Hivi ni kweli kuwa wenye herufi "M" kwenye kiganja wana bahati sana?

Hivi ni kweli kuwa wenye herufi "M" kwenye kiganja wana bahati sana?

Waswahili wana msemo, lisemwalo lipo.
Ni mara nyingi Sana nimekuwa nikisikia tetesi kuwa, watu wenye viganja vyenye alama ya "M " wana bahati Sana, Kwa upande wangu mimi ni muumini mzuri sana Wa Mungu, ila mkono wangu wa kulia una alama ya "M " wa kushoto hauna, binafsi nimekuwa na bahati Sana ktk maisha yangu, na hili nimeanza kuamini kuwa ni kweli kiganja chenye "M"ni bahati kubwa ukiwa nacho.
Nakumbuka ilikuwa 5/january/2012 nilipoamka asubuhi nyumbani nikiwa Sina hata cent, chakula ndani kilikuwa kimeisha, na sukari ilikuwa hamna, nilikuwa nimechanganyikiwa kabisa maana biashara yangu ilianguka
ilipotimia saa 2:30 asubuhi ile, simu yangu iliita, namba Ilikuwa ngeni, nilipokea na sauti ya kike ikasikika, ilikuwa ni girlfriend wangu Wa zamani anayeishi Kwa sasa Canada, alikuwa amekuja Tanzania bila kunitaarifu, yeye tayari ana uraia wa Canada na kaolewa na mzungu, alikuwa Amekuja kusalimia ndugu zake Arusha, nikaongea naye mambo mengi kisha nikamtania Kama kumjaribu anikumbuke basi hata hela ya soda, akaniambia nisubiri kidogo, nami nikaondoka kwenda kuhangaika angalau nipate hata pesa ya kununulia hata unga, ilipotimia saa 5 nikawa nimerudi nyumbani na sh 5000 tu niliyokuwa nimepewa na rafiki yangu.
Nikamkuta Mke wangu amechuma kisamvu anakichemsha bila kujua kitaliwa na nini.
Nikampatia ile elfu 5,nikakaa ndani nikiwa na mawazo ile mbaya, nikisubiria msosi nile, ilipotimia saa 6:30 mchana, sms ikaingia kwenye simu yangu, nilipotazama ilikuwa ni m pesa, yule girlfriend wangu alikuwa kanitumia sh 950,000 ,moyo wangu Ulienda kasi Kwa mapigo yaani sikuweza kuamini, nikahisi labda alikosea tu, nikatoka mbio ndani kwenda kutoa ile pesa, akawa ananipigia sipokei, baadae akatuma sms nadhani umepata pesa niliyokutumia, sikujibu, wakati nakaribia kwenye kibanda cha m pesa ili nitoe pesa, nikaokota pochi iliyokuwa imetuna na kuiweka mfukoni.
Nilizitoa pesa Haraka Sana, kisha nikamtaarifu kuwa nimepata na kumshukuru Sana, wakati narudi nyumbani nikaitazama ile pochi kuona ni kitu gani kilikuwemo, Duh! sikuamini tena, pochi haikuwa na anuani wala ID yoyote, ilikuwa na sh laki mbili, Kwa kweli sitaisahau hiyo Siku.
Siandiki kuwa furahisha watu, bali ni kweli tupu.
Tangia kipindi hicho hadi leo, kila nalofanya linakuwa.


Kiganja changu
Ni Mungu tu ilifikia mahali aliachia baraka zake kwako mkuu,sina uhakika sana na sijawahi kufanya research ila naamini karibu aslimia 90 ya binadamu wana hiyo herufi M kwenye mikono yao including me na sidhani kama ina maana yoyote.
 
Mi nilisikia wazee wakisema, ukikuta mtu ana hiyo alama basi ujue kuwa kwenye uzao wao[Tumbo moja katika familia] wakwanza kuzaliwa ni mtoto wa kiume, tofauti na hiyo alama wakwanza katika huo uzao ni mtoto wa kike.
 
...waswahili bana...watu wa kutafta shortcuts kwa kila jambo....wakitoka kwenye viganjwa wataamia kwenye K fupi na ndefu n.k n.k....fanyeni kazi kwa bidii mtoke...tofauti za viganja ni sawa na tafauti za ufupi na urefu wa watu...ama unene na wembamba.....ni maumbile tu.....
 
Haya ni matokeo ya unajimu na utabiri. pia yawezekana kuhusishwa na ushirikina. Mafanikio ya kweli utayapata kwanza kwa iumtegemea na kumwomba Mungu. pili jitihada zako binafsi kama kujiendeleza kielimu au kujituma ktk kazi au kuwa mvumilivu au bidii ktk kazi au mipango mizuri na kuepuka matumizi mabaya ya rasilimali, lakini zaidi ya yote utafanikiwa ikiwa una sifa nyingi ktk hizi nilizozitaja. tuachane na herufi za kiganjani kwani ni sawa na kuturudisha kwenye utawala wa JK
 
Haya ni matokeo ya unajimu na utabiri. pia yawezekana kuhusishwa na ushirikina. Mafanikio ya kweli utayapata kwanza kwa iumtegemea na kumwomba Mungu. pili jitihada zako binafsi kama kujiendeleza kielimu au kujituma ktk kazi au kuwa mvumilivu au bidii ktk kazi au mipango mizuri na kuepuka matumizi mabaya ya rasilimali, lakini zaidi ya yote utafanikiwa ikiwa una sifa nyingi ktk hizi nilizozitaja. tuachane na herufi za kiganjani kwani ni sawa na kuturudisha kwenye utawala wa JK
...exactly....hata Mungu huwa anawasaidia wanaojisaidia....kuna watu wanashinda makanisani huko wakitafta upako na kuacha kufanya kazi....na matokeo yake wamebaki kuwa maskini wa kutupwa...huku wakiwapelekea hao manabii hata kile kidogo wanachopata....
 
HERUFI ''M'' INA ASHIRIA WEWE MTU WA BAHATI KUBWA UNAWEZA KUWA NA PESA NYINGI AU KUWA KIONGOZI MKUU KATIKA MAMBO YA SIASA AU KUWA WEWE MTU MWENYE AFYA NZURI, AU KUWA NI MWANASHERIA AU HAKIMU AU KUWA MTU MAARUFU SANA. HERUFI ''M'' KWENYE KIGANJA CHAKO CHA MKONO WA KULIA INA ASHIRIA MAMBO MAZURI YA MAISHA YAKO YA BAADAE UTAFANIKIWA JITAHIDI.
What%25E2%2580%2599s%2Bso%2Bspecial%2Babout%2Ban%2B%25E2%2580%2598M%25E2%2580%2599%2Bon%2Bthe%2BPalm%2Bof%2Bthe%2BHand.jpg

Source Muugwana Blog

Acha huo Ushirikina. Unawapa watu matumaini ya uwongo.
 
h
HERUFI ''M'' INA ASHIRIA WEWE MTU WA BAHATI KUBWA UNAWEZA KUWA NA PESA NYINGI AU KUWA KIONGOZI MKUU KATIKA MAMBO YA SIASA AU KUWA WEWE MTU MWENYE AFYA NZURI, AU KUWA NI MWANASHERIA AU HAKIMU AU KUWA MTU MAARUFU SANA. HERUFI ''M'' KWENYE KIGANJA CHAKO CHA MKONO WA KULIA INA ASHIRIA MAMBO MAZURI YA MAISHA YAKO YA BAADAE UTAFANIKIWA JITAHIDI.
What%25E2%2580%2599s%2Bso%2Bspecial%2Babout%2Ban%2B%25E2%2580%2598M%25E2%2580%2599%2Bon%2Bthe%2BPalm%2Bof%2Bthe%2BHand.jpg

Source Muugwana Blog
hata sie wenye majina yanayoanza na herufi M.
 
HERUFI ''M'' INA ASHIRIA WEWE MTU WA BAHATI KUBWA UNAWEZA KUWA NA PESA NYINGI AU KUWA KIONGOZI MKUU KATIKA MAMBO YA SIASA AU KUWA WEWE MTU MWENYE AFYA NZURI, AU KUWA NI MWANASHERIA AU HAKIMU AU KUWA MTU MAARUFU SANA. HERUFI ''M'' KWENYE KIGANJA CHAKO CHA MKONO WA KULIA INA ASHIRIA MAMBO MAZURI YA MAISHA YAKO YA BAADAE UTAFANIKIWA JITAHIDI.
What%25E2%2580%2599s%2Bso%2Bspecial%2Babout%2Ban%2B%25E2%2580%2598M%25E2%2580%2599%2Bon%2Bthe%2BPalm%2Bof%2Bthe%2BHand.jpg

Source Muugwana Blog
Sio kweli. Mi ninayo na nina changamoto kibao!
 
HERUFI ''M'' INA ASHIRIA WEWE MTU WA BAHATI KUBWA UNAWEZA KUWA NA PESA NYINGI AU KUWA KIONGOZI MKUU KATIKA MAMBO YA SIASA AU KUWA WEWE MTU MWENYE AFYA NZURI, AU KUWA NI MWANASHERIA AU HAKIMU AU KUWA MTU MAARUFU SANA. HERUFI ''M'' KWENYE KIGANJA CHAKO CHA MKONO WA KULIA INA ASHIRIA MAMBO MAZURI YA MAISHA YAKO YA BAADAE UTAFANIKIWA JITAHIDI.
What%25E2%2580%2599s%2Bso%2Bspecial%2Babout%2Ban%2B%25E2%2580%2598M%25E2%2580%2599%2Bon%2Bthe%2BPalm%2Bof%2Bthe%2BHand.jpg

Source Muugwana Blog
Dah.. ebwana sasa hapo "M" iko wapi? Mie naona kama ipo "yǒu" ya kichina tu. Wewe lala tu nyumbani na "M" usubirie wakuletee
 
Muache kuwateka watu akil hiyo sayance hamna juhudi zako ndo mafanikio yako...acha kujishulisha ukifuatlia herufi M za mikono
 
AISEE MAMBO YA KUFIKIRIKA HAYA WEWE ULIONA WAPI HERUFI INA BAHATI WAKATI
INABIDI UTAFUTE KWA JASHO LAKO NDO UPATE AISEE MAKUBWA MADOGO YANA........................
 
Waswahili wana msemo, lisemwalo lipo.
Ni mara nyingi Sana nimekuwa nikisikia tetesi kuwa, watu wenye viganja vyenye alama ya "M " wana bahati Sana, Kwa upande wangu mimi ni muumini mzuri sana Wa Mungu, ila mkono wangu wa kulia una alama ya "M " wa kushoto hauna, binafsi nimekuwa na bahati Sana ktk maisha yangu, na hili nimeanza kuamini kuwa ni kweli kiganja chenye "M"ni bahati kubwa ukiwa nacho.
Nakumbuka ilikuwa 5/january/2012 nilipoamka asubuhi nyumbani nikiwa Sina hata cent, chakula ndani kilikuwa kimeisha, na sukari ilikuwa hamna, nilikuwa nimechanganyikiwa kabisa maana biashara yangu ilianguka
ilipotimia saa 2:30 asubuhi ile, simu yangu iliita, namba Ilikuwa ngeni, nilipokea na sauti ya kike ikasikika, ilikuwa ni girlfriend wangu Wa zamani anayeishi Kwa sasa Canada, alikuwa amekuja Tanzania bila kunitaarifu, yeye tayari ana uraia wa Canada na kaolewa na mzungu, alikuwa Amekuja kusalimia ndugu zake Arusha, nikaongea naye mambo mengi kisha nikamtania Kama kumjaribu anikumbuke basi hata hela ya soda, akaniambia nisubiri kidogo, nami nikaondoka kwenda kuhangaika angalau nipate hata pesa ya kununulia hata unga, ilipotimia saa 5 nikawa nimerudi nyumbani na sh 5000 tu niliyokuwa nimepewa na rafiki yangu.
Nikamkuta Mke wangu amechuma kisamvu anakichemsha bila kujua kitaliwa na nini.
Nikampatia ile elfu 5,nikakaa ndani nikiwa na mawazo ile mbaya, nikisubiria msosi nile, ilipotimia saa 6:30 mchana, sms ikaingia kwenye simu yangu, nilipotazama ilikuwa ni m pesa, yule girlfriend wangu alikuwa kanitumia sh 950,000 ,moyo wangu Ulienda kasi Kwa mapigo yaani sikuweza kuamini, nikahisi labda alikosea tu, nikatoka mbio ndani kwenda kutoa ile pesa, akawa ananipigia sipokei, baadae akatuma sms nadhani umepata pesa niliyokutumia, sikujibu, wakati nakaribia kwenye kibanda cha m pesa ili nitoe pesa, nikaokota pochi iliyokuwa imetuna na kuiweka mfukoni.
Nilizitoa pesa Haraka Sana, kisha nikamtaarifu kuwa nimepata na kumshukuru Sana, wakati narudi nyumbani nikaitazama ile pochi kuona ni kitu gani kilikuwemo, Duh! sikuamini tena, pochi haikuwa na anuani wala ID yoyote, ilikuwa na sh laki mbili, Kwa kweli sitaisahau hiyo Siku.
Siandiki kuwa furahisha watu, bali ni kweli tupu.
Tangia kipindi hicho hadi leo, kila nalofanya linakuwa.


Kiganja changu

Hiyo si bahati ni wizi tu unakusumbuwa, si ungetangaza hayo maeneo, tena hii ishu si ya siku nyingi kwa kuwa inahusu M-Pesa ina maana redio zilishakuwepo zenye huduma ya ukarimu, ungeenda hata huko kumtafuta mwenye pochi yake!
 
Back
Top Bottom