Hivi vitambulisho vya Askari/ Wanajeshi vina kazi gani kwa raia?

Hivi vitambulisho vya Askari/ Wanajeshi vina kazi gani kwa raia?

othiambo

JF-Expert Member
Joined
Nov 15, 2014
Posts
1,995
Reaction score
2,795
Hali zenu waungwana.

Hili swali huwa najiuliza sana na sipati majibu, hivi hawa watu vitambulisho hivi vimekua ndio kimbilio na nguzo ya utemi kwa wananchi?

Sababu ya swali langu ni jana kipindi narudi nyumbani kufika kituoni magari hakuna; ghafla ikaja daladala ikitangaza nauli 500 katikati ya safari, mama mmoja akadai mi mia tano sina nina mia nne wakabishana kidogo ndipo mama alipodakia: Hoo! unajua mimi nani au nitoe kitambulisho changu, nikabaki nastaajabu, maskini konda alinywea hapo ndipo nikajua Watanzania kweli hatujui haki zetu. Nikabaki najiuliza maswali makubwa matatu, hasa swali la tatu.

1. Hivi yule Mama na kitambulisho chake hajui njia hii haina usajili na magari, hata tiketi hatupati ndiyo maana makonda wanatuogelea, mbona wanabadili route na hatung'aki?

2. Hivi yule mama mbona bajaji huwa zinapandwa kwa 500 hadi 1000 njia ikiwa mbovu na hawapingi, ikamuume 100 tu?

3. Hivi hawa wenye vitambulisho mbona kwenye vikao vya maendeleo hatuwaoni wakihimiza kwa vitambulisho vyao, maana kama barabara yetu ingekamilika, hawa makonda wasinge tuogelea kiasi hiki na tungebishana kimantiki.

Maana ilbidi iwe imekamilika kitambo sema watu wameruka judo na wenye vitambulisho wanalijua hili na tunaishi nao mitaani. Watu walishalipwa malipo ya kubomolewa kupisha barabara tangu Jakaya, matokeo yake vikitokea vikao wanafuatwa wazee wetu wasiojua pa kutokea tena wanapewa maswali ya kuwauliza viongozi maana majibu yashaandaliwa.

MSITUTISHE NA VITAMBULISHO VYENU BWANA
.
 
Yani umeuliza maswali na kujijibu mwenyewe wananzengo tuchangie nini sasa?
kwakua nilikua najua ila si kila mtu anajua tunafunguana mawazo hapo........unaweza hata wewe siku ukashadadia jambo kwenye umati bila kuchunguza mzunguko wa ukishadadiacho.nashukuru kwa kujua.
 
Mkuu unatoaje lawama kwa wapiganaji wetu kisa huyo raia aliyetoroka mafunzo ya mgambo! To be honest sijawahi ona makamanda wetu wanaleta ubabe kisa tu wana mamlaka ktk nchi.

5/5
Wengi tu kakangu kama M/MUNGU kakujaalia moyo huo shukuru sana vyeo vinatia kibri.
 
Sema tu hii nchi watu wengi hawana hata ABC ya sheria
Hata Mabeyo haruhusiwi kupanda gari ya umma bure sembuse Sajenti, koplo au Private soldier
Ndio maana serikali inajiamulia tu jambo lolote na wananchi kimya
 
Sema tu hii nchi watu wengi hawana hata ABC ya sheria
Hata Mabeyo haruhusiwi kupanda gari ya umma bure sembuse Sajenti, koplo au Private soldier
Ndio maana serikali inajiamulia tu jambo lolote na wananchi kimya
Kiukweli Watanzania ni mbumbumbu Sana wa sheria.
Vitu vingi vinafanywa kimazoea na watu wanashindwa kuhoji.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hajakutana na mwehu. Kitambulisho utatoa na nauli niliyoitaja utaitoa. Vinginevyo dere geuza gari
 
othiambo, daa et msitutishe😂😂😂 yani kaambiwa tu kitambulisho kawa mpole Sasa angekuwa kavaa full battle combat si ndo angekojoa ila mkuu uyo sio mwenzetu zilikuwa za zama hizooo tunapanda bus bureee kigoma to dar kula mgahawan Bure unasema kikwete Ata Lipa 😂😂😂saiz huo ujinga haupo Tena zama zimebadika
 
daa et msitutishe😂😂😂 yani kaambiwa tu kitambulisho kawa mpole Sasa angekuwa kavaa full battle combat si ndo angekojoa ila mkuu uyo sio mwenzetu zilikuwa za zama hizooo tunapanda bus bureee kigoma to dar kula mgahawan Bure unasema kikwete Ata Lipa 😂😂😂saiz huo ujinga haupo Tena zama zimebadika
Kuna vitu Katika hii dunia vinamfanya mtu kua mnyonge mara zote maradhi,umaskini na elimu hivi vitu vinamnyima mtu utashi....nini askari hata ukiwa na nduguyo au jirani anajipata kipesa tu wengine humwogopa mtu huyo...,mtu anawaza mi nipelekwe polisi sasa hivi nina hela ya kutokea.
 
Sema tu hii nchi watu wengi hawana hata ABC ya sheria
Hata Mabeyo haruhusiwi kupanda gari ya umma bure sembuse Sajenti, koplo au Private soldier
Ndio maana serikali inajiamulia tu jambo lolote na wananchi kimya
kweli kabisa na wengi hatujui haki wala wajibu wetu.
 
Mkuu unatoaje lawama kwa wapiganaji wetu kisa huyo raia aliyetoroka mafunzo ya mgambo! To be honest sijawahi ona makamanda wetu wanaleta ubabe kisa tu wana mamlaka ktk nchi.

5/5
well said
 
Back
Top Bottom