Hivi unajisikiaje kushindwa kuwatunza wazazi wako?

Hivi unajisikiaje kushindwa kuwatunza wazazi wako?

Hapana.

Mimi nishawafungulia watu biashara hapahapa JF, wala siwajui, wamenililia tu nikawapa msada.
Hivyo, ninapoandika mambo ya principle, si kwa uchoyo.

Uchoyo hapa ni kumnyenga mtoto.

Yani wewe mzazi umeishi miaka kibao, umepata muda wa kujiandaa na miaka ya uzeeni.

Hujajiandaa, umefeli maisha. Kumnyenga mtoto ni vibaya, ulitakiwa kumuandaa na kumuacha ahudumie watoto wake na yeye ajiandae kwa maisha ya uzeeni.

Kama umeyapatia maisha, uko vizuri, ndiyo kabisaa kumnyenga mtoto vibaya

Badala ya kumuachia mtoto naye ajipange kuhudumia watoto wake, mnamuongezea mzigo awe anahudumia wazazi na watoto.

Kuhudumia wazazi ni optional, si lazima.

Kuhudumia watoto ndiyo lazima.

Wazazi hujawaleta duniani, wamekuleta wao.

Watoto umewaleta duniani.
Sawa Mkuu....mi naumia sana kuona nashindwa saidia mama yangu
 
Sielewi kabisa mkuu
Kuna mambo mengine unaweza kufanya kwa nia nzuri kabisa, kumbe ndiyo unaharibu.
Unaweza kuwa na nia ya kusaidia, uwezo huna, nia yako nzuri inaweza kukuletea ugonjwa wa moyo buree.

Maisha yana kupata na kukosa, ukiweza ku hustle mpaka ukapata, sawa, saidia unayetaka.

Ukikosa na ushafanya jitihada zote, usijione mnyonge sana kwa kukosa ukajitia jakamoyo litakalokuzidishia simanzi bure bila tija.

Kama una watu waelewa watakuelewa tu, kama wasipokuelewa, hilo ni tatizo lao, si lako.
 
Kuna mambo mengine unaweza kufanya kwa nia nzuri kabisa, kumbe ndiyo unaharibu.
Unaweza kuwa na nia ya kusaidia, uwezo huna, nia yako nzuri inaweza kukuletea ugonjwa wa moyo buree.

Maisha yana kupata na kukosa, ukiweza ku hustle mpaka ukapata, sawa, saidia unayetaka.

Ukikosa na ushafanya jitihada zote, usijione mnyonge sana kwa kukosa ukajitia jakamoyo litakalokuzidishia simanzi bure bila tija.

Kama una watu waelewa watakuelewa tu, kama wasipokuelewa, hilo ni tatizo lao, si lako.
Asante mkuu
 
Yaan wamekulea kwa shida, wamekusomesha kwa shida ila kaz uliyopata na tayari una familia inayokutegemea then hiyo familia yako ikakufanya ukashindwa kutunza wazazi au kuwasaidia wazazi, huenda kuna muda wanakusaidia wewe kwa kidogo walichonacho kwa sababu wanaona magumu yako.

Unajisikiaje eti? 😭😭😭😭😭
Ni kazi ya wazazi kulea watoto wao, na siyo kutegemea kwamba hao watoto watawalea wao wakisha kuwa wakubwa. Ila kama watoto wana uwezo siyo mbaya wakilea wazazi wao pia. Jukumu la watoto wakishakua ni kulea watoto wao pia. Forward generational support, not the reverse
 
Ni kazi ya wazazi kulea watoto wao, na siyo kutegemea kwamba hao watoto watawalea wao wakisha kuwa wakubwa. Ila kama watoto wana uwezo siyo mbaya wakilea wazazi wao pia. Jukumu la watoto wakishakua ni kulea watoto wao pia. Forward generational support, not the reverse
Sawa mkuu
 
Iko hivi:

Si wajibu wa mtoto kumtunza mzazi, ila ni wajibu wa mzazi kumtunza mtoto. Waafrika hapo ndo uwa tunafeli. Unamsomesha mtoto ili aje akusaidie, yaani kukusaidia kwa maana ya kuanza kukuhudumia kiuchumi.

Kama unamwandaa mtoto wako aje kukusaidia wewe, kizazi chake kitasaidiwa na nani?!. Pambana. Kama unamsomesha mtoto aje kukusaidia labda aje kukusaidia kuendesha biashara zako. Sio umwandae mtoto kumbebesha taabu zako za kiuchumi. Nae anazake.
Amen to this! On point
 
Waafrika tulishakosea kitendo Cha wazazi kusomesha Ili mtoto aje kisaidia na ndio maana kuuwa mzizi wa umaskini ndani ya nyumba zetu ni ngumu mnooo utakuta kijana kapata kazi apo apo anatakiwa kusomesha wadogo zake wakati huo huo anatunza wazazi baada ya miaka mitano inabid aoe wakati huo hajajenga inabidi alipe Kodi atunze mke na Bado familia inamwangalia ni ngumu kuuwa chain ya umaskini ndani ya familia kila kizazi kinaanza upya .
 
Mzazi anatamani kukuona wewe ukifanikiwa na sio kua chuma ulete kwako.
Ukiona mzazi anataka ufanikiwe ili umsaifie aisee wewe ni fursa kwake.
 
Waafrika tulishakosea kitendo Cha wazazi kusomesha Ili mtoto aje kisaidia na ndio maana kuuwa mzizi wa umaskini ndani ya nyumba zetu ni ngumu mnooo utakuta kijana kapata kazi apo apo anatakiwa kusomesha wadogo zake wakati huo huo anatunza wazazi baada ya miaka mitano inabid aoe wakati huo hajajenga inabidi alipe Kodi atunze mke na Bado familia inamwangalia ni ngumu kuuwa chain ya umaskini ndani ya familia kila kizazi kinaanza upya .
🙏👊mkuu
 
Back
Top Bottom