Hivi ni nini hekima iliyopo nyuma ya ruhusa ya kuoana ndugu?

Tatizo ni kwamba umeaminishwa kuwa damu yakowatu ambao sio damu yako.

Maana yake hujui nini maana ya damu yako.

Usijifanye hekma wala nini, ila ukae ukijua kuwa kuoana kuna kumuoa aliyekaribu kinasaba au kumuoa aliyembali kinasaba.

Sasa katika waliokaribu kinasaba ndio hao, utake ndio hivyo usitake ni hivyo, waite ndugu zako ila unaweza kuwaoa.

Full stop.
 
Lete andiko kutoka kwenye biblia linalo sema ni kosa kumuoa mtoto wa shangazi yako mama ndogo baba mdogo
Yapo mkuu tena sio Moja ngoja nikupe machache...
Walawi 18:6-20 (NIV)

""Msiifanye aibu miili yenu kwa kuifunua kwa njia ya kufanya ngono; kama vile kitendo cha kumwoa dada yako wa kambo, mwanamke wa baba yako,
na kufunua aibu yake. Usifunue aibu ya binti wa mwanao au wa binti wa binti yako, kwa maana huo ni uchafu wako wenyewe.
Usifunue aibu ya binti ya dada yako au ya dada ya baba yako, kwa maana huyo ni jamaa yako wa karibu, ni uchafu wako wenyewe. Usifunue aibu ya binti ya kaka yako, binti ya dada yako, kwa maana huyo ni jamaa yako wa karibu.
Usifunue aibu ya binti ya mke wa baba yako, aliyezaliwa nyumbani mwako au wa binti wa mke wa mwanao, naye ni mwenzake. Usifunue aibu ya binti ya mke wa mwanao au wa mke wa ndugu yako; kwa maana huyo ni jamaa yako wa karibu. Usifunue aibu ya mke wa mwanaume mwenzako kwa kuwa hiyo ni aibu ya mume mwenzako."


pia mkuu unaweza ukasoma na

walawi 20:17-21

"Ikiwa mtu ataoa dada yake, binti wa baba yake au binti wa mama yake, na wao wakafanya tendo la ndoa, hiyo ni aibu. Wataondolewa hadharani kati ya watu wao.
Amemtia aibu dada yake na atachukuliwa kuwa na hatia. Ikiwa mtu ataoa mke na mama yake, ni jambo la uchafu. Watachomwa moto yeye na huyo mwanamke, ili kwamba uchafu wao usionekane kati ya watu wao. Ikiwa mtu ataoa dada ya mkewe, jambo hilo ni uchafu mkubwa;
wao wawili wataondolewa hadharani kati ya watu wao; watapata adhabu ya dhambi zao. Ikiwa mtu ataoa mke na mama na binti zake, jambo hilo ni uovu; wao na wote watakaojiunga nao watachomwa moto, ili kwamba uovu huo usiwe kati yenu."


mkuu hayo ni machache tu yako mengi....
 
Ukweli ni kwamba hata pamoja na dini ya kiislam kuruhusu kuoana binamu,lakini jambo hili hutokea mara chache sana tena kwa dharula,labda mmetiana mimba au mmefumwa mnaibana kinyemera.

Ni jambo ambalo kimaadili halivutii.
 
[emoji706]
 
Yapo mkuu tena sio Moja ngoja nikupe machache...
Walawi 18:6-20 (NIV)

""Msiifanye aibu miili yenu kwa kuifunua kwa njia ya kufanya ngono; kama vile kitendo cha kumwoa dada yako wa kambo, mwanamke wa baba yako,
na kufunua aibu yake. Usifunue aibu ya binti wa mwanao au wa binti wa binti yako, kwa maana huo ni uchafu wako wenyewe.
Usifunue aibu ya binti ya dada yako au ya dada ya baba yako, kwa maana huyo ni jamaa yako wa karibu, ni uchafu wako wenyewe. Usifunue aibu ya binti ya kaka yako, binti ya dada yako, kwa maana huyo ni jamaa yako wa karibu.
Usifunue aibu ya binti ya mke wa baba yako, aliyezaliwa nyumbani mwako au wa binti wa mke wa mwanao, naye ni mwenzake. Usifunue aibu ya binti ya mke wa mwanao au wa mke wa ndugu yako; kwa maana huyo ni jamaa yako wa karibu. Usifunue aibu ya mke wa mwanaume mwenzako kwa kuwa hiyo ni aibu ya mume mwenzako."


pia mkuu unaweza ukasoma na

walawi 20:17-21

Ikiwa mtu ataoa dada yake, binti wa baba yake au binti wa mama yake, na wao wakafanya tendo la ndoa, hiyo ni aibu. Wataondolewa hadharani kati ya watu wao.
Amemtia aibu dada yake na atachukuliwa kuwa na hatia. Ikiwa mtu ataoa mke na mama yake, ni jambo la uchafu. Watachomwa moto yeye na huyo mwanamke, ili kwamba uchafu wao usionekane kati ya watu wao. Ikiwa mtu ataoa dada ya mkewe, jambo hilo ni uchafu mkubwa;
wao wawili wataondolewa hadharani kati ya watu wao; watapata adhabu ya dhambi zao. Ikiwa mtu ataoa mke na mama na binti zake, jambo hilo ni uovu; wao na wote watakaojiunga nao watachomwa moto, ili kwamba uovu huo usiwe kati yenu."


mkuu hayo ni machache tu yako mengi....
 
Walawi 18 imeeleza vyema tu,kuliko hata hiyo Quran yako unayodhani Ina Kila kitu.
 
Hakuna tofauti,wote mnamfata Muhamad
 
Ukweli ni kwamba hata pamoja na dini ya kiislam kuruhusu kuoana binamu,lakini jambo hili hutokea mara chache sana tena kwa dharula,labda mmetiana mimba au mmefumwa mnaibana kinyemera.

Ni jambo ambalo kimaadili halivutii.
Haya ni ma Mila ya wahindi na waarabu eti ni wivu Mali isitoke nje ya familia ndio maana kwenye familia za wahindi na waarabu ndani Wana mazezeta au wenye mtindio wa UBONGO. Sasa sisi wa kuletewa dini tumebeba Kila kitu hata hayo mamila ya hovyo ila kimsingi makabila halisi ya kiafrika hilo halikubaliki.na ni laana
 
Hii laana hii🤓🤓🤓🙌🙌🙌😂😂
 
Hakuna tofauti,wote mnamfata Muhamad
Huyu mtu ingekuwa ameibuka Karne hii angekuwa jela.

❗ Ndoa za watoto wadogo alioa katoto ambalo kwa bongo Ukifanya hivyo ni ubakaji miaka 30 jela

❗ Hizi ndoa za maharimu ( close related blood) nayo ingekuwa jela

❗ Polygamy ( kosa la kutoa wake wengi nayo ni jela)

❗ Kugandamiza haki za wanawake, kuwafunika manguo meusi gubigubi, kuwakataza kushiriki kwenye siasa na maamuzi nayo ilikuwa jela
 
Kulinda amali na tunu za ukoo
Magonjwa
Ngekewa
Bahati
Mali
Ukwasi



Sent using Jamii Forums mobile app
 



Watoto wa Adam walioona ndugu pia , hii imekaaje ?
 
Uchoyo wa wahindi, waarabu na wenyewe asili hiyo kusambaza utajiri nje ya familia.
 
Hivi hamuoni kinyaa, unaingizaje hiyo kitu kwa damu yako mwenyewe?! Hushindwi kubaka mwanao wewe
 
Ni kwanini kuoana ndugu kunakatazwa?
Sababu kubwa ni kwamba kuna magonjwa ya kurithi, kwaiyo mkioana ndugu ni rahisi watoto kuzaliwa na hayo magonjwa kwakua 'gene' za wazazi zinakua zinafanana kwa kiasi kikubwa. Magonjwa kama albinism, sickle cell, pumu n.k. Kwa waliosoma biology (genetics) watanielewa kwenye 'dominant gene' na recessive gene' 'homozygous' na heterozygous'.

Kwaiyo hata wazee wetu hawakua wapumbavu walikua wanalitambua hili. Ndo maana kuna makabila ilikua ikigundulika ndugu mnanyandua adhabu yake ni kifo.

Hii kitu inaaply hata kwa mifugo (kuku,ng'ombe, mbuzi nguruwe n.k), ukitaka mifugo yako uzao wake uendelee vizuri usikubali wapandane ndugu, tafuta dume la mbali kabisa. Bila hivyo vizazi vinavyoendela vinazidi kua dhaifu na vidogo zaidi.
 
Mkuu avogadro sometimes kama Hujui sheria inabidi ukae tu kimya usijiabishe mbele za watu...

Kuhusu Ndoa ya Watoto

Sheria ya Tanzania iliruhusu Mwanaume kumuoa mwanamke mwenye miaka 13 imebadilishwa nafikiri hata miaka 10 haifiki ikaongeza umri mpaka sasa ni miaka 15 Ruksa kuolewa au 14 kwa pendekezo la wazazi...
Soma sheria ya Ndoa 1971 kifungu cha 13(1) na (2)

Na kuhusu polygamy

Nakurudisha kwenye sheria hiyo hiyo ya ndoa sio kosa nenda kasome sheria hiyo kifungu cha 9 (3) na kifungu cha 10,Kinaeleza kuhusu aina za Ndoa Tanzania zimesema ni Monogamous na Polygamous... Na zimeelezea vizur kabisa nini maana zake na zinafungwaje nafikiri Go and read that..

Hata hivyo biblia yako pia iliruhusu ndoa hizo ukitaka ushahidi nitakuleta hapa nakuelimisha kwanza kuhus sheria

Kugandamiza haki za wanawake
Umesema kugandamiza haki na ukasema ikiwemo mojawapo kuwafunika manguo,kuwakataza kushirki katika utawala....
Sasa hapa siendi kwenye sheria ntaenda kwe ye bible yako..

Bible ndo kitabu cha kwanza kumgandamiza mwanamke mwanamke hakuhesabiwa kitu katika biblia..
  • Unafahamu kuwa watoto wa Yakobo wako 13 mmoja ni mwanamke lakini kwakuwa tu ni mwanamke Hakuhesabiwa na unasikia wanakuambia kuna watoto 12 wa yakobo? Na makabila 12 ya israel je hilo kabila lake la huyo mwanamke kwanini halitajwi...kwa sababu biblia imekuwa kandamizi sana kuhusu mwanamke...
  • Hakuna mtume wala nabii wa Kike aliyepewa heshima kwenye biblia..
  • Wanawake walihesabiwa kama wazazi tu na sio watawala wa kiserkali wala kisiasa wala kidini...
Kuhusu kutawala umetoa hasira kabisa kwa waislamu..ngoja bhasi nilete ushaihidi kwamba nyote mko sawa...

Kuhusu kufunika kichwa

1 wakorintho 11:5-6,10,13,16

" Bali kila mwanamke asalipo, au anapohutubu, bila kufunika kichwa, yuaaibisha kichwa chake; kwa maana ni sawasawa na yule aliyenyolewa......


Maana mwanamke asipofunikwa na akatwe nywele. Au ikiwa ni aibu mwanamke kukatwa nywele zake au kunyolewa, na afunikwe.
Kwa hiyo imempasa mwanamke awe na dalili ya kumilikiwa kichwani, kwa ajili ya malaika.Je! Inapendeza mwanamke amwombe Mungu asipofunikwa kichwa?

Lakini mtu ye yote akitaka kuleta fitina, sisi hatuna desturi kama hiyo, wala makanisa ya Mungu."

kuwakataza katika utawala wanawake na kuwanyima priorit na kuwanyamazisha

1 Timotheo 2:11-14

"Mwanamke na ajifunze katika utulivu, akitii kwa kila namna, Simpi mwanamke ruhusa ya kufundisha, wala kumtawala mwanamume, bali awe katika utulivu,
Kwa maana Adamu ndiye aliyeumbwa kwanza, na Hawa baadaye, "Wala Adamu hakudanganywa, ila mwanamke alidanganywa kabisa akaingia katika hali ya kukosa."


Pia unaweza ukapitia hapa

1 wakorintho 14:34-38

"Wanawake na wanyamaze katika kanisa, maana hawana ruhusa kunena bali watii, kama vile inenavyo torati nayo.
Nao wakitaka kujifunza neno lo lote, na wawaulize waume zao wenyewe nyumbani mwao; maana ni aibu wanawake kunena katika kanisa.
Au je! Neno la Mungu lilitoka kwenu? Au kuwafikia ninyi peke yenu?
Mtu akijiona kuwa ni nabii au mtu wa rohoni, na ayatambue hayo ninayowaandikia, ya kwamba ni maagizo ya Bwana.
Lakini mtu akiwa mjinga, na awe mjinga..........


MY TAKE ON THIS
Mkuu dini zote hizi tatu zinafanana kimuuundo so usitukane nyingine ukadhani uko salama zote ziko sawa....

KUHUSU USTAARABU WA WAARABU..

wengi mmetukana sana kuhusu Ustaarabu wa waarabu bila kujali hata Mtume wenu Paulo,Alipopewa utume (kama anavyosema) kabla ya kwenda kukutana na wanafunzi wa Yesu alienda kwanza uarabuni na kupata ustaarabu wa Waarabu...

Soma wagalatia 1:16-18


"Alipoona vema kumdhihirisha Mwanawe ndani yangu, ili niwahubiri Mataifa habari zake; mara sikufanya shauri na watu wenye mwili na damu;
wala sikupanda kwenda Yerusalemu kwa hao waliokuwa mitume kabla yangu;
bali nalikwenda zangu Uarabuni, kisha nikarudi tena Dameski.
Kisha,
baada ya miaka mitatu, nalipanda kwenda Yerusalemu ili nionane na Kefa, nikakaa kwake siku kumi na tano."
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…