Hivi TRA watakubali ku register kampuni ikiwa ofisi nataka ziwe nyumbani?

Hivi TRA watakubali ku register kampuni ikiwa ofisi nataka ziwe nyumbani?

Kwa kuwa ni ya kupanga utawalipa kodi ya zuio TRA. Maana hapo ni kama umepanga ofisi tu. Unajua kinachotakiwa ni biashara iwe na anuani inayotambulika. Haya mengine ni ziada tu.
Hapo nimekuelewa mkuu
 
Nimesoma posts zako kuna kitu hapa unachanganya, formula ya T.R.A ya kukukadiria wakuweke kundi gani la kodi kwa mwaka, wanaangalia mtaji wako halisi kutegemea na biashara unayotaka kufanya, unawaambia unategemea kupata faida kiasi gani Kwa siku,mwezi,mwaka halafu ndo annual income yako ambayo ni net profit baada ya kutoa matumizi yote ikiwemo kodi ya nyumba,chumba/frame unayotegemea kufanyia biashara ndo inawaambia wewe upo kundi gani la kodi. Ndo maana kwenye formula yao wamelazimisha mtu aweke kodi ya nyumba/chumba Cha biashara.

Hata kama ni nyumba yako unaandika mkataba wa kupanga wenye thamani na nyumba/chumba kama hicho maeneo hayo.(Ni Kwa faida yako), kwasababu kwa mfano faida yako baada ya kutoa vitu vyote (kasoro kodi ya nyumba)kwa mwaka ni milioni 5. Ungepigiwa hesabu za watu wanaopata faida ya milioni 5 Kwa mwaka, ila kama ungejumlishiwa kodi ya nyumba tuseme laki 1 na nusu Kwa mwezi, sawa na milioni 1 na laki 8 Kwa mwaka, ingetolewa kwenye Ile milioni 5 na kubaki milioni 3 laki 2. Kwahiyo ungepigiwa hesabu za watu wanaopata faida ya milioni 3 laki 2. Ndo maana wanalazimisha ulete mkataba wa kupanga nyumba/chumba ni kwa faida yako.

Tatizo T.R.A hawatoi ufafanuzi wa kutosha kuelewesha watu vizuri. Mtu anahisi kueleza haupangi ofisi ni nyumba yako ni dili kumbe anajipunguzia matumizi faida ionekane kubwa na kodi iongezeke pia, kwa wazoefu hata kama nyumba ni yake anaiandikia mkataba Ili iwe sehemu ya matumizi kodi ipungue. Soma kwa makini maelezo yangu utaelewa. Usipoelewa tafuta mfanyabiashara wa kati mwenye uzoefu wa kukwepa kodi akueleweshe.
Kodi ya pango (Withholding Tax) ambayo ndio chanzo cha mjadala mlipaji halisi ni mmiliki wa jengo(Mpangishaji) kwakua naye anafanya biashara ya kupangisha hivyo sheria inamtaka naye kulipa kodi ila kinachotokea ni kwamba mara nyingi mmiliki wa jengo ni ngumu kupatikana wakati wa makadirio hivyo basi hii kodi huingia kwa mpangaji ambapo mpangaji hulazimika kukata malipo haya kwa mwenye nyumba wakati analipa pango kwa mwenye nyumba kitu ambacho mara nyingi huwa sio rahisi na kupelekea mpangaji kuubeba mzigo wa kuilipa kodi hii kwasababu ukigoma kumlipia mwenye nyumba mwisho wa siku hata iyo fremu ya biashara unaiweza kuikosa.

Pia kama wewe ndio mmiliki wa jengo unalofanyia biashara sheria haikulazimishi kulipa kodi ya zuio unachotakiwa kufanya ni kuonesha kuwa wewe ni mmiliki halisi, mfano hati ya nyumba au bills za umeme au maji, afisa akijilizisha kuwa wewe ni mmiliki halisi hautailipa hii kodi. Kwa suala lako kwa kua wewe unamiliki unataka kumiliki kampuni ili usilipe hii kodi ni kwamba ilo jengo linatakiwa limilikiwe na kampuni tofauti na hapo italazimu mmiliki alipe japo huwa ngumu kwa wenye majengo kukubali kama nilivyo eleza hapo juu hivo mzigo utakurudia tena muu.

Maelezo ya ziada, kiufupi ni kwamba walipa kodi tunaweza kuwagawanya katika makundi matatu.

Walipa kodi wadogo, Walipa kodi wakati na Walipa kodi wakubwa

Idara ya kodi za ndani huudumia walipa kodi wa kati na wadogo, kwa leo nitazungumzia walipa kodi wadogo, na sifa kubwa ya walipa kodi wadogo ni wale ambao wastani wa mauzo yao kwa mwaka hayazidi 100M. katika kundi hili sheria haikulazimu kutunza kumbukumbu (mauzo na manunuzi ya matumizi ya biashara ila pia haukatazwi kutunza.

Sasa ambacho hufanyika unavyoenda kwa afisa wa kodi kwaajili ya makadirio afisa hukufanyia mahojiano ili kutambua kundi lipi unastahili kulingana na biashara yako(wastani wa mauzo kwa siku) makundi ya kodi kwa wafanyabiashara wadogo yamegawanyika kama ifuatavyo

Viwango vya kodi wafanyabiashara wadogo wakazi Mauzo kwa mwaka Uzingatiaji wa kifungu cha 35 cha Sheria ya Usimamizi wa Kodi (Utunzaji wa kumbukumbu)

Asiyetunza KumbukumbuAnayetunza Kumbukumbu


Mauzo yasiyozidi sh. 4,000,000/=Halipi kodiHalipi kodi
Mauzo yanayozidi sh. 4,000,000/= na hayazidi sh. 7,000,000/=Sh.100,000/=3% ya mauzo yanayozidi sh. 4,000,000/
Mauzo yanayozidi Sh. 7,000,000/= na hayazidi sh.11,000,0000/Sh. 250,000/=Sh. 90,000/= +3% ya mauzo yanayozidi Sh. 7,000,000/=
Mauzo yanayozidi 11,000,000 na hayaidi 100,000,000/=

Huyu analazimika kuwa na mashine ya kutolea risiti(EFD0 hivo hapa hausiki sharia inamlizimu kutunza kumbukumbu.Asilimia 3.5 ya Mauzo
Intern mstaafu
 
Back
Top Bottom