
 
Ni kweli kabisa thread nyingine humu jamvini zinapotupotezea. Leteni vitu vya kutuletea mabadiliko in the positive sense.
Kwa upande wangu nyama ni nyama tu mradi haina madhara mwilini. Mnaotafuta kupumzika bongo hii hamna maana kwani tunatakiwa tufanye kazi masaa 24 siku 7 kwa wiki kama kweli tunataka kujiletea maendeleo. Tuna mambo mengi mazito mazito ya kupambana nayo taifa hili nalo liwe taifa lenye handhi. Nendeni Kenya mkaone, nendeni India mkaone hakuna kulala ukilala wafa kwa njaa na kwa hali hiyo ukikutana na myama kibudu utamla tuuu...njaa haina dini, kabila au taifa.
 
Back
Top Bottom