Hivi ni kweli usimkopeshe rafiki yako kama ni wa kike?

Hivi ni kweli usimkopeshe rafiki yako kama ni wa kike?

Infiniteposibilities

Senior Member
Joined
Jan 31, 2018
Posts
141
Reaction score
218
Mwenzenu Mangi nimepigwa na kitu kizito. Yaani siamini. Nimekuwa na kiherehere cha kuwatetea wanawake kwenye karibu kila nyuzi zinazomponda mwanamke lakini hivi karibuni nimepigwa tukio hadi fikra zangu zimeyumba. Naomba wanawake mtanijibu maswali hapo chini lakini wanaume wenzangu mnisaidie pia kujibu.

Ni hivii kuna dada nilikutana nae kwenye shughuli maalumu ya kikazi ambako lilitukutanisha wafanyakazi wachache wa idara moja. Baada ya shughuli ya kikazi kuisha liliundwa group la umoja wa kuendeleza mahusiano baada ya kazi kuisha kwa maana ya shida na raha.

Uhusiano wa kirafiki uliendelea kati ya wanagroup tukichati mara Kwa mara na kuweka mipango ya kusaidiana.
Sasa siku moja huyo dada alinitumia meseji akiniomba nimkopeshe kiasi fulani cha pesa.Aliniahidi kunirudishia baada ya siku kadhaa.Kwa kuwa nilijua ni rafiki na tupo nae group moja sikumbania.Nilipomkubalia na kumuuliza nimtumie kwa njia gani? Alifurahi akaniomba nimuongezee kiasi zaidi ya kile alichoomba. Hapa Mangi nilisita kidogo nikamdanganya kuwa kuna mtu mwingine nilishamuazima ila angewahi kidogo tu njngempatia.

Mapichapicha yakaanza sasa baada ya siku ya kurejesha kufika. Nakumbuka nilichelewa kama siku mbili hivi kumuuliza kuhusu kinirejeshea fedha zangu. Yaani ni kama alijikausha akisikilizia kama nitamshtua au?
Baada ya kumtumia ujumbe akanijibu usjali niko kwenye kikao fulani nitakutumia baada ya kikao kwisha.. Nikamjibu poa. Mara siku ikaisha ikawa usiku ikawa mchana kajikausha. Kesho yake nikampigia hakupokea. Nikamtumia ujumbe akanijibu nitakutumia leo usjali.Nikaona isiwe tabu nikamsikilizia lakini wapi.Nayo ikapita ikawa usiku ikawa mchana.
Hiyo keshokutwa sasa nikawa nampigia hapokei basi nikaamua kumuandikia meseji moja tu kuwa naomba unirudishie hiyo fedha yangu siku yoyote utakayoona inafaa.Kumbuka hapo zimeshapita siku nne tangu ile siku aliyoniahidi.
Baada ya kumtumia hiyo meseji hajawahi kunijibu wala kunitumia fedha yangu.

Hii ni wiki ya pili sasa.Nahisi alifurahi na kusisimka sana baada ya kuona ule ujumbe wa mwisho.Kuwa sasa huyu fala kashanikatia tamaa.

Hivyo ndivyo jinsi nilivyopigwa hadi siamini maana ukimuona huyo dada huwezi mdhania ukimlinganisha na kazi anayofanya.
Sasa naomba niwaulize wanawake lakini pia na wanaume wenzangu maana nakaribia kukosa imani na mwanamke yeyote.
1)Hivi huyu dada atakuwa ni tapeli au ni aina ya wale wanawake wanaofikiri ukimkopa mwanaume ni kama umechukua msaada na hivyo haupaswi kurudisha tena?
2)Je huyu mwanamke ndio Ile aina ya wanawake ambao kwao kurejesha mkopo ni kutarajia mkopeshaji alegee na kumtaka kimahusiano ili rejesho lifanyike kwa njia isiyo rasmi.?
3)Je wanaume tukiwakopesha wanawake hatupaswi kuwadai maana ni haki yao kupewa(kama si kuhongwa) fedha na wanaume?
3)Je, kumdai mwanamke fedha ni kujishusha na kujidharaulisha uanaume wako?
4)Je, ni kweli kuwa mwanamke kukupa hela yake ni ngumu kama ngamia kupita tundu ya sindano lakini mwanamke kuipata hela ya mwanaume ni rahisi kama kumsukuma mlevi.?
Naombeni majibu yenu ili tu nirekebishe mtazamo wangu.

Asanteni.
 
Mwenzenu Mangi nimepigwa na kitu kizito.Yani siamini.Nimekuwa na kiherehere cha kuwatetea wanawake kwenye karibu kila nyuzi zinazomponda mwanamke lakini hivi karibuni nimepigwa tukio hadi fikra zangu zimeyumba.Naomba wanawake mtanijibu maswali hapo chini lakini wanaume wenzangu mnisaidie kujibu.

Ni hivii kuna dada nilikutana nae kweye shughuli maalumu ya kikazi ambalo lilitukutanisha wafanyakazi wachache wa idara moja.Baada ya shughuli ya kikazi kuisha liliundwa group la umoja wa kuendeleza mahusiano baada ya kazi kuisha kwa maana ya shidana raha.
Uhusiano wa kirafiki uliendelea kati ya wanagroup tukichati mara Kwa mara na kuweka mipango ya kusaidiana.
Sasa siku moja huyo dada alinitumia meseji akiniomba nimkopeshe kiasi Fulani cha pesa.Aliniahidi kinirudishia baada ya siku kadhaa.Kwa kuwa nilijua ni rafiki na tupo nae group moja sikumbania.Nilipomkibalia na kumuuliza nimtumie kwa njia gani? Alifurahi akaniomba nimuongezee kiasi zaidi ya kile alichoomba.Hapa Mangi nilisiya kidogo nikamdanganya kuwa kina mtu mwingine nilishamuazima ila angewaahi tu njngempatia.
Mapichapicha yakaanza sasa baada ya siku ya kurejesha kufika.Nakumbuka nilichelewa kama siku mbili hivi kumuuliza kuhusu kinirejeshea fedha zangu.Yani ni kama alijikausha akisikjlizia kama ntamshtua.
Baada ya kumtumia ujumbe akanijibu usjali Niko kwenye kikao fulani ntakutumia.Nikamjibu poa.Mara siku ikaisha ikawa usiku ikawa mchana kajikausha.Kesho yake nikampigia hakupokea.Nikamtumia ujumbe akanijibu nitakutumia leo usjali.Nikaona isiwe tabu nikamsikilizia lakini wapi.Nayo ikapita ikawa usiku ikawa mchana.
Hiyo keshokutwa nikawa nampigia hapokei basi nikaamua kumuandikia meseji moja tu kuwa naomba unirudishie hiyo fedha yangu siku yoyote utakayoona inafaa.Kumbuka hapo zimeshapita siku nne tangu ile siku aliyoniahidi.
Baada ya kumtumia hiyo meseji hajawahi kunijibu wala kunitumia fedha yangu.Hii ni wiki ya pili sasa.Nahisi alifurahi na kusisimka sana Aabaada ya kuona ule ujumbe wa mwisho.Kuwa sasa huyu fala kashanikatia tamaa.

Hivyo ndivyo jinsi nilivyopigwa hadi siamini maana ukimuona huyo dada huwezi na kazi anayofanya huwezi kumdhania.
Sasa naomba niwaulize wanawake lakini pia na wanaume wenzangu maana nakaribia kukosa imani na mwanamke yeyote.
1)Hivi huyu dada atakuwa ni tapeli au ni aina ya wale wanawake wanaofikiri ukimkopa mwanaume ni kama umechukua msaada na hivyo haupaswi kurudisha tena?
2)Je huyu mwanamke ndio Ile aina ya wanawake ambao kwao kurejesha mkopo ni kutarajia mkopeshaji alegee na kumtaka kimahusiano ili rejesho lifanyike kwa njia isiyo rasmi.?
3)Je wanaume tukiwakopesha wanawake hatupaswi kuwadai maana ni haki yao kupewa(kama si kuhongwa) fedha na wanaume?
3)Je, kumdai mwanamke fedha ni kujishusha na kujidharaulisha uanaume wako?
4)Je, ni kweli kuwa mwanamke kukupa hela yake ni ngumu kama ngamia kupita tundu ya sindano lakini mwanamke kuipata hela ya mwanaume ni rahisi kama kumsukuma mlevi.?
Naombeni majibu yenu ili tu nirekebishe mtazamo wangu.Asanteni.
Wanawake wengi akikuomba ela wewe mwanaume ujue anataka akulipe in-kind
 
Nash



Ye hakuniomba.Alinikopa.
iwe alikuomba au aliomba mkopo ndivyo walivyo...
Mimi kuna binti mmoja aliniomba mwaka jana nimkopeshe fedha aongeze kwenye kodi, anafanya huduma za miamala na huwa hata kama sina ela au niko mbali naweza mwambie atume akatuma so sikuona shida kumpatia.
Baada ya hapo akawa na maneno mengi ikabidi nimsamehe tu maana hata huduma ya kunirushia fedha ilikuwa ishaanza kutia mashaka.
 
Mimi nilimkopea mmoja
Shs 15k tu lakini hakunilipa mpaka leo na alikuwa anaingiza pesa kuliko mimi.

Nimejifunza kuishi kutokukopesha kwa mtu yeyote, kama naona kuna umuhimu wa kutoa pesa kwa mtu husika nampatia tu kiasi ambacho hakitaathiri akili yangu.
 
Back
Top Bottom