Hivi TCRA wanaweza kutupa sababu za msingi kwa nini bei ya internet Tanzania ni zaidi ya mara kumi ya bei ya internet Rwanda?

Hivi TCRA wanaweza kutupa sababu za msingi kwa nini bei ya internet Tanzania ni zaidi ya mara kumi ya bei ya internet Rwanda?

Kwahiyo mkuu umeamini kabisa 1GB kwa Tanzania ni wastani wa Tsh. 11,500/-?
Nadhani Mkuu Rushanju amekujibu vizuri na umakini sana. Nunua airtime ya kama Tshs 20,000 bila kuingia kwenye kifurushi cha data halafu download mziki mmoja tu ndio utajua uhalisi wa bei ya 1GB hapa Tanzania

Ukitaka kujua kuwa bei ya data ni kubwa, weka salio bila kujiunga halafu endelea ndo utajua thamani halisi ya kifurusi. Hicho ndo kimefanyiwa tafiti. Haya mambo ya kujiunga ni uhuni tu
 
Nadhani ungeweka wazi hiyo 1GB kwa 11,500 ina maanisha nini hasa.
Mimi kwa matumizi yangu shilingi mia tano tu napata wastani wa MB 500 - 1GB kupitia Halotel.
Nikiwa na 10,000 napata GBs za kumwaga za kutumia zaidi ya siku 30.
Hebu tusaidie hizo MB 500 mpka 1 GB unapataje?
 
Nadhani kuna kitongoji huko Rwanda kinaitwa TZ ndio mtandao bei hiyo
Kwa nini usifanye majaribio; nunua airtime ya kama Tshs 20,000 bila kuingia kwenye kifurushi cha data halafu download mziki mmoja tu ndio utajua uhalisi wa bei ya 1GB ndio utajua kama unaishi Tanzania au kitongoji huko Rwanda kinaitwa Tanzania
 
Jama jama wastani gb 1 ni 11000/= ivi kuna tz nyingine au ni hii moja
Ubishi wa nini? Nunua airtime ya kama Tshs 30,000 bila kuingia kwenye vifurushi halafu fanya mambo yanayotumia data, wala usiguse simu ya kuongea, kisha rudi hapa uposti tena
 
Kwani mkuu GB 1 wewe huwa unainunua kwa shilingi elfu 11500 au hujui tafiti zimefanyiwa ulaya
Kwahiyo mkuu umeamini kabisa 1GB kwa Tanzania ni wastani wa Tsh. 11,500/-?
Jama jama wastani gb 1 ni 11000/= ivi kuna tz nyingine au ni hii moja
Hamuwezi elewa kilichowekwa hapo mpaka uwe umesoma shule za kweli, sio shule za kata, au uwe ulisoma hesabu vema.

Kilichowekwa hapo ni halisi kabisa.
Sababu,
1. Huo ni wastani (sasa namna yakutafuta wastani kajitafutie mwenyewe.

2. Hizi unazozozipata 1GB kwa 2500, mara mb 500 tsh 700/- ni OFA

Narudia ni tena OFA ndio maana hazidumu, kila siku vifurushi vipya, wiki moja kinakuja kipya.

Ebu tuambieni mnanunuaje internet data zenu kama sio kwenye OFA MAALUMU na YA KWAKO TU. Mara YATOSHA, ikifika mwezi mpya kinapotea. Na ndio maana hizi Ofa zinatifauti kutoka mtu mmoja kwenda mwingine lakini wote wateja wa kampuni moja.

3. Nawapa zoezi nenda moja kwa moja kanunue internet bila kuingia kwenye vifurushi maalumu vya ofa uone bei halisi.

Utakuta 300mb kwa tsh 2000/= masaa 24.

Unabisha?angalia chini hapa
Screenshot_20191211-111113_Phone~2.jpeg
Screenshot_20191211-110956_Phone~2.jpeg


Sasa angalia hapa 70mb tsh 500, 250 mb tsh 1000, kwa saa 24.

Isikuchanganye hiyo tsh 2000 1GB ndani ya hizo mb 700 ni za Facebook na Whatsapp. 300+ zilizobaki ndio zipo huru tena limited within time.

Utafiti hupingwa kwa utafiti. Ni akili ndogo tu ndio huwa zinabishia Mambo makubwa
 
Kuna mambo kadhaa lazima uzingatie. Unaweza ukaweka 1GB na kuwa unatumia kwa ajili ya WhatsApp message tu, inaweza kukaa zaidi ya siku 30. Sasa lazima uangalie bei kwa namna inayotoa ulinganifu, kwa mfani, IGB ita download data kiasi gani kwa nchi mbalimbali, sasa hiyo ndio itakupa ulinganifu wa bei. Utakuta kwa Rwanda labda, 1 GB uta download kitabu kizima chenye chapter 10, wakati Tanzania uta download chapta moja tu ya kitabu hicho.

Halafu, ukitaka kujua uhalisi wa bei, nunua airtime ya kama Tshs 20,000 bila kuingia kwenye kifurushi cha data halafu download mziki mmoja tu ndio utajua uhalisi wa bei ya 1GB hapa Tanzania
Huo mfano uliotoa sio mzuri tafuta mwingine. Halafu umeanzisha mada iko kushoto sawa sawa na kusema mchana ni usiku na usiku ndio mchana Ha ha. Yaani kama ni promo ya RW basi huenda kuna cheo mnatafuta huko RW kwa Pk kwa promo za ajabu. Jitahidi huenda ukapata u DC wa Gisenyi

Hakuna Tanzania bei ya bando hiyo.mfano kampuni zote kuna night packs ambapo i.e halotel
Unapata GB 10 kwa 1,500/= Tshs tu. Nadhani TTCL ni 1000/ ths kwa 10 gb. Hii ni kila siku Night packz.

Kawaida.

I.e. Halotel 10,000/= unapata GB 10. Hiyo ndio hali halisi uliweka vocha leo.

Haijalishi source ya data umeipata wapi hali halisi sio sahihi na data zako.
Sasa wewe ng'angania hapo hapo hatuwezi kukulazimisha. Ila unawadanganya wa Rwanda wenzako.
 
Achana na ofa za usiku bana, utafiti unazungumzia mtu anapo nunua internet kwa matumizi ya kazi sio mb zenu za kukesha usiku kuangalia umbea instagram.

Fikiria mtu mwenye kampuni anaenunua internent kwa matumizi ya ofisi. Unadhani huwa anajiunga night pack? Mbona elimu Tanzania imekuwa ndogo sana?

Watu wanaonunua internent kwa matumizi halisi na ya kazi, wananunua kwa GB na hizo ndizo hutafutiwa Wastani. Nimeeleza juu kutafuta wastani rudi shule sio kazi yangu.

Pili rejea post ya juu kabla ya hii nimeeleza pia kitu kitakusaidia

wakurochi
 
Kwa nini usifanye majaribio; nunua airtime ya kama Tshs 20,000 bila kuingia kwenye kifurushi cha data halafu download mziki mmoja tu ndio utajua uhalisi wa bei ya 1GB ndio utajua kama unaishi Tanzania au kitongoji huko Rwanda kinaitwa Tanzania
Hiyo data yako ni ya 2018.

Unacho suggest hakina maana sababu halotel wana package ya

Internet only
Internet +calls+sms+social media
Youtube only
Calls only
N.k

Wame programm hivyo sasa wewe unasema mtu asijiunge, hapo juu ataingia mfumo gani. Mbona unaanzisha mawazo ya kufirika yasioeleweka.

Hao kwenye source mbona hawajasema usijunge wewe umeipata wapi mjomba ?

Ndio maana kuna package kutokana na taste na biashara na mipango.
 
Na jamaa wameng'ang'ania mifano ya tubifurushi vyao twa elfu 1 kuingia insta kuchambana na dada zao. Wana sahau utafiti una base sana kwenye matumizi ya watu wanaotumia internet for significance, kwa mfano ofisi, kampuni, viwandani, na uendeshaji wa kila siku.
Hao ni voda mzee baba, tafiti zao zipo sawa. Hizo bundle wanazo nunua chini hapo huwa ni promo na huwa haziduku

View attachment 1288466
 
changanya na akili zako kabla ya kudadavua mambo, bei ya GB 1 kwa tz haizidi tsh 3000 on average nkimaanisha mitandao tafaut tafaut, mfano airtel gb moja ni 1000 voda gb 1 ni 2000:

kenya gb 1 ni 500ksh ambayo ni kama 12,000tsh:
tatizo linakujaga pale taarifa zinatoka nchi za mbele na watu wa uku bila uelewa mnaichukua kama ilivo: taarifa rasmi hua znatoka serikalini sio kwenye muungano wowote wa nchi za nje
 
Na jamaa wameng'ang'ania mifano ya tubifurushi vyao twa elfu 1 kuingia insta kuchambana na dada zao. Wana sahau utafiti una base sana kwenye matumizi ya watu wanaotumia internet for significance, kwa mfano ofisi, kampuni, viwandani, na uendeshaji wa kila siku.

matumizi ya ofisini ni more cheap than mtu mmoja mmoja
 
Mkuu, tunapoongelea bei ya data usikaze fikra kwenye vifurushi vya makampuni ya simu. Sana sana angalia labda subscription rates za data kwa mwezi

haiwezekani kwa sababu watu hawanunui hio GB 1 kwa hio bei tajwa hapo, research inaongelea kama hujaweka bundle inamaanisha gb moja itaisha kwa hio bei lakini watu hawafanyi hivo, sidhan kama kuna mtu anatumiaga akiweka tu salio bila kuunga discount ya vifurushi

ni sawa sawa leo ulalamike gharama ya kupanda kiazi kimoja mpaka kikue ni kubwa wakati watu wanalima viazi vingi kwa pamoja
 
Na jamaa wameng'ang'ania mifano ya tubifurushi vyao twa elfu 1 kuingia insta kuchambana na dada zao. Wana sahau utafiti una base sana kwenye matumizi ya watu wanaotumia internet for significance, kwa mfano ofisi, kampuni, viwandani, na uendeshaji wa kila siku.
Vifurushi vimetuharibu akili. Tumesahau bila hivi vifurushi huduma za simu bei sana.

Mtu anakazana buku unapata 1gb anasahau masharti ya kutumia hiyo gb.

Anayebisha utafiti aje na bei za Data kwenye mitandao bila masharti aone kama haifiki hiyo 11,000.
 
haiwezekani kwa sababu watu hawanunui hio GB 1 kwa hio bei tajwa hapo, research inaongelea kama hujaweka bundle inamaanisha gb moja itaisha kwa hio bei lakini watu hawafanyi hivo, sidhan kama kuna mtu anatumiaga akiweka tu salio bila kuunga discount ya vifurushi

ni sawa sawa leo ulalamike gharama ya kupanda kiazi kimoja mpaka kikue ni kubwa wakati watu wanalima viazi vingi kwa pamoja
Mkuu kuna ofisi /kampuni wana huduma za After paid. Hizi hazina kujiunga na vifurushi. Au kuna nyingine ukipewa muda wa salio huwezi kujiunga.

Umefikiria kila anayetumia data LAZIMA ajiunge na vifurushi.
 
Mkuu kuna ofisi /kampuni wana huduma za After paid. Hizi hazina kujiunga na vifurushi. Au kuna nyingine ukipewa muda wa salio huwezi kujiunga.

Umefikiria kila anayetumia data LAZIMA ajiunge na vifurushi.

ambao hawajiungi vifurushi ni makampuni tu: end users hakuna ambae hajiungi vifurushi, ni sawa sawa ukute nguo inauzwa 100,000 alafu kuna discount ya 70,000 wewe hutaki discount unataka kununua kwa 100,000: hicho ndo mnachotaka kuaminisha watu, and afterall these days hakuna makampuni yanaonunua data kwa limits kama zaman kabla ya vifurushi , mfano airtel hawawezi nunua 1000GB kwa mwezi kutoka ttcl kwa sababu huezi jua watumiaji wako watanunua kiasi gan: mnachowaaminisha watu ni total madness:

the only limitation iliobaki ni spidi tu vingine vote vipo very normal kiasi kwamba mbna kuna mitandao usiku wanatoa internet very very cheap hata kushinda hizo bei tajwa: nakumbuka kuna kipindi nlikuaga mteja wa halotel zaman internet ilikua free of charge usiku for all google products including youtube: hakuna nchi ukanda wetu wana cheap internet kushiinda sisi
 
changanya na akili zako kabla ya kudadavua mambo, bei ya GB 1 kwa tz haizidi tsh 3000 on average nkimaanisha mitandao tafaut tafaut, mfano airtel gb moja ni 1000 voda gb 1 ni 2000:

kenya gb 1 ni 500ksh ambayo ni kama 12,000tsh:
tatizo linakujaga pale taarifa zinatoka nchi za mbele na watu wa uku bila uelewa mnaichukua kama ilivo: taarifa rasmi hua znatoka serikalini sio kwenye muungano wowote wa nchi za nje

'500ksh=12,000tsh'

Hesabu ni janga la kitaifa.
 
Back
Top Bottom