Hivi ni kwanini siku hizi watu hawapigani mitaani kama miaka ya 1980s?

Ustaarabu husaidia kuondoa tabia za kishenzi na kuzaa tabia za kiungwana. Kadiri muda unavyokwenda ndio binadaam wanazidi kustaarabika na kutumia njia nyingine kutatua matatizo yao badala ya kupigana. Hata ukienda nchi zilizoendelea utakuta kiwango cha kupigana kiko chini kulinganisha na nchi zinazoendelea.
 
Siwezi kupigana kwa sasa ukimgusa tu mtu huyo ananyooka mazima polisi unasongeshwa mbele kuingia bure kutoka pesa ya nini yote kusumbuana maisha yenyewe magumu
 
Daaah! mleta mada umenikumbusha mbali miaka ya 1995_2000 kesi nyingi sana nilipelekewa nyumbani.Kwanza kunadogo alipokea ndosi/teke la kivandame alivunjika mkono,kesi ambayo ndiyo ukawa mwisho wa kupigana ni pale kijana mmoja nilimpa free header na alizimia 30minutes hapo ndipo kijasho chembamba kilinitoka na kuvua gloves rasmi.
 
Acha fix wewe...eti nilimtumia dogo mwembamba kama fimbo...
 
Siku hizi watu wanaogopa kupigana kwa sababu vichwa vya watu wengine vimeoza, zamani ilikuwa mkizipanga mara dakika tu! watu wenye busara hao wamefika lakini siku izi ni hatare! unapigika mpaka unakimbilia polisi ukiingia ndani polisi wanakuvutia nje, unapigika tena. We mwenyewe si unaona siku hizi ukigonga mtu na gari lazima wakuue.
 
Huu uzi kwa sisi wakongwe ndio pahala pake. Nakumbuka enzi zile nasoma msingi nilikua mwoga kupigana basi nikawa napigwa na wengi darasani nakarbia list ya mwisho kupigana siku nikadundwa ikanibidi nikashtak nyumban nikaambiwa olee wako kesho urudi umepigwa. Hapo ikawa kama moto umemwagiwa petrol nataman kukuche nikalipize kisasi. Kusema kweli tulikua tuna utaratibu wa kuanzisha mapambano mpaka anajulikana mbabe wa darasa na shule. Basi ikaandaliwa. Pambano nirudiane na mpinzan wangu nilimpa kipigo cha kutisha, nikawa kila mambano nashinda watu wakawa wananishangaa siku nikampiga mbabe wa darasa la sita na mim nipo la 4. Basi nikaanza kuogopwa shule nzima habar zikafika hadi mtaani kuwa ninagawa ngumi atarii. Mtu akionewa anakuja kwangu yani nilikua nikipewa taarifa ya kusulubisha mtu nahisi furaha kwani nilishaonewa sana na nawaza tu mbinu Mpya za kupigana. Duu huwa nacheka sana nikikumbuka zile. Enziii
 
Mi nitampiga mwizi tu hao wengine hata siwagusi maana anaweza kufa ikala kwako bora mwizi mnapiga wengi
 
Siku hizi watu wanapigana kidijitali zaidi. Mkikosana mtaani mnapigana kupitia mitandao kama facebook, instagram and the like kwa kuandikana matusi, kuanika siri au mambo binafsi hadharani, kubandika picha za kudharirishana n.k.
 
nakumbuka kitambo kuna mjamaa alimdunda tizo flani watu wanamuliza sababu nini mbona una mpiga tozi wa watu mjamaa asemi yeye alikua anarusha miteke tu kama bruce alaf mjamaa likua anacheza karate sijui ile miteke ilikua noma..badae nakuja kuambiwa sababu ilikua sh. 100 tu mtu kala kichapo teh teh

siku izi kila mtu na mishe zake watu wanapiga na pesa..
 
Miaka hiyo chakula kilikuwa kingi kwa hiyo watu walikuwa wanashiba alafu kazi hawana nguvu zao wanatumia vipi ndio hizo ngumi. Sasa miaka hii watu Dar wanashindia maindi ya kuchoma na ndimu nguvu ya kupigana anaitoa wapi?
 
Mayai ya kuku wa kisasa, chipsi za mafuta ya trans .. foma vyakula mchicha, mahindi, mpunga nk kulimwa kwa kutegemea mbolea za viwandani nk, hapo kupigana ni kujipa tiketi ya kwenda ahera.
Mbolea toka vyoo vya watu hasa wa Mbezi beach wanaokula chips mayai utapata nini?
 
Zamani unapigana ukipigwa ukaenda kushitaki nyumbani na kwenyewe unasulubiwa sasa kinachofuata hapo ustafute uchochoro wa kujificha unatafuta namna ya kujitetea hapo lazima pachimbike nakumbuka mwaka 94 nilipigwa kichwa kimoja tu chini kesho yake nikaanza kumsaka adui nikamkuta kijiweni na washikaji sikusubiri nikamvaa mazima zilipgwa kama dakika saba nikambahatsha ngumi ya kidevu na yeye chini sikumpa nafasi ni mashambulizi mpaka akawa anavuja damu nikamuacha
 
Miaka niliwahi kutembeza kichapo kijiji kizima mpaka wakaniita King of the Village.
 
People Siku hizi ni waoga kama kunguru wa Dasalama
 
Life style imebadilika sana, pia ustaarabu umeongezeka.
 
Maisha yamekuwa magumu kila MTU anapigana Na maisha
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…