KalamuTena
JF-Expert Member
- Jul 7, 2018
- 13,187
- 17,167
Mkuu, nimeishia hapo kuisoma mada yako.Naona kumekuwepo na hali ya upotoshaji nchini kuwa hatua za lockdown hazina manufaa! Hili naona kama ni upotoshaji ambao unasababishwa na ukweli kwamba viongozi wengi wameingiza siasa kwenye vita dhidi ya corona na matokeo yake ndo haya ya upotoshaji pamoja na mambo mengine.
Kiufupi, "Lockdown" ukisikiliza anavyoielezea Magufuli utajua kwamba, huenda hajui maana yake ni nini, au anatoa maelezo tofauti kabisa na maana halisi ya 'lockdown' na kwa nini inatumika sehemu nyingi duniani.
Lakini moja kwa moja, ukiunganisha mambo mengi anayoyaweka Rais kwenye hotuba zake kuhusu COVID-19, moja kwa moja utajua wazi kwamba yote yanafanywa kipotoshaji maksudi kabisa kwa sababu zake mwenyewe.
Kwa mfano: 'Lockdown' haina maana kwamba watu huko vijijini wasiende mashambani kulima. Hata huko kwingine kuliko na 'lockdown' sehemu ambazo hakuna misongamano ya watu shughuli zinaendelea kama kawaida.
Hakuelewa, au anapotosha maksudi maana na manufaa ya 'lockdown'. Kupotosha maksudi kunaungwa mkono na mambo mengine anayoingiza kwenye hotuba zake.
Halafu anajichanganya sana, tena nadhani maksudi akidhani watu anaohutubia hawaelewi.
Hao watalii waliojaza ndege hadi August wanatoka wapi, na hizo ndege zitakazokuja Tanzania ni za wapi? China labda?
Na bado anaendelea na vita:Anadhani kuna watu mahali fulani wapo wanategeshea kutuambukiza waTanzania kwa maksudi mazima na COVID-19!
Hawa watu tuliwakosea kitu gani?