Hivi ni lazima kila raia wa Tanzania awe na kovu la ile sindano ya ndui begani?

Hivi ni lazima kila raia wa Tanzania awe na kovu la ile sindano ya ndui begani?

Hoja yako ni hiyo tu? Duh.....
[emoji124] [emoji124] [emoji124] [emoji124] [emoji124] [emoji124] [emoji124] [emoji124] ngoja nipite tu kwanza!!
 
Hiyo siyo chanjo mkuu ni alama ya mtanzania iliyobuniwa na wakoloni kutofautisha wakoloni Wa Tanzania na Wa mataifa mengine, mfano wakenya hawachomwi begani ila ni katikati ya mkono. Hiyo ilwasaidia wakoloni kutofautisha watz na wakenya
 
Habari za muda huu wadau,

Naleta mapendekezo kwa Serikali ya jamhuri ya muungano wa Tanzania kwamba ni vyema sasa tukatafuta utaratibu mwingine wa kutoa chanjo ya ndui kwa sababu za kiusalama.

Hii chanjo kwa sasa imekuwa kama alama ya mtanzania hii ni sawa na mfugaji kuweka alama yake katika mifugo jambo ambalo ni hatari sana kwa usalama wa taifa letu.

Kila mtanzania ukimkagua kwenye bega la kushoto ana alama hii ni hatari sana.

Ningeshauri Serikali kuja na chanjo ambayo haiachi alama kwenye bega kwa sababu niliyoieleza hapo juu.
Nashukuru endapo Serikali italifanyia kazi wazo langu.

Kwanza sijaona hatari yoyote ya kiusalama hapo, lakini pia Watz wanachanjwa kulia na si kushoto. Pengine wewe si Mtz na unajistukia hahahahah
 
Shyeeeh...!!! basi sawa tumekusikia tutawachora tattoo ya John The Rhino kwenye tako la kushoto.

Hii si imekaa poa au bado unahofu na usalama wa t!go Pesa pia?
 
Usalama UPI unaongea wewe?

Hii ni moja ya chanjo ktk program ya chanjo za kuzuia mgonjwa wanazochanjwa watoto.

Na baadhi huacha alama ktk mwili.

Shida ni nini hapo.
 
Shyeeeh...!!! basi sawa tumekusikia tutawachora tattoo ya John The Rhino kwenye tako la kushoto.

Hii si imekaa poa au bado unahofu na usalama wa t!go Pesa pia?
Ha ha kuwa siriaz bana
 
Chanjo ya ndui( bega la kushoto) mara ya mwisho ilichanjwa mwaka 1979....watanzania waliozaliwa miaka ya kuanzia '80 hawana alama hiyo!bega la kulia ni alama ya chanjo ya kifua kikuu!
Mbona maambukizi ya TB bado yapo pale pale?
 
Inahatarisha usalama kwa sababu kumchoma sindano mtoto mdogo hivyo unamfundisha roho mbaya, ujambazi na wizi.
Ndiyo maana majambazi wengi wana ndui, infact ili ujue kama huyu ni jambazi muombe uone kama ana alama ya ndui au la kisha hatua zingine za kulala chini na kuporwa zifuate.

Pia NDUI ni acronym ya Naomba Dua Uwe Inferior huu ni mpango wa serikali wa kuhakikisha tunadhibitiwa tangu utoto ili tukubaliane na takwa lolote la serikali kutokana na kutiwa uoga.
 
Ktk kumbujumbu zangu, ilishawahi kutokea rabusha kidogo nadhani South km sikosei. Kuna watz walioumia pale walipotafuta wakiwa wamejificha kwenye kundi la watu ili wasirudishwe kwa nguvu home. Ikatumika mbinu ya alama hiyo ya bega la kushoto.

Inaleta picha kuwa km wangekuwa na nia ya kuwafanyia mabaya, ingekuwa rahisi kwa kuponzwa na alama ya ndui.
 
Kama Baadhi Ya Makabila Yanaweka Alama Zao Na Hakuna Madhara Iweje Hii
Mfano Wagogo,Wamaasai,Wamakonde Na Wengine Wengi Wana Alama Zao Hakuna Madhara
 
Back
Top Bottom