Hivi ni kwanini siku hizi watu hawapigani mitaani kama miaka ya 1980s?

Hivi ni kwanini siku hizi watu hawapigani mitaani kama miaka ya 1980s?

Nakumbuka miaka ya 80-90 ilikuwa jambo la kawaida kukuta jamaa wanapigana mitaani halafu watu wanashangilia sana.
Yaani ukiwa mtemi au gangwe basi unaonekana wa maana sana. Hata baadhi ya disco ilikuwa lazima ziishe kwa ngumi.
Kwa wale wa Iringa mtawakumbuka kina cool 9, shedadi, Ray nk
Ustaarabu husaidia kuondoa tabia za kishenzi na kuzaa tabia za kiungwana. Kadiri muda unavyokwenda ndio binadaam wanazidi kustaarabika na kutumia njia nyingine kutatua matatizo yao badala ya kupigana. Hata ukienda nchi zilizoendelea utakuta kiwango cha kupigana kiko chini kulinganisha na nchi zinazoendelea.
 
Siwezi kupigana kwa sasa ukimgusa tu mtu huyo ananyooka mazima polisi unasongeshwa mbele kuingia bure kutoka pesa ya nini yote kusumbuana maisha yenyewe magumu
 
Daaah! mleta mada umenikumbusha mbali miaka ya 1995_2000 kesi nyingi sana nilipelekewa nyumbani.Kwanza kunadogo alipokea ndosi/teke la kivandame alivunjika mkono,kesi ambayo ndiyo ukawa mwisho wa kupigana ni pale kijana mmoja nilimpa free header na alizimia 30minutes hapo ndipo kijasho chembamba kilinitoka na kuvua gloves rasmi.
 
Mleta mada unanikumbusha mbali sana 1981 ama 1982 kama sijakosea kuna dogo flan aliingia anga zangu kijijin huko mbarali kwa kumtongoza mchepuko wangu. Nilitembeza vitasa kijiji kizima kwa madogo wote wenye umri kama wake. Maumiv makal sana niliwakabiz kwa kosa la mtu mmoja. Yan nilikuwa na bwaka nikiibuka 10 ardhin nikizama nikichomoza 20 wengine chali. Nikamchukua dogo mwengine mwembamba hiv nikamtumia kama fimbo kwa kuwacharaza. Ila kwasasa nimejikita zaid kusaka hela uzee nao ndio huo. Ila miaka iyo ya themanini nilikuwa mtemi sana
Acha fix wewe...eti nilimtumia dogo mwembamba kama fimbo...
 
Siku hizi watu wanaogopa kupigana kwa sababu vichwa vya watu wengine vimeoza, zamani ilikuwa mkizipanga mara dakika tu! watu wenye busara hao wamefika lakini siku izi ni hatare! unapigika mpaka unakimbilia polisi ukiingia ndani polisi wanakuvutia nje, unapigika tena. We mwenyewe si unaona siku hizi ukigonga mtu na gari lazima wakuue.
 
Huu uzi kwa sisi wakongwe ndio pahala pake. Nakumbuka enzi zile nasoma msingi nilikua mwoga kupigana basi nikawa napigwa na wengi darasani nakarbia list ya mwisho kupigana siku nikadundwa ikanibidi nikashtak nyumban nikaambiwa olee wako kesho urudi umepigwa. Hapo ikawa kama moto umemwagiwa petrol nataman kukuche nikalipize kisasi. Kusema kweli tulikua tuna utaratibu wa kuanzisha mapambano mpaka anajulikana mbabe wa darasa na shule. Basi ikaandaliwa. Pambano nirudiane na mpinzan wangu nilimpa kipigo cha kutisha, nikawa kila mambano nashinda watu wakawa wananishangaa siku nikampiga mbabe wa darasa la sita na mim nipo la 4. Basi nikaanza kuogopwa shule nzima habar zikafika hadi mtaani kuwa ninagawa ngumi atarii. Mtu akionewa anakuja kwangu yani nilikua nikipewa taarifa ya kusulubisha mtu nahisi furaha kwani nilishaonewa sana na nawaza tu mbinu Mpya za kupigana. Duu huwa nacheka sana nikikumbuka zile. Enziii
 
Mi nitampiga mwizi tu hao wengine hata siwagusi maana anaweza kufa ikala kwako bora mwizi mnapiga wengi
 
Siku hizi watu wanapigana kidijitali zaidi. Mkikosana mtaani mnapigana kupitia mitandao kama facebook, instagram and the like kwa kuandikana matusi, kuanika siri au mambo binafsi hadharani, kubandika picha za kudharirishana n.k.
 
nakumbuka kitambo kuna mjamaa alimdunda tizo flani watu wanamuliza sababu nini mbona una mpiga tozi wa watu mjamaa asemi yeye alikua anarusha miteke tu kama bruce alaf mjamaa likua anacheza karate sijui ile miteke ilikua noma..badae nakuja kuambiwa sababu ilikua sh. 100 tu mtu kala kichapo teh teh

siku izi kila mtu na mishe zake watu wanapiga na pesa..
 
Mayai ya kuku wa kisasa, chipsi za mafuta ya trans .. foma vyakula mchicha, mahindi, mpunga nk kulimwa kwa kutegemea mbolea za viwandani nk, hapo kupigana ni kujipa tiketi ya kwenda ahera.
Mbolea toka vyoo vya watu hasa wa Mbezi beach wanaokula chips mayai utapata nini?
 
Zamani unapigana ukipigwa ukaenda kushitaki nyumbani na kwenyewe unasulubiwa sasa kinachofuata hapo ustafute uchochoro wa kujificha unatafuta namna ya kujitetea hapo lazima pachimbike nakumbuka mwaka 94 nilipigwa kichwa kimoja tu chini kesho yake nikaanza kumsaka adui nikamkuta kijiweni na washikaji sikusubiri nikamvaa mazima zilipgwa kama dakika saba nikambahatsha ngumi ya kidevu na yeye chini sikumpa nafasi ni mashambulizi mpaka akawa anavuja damu nikamuacha
 
Miaka niliwahi kutembeza kichapo kijiji kizima mpaka wakaniita King of the Village.
 
People Siku hizi ni waoga kama kunguru wa Dasalama
 
Life style imebadilika sana, pia ustaarabu umeongezeka.
 
Maisha yamekuwa magumu kila MTU anapigana Na maisha
 
Back
Top Bottom