Hivi raraa reree hizi likes unazogawaga uzi mzima unatumia BOT au nini?

Hivi raraa reree hizi likes unazogawaga uzi mzima unatumia BOT au nini?

Huyu jamaa,kila ninachocomment humu jf lazima alike.na mbaya zaidi sijawahi kuona amecomment popote wala kuanzisha uzi.
Huyu jamaa ni nani wakuu?
 
Katika huu ulimwengu wa teknolojia, hilo ni swali la kipuuzi sana.

Hakuna mtu anayeweza kufanya kazi hiyo kwa sasa labda awe zumbukuku kwelikweli (anayelipwa na Max ili ajiketishe tu awape motisha za likes wanajukwaa).

Mhusika hasa huwa anakomenti (labda na kulaiki) hapa na pale ili aonekane kuwa mtumiaji halai (active user).

Hata YouTube na soshomedia zingine wanatumia hizo app bots, hata kukomenti na kuwasiliana na wanajukwaa husika.
 
Mtu wa maana sana huyu apewe u-platinum member ila magarasa kama kina mwashambwa yashushwe vyeo na kuwa kama anachokuwa nacho new member
 
raraa reree anamiliki NGO moja pale masaki, na ni mwalimu wa chuo kikuu MUHAS. Kuna kampun moja ya forwarding na clearence iko mnaz mmoja ya kwake. Na ile dul monte pale toangoma ana hisa nayo.

Raraa reree ni mtu makini sana hata mke wake ananijua
Duuh mwanangu raraa reree kumbe mtu mkubwa hivi kwenye hiyo NGO hamuuzi hisa nije kununua nina 2B hapa hazina kazi
 
Huyu mwamba yeye hajui kukoment, yy n mwendo wa like tu
Yawezekana kabisa huyo ni mtu wa Internet Surveillances wa wale jamaa wavaa Kaunda suti. Atakuwa anatumia Spyware for Internet Surveillance, and Social Engineering. Spyware Kama PEGASUS (Teknolojia ya mu-Israel ) itakuwa inafahya kazi yake.
 
Kuwa off wiki ambazo walevi wenzio ndo wamebananika kazini shida sana.

Ngoja nipoteze muda kuongelea hili swala la raraa reree

Huyu ndugu yetu ana kiwanda cha likes, hebu nipe siri na mm niwe natoa likes hvo, au jamaa ni BOT?
Anakuja na hiii ana-like 😂🌝
 
Wakuu,

Ni muda sasa nimekua nikipata likes za bwana raraa reree, kuna faraja Fulani kupata like kwamba umeandika kitu chenye maana lakini raraa reree hu-like comment yoyote hata ya hovyo na zaidi hu-like comment zote kwenye nyuzi zote hili ni gumu kwa kawaida

Isije kuwa raraa reree ni mtu Fulani wa kitengo mwenye software inayomsaidia kupata taarifa zetu kwa ku-like kila comment kwenye kila Uzi maana huko nyuma palikua na madai kwamba mtu akikutumia msg private kule ukijibu basi ana uwezo wa kukufahamu wewe ni nani

Mwisho sijawahi ona comment yake huyu bwana
 
Back
Top Bottom