Hivi ni kweli ile Ikulu ya Dar Magogoni ulikuwa msikiti zama hizo?

Hivi ni kweli ile Ikulu ya Dar Magogoni ulikuwa msikiti zama hizo?

20230520_142653.jpg
 
Nilijumuika siku moja nje ya nyumba ya ibada nikawa naondoa uchovu kwa kupiga vikombe viwili vitatu vya kahawa pakawa na story inaendelea kuhusu miaka ya mwanzo ya nchi yetu nikasikia mtu mmoja akihanikiza kwa sauti ya jazba kwamba rais wetu wa kwanza aliibatiza hii nchi.

Inawezekana ikawa kweli labda huyu rais aligeuza msikiti kuwa ikulu ikiwa aliweza kulipiga maji taifa zima angeshindwaje jambo dogo kama hilo?
 
Uongo wa mashehe tumbo
Ni kweli,hadi leo pale Ikulu mlangoni kuna maandishi ya sura moja wapo za Quran, infact ilikua ni chuo cha mafunzo ya dini,taasisi kubwa ya dini. Eneo lile lilikua likimilikiwa na familia ya Mzee Tambaza,alimiliki eneo kubwa sana kuanzia Upanga mpaka posta baharini.

Naomba kuambatanisha na ushahidi wa video ambapo hadi leo upo pale Ikulu.

Screenshot_20230512-084827.png
 
Nilijumuika siku moja nje ya nyumba ya ibada nikawa naondoa uchovu kwa kupiga vikombe viwili vitatu vya kahawa pakawa na story inaendelea kuhusu miaka ya mwanzo ya nchi yetu nikasikia mtu mmoja akihanikiza kwa sauti ya jazba kwamba rais wetu wa kwanza aliibatiza hii nchi.

Inawezekana ikawa kweli labda huyu rais aligeuza msikiti kuwa ikulu ikiwa aliweza kulipiga maji taifa zima angeshindwaje jambo dogo kama hilo?
I am slways amazed by a man's capacity to dream.
 
Nilijumuika siku moja nje ya nyumba ya ibada nikawa naondoa uchovu kwa kupiga vikombe viwili vitatu vya kahawa pakawa na story inaendelea kuhusu miaka ya mwanzo ya nchi yetu nikasikia mtu mmoja akihanikiza kwa sauti ya jazba kwamba rais wetu wa kwanza aliibatiza hii nchi.

Inawezekana ikawa kweli labda huyu rais aligeuza msikiti kuwa ikulu ikiwa aliweza kulipiga maji taifa zima angeshindwaje jambo dogo kama hilo?
Ina sense hii usemayo
 
Nilijumuika siku moja nje ya nyumba ya ibada nikawa naondoa uchovu kwa kupiga vikombe viwili vitatu vya kahawa pakawa na story inaendelea kuhusu miaka ya mwanzo ya nchi yetu nikasikia mtu mmoja akihanikiza kwa sauti ya jazba kwamba rais wetu wa kwanza aliibatiza hii nchi.

Inawezekana ikawa kweli labda huyu rais aligeuza msikiti kuwa ikulu ikiwa aliweza kulipiga maji taifa zima angeshindwaje jambo dogo kama hilo?
Ngoma nzito ,inamana palitekwa?
 
Ni kweli,hadi leo pale Ikulu mlangoni kuna maandishi ya sura moja wapo za Quran, infact ilikua ni chuo cha mafunzo ya dini,taasisi kubwa ya dini. Eneo lile lilikua likimilikiwa na familia ya Mzee Tambaza,alimiliki eneo kubwa sana kuanzia Upanga mpaka posta baharini.

Naomba kuambatanisha na ushahidi wa video ambapo hadi leo upo pale Ikulu.
View attachment 2629211
View attachment 2629208
Asante kwa taarifa,hii ndio raha ya jamii forum, "we dare to talk"
 
Anaeijua historia ya Ikulu ya Magogoni atusimulie, naambiwa ulikuwa msikiti, mzungu akapapenda akageuza makazi yake kisha kuwa Ikulu.

Hili lina ukweli wowote?

Naomba kujuzwa.
Troiker,
Kuna video hapa inaeleza historia ya Ikulu na muelezaji ni Abdallah Mohamed Saleh maarufu kwa jina la Abdallah Tambaza.

Abdallah ni kinying'inya cha ukoo wa Tambaza wamiliki enzi hizo za ardhi ilipo hii leo Ikulu ambayo imejengwa zaidi ya miaka 150 iliyopita.

Abdallah anaijua historia yote ya babu zake kwa majina yao historia ambayo imerithiwa kutoka kizazi kimoja hadi kingine kwa takriban miaka 200.

Ukimuuliza Abdallah huyo Abdallah aliepewa yeye jina lake ni nani atakushangaza kwani atakutajia na jina la mkewe na wapi waliishi na atakuonyesha hivi sasa kinying'inya mwenye jina la huyo Bi Mkubwa.

Huyu ndiye Abdallah Tambaza aliyeeleza historia ya Ikulu na baadhi ya makaburi ya babu zake yamo ndani ya ua wa Ikulu na ndani ya ua wa ofisi za serikali Magogoni pale Central Establishment.

Hermann von Wissmann aliyeleta jeshi la mamluki kutoka Sudan na Mozambique kuja kupigana na Abushiri bin Salim na Mtwa Mkwawa aliishi katika jengo hilo kama Gavana wa pili wa Germany Ostafrika.

Wissmann ndiye aliyemleta Chief Mohosh Shangaan na Sykes Mbuwane katika ardhi ya Tanganyika kutoka Mozambique na koo hizi mbili zikajakuwa maarufu sana katika mji wa Dar-es-Salaam na katika historia ya kudai uhuru wa Tanganyika.

Hawa Wazulu, Wanubi kutoka Sudan na Wamanyema kutoka Belgian Congo waliwakuta wenyeji wa Dar-es-Salaam akina Tambaza na Chaurembo na koo myingine bado wanahodhi ardhi zao ndani ya utawala wa Wajerumani.

Ndiyo unakuta Kariakoo kulikuwa na Msikiti wa Mtoro, Magomeni Msikiti wa Ndungumbi na Mwinyimkuu wote hawa ndugu kwa nasaba na Uislam.

Sehemu ya Kitumbini pakajengwa Msikiti wa Ibadh, Msikiti wa Waarabu kutoka Yemen na msikiti wa Sunni uliojengwa na Wahindi.

Hali ni hivi kuanzia Mbwamaji, Msasani, Kunduchi hadi Bagamoyo.

Wakoloni baada ya kuchukua jengo lile la Waislam na kufanya makazi ya serikali hawakuweza tena kugusa ardhi zilizokuwa na misikiti na ardhi hizo zikabakia kuwa wakfu hadi hii leo ingawa pakazuka matatizo ya mali za Waislam baada ya uhuru kupatikana mwaka wa 1961.
 
Ikulu sasa ipo Dodoma ni muda wenu ndugu zetu waislam kudai hilo jengo na uzuri rais wa nchi ni muislam hivyo tumieni nafasi hiyo adhimu kudai jengo lenu

Maendeleo hayana chama
Kin...
Si kazi ya Rais Muislam kushughulika na mambo ya Waislam.
Rais yuko pale kuwashughulikia wananchi wa imani zote.

Au una hofu Rais ambae si Muislam haweze kuwafanyia Waislam uadilifu?

Kama Waislam kudai vitu kwa nini husemi wadai kiwanja walipojenga ofisi ya African Association ambako leo kuna Ofisi Ndogo ya CCM?

Au kwa nini wasidai jengo la Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika ambalo leo linamilikiwa na serikali?

Au kwa nini wasijdai mali za EAMWS?

Kama kudai Waislam wana mengi ya kudai katika historia ya uhuru wa Tanganyika katika hali na mali.

Unataka Waislam wadai hadi ihsani zao?

1684667782666.jpeg

Hili ni Jengo la Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika lililojengwa mwaka wa 1936 kama shule kwa ajili ya watoto wa Kiislam Al Jamiatul Islamiyya Muslim School leo ni Shule ya Msingi ya Lumumba.​
 
Back
Top Bottom