Hivi ni kweli usimkopeshe rafiki yako kama ni wa kike?

Hivi ni kweli usimkopeshe rafiki yako kama ni wa kike?

Mwenzenu Mangi nimepigwa na kitu kizito. Yaani siamini. Nimekuwa na kiherehere cha kuwatetea wanawake kwenye karibu kila nyuzi zinazomponda mwanamke lakini hivi karibuni nimepigwa tukio hadi fikra zangu zimeyumba. Naomba wanawake mtanijibu maswali hapo chini lakini wanaume wenzangu mnisaidie pia kujibu.

Ni hivii kuna dada nilikutana nae kwenye shughuli maalumu ya kikazi ambako lilitukutanisha wafanyakazi wachache wa idara moja. Baada ya shughuli ya kikazi kuisha liliundwa group la umoja wa kuendeleza mahusiano baada ya kazi kuisha kwa maana ya shida na raha.

Uhusiano wa kirafiki uliendelea kati ya wanagroup tukichati mara Kwa mara na kuweka mipango ya kusaidiana.
Sasa siku moja huyo dada alinitumia meseji akiniomba nimkopeshe kiasi fulani cha pesa.Aliniahidi kunirudishia baada ya siku kadhaa.Kwa kuwa nilijua ni rafiki na tupo nae group moja sikumbania.Nilipomkubalia na kumuuliza nimtumie kwa njia gani? Alifurahi akaniomba nimuongezee kiasi zaidi ya kile alichoomba. Hapa Mangi nilisita kidogo nikamdanganya kuwa kuna mtu mwingine nilishamuazima ila angewahi kidogo tu njngempatia.

Mapichapicha yakaanza sasa baada ya siku ya kurejesha kufika. Nakumbuka nilichelewa kama siku mbili hivi kumuuliza kuhusu kinirejeshea fedha zangu. Yaani ni kama alijikausha akisikilizia kama nitamshtua au?
Baada ya kumtumia ujumbe akanijibu usjali niko kwenye kikao fulani nitakutumia baada ya kikao kwisha.. Nikamjibu poa. Mara siku ikaisha ikawa usiku ikawa mchana kajikausha. Kesho yake nikampigia hakupokea. Nikamtumia ujumbe akanijibu nitakutumia leo usjali.Nikaona isiwe tabu nikamsikilizia lakini wapi.Nayo ikapita ikawa usiku ikawa mchana.
Hiyo keshokutwa sasa nikawa nampigia hapokei basi nikaamua kumuandikia meseji moja tu kuwa naomba unirudishie hiyo fedha yangu siku yoyote utakayoona inafaa.Kumbuka hapo zimeshapita siku nne tangu ile siku aliyoniahidi.
Baada ya kumtumia hiyo meseji hajawahi kunijibu wala kunitumia fedha yangu.

Hii ni wiki ya pili sasa.Nahisi alifurahi na kusisimka sana baada ya kuona ule ujumbe wa mwisho.Kuwa sasa huyu fala kashanikatia tamaa.

Hivyo ndivyo jinsi nilivyopigwa hadi siamini maana ukimuona huyo dada huwezi mdhania ukimlinganisha na kazi anayofanya.
Sasa naomba niwaulize wanawake lakini pia na wanaume wenzangu maana nakaribia kukosa imani na mwanamke yeyote.
1)Hivi huyu dada atakuwa ni tapeli au ni aina ya wale wanawake wanaofikiri ukimkopa mwanaume ni kama umechukua msaada na hivyo haupaswi kurudisha tena?
2)Je huyu mwanamke ndio Ile aina ya wanawake ambao kwao kurejesha mkopo ni kutarajia mkopeshaji alegee na kumtaka kimahusiano ili rejesho lifanyike kwa njia isiyo rasmi.?
3)Je wanaume tukiwakopesha wanawake hatupaswi kuwadai maana ni haki yao kupewa(kama si kuhongwa) fedha na wanaume?
3)Je, kumdai mwanamke fedha ni kujishusha na kujidharaulisha uanaume wako?
4)Je, ni kweli kuwa mwanamke kukupa hela yake ni ngumu kama ngamia kupita tundu ya sindano lakini mwanamke kuipata hela ya mwanaume ni rahisi kama kumsukuma mlevi.?
Naombeni majibu yenu ili tu nirekebishe mtazamo wangu.

Asanteni.
Hana kwa wakati huo ila akipata atairudisha
 
Usikopeshe mtu kama huna uthubutu wa kupoteza kiasi chote ulichokopesha.

Vinginevyo mkopaji aje ni hati za viapo toka mahakama kuu na ziwe na mihuri ya makama ya rufani😂😂😂😂. Vinginevyo aende benk au kausha damu.

Na kama ni lazma sana kukopesha, kopesha mwanaume maana anafaa kukoromea. Ukikopesha mwanamke hatalipa, ukimuwashia moto atajifanya ni mgogoro wa kimapenzi, na jamii itaamini hivyo.

Nitatoa visa vyangu vichache iwe ni funzo kwa wengine.
Karibu.Kama nimekuelewa vile ndio maana nilistop kumfuatilia maana mwisho wake naweza kuzushiwa
 
Ukiona mtu anakwambia umkopeshe pesa na hamna ukaribu naye sana ujue ameshakopa kwa watu wake wa karibu anaofahamiana nao sana kiasi cha kwamba amekuwa hakopesheki anaona atafute watu wapya wa kuwakopa. Bora umuazime pesa ndugu yako wa familia moja, hata asiporudisha kama mlivyokubaliana anaweza kuirudisha kivingine maana hamuachi kushirikiana.

Mtu anaomba umuazime pesa mwambie aache mali kama dhamana inayothaminishika na kiasi cha pesa anachotaka umuazime ili kutengeneza uwajibikaji kwa wote kwamba yeye ana pesa yako na wewe una tv au laptop yake akizingua unapiga bei.
 
Bora wewe ulikopesha mm nilipewa nimfanyie kazi tena bila hata advance, nikaipiga ile kazi nikamaliza na siku ya kumkabidhi nilikodi hadi boda boda kumpelekea. kufika pale akaniambia hela atanipa baada ya siku mbili mbele..

hizo siku mbili ni miez kadha sasa kila nikipiga sim anasema badae kesho, kesho inazaa badae inakuwa kesho tena nimedai mpka nimechoka nimeona tu nimuachie Mungu
Pole muhanga mwenzangu
 
Kisa 1
Miaka mingi kidogo iliyopita, nilikuwa nafanya miamala kwenye Mpesa moja nzurii yenye makochi ya wateja.

Hapo aliajiriwa dada mmoja anayeonekana kuwa mtulivu na msabato wa kweli. Binafsi nimekuwa nikiwaheshimu sana wasabato kutokana na busara na utulivu wao.

Mara nyingi nilikuwa nakaa kwenye kochi nikifanya miamala,na kupiga story kidogo. Siku, miezi ikasogea, tukawa tumezoeana sana.

Long story short siku moja nafika namkuta analia mwekunduuu; baadae ikabainika aliibiwa zaidi ya 1M kwa utapeli. Nikampa pole nikamuacha analia pale.

Nilimuonea huruma ila nilikuwa na uzoefu wa kuponzwa na huruma zangu huko nyuma. So nikasema ngoja nijikaushe niende zangu.

Kesho yake ananipigia, ananiambia hela iliyoibwa, bosi wake anataka alipe yeye. Boss anasema yeye hajali cha nini wala nini, anataka hela yake na yeye ana nusu tu. Hivyo anaomba nimkopeshe kiasi kilichopaki na angenirudishia mshahara wake unaofuata. Nikachomoa ki dizaini.

Baada ya siku chache baadae, ananiambia amepata ajira kwenye shirika flani ila hajalipa hela iliyopotea. Sasa wasiwasi wake ni kuwa akienda kwa mwajiri mpya, mwajiri wa mwanzo atamripoti kuwa kamuibia ndio katorokea huko; so atafukuzwa kazi kabla ya kuanza. Nikaingiwa na huruma nikamkopesha ili anirudishie akifika kwa mwajiri wake mpya

Nikamkopesha, akaanza kazi mpya, nikamsubiria miezi hatimae mwaka halipi. Hadithi tu.

Mwisho , akaniambia hanilipi maana kipato chake kidogo, nikitaka anilipe, nimtafutie kazi inayolipa zaidi ya hiyo anayofanya. Nikachukia , nikamuambia nitamchukulia hatua kali. Akaniambia, siwezi kumfanya chochote yeye yuko na yesu na anajua kipato chake hakitoshi.

Long story short ni zaidi ya miaka 5 sijalipwa, niliacha kuulizia tena deni na namba nikafuta.

Sina nia ya kulipiza kisasi. Ili niishi bila bila hasira niliamua kuli neutralize deni hilo.
 
Wapo wanawake wanaokopesheka hela na kuirudisha kwa muda wa makubaliano

Ila wengi ukimkopesha anataka akulipe " in kind"
 
Mimi nilimkopea mmoja s
Shs 15k tu lakini hakunilipa mpaka leo alikuwa anaingiza pesa kuliko mimi.

Nimefljifunza kuishi kutokukopesha kwa mtu yeyote, kama naona kuna umuhimu wa kutoa pesa kwa mtu husika nampatia tu kiasi ambacho hakitaathiri akili yangu.
Mkuu ata mimi kuna mmoja alinikopa laki na nusu afate mzingo akishauza ata nilipata pesa yangu mpaka sasa hivi hajanilipa na anafanya biashara na mimi sifanyi biashara.
 
Back
Top Bottom