Hivi tatizo la kutosikia vizuri ni tatizo kubwa zaidi duniani?

Hivi tatizo la kutosikia vizuri ni tatizo kubwa zaidi duniani?

Kuweza kuishinda hiyo hali inabidi kwanza uifunze nafsi yako kupokea watu kama walivyo. Usiwe mtu wa kuonesha kuchukizwa kwa namna unavyotendewa, maana unapoonesha negative reaction wao ndiyo huwa unawaburudisha zaidi. Kuwa mtu wa kutulia, usikunje sura, always be neutral pale unapotendewa vibaya, mwisho utamfanya akutendaye aanze kujiona kuwa alifanyalo anakosea.

Hii situation nilikutana nayo kwa mara ya kwanza nikiwa advanced level. Licha ya namna nikivyotendewa na baadhi ya wanafunzi ila sikuwahi kukorofishana na yeyote maana sikuwa naonesha kuwazingatia juu ya matendo yao.
 
Salaam,

Imenibidi niulize Kwa maana Hali Halisi niionavyo na nikiwa kama mhanga mmojawapo inanifkirisha sana. Nasema hivi sababu Kuna baadhi ya watu jinsi wanavyotendea wenye matatizo ya usikivu ni kama kuwafanya vituko. Hugeuza tatizo lao kuwa utambulisho badala ya kumsaidia.unakuta uko eneo lenye mkusanyiko anakufata mtu "choo Kiko wapi"?.. wakati unatarajia kumjibu anakuja au anadakia mtu "haskii vizuri"

Kwa Namna hii inakuwa anamnuong'onyeza yule mwenye tatizo badala ya kumsaidia. Hawa watu wako beneti mda wote attention kuhakikisha hakuna anaekuongeasha.hata salamu. Na hawa ndo wale wakishajua husikii vema basi hata salamu hakupi,anakupita kama sanamu hata ukimsalimia "habari yako" hakujibu. Mwingine unakuta ni Mzee kabisa,unatarajia atakuwa tofauti na labda sababu ya ukomavu kiakili lakini nae eti unamsalimia hajibu.nabaki naduwaa!.

Kuna wakati najiuliza matatizo ya sikio ndio makubwa kuliko yote,mbona mtu haoni vizuri anavaa miwani hafanyiwi hivi? Kuna watu bila miwani hawawezi hata kutembea barabarani,kusoma hawawezi kabisa,why hawapitii masaibu kama wenye usikivu hafifu?

Basi angalau iwe Kwa watu Baki,tunayapitia pia na Kwa tunaowaona wapendwa na ndugu zetu.maumivu yake sio madogo. Achana na ndugu na wapendwa Kuna nyumba ya ibada.nliwahi fanyiwa jambo nkajikuta nachukia kuingia nyumba ya ibada. Kwenye maofisi hasa ya umma Hadi tunaogopa.maana kama wenye masikio Yao tu wanakiona Cha moto vipi wewe mwenye masikio mazito🤣

Lakini pamoja na kukutana nawatu wenye kutibua hisia na maumivu,bado Kuna watu wema hata mie nakutana nao,ni watu waelewa,wako friendly hawajali kabisa ukiwa open unafurahia wanakusahaulisha hata shida zako..Mwenyezi Mungu awatunze sana!

Nb:Abigail ni muhanga wa Hilo tatizo na nilijua nko mwenyewe ama tuko wachache lakini nilivyojiunga kwenye jamii za wenye Hilo tatizo ndipo nkajua tupo wengi sana,asilimia kubwa ni vijana.japo vyanzo vya shida vinafanana na wengine havifanani,katika kushea changamoto wanazopitia nikaobserve mengi mojawapo ni Hilo.
Yes tatizo ni kubwa sana,nashangaa sioni serikali ikilipa kipaumbele walau kutoa misaada.Niliwahi kuhudhuria huduma moja inayotolewa na wafadhili kutoka Marekani STAR KEY ya vifaa vya kuongeza usikivu-hearing aids,watu walikuwepo pale ni zaidi ya elf 3,na walianza kufika pale kuanzia saa 11 alfajiri,mtu mmoja aliniambia Mwanza watu walijaza uwanja wa mpira,sasa kwa hali hii inaonyesha kuwa hali ni mbaya sana na tatizo ni kubwa...
 
Nilikuwa nakutafuta
Ukweli ni kwamba wanaosema hivi na hivi pale usiposikia wapuuze tu..

Mimi naamini katika kuhustle licha ya kuwa kiziwi wanaosikia wananisarenda hasa wanapoleta dharau ..
Pambana ujisimamie kiuchumi,kijamii na kihisia. Ukiwa bize na wasemacho watu juu yako nakuapia hutoboi na unaweza kukumbwa na Sonoma kisha ukaanza kujifungia ndani.

Never give up..
Mwarain wa Mwanza si ndiyo?
 
Kuweza kuishinda hiyo hali inabidi kwanza uifunze nafsi yako kupokea watu kama walivyo. Usiwe mtu wa kuonesha kuchukizwa kwa namna unavyotendewa, maana unapoonesha negative reaction wao ndiyo huwa unawaburudisha zaidi. Kuwa mtu wa kutulia, usikunje sura, always be neutral pale unapotendewa vibaya, mwisho utamfanya akutendaye aanze kujiona kuwa alifanyalo anakosea.

Hii situation nilikutana nayo kwa mara ya kwanza nikiwa advanced level. Licha ya namna nikivyotendewa na baadhi ya wanafunzi ila sikuwahi kukorofishana na yeyote maana sikuwa naonesha kuwazingatia juu ya matendo yao.
Najitahidi
 
Hakuna.labda madawa ya mizizi unywe unaambiwa sijui yanaenda kuamsha mishipa ya fahamu inayodili na usikivu
Mimi sijawahi
Dawa za asili zipo usiwe mbishi Kwa kila kitu Mimi mzee wangu alikuwa hasikii .

Ila kuna Dawa alitumia akapona .

Nipo Bukoba Ila nikifika DSM Kwa mzee nitamuuliza hiyo Dawa.

Dawa zipo na zinatibu
 
Nb:Abigail ni muhanga wa Hilo tatizo na nilijua nko mwenyewe ama tuko wachache lakini nilivyojiunga kwenye jamii za wenye Hilo tatizo ndipo nkajua tupo wengi sana,asilimia kubwa ni vijana.japo vyanzo vya shida vinafanana na wengine havifanani,katika kushea changamoto wanazopitia nikaobserve mengi mojawapo ni Hilo.
Nimekaa na kuishi na mtu asiesikia vizuri nakuelewa sana jinsi gani unajisikia
 
Imenisaidia sana hii,mtu akinisemesha na sikumsikia vizuri huwa namwambia ongeza sauti masikio yangu hayasikii vizuri,akimumunya maneno namwabia tena ongeza sauti mimi nina shida ya masikio,huwa ninaongea kwa ujasiri,kwahiyo hainiumizi sana ingawa mwanzoni nilikuwa naona aibu na kujitenga na watu ili nisijulikane hali yangu...
 
Yes tatizo ni kubwa sana,nashangaa sioni serikali ikilipa kipaumbele walau kutoa misaada.Niliwahi kuhudhuria huduma moja inayotolewa na wafadhili kutoka Marekani STAR KEY ya vifaa vya kuongeza usikivu-hearing aids,watu walikuwepo pale ni zaidi ya elf 3,na walianza kufika pale kuanzia saa 11 alfajiri,mtu mmoja aliniambia Mwanza watu walijaza uwanja wa mpira,sasa kwa hali hii inaonyesha kuwa hali ni mbaya sana na tatizo ni kubwa...
Sema tatizo lipo Kwa wengi sana
Sio kubwa sana.
Ni kweli.leo ukisema serikali iwape nauli wote Kila Kona wafike pale uwanja wa mkapa patafurika
 
Wengine vichwa vibovu
Matokeo ukimwambia aongeze sauti anakufokea.
Imenisaidia sana hii,mtu akinisemesha na sikumsikia vizuri huwa namwambia ongeza sauti masikio yangu hayasikii vizuri,akimumunya maneno namwabia tena ongeza sauti mimi nina shida ya masikio,huwa ninaongea kwa ujasiri,kwahiyo hainiumizi sana ingawa mwanzoni nilikuwa naona aibu na kujitenga na watu ili nisijulikane hali yangu...
 
Back
Top Bottom