Hivi ni nani anawadanganya watanzania kuwa lockdown haifanyi kazi? Hata kama tumeigomea, tuache kupotoshana!

Hivi ni nani anawadanganya watanzania kuwa lockdown haifanyi kazi? Hata kama tumeigomea, tuache kupotoshana!

Ajabu sana, wenye akili zao wamepiga lockdown, wametoa elimu na watu wameelimika na sasa wanaanza kufungua hizo lockdown kwa tahadhari kubwa sana, tunawaona hata kwenye supermarkets zao na maeneo mbalimbali walivyo na nidhamu ya hali ya juu (tunajipa moyo kwamba wanatuiga), upuuzi mtupu, sisi hakuna elimu iliyotolewa hata theluthi kulinganisha na kwao, zaidi tunaambiana tusitishane na huku watu wakiendelea kuteketea na kimdudu kikiendelea kusambaa, usipinge kwa kuwa halijakufika, na ukipinga likaja kukufika uje uunge mkono hoja usikae kimya kwa aibu, Lockdown ilitakiwa sana tu na siyo ya milele bali ya muda tu na elimu itolewe kwa kila njia, wale waliokuwa wakizika usiku wasambaze vipeperushi kutoa elimu namna ya kujikinga tukitoka, watu wangeogopa na wangeishi kwa tahadhari ya hali ya juu na ingesaidia sana kupunguza hofu iliyoko mtaani kwa sasa, kila mtu anamuogopa mwenzie, na wala kusingekuwa na mazishi ya usiku. Shule zimepigwa lockdown hakuna mishahara kwa walimu na wafanyakazi wengine wa shule, kwao tunaona ni sawa lokdaun ila kwenu nyinyi siyo sawa kwa sababu gani? Hakuna nchi hata jirani zetu aliyekufa kwa njaa, sisi tunakula sana ama vipi? Nimeagiza popcorns nyingine.
 
Asiyeamini ktk hili ni ubishi tu lakini ndio njia maridhawa ya kupunguza makali ya virusi popote duniani.
 
We umeshakufa or?
Hii ni brain kama ya anaekuongoza, inaonesha hupendi kabisa kitu kinaitwa strategy setting, crisis management and logistics ambapo namba au data zinahitajika sana kufanya analysis kabla ya kuchukua maamuzi.

Ukiwa na bahati mbaya ya kupata kiongozi asiyekuwa keen kwenye mambo hayo (lack of attentiveness to detail) lazima utapuuza hizo details na badala yake utaopt kwa waganga wa kienyeji maana huko hakuna namba wala matumizi ya akili.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nchi hii haina Uwezo huo wa kuwagawia Raia chakula..... Hilo moja.

Pili.
Huwa kuna baadhi ya Maeneo huwa na njaa na Serikali hupeleka chakula cha msaada, I hope unajua Kile kinachotokea!
Nyie si mnasema Tanzania inalisha majirani wote? Iweje nyie mshindwe kuwalisha raia wenu?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hakuna nchi ambayo haitaabiki na corona Ulaya, lkn waliofanya lockdown hawako vizuri zaidi kuliko waliofanya ndicho nilichomaanisha, na kama una ushahidi kwamba Sweden imeathirika zaidi na corona kuliko nchi nyingine za Ulaya, karibu uweke hapa, ...
German wamefanya Lockdown na ni mfano wa kuigwa.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ukishashiba unadhani kila mtu ni fisadi tajiri kama wewe!?

Kuna tunaobangaiza kutoka nje kila siku kwenda kutafuta huku na kule ili tusife njaa!

Wewe uko bize unaleta mifano ya ulaya! Bongo na ulaya wapi na wapi?

Hizo shule zenu za kata hazikuwafunza majedwali ya kuoanisha vinavyofanana?

Halafu, umezuiwa kujifungia? Kwanini usijifungie? Unataka kusindikizwa na kila mtu una ajenda gani?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Watanzania tuna shida kubwa sana yaani Kiongozi anasema yeye Uchumi kwake ndiyo priority namba moja swala maisha ya watu baadaye halafu kuna mazwazwa yanapiga makofi [emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]
Tulinyimwa shule ili tushangilie kila kitu watakachosema watawala, usitulaumu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Yaani hatua zote zinazotangazwa na Serikali huzisikii au wewe kwako hatua ni lockdown tu?

Hao nchi jirani hawatufungii sisi mipaka bali wanajifungia wao wenyewe, mbona hawakuzuia maloli ya mizigo kuingia kwao kama kweli wako serious? na ninakuhakikishia haitopita majuma mawili hao unaowasifia eti wametufungia mipaka wataifungua

Sent using Jamii Forums mobile app
Zambia zimepita wiki mbili bado wametufungia.

Ni hatua gani zinazotangazwa na serikali, kuendelea na mikusanyiko makanisani, misikitini, sokoni na kuwasifu wasiovaa barakoa.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ndiyo, inawezekana..., hakuna anayelikataa hilo.
Upotoshaji ni hapo mnaposisitiza kuwa maana ya lockdown ni kusitisha shughuli zote. Hii siyo kweli

Na ni mhimu kujua maana ya kuweka 'lockdown' ni nini. Sisi tunakataa tu bila hata ya kuelewa 'lockdown' inakusudia kufanya nini.

Sio swala la kuzuia tu watu wasitoke nje, au wasifanye shughuli zozote wakiwa wanafuata maelekezo yote ya kuzuia maambukizi.

Sisi tunahimiza watu waende makanisani, huku tukifunga shule zote. Hapo huone 'contradiction' yoyote na kuonyesha kwamba tunaamua tu kufanya yanayotupendeza bila hata ya kuweka fikra nyuma yake?
Toa tafsiri sahihi ya lockdown

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Dar ilitakiwa lockdown, pia kuna partial lockdowns ambapo siyo wote wanazuiliwa, inaweza kuwa ni sehemu ama eneo fulani, ama pia watu Fulani kutokana na maambukizi.

Kinachofanyika sasahivi Tanzania ni kwamba hakuna hatua zozote ambazo zinapigiwa kampeni na serikali, zaidi ya kauli ambazo zinasababisha wananchi kuona ni kawaida tu na kuacha kuchukuwa hatua!

Sasa hadi mipaka tufungiwe ndo unasema lockdown ni mbaya?
Yani unavyo shupaa utadhani hauijui Tanzania...in Tanzania lockdown won't work bro and will never work
 
Naona kumekuwepo na hali ya upotoshaji nchini kuwa hatua za lockdown hazina manufaa! Hili naona kama ni upotoshaji ambao unasababishwa na ukweli kwamba viongozi wengi wameingiza siasa kwenye vita dhidi ya corona na matokeo yake ndo haya ya upotoshaji pamoja na mambo mengine.

Mifano iko mingi, lakini kuna mfano nilioamuwa kuutumia kujenga hoja yangu. Mfano huu ni wa gavana wa Ohio kule marekani anayeitwa Mike Dewine! Huyu alichukuwa hatua zote kabla ya Trump! Pamoja na kwamba Trump anaogopeka na viongozi wengi ndani ya republican mfano maseneta na magavana, huwa wana wasiwasi kupingana naye kwasababu ya umaarufu alio nao ndani ya chama cha Tembo ama Republicans!

Sasa huyu alichukuwa hatua za lockdown toka mwanzo kabisa wakati Trump akiwa analeta utani na gonjwa hilo! Matokeo yake, jimbo lake linafanya vizuri sana na yeye amekuwa maarufu siyo tu kule Ohio, bali marekani nzima! Alikuwa na guts za kufanya maamuzi sahihi ya kulinda raia wake kuliko rais wa nchi! Na wananchi wanasema hatua hizo alitakiwa azichukuwe Trump mwenyewe, na pengine mikusanyiko iliyokuwa ikiendelea kwenye majimbo mengine mfano New York, New Orleans na kwingineko ambako michezo iliendelea kama kawaida na mikusanyiko mingine kama makanisani nk, ambapo matokeo yake ndo haya tunayoyaona wanakufa kwa kasi na maambukizi ambayo yalikuwa tayari yametapakaa.

Jimbo lake lina maambukizi machache na vifo vichache sana, na wameshaanza kufungua taratibu taratibu. Pia jimboni kwake alifanya mkakati siyo wa total lockdown, hiyo ni baadhi tu ya sehemu. Wale wanaojitetea kuwa lockdown ni mbaya, wanawaongopea wananchi kwa manufaa yao binafsi, most likely uchaguzi. Ni bora waseme lockdown siyo njia muafaka kwasababu ya mfumo wetu wa uchumi ulivyo na maisha ya wananchi wake, lakini haina maana kuwa partial lockdowns hazifai. Na lockdowns kwenye maeneo korofi. Lakini pia tulipuuza tokea mwanzo na kuanza kusema wapinzani wanataka wananchi wafe na njaa! Hii ni propaganda ambayo matokeo yake si mazuri kwenye jamii inayokabiliana na janga hatari linalochukuwa maisha ya watu kila siku na pengine kila saa duniani.



Bila kupoteza muda, naweka hiki kipande hapo chini chenye kusapoti ninachokisema, pia link kama ukitaka kusoma habari yote na kujiridhisha wewe mwenyewe kuwa nisemayo ni kweli.

Mike Dewine gavana wa Ohio, alipata umaarufu hata kumzidi Trump ambaye naye akaanzisha utaratibu wa kuongea na waandishi kila siku, jambo ambalo Dewine alikuwa akilifanya jimboni kwake kila siku saa nane mchana, na wakati huo wana Ohio wanakuwa kwenye luninga zao wakimsikiliza. Ndiyo wakaanzisha usemi wa “it’s 2’oclock somewhere...wine with mr Dewine”, ambapo wanapata wine wakimsikiliza Dewine. Wala hawa kuwa na habari na Trump!


A Republican, he took early and bold actions to lock down his state, even as the head of his party, President Trump, dismissed the threat of the pandemic.



Ohio’s G.O.P. Governor Splits From Trump, and Rises in Popularity

Kwahiyo ndugu watanzania wenzangu, kabla ya kufanya upotoshaji, jiridhishe kwa kautafiti kidogo tu ili uweze kuwa huru kifikra! Ikifkia mahali unamkabidhi mtu mwingine afikirie kwa niaba yako, ujuwe kuna shida kubwa sana! Kusema lockdown haisaidii, ni sawa pia na kusema “to hell with social distancing”. Huwezi kuwaambia watu wafuate masharti kwa ugonjwa ambao siyo hatari kabisa kwa jinsi unavyochuliwa kutokana na hatua za viongozi wetu.

Siyo sahihi kusema lockdown haisaidii kwasababu zenu za kisiasa! Kwanza ingekuwa ni kwetu, huyo Dewine angekiona cha mtemakuni! Lakini kwasababu ya kiasi cha demokrasia na mfumo wao wa uongozi, Dewine aliweza kuchukuwa maamuzi muhimu kwenye jimbo lake kinyume na rais wa nchi! Na ameonekana kwamba alikuwa sahihi na kiongozi shupavu! Nyota yake inang’ara! Trump hawezi tena kusema kuwa lockdown haisaidii! Na Tanzania siyo sahihi kusema hivyo, semeni tu hamkuchagua lockdowns kwasababu mtakufa njaa.

Mag3 Nguruvi3 JokaKuu Kalamu1 imhotep Detective J

Mkuu hoja apa ni njaa

Serikali haina uwezo wa kuwapa at nusu kibaba cha dona wananchi wake kwa mwez mzima

Na ww unatakiwa utuambia hyo partial lockdown waliwafanyia nn wananchi wao!?


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom