Hivi tungekodi kampuni ya Uingereza kuchunguza makinikia tungejua tulichojua?

Unapoteza nguvu na wakati bure. Aliyetuaminisha ni mchanga ni nani kama sio hao acacia wakiungwa mkono na washirika wao serikalini.
Magufuli alichofanya ni kuweza kuweka wazi kilichokua ndani ya huo uliyoitwa mchanga na hao wezi.
 
Unapoteza nguvu na wakati bure. Aliyetuaminisha ni mchanga ni nani kama sio hao acacia wakiungwa mkono na washirika wao serikalini.
Magufuli alichofanya ni kuweza kuweka wazi kilichokua ndani ya huo uliyoitwa mchanga na hao wezi.
kmbwembwe soma contributors wote humu utaelimika na kuondokana na uelewa potofu uliokuwa nao kabla. Watu wanakupa takwimu lakini wewe umeng'ang'ania kwenye uwongo wa Mwendazake
 
Hujui tu, jiwe kachakachua vitu vingi saaana. Nasema hujui kitu na hakika mtaji wa Jiwe ni watanzania wajinga walio wengi. Hivi inakuingia akilini kampuni ikwepe kodi ya TZS Trillion 450 halafu ulipwe million 300; na ambayo nayo isilipwe.
Wewe ndio mjing kama huelewi kwa nini kampuni ya wezi isiweze oneshwa tangu miaka 20 na zaidi imedhulumu kiasi gani kodi hadi kiasi hakilipiki.
 
kmbwembwe soma contributors wote humu utaelimika na kuondokana na uelewa potofu uliokuwa nao kabla. Watu wanakupa takwimu lakini wewe umeng'ang'ania kwenye uwongo wa Mwendazake
Mimi nimeng'anga'ania kwenye ukweli wa mwenda zake. Namwamini kiitikadi kwangu ni comrade.
Hebu nikuulize. Magufuli aliposema itawezekana lami toka mwanza hadi mtwara hapakua waliyosema anaongopa? Je ilitokea haikutokea tena bado akiwa waziri tu wa miundombinu sio rais? Anyway ni suala la mtazamo.
Nyie mnaoamini consultants wa kingereza na ulaya ndio wanajua hicho wanacholipwa hakika ni unyonyaji tu.
 
Ujinga wetu waafrika ni kudhani kila tatizo letu basi chanzo ni mzungu na pale inapotokea Kati yetu mtu kuja na wazo tofauti huonwa kama wakala wa mabeberu mleta mada ana majibu yake na upande wake tayali hata akipewa takwimu atapinga tu.
 
Unapoteza nguvu na wakati bure. Aliyetuaminisha ni mchanga ni nani kama sio hao acacia wakiungwa mkono na washirika wao serikalini.
Magufuli alichofanya ni kuweza kuweka wazi kilichokua ndani ya huo uliyoitwa mchanga na hao wezi.
Kwahiyo copper concentrates ni mchanga, sio?! Au hiyo ripoti imeandikwa wakati wa Magufuli?!

Unajua watu aina yako ni majanga sana kwa taifa kwa sababu ni wavivu wa kusoma!! Nimekuwekea hapo ripoti, SOMA!! Kabla hujapatikana msamiati wa makinikia jina lilokuwa linatumika ni MCHANGA WA DHAHABU na sio MCHANGA!!
 
Wabongo wana kasumba za kifala kweli😂tumerudishwa zama za kuamini mzungu ana akili kuliko sisi! Wewe unataka ulindiwe rasilimali halafu unaomba consultancy kwa mwizi😅 hizi ndio akili za makamba yani mwizi aje akufungie system ya usalama ndani mwako kisha utegemee utabaki salama.
 
Yani we bado upo gizani, ile report ya makinikia ilikuwa ni blahblah za awamu danganyifu iliyopita. Hakuna la maana baada ya pale na makinikia yanatoka kama kawaida tangu mwendazake akiwepo ni kiini macho, ni upupu mtupu hakuna cha nini wala nini.
 
Stuxnet, hawa ndo wafuasi wa JPM!!
 
Extrovert,

Let's assume serikali inakuambia pendekeza ONE LAW FIRM in Tanzania wenye uzoefu na consultancy kwenye field ya mafuta na gesi... je, utapendekeza kampuni ipi ili tuchunguze profile zao?!

Kama sio law firm, unaweza kunitajia MTANZANIA mmoja TU mwenye hizo sifa ili nae tufuatilie CV yake?!
 
Na mbaya zaidi, ulikuwa ni ukaguzi wa upande mmoja... eti mnaikagua Acacia lakini Inspection Team YOTE inatoka serikalini na Acacia hawakuruhusiwa kutia pua!!

Sasa sijui ni nani angeamini ripoti ya aina hiyo zaidi ya misukule wake!! Matokeo yake ndo yale, ripoti inasema tunadai Sh 420 Trillion wakati tulichoambulia hakifiki hata 0.5% ya hizo 420 Trillion!
 
eti akachakachua, sasa kwanini hawakwenda mahakamani kama walivyodai??

na ulivyo kolo sasa eti ni 0.7 hivi wewe kontena unalijua au unaongea ushubwada
hivi kwa akili tu ya kawaida tu hata ile ya kuvukia barabara ni mwekezaji ambae atarisk kusafirisha kontena ili achenjue 0.7 ya dhahabu na silver???? lazima kutakuwa na shida mahali kwenye fikra zako
 
Magufuli hatabaki kuwa Magufuli pamoja na uongo wake au ufisadi wake au chchote kile alichokifanya vibaya.

Lakini kamwe hatokuja tokea kiongozi au Rais mwenye msimamo kama Magufuli. He was the best president. Hayupo, hatukonae tena, he has gone wacha apumzike kwa amani.

Magu alikemea madudu waziwazi, Magu alipenda nchi yake, Magu alikuwa mzalendo wa kweli kweli, Magu alikuwa Rais wa tofauti na watangulizi wake. Hakuna atakae mfikia kwa uongozi wake.
 
Mkuu kama upo serikali au taasisi yoyote ya serikali basi kula kulingana na urefu wa kamba yako. Huu ndiyo msemo wa sasa.

Usifikiri watanzania ni wajinga kama wewe. Watanzania wa Sasa ni waelewa kuliko hata ninyi mnaojiita viongozi. Hakuna mtanzania asiyejua kuwa nchi hii ni shamba la babi. Hakuna mtanzania asiyejua kuwa nchi hii wachache wenye roho za kifisadi ndiyo wanaofaidi.
Hakuna mtanzania asiyejua kuwa nchi hii kila kiongozi alioko madarakani wanajilimbikizia Mali kutoka kwa watanzania maskini wanaotafuta pesa zao ki halali.

Kwahiyo, wewe kama mfuasi wa waziri mwenye dhamana na upo kwa ajili ya kumtetea aina shida. Wewe endelea kumtetea ili uweze kuingia chooni na kutoka.

Tuache sisi ambao tunawatafutia na kuchukua kirahisi kwetu. Hapa najua huwezi kuelewa kwasababu upo kwa ajili ya kutetea mafisadi wa nchi hii.
 
Ametuachia population ya wajinga wengi sana kama huyu @kmbwembwe, wanapinga kila anachofanya Rais Samia na Makamba.
Hawa ndiyo wanaoitwa wazalendo. Nchi ikipewa wazalendo waongoze tutakuwa taifa la wapumbavu.

Afadhali tuongozwe na mafisadi. Angalau enzi za mafisadi hela tunaiona tofauti na enzi za wazalendo.

Mungu ibariki Tanzania.
 
Magu alikemea madudu waziwazi, Magu alipenda nchi yake, Magu alikuwa mzalendo wa kweli kweli, Magu alikuwa Rais wa tofauti na watangulizi wake. Hakuna atakae mfikia kwa uongozi wake.
Na tuzidi kumwombea apumzike na kamwe tusipate Rais mwingine anayefanana na huyu mzalendo Magu"fool".
 
hiyo inaitwa Consultancy firm...tena ni international... nionyeshe consultancy firm ya oil and gas iliyopo Tanzania ambayo ishawahi kufanya kazi hata Malawi..

Huo sio mkataba wa kuuza na kununua vitumbua, huo ni mkataba unaozungumzia trilioni of money na wadau kutoka kila Pembe ya dunia ambao wameweka hela yao na mwisho wa siku wanahitaji return na faida within the time limit....

Labda tuache kila kitu mpaka siku tukipata akili au tukubali kuliwa kidogo kwa kuweka uzalendo mbele na kushirikisha wadau wa dunia wenye uelewa wa mabiashara haya ya kimafia miaka nenda rudi.... Dunia ya sasa na mabiashara ya sasa kuliwa lazima uliwe au vinginevyo uache kila kitu ili usiliwe....
 
Mpaka anafuatwa consultancy kutoka Ulaya ujue uzoefu wa hawa wa ndani ni mbaya. Hawana ushindani unaotakiwa kuweza kupewa kazi (competence), naamini wizara mpaka kuwafuata hao waingereza watakuwa wamejiridhisha vya kutosha.

Kumbuka katika team ya wizara kuna mtu kama Mataragio huyu ni mtaalam wa haya masuala aliyewahi kufanya kazi USA.
 
Jibu swali very simple; Je tulilipwa zile USD 190 Billion zinazotokea kwenye ukokotozi wa ripoti ya PROF Mruma ya Kg 7 per container?

Kama hatukulipwa basi mjinga ni Magufuli, wewe Just Distinctions na wenzenu wengine ambao mnaamini kulikuwa kg 7 za dhahabu

Unajiita Just Distinctions halafu huwezi ku grasp simple maths and logic?? Au ndiyo wa vyeti feki
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…