Hivi Vijana wa CHADEMA Wanatumia kitu gani kinachoharibu uwezo wao wa kufikiri na kujenga hoja? Mbona hawana adabu wala hekima?

Hivi Vijana wa CHADEMA Wanatumia kitu gani kinachoharibu uwezo wao wa kufikiri na kujenga hoja? Mbona hawana adabu wala hekima?

Lucas Mwashambwa

JF-Expert Member
Joined
Jul 28, 2022
Posts
28,722
Reaction score
20,610
Ndugu zangu nimeuliza nipate kusaidiwa kupewa majibu maana nikiangalia na kufuatilia kwa makini naona hatari kubwa Sana iliyopo mbele ya chama hiki, wataalamu wanasema kuwa ukitaka kujuwa urefu wa maisha ya chama chochote Basi huna budi kuangalia uwezo wa kiuongozi wa vijana waliopoo katika chama husika ambao ndio hasa watakao kuwa viongozi wa kesho

Lakini ukiangalia na kutupia jicho kwa vijana waliopoo ndani ya chama hiki na ambao ndio viongozi kwa Sasa kiukweli unasikitika Sana na kuwaza sijuwi wanakula vitu gani huko chamani kwao,

Ni vijana waliokosa adabu hekima busara unyenyekevu na staha, Ni vijana waliojaa matusi utazani wameopolewa kwenye pipa la Pombe ya kienyeji, Ni vijana ambao kwao yoyote na wa umri wowote na wa cheo chochote anaweza kutukanwa matusi yote yanayoandikika na yasiyo andikika, Ni vijana waliojaa mihemuko na kuripuka Kama Moto wa gesi,

Kibaya zaidi vijana Hawa wa chadema Ni Kama hawana mlezi, hawana mtu aliyesimama Kama mzazi wao kimalezi, Hawana mtu wa kuwaongoza na kuwafunda, hawana mtu wakuwapa maelekezo, hawana mtu wa kuwachunga ili wakue kiuongozi, hawana mtu wakuwafunga breki ya midomo yao, Hawana mtu anayeweza Akazungumza wakamsikiliza na kumheshimu, hawana wazee huko, Ni vijana waliozibuka na kuzuzuka, Ni vijana wanao jazana ujinga muda wote, Ni vijana waliokosa muunganiko wa ubongo na midomo yao, hawana muunganiko wa akili na vidole vyao

Ni vijana wanao hisi kuwa huo ndio ushujaa, ukamanda wenyewe, ujana wenyewe. Chadema itafika muda kitakosa viongozi na kwa kuwa Hawa ndio kwa umoja wao wa kujazana ujinga na kukosa adabu na heshima watajikuta mmoja wao anakuwa kiongozi mkuu wa chama, hapa ndipo chama hiki kitakapozidi kupiga mueleka Zaid ya hapa kilipo, ndipo kitazidi kusereleka kuelekea shimoni, ndipo kitakapozidi kusambaratika, ndipo kitakapozidi kupuuzwa Zaid ya hapa

Maana hakuna atakaye kuwa tayari kuwasikiliza watu Kama Hawa waliojaa matusi, watu ambao wapo tayari kumtukana yoyote yule kwa matusi ya nguoni bila kosa lolote kisa tu katofautiana nao, hakuna ambaye yupo tayari na atakuwa tayari kwenda kwenye mkutano wao kusikiliza mimatusi tu, hayupo mtu wa namna hii hata siku moja

Sina cha kuwashauri vijana Hawa waliokosa adabu na hekima maana hiyo siyo kazi yangu, Nachoweza kuwaasa ni kimoja tu kuwa watukanane huko huko lakini ikija kwenye mamlaka ya nchi lazima waiheshimu Sana maana wasije wakafikiri kuwa Rais wa nchi Ni sawa na Rais wa Bao, lazima wajuwe kuwa Rais Ni mkuu wa nchi na kiongozi wa vikosi vyote vya ulinzi na usalama aliye apa kuilinda nchi hii kwa nguvu zake zote ili iwe na amani na utulivu, hivyo hakuna anayeweza kuwavumilia watu wanao hatarisha usalama wa Taifa, lazima watawajibika na kuwajibishwa kwa mujibu wa Sheria za nchi yetu

Kazi iendeleee, Mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na sauti

Lucas Mwashambwa, kijana mzalendo na mpenda nchi yangu
 
Ni vijana wangapi kati ya hao uliowaita wana matusi mmewahi kuwapeleka mahakamani kwa hayo makosa yao mkashinda kesi?

Mimi huwa naona mara nyingi wao hushinda tu, kumbe basi, kinachoitwa tusi na shabiki au mwanachama wa CCM, hakitambuliki hivyo kwenye hii jamii tuliyopo kwa ujumla wake.

Ndio maana CCM mna tabia nyingi za ajabu ambazo wengine tunazishangaa, ila nyie mnaziona za kawaida tu, uvunjifu wa sheria kama kuzuia mikutano ya hadhara ya kisiasa, na kuwapiga wapinzani ni mifano michache.
 
Ni vijana wangapi kati ya hao uliowaita wana matusi mmewahi kuwapeleka mahakamani kwa hayo makosa yao mkashinda kesi?

Mimi huwa naona mara nyingi wao hushinda tu, kumbe basi kinachoitwa tusi na shabiki au mwanachama wa CCM, hakitambuliki hivyo kwenye jamii tuliyopo kwa ujumla wake.
Hivi kwamba wewe huoni namna wanavyotukana viongozi wa serikali na yeyote anayetofautiana nao ?
 
Nimeandika hapa ili mpate kusaidiwa kupitia mawazo ya watu japo sijuwi Kama mnaweza kubadilika kwa hatua mliyofikia kwa Sasa ya kuporomosha matusi utazani gari lililokata breki
Peleka uchawa wako huko lumumba
 
Kama huwezi kumkalipia Tulia, na unyamaze kimya. Usijifiche mgongoni mwa CHADEMA.
Tulia alikuwa anamaanisha kuwa lazima kuwepo kuheshimiana na kukosoana kwa heshima na busara na lazima tujifunze kuvumiliana tunapotofautiana na tubishane kwa hoja, siyo matusi Kama mnavyo fanya nyie, na kauli ya kusema kunyooka na mtu maana yake Ni kwa hoja na kutoa taarifa mahali panapohusika
 
Ulinukuu vibaya na hukuielewa kauli ya mh spika

Shida inaanzia hapo, ukishakuwa bias huwezi kusikilizwa. Wewe ni bias ndio maana nakuona Kama msaka fursa. CCM akitamka neno baya hajaeleweka vizuri. Ila kwa CHADEMA neno lolote sio zuri.

Nimeisikia clip nzima Mara nyingi, kawaambia vijana wanyooke na atakaye msema vibaya Rais iwe ndani ya chama au nje ya chama.
 
Ndio maana alisema iwe ndani au nje ya chama akimaanisha Ni lazima tuijenge utamaduni wa kuheshimiana na kukosoana kwa heshima na adabu, kunyooka nao maana yake kutoa taarifa mahali husika ili hatua za kisheria zichukuliwe kwa utaratibu wa kisheria
Shida inaanzia hapo, ukishakuwa bias huwezi kusikilizwa. Wewe ni bias ndio maana nakuona Kama msaka fursa. CCM akitamka neno baya hajaeleweka vizuri. Ila kwa CHADEMA neno lolote sio zuri.

Nimeisikia clip nzima Mara nyingi, kawaambia vijana wanyooke na atakaye msema vibaya Rais iwe ndani ya chama au nje ya chama.
 
Tulia alikuwa anamaanisha kuwa lazima kuwepo kuheshimiana na kukosoana kwa heshima na busara na lazima tujifunze kuvumiliana tunapotofautiana na tubishane kwa hoja, siyo matusi Kama mnavyo fanya nyie, na kauli ya kusema kunyooka na mtu maana yake Ni kwa hoja na kutoa taarifa mahali panapohusika

Hayo umeyasema wewe ili Tulia akuone unamtetea. Lakini kiukweli Tulia ni mchochezi uspika wa kupewa umemlewesha anaona wengine hawafai kabisa.
 
Back
Top Bottom