Sister Abigail
JF-Expert Member
- Sep 2, 2020
- 2,886
- 9,088
- Thread starter
-
- #21
Kama unafanya Biashara inayohitaji mazunguzo Sana tafuta msaidizi wa kuwa nae katika eneo lako la Kazi .
Sawa pole utapata msaadaHaihitaji mazungumzo sana.japo nimeiacha Kwa Sasa napanga kubadili.lakini kwanini kama unajua mtu ana shida usiwe sehemu ya msaada kwake badala uwe kikwazo kwake?
Unajua huyu mtu ana weza kupata tabu kufanya hiki ila mie naweza sogea Kari u saidia kuliko kukaa mbali na kushoot "hawezi huyo"
Then unaendelea na yako.inaleta matokeo gani?
Na sio Kila biashara inamudu kumlipa mtu.wengine ndo tunaanza from scratch
Tunawavimilia but wanaumizaHiyo ndio changamoto, wanasababisha watu wanakua na msongo wa mawazo bila kupenda, sema cha muhimu ni kuangalia namna ya kukabiliana nao tu kwa maana hakuna siku itatokea jamii ikaacha kabisa ubaguzi.
Ndio walimwengu, ni mwendo wa kuvumiliana tu na kuishi kwa kujizingatia wewe kwanza then ndio uanze kuchagua watu wa kuwa nao karibu kwa maana wale ambao wanakuzingatia na wewe unawazingatia wasio kuzingatia unapiga chini.Tunawavimilia but wanaumiza
AsantePole nitakutafuta,na utashangaa
Asante.nimeelewaNdio walimwengu, ni mwendo wa kuvumiliana tu na kuishi kwa kujizingatia wewe kwanza then ndio uanze kuchagua watu wa kuwa nao karibu kwa maana wale ambao wanakuzingatia na wewe unawazingatia wasio kuzingatia unapiga chini.
Kama unasikia kiasi naona sio sawa watu kudakia kwa watu wanaokusemesha ila kama husikii kabisa, mtu akikusemesha mara 2 hadi 3 mtu anaekufahamu anaweza kuitikia kwa niaba yako kwa kusema una tatizo la kutokusikia vizuriSalaam,
Imenibidi niulize Kwa maana Hali Halisi niionavyo na nikiwa kama mhanga mmojawapo inanifkirisha sana. Nasema hivi sababu Kuna baadhi ya watu jinsi wanavyotendea wenye matatizo ya usikivu ni kama kuwafanya vituko. Hugeuza tatizo lao kuwa utambulisho badala ya kumsaidia.unakuta uko eneo lenye mkusanyiko anakufata mtu "choo Kiko wapi"?.. wakati unatarajia kumjibu anakuja au anadakia mtu "haskii vizuri"
Kwa Namna hii inakuwa anamnuong'onyeza yule mwenye tatizo badala ya kumsaidia. Hawa watu wako beneti mda wote attention kuhakikisha hakuna anaekuongeasha.hata salamu. Na hawa ndo wale wakishajua husikii vema basi hata salamu hakupi,anakupita kama sanamu hata ukimsalimia "habari yako" hakujibu. Mwingine unakuta ni Mzee kabisa,unatarajia atakuwa tofauti na labda sababu ya ukomavu kiakili lakini nae eti unamsalimia hajibu.nabaki naduwaa!.
Kuna wakati najiuliza matatizo ya sikio ndio makubwa kuliko yote,mbona mtu haoni vizuri anavaa miwani hafanyiwi hivi? Kuna watu bila miwani hawawezi hata kutembea barabarani,kusoma hawawezi kabisa,why hawapitii masaibu kama wenye usikivu hafifu?
Basi angalau iwe Kwa watu Baki,tunayapitia pia na Kwa tunaowaona wapendwa na ndugu zetu.maumivu yake sio madogo. Achana na ndugu na wapendwa Kuna nyumba ya ibada.nliwahi fanyiwa jambo nkajikuta nachukia kuingia nyumba ya ibada. Kwenye maofisi hasa ya umma Hadi tunaogopa.maana kama wenye masikio Yao tu wanakiona Cha moto vipi wewe mwenye masikio mazito🤣
Lakini pamoja na kukutana nawatu wenye kutibua hisia na maumivu,bado Kuna watu wema hata mie nakutana nao,ni watu waelewa,wako friendly hawajali kabisa ukiwa open unafurahia wanakusahaulisha hata shida zako..Mwenyezi Mungu awatunze sana!
Nb:Abigail ni muhanga wa Hilo tatizo na nilijua nko mwenyewe ama tuko wachache lakini nilivyojiunga kwenye jamii za wenye Hilo tatizo ndipo nkajua tupo wengi sana,asilimia kubwa ni vijana.japo vyanzo vya shida vinafanana na wengine havifanani,katika kushea changamoto wanazopitia nikaobserve mengi mojawapo ni Hilo.
Uzi ufungwe Kwa hii commentNi wewe tu unavyojiweka, kuna sehemu nyingine unakuta mlemavu ndio kila kitu yaani kwenye kitengo/ group/ au sehemu yenye maamuzi fulani kijamii bila yeye hamtoboi.
Jiamini,Jithamini,weka mipaka na hakikikisha watu wanafuata kanuni na taratibu zako iwe kifamilia ,kimapenzi ,kikazi n.k.
Onyesha thamani yako wengine watafuata.
I feel for you, pole sana 😔Asante.nshapita huko kwenye hearing aid.ukweli mchungu zinazidisha tatizo na kuzalisha maumivu ndani ya sikio
Kati ya 100 basi 80 zinawashinda.
Je akifanya hivo nikiwa na maongezi tumefika mbali. Mimi na muulizaji utatafsirije?Kama unasikia kiasi naona sio sawa watu kudakia kwa watu wanaokusemesha ila kama husikii kabisa, mtu akikusemesha mara 2 hadi 3 mtu anaekufahamu anaweza kuitikia kwa niaba yako kwa kusema una tatizo la kutokusikia vizuri
Nilikua nasambaza gesi majumbani nikakutana na visa viwili vya aina hii, sasa kwakuwa mimi ni mtu wa kusalimia kila mtu nikishaingia getini alafu mwenye matani mengi nilijifunza kwamba mtu ambae hasikii vizuri ukimsemesha mara 2 asipoitikia unaona ni dharau kumbe sivyo ndio maana nikasema mtu anaejua tatizo lako akiwepo karibu lazima atamjibu yule anaekusemesha ili kuondoa sintofaham.
Kabisa mkuu. Kama umetokea familia duni ukiwa na changamoto hiyo matesoKukosa kutosikia ni ulemavu na tatizo kubwa Sana .
Hili tatizo ni kumuomba Mungu usilipate maana ukiwa unatoka broke family na haupo vizuri litakukosesha fursa nyingi na Kuonekana haufai.
Nilichogundua mawasoliano yabeba sehemu kubwa ya mafanikio ya MTU .
Samehe tu mkuu na usiwazingatie kama hao wakukupa stress zaidi ignoreNi njia ya kuonyesha natambua uwepo wa mtu na naheshimu.tena tukiwa karibu kama hatua mbili.
Siwasalimii Tena.
Kuna wakati najiuliza hawa wenzangu ukoo wao mzima hawana shida au tatizo?
Kuna mmoja ni mama wa makamo alinitukana masikio kisa sikumuelewa huku yeye analea mjukuu ana autiism kalemaa.
Nlishangaa
Mimi pia. Hata simu sipokei labda SMS ukipiga simu naiangalia weeee mpaka inakata.Hata mimi Nina tatizo la kusikia na nimepitia mengi
Una mtia ngumi kumamamake zakeUnasema kweli kabisa unakuta mtu umemsikia vizuri tuu ilainatokea jitu linaanza HASIKII HUYOOO inatiaga hasira
Je umetumia tiba za Asili sijajua ukubwa wa tatizo lako Ila huwa zipo tibaMimi pia. Hata simu sipokei labda SMS ukipiga simu naiangalia weeee mpaka inakata.
Lakini ukituma SMS ndani ya sekunde nimeshaijibu.
Kuna kazi zingine nakosa sababu ya tatizo hili la usikivu.
Kuna interview kibao nimefanya ila wakijua tu changamoto yangu basi ndio imetoka hiyo hata kama nimejibu vizuri maswali yangu
Nilidhani ni mimi tu...Dah inakele mwanzoni nilikuwa ngumi saiv nawaachia tuSalaam,
Imenibidi niulize Kwa maana Hali Halisi niionavyo na nikiwa kama mhanga mmojawapo inanifkirisha sana. Nasema hivi sababu Kuna baadhi ya watu jinsi wanavyotendea wenye matatizo ya usikivu ni kama kuwafanya vituko. Hugeuza tatizo lao kuwa utambulisho badala ya kumsaidia.unakuta uko eneo lenye mkusanyiko anakufata mtu "choo Kiko wapi"?.. wakati unatarajia kumjibu anakuja au anadakia mtu "haskii vizuri"
Kwa Namna hii inakuwa anamnuong'onyeza yule mwenye tatizo badala ya kumsaidia. Hawa watu wako beneti mda wote attention kuhakikisha hakuna anaekuongeasha.hata salamu. Na hawa ndo wale wakishajua husikii vema basi hata salamu hakupi,anakupita kama sanamu hata ukimsalimia "habari yako" hakujibu. Mwingine unakuta ni Mzee kabisa,unatarajia atakuwa tofauti na labda sababu ya ukomavu kiakili lakini nae eti unamsalimia hajibu.nabaki naduwaa!.
Kuna wakati najiuliza matatizo ya sikio ndio makubwa kuliko yote,mbona mtu haoni vizuri anavaa miwani hafanyiwi hivi? Kuna watu bila miwani hawawezi hata kutembea barabarani,kusoma hawawezi kabisa,why hawapitii masaibu kama wenye usikivu hafifu?
Basi angalau iwe Kwa watu Baki,tunayapitia pia na Kwa tunaowaona wapendwa na ndugu zetu.maumivu yake sio madogo. Achana na ndugu na wapendwa Kuna nyumba ya ibada.nliwahi fanyiwa jambo nkajikuta nachukia kuingia nyumba ya ibada. Kwenye maofisi hasa ya umma Hadi tunaogopa.maana kama wenye masikio Yao tu wanakiona Cha moto vipi wewe mwenye masikio mazito🤣
Lakini pamoja na kukutana nawatu wenye kutibua hisia na maumivu,bado Kuna watu wema hata mie nakutana nao,ni watu waelewa,wako friendly hawajali kabisa ukiwa open unafurahia wanakusahaulisha hata shida zako..Mwenyezi Mungu awatunze sana!
Nb:Abigail ni muhanga wa Hilo tatizo na nilijua nko mwenyewe ama tuko wachache lakini nilivyojiunga kwenye jamii za wenye Hilo tatizo ndipo nkajua tupo wengi sana,asilimia kubwa ni vijana.japo vyanzo vya shida vinafanana na wengine havifanani,katika kushea changamoto wanazopitia nikaobserve mengi mojawapo ni Hilo.
Nimeenda sana CCRBT wanasema mishipa imekauka. Kuongea na mtu mpaka nimtazame usoniJe umetumia tiba za Asili sijajua ukubwa wa tatizo lako Ila huwa zipo tiba