Hivi wale Waislam wa kipindi kile walipotelea wapi?

Hivi wale Waislam wa kipindi kile walipotelea wapi?

Robert Heriel Mtibeli

JF-Expert Member
Joined
Mar 24, 2018
Posts
28,297
Reaction score
68,017
Kwema Wakuu!

Nimewakumbuka Sana! Hivi wako wapi? Mko wapi? Tafadhali naombeni mnijibu!

Taikon nitawarudisha na kuwapeleka mpaka kijiji cha Makanya huko nilikozaliwa, pengine labda Waislam hao ndipo walipokuwa wanapatikana lakini hapana, nilibahatika kuwaona wakati Fulani nilipoenda Morogoro miaka ya 2006 Kurudi nyuma.

Hii ni kusema Waislam hawa walikuwa wapo nchi nzima. Sasa iweje wapotee wote na tusijue waliko?

Miaka hiyo ni mtoto mdogo kabisa, nikiwa na watoto wenzangu, nilishuhudia misafara yenye kundi kubwa la watu waliovalia kanzu za namna na rangi tofautitofauti, kichwani wakiwa wamevalia Barakashia na malemba yenye kuvutia haswa. Mavazi hayo yaliwatambulisha Kama Waislam.

Mikononi mwao walikuwa wamebeba Ngoma Kwa Baadhi Yao, huku wengine wakiwa wamebeba Milingoti mifupi na mirefu yenye bendera za namna kadhaa; zilizoandikwa maandishi ya kiarabu. Kwa kipindi kile sikuweza kujua zinamaandishi yanayomaanisha nini.

Ngoma zilipigwa na nyimbo zikaimbwa huku msafara huo ukikatiza mtaa Kwa mtaa, barabara Kwa barabara. Huku waislam hao wakicheza Kwa furaha ungedhani wameishinda Dunia.

Hisia zilizokuwa zinakuja kichwani mwangu Taikon ambaye nilikuwa nikiufuata msafara huo aidha Kwa kuvutiwa au kushangaa, nilifikiri Dunia ndio ilikuwa inafika mwisho wake. Waliimba Kwa msisimko, walionyesha hamasa.

Ngoja nijaribu kuimba kadiri ya nilivyoyasikia maneno ya moja ya wimbo zile, ingawaje naweza nisipatie sana!; Hivyo mtanisamehe na wenye kujua mtaweka marekebisho;

"Allah maulana! Allah maulana Saidina Huayallah. Huayallah! Huayallah (mtume) Huayallah! (Karima) Huayallah!"

"Mtume Yallah! Yallah!. Karma Yallah! Yallah×2"

Basi wakawa wanapita huku na huko wakisherekea.

Ilikuwa ni ngumu sikukuu ya Maulidi au ya Idi kupita bila ya misafara hii mirefu yenye watu wengi mno wakizunguka majira ya Jioni kabisa baada ya Kula na kunywa na kufurahia chakula.

Hiyo ndio namna nilivyozitambua sikukuu za kiislam nyakati zile nikiwa ndio naanza kupata Uelewa wa Dunia.

Sasa Taikon najiuliza, mambo Yale mbona yalipotea?

Waislam wale walitoweka na kuyeyuka Kama Moshi?

Au je Baadhi ya Maeneo bado desturi hii inaendelea?

Kwa kweli napenda kuwashauri Waislam wote wa Zama hizi.

Ile Desturi ni nzuri mno. Ingawaje Mimi sio Muislam lakini desturi Ile ya kuzunguka mitaani na misafara yenye Ngoma, bendera mkicheza Kwa furaha kufurahia sikukuu zenu ni moja ya mambo yaliyowafanya Spesho katika usheherekeaji wa sikukuu tofauti na dini zingine.

Watoto waliovalishwa vizuri, Wamama waliojitanda, Wababa na Wazee waliovaa vizuri kanzu zao mpya na Kama sio mpya basi Safi walishiriki katika misafara hii. Iweje leo badala ya Waislam kufurahia Kwa namna hiyo wanaishia kwenda kwenye Matamasha ya muziki ya kidunia, Bora lingekuwa tamasha la Dini.

Wako wapi waislam wale? Uko wapi uislam ule?

Wao wapi waislam wale ambao Sisi Wakristo wa Enzi hizo tukiwa watoto tulikuwa tunashirikiana nao kuutafuta Mwezi! Hivi unakumbuka?

Makundi Kwa makundi ya watu Majira ya Jioni jua likiwa limezama yalisimama kutazama angani upande wa Magharibi kuutafuta mwezi.

Ilikuwa ni sifa na Jambo la kujivunia kuwa WA Kwanza kuuona mwezi mwandamo wa mfungo wa Ramadhan.

Sio watoto, sio wamama wala wazee, kila mmoja alihangaika kuutazama mwezi mchanga.

Na Kama kundi Lenu lingechelewa kuuona mwezi basi Kwa mbali ungesikia sauti kutoka mtaa wa pili au mbali kidogo zikiimba;
" Mwezi! Mwezi! Mwezi×"

Hali hiyo ingekufanya uzidishe kukaza macho kuuona mwezi.
Ilikuwa bahati mbaya Sana Kama macho yako yalishindwa kuuona mwezi mpaka ulipozama kwani haukaagi angani muda mrefu.

Wapo wapi wale Waislam?

Maana hawa wa sasa nahisi Kama sio. Hawa wanasubiri watangaziwe redio, luningani na mitandao ya kijamii.
Hawajishughulishi.

Wanataka wengine wawaonee huo mwezi. Loooh!

Sisemi kuwasema vibaya, Ila nazungumzia utamu na zile Raha za uislamu wa kipindi kile ambao ulileta shamrashamra na kutufanya mpaka Sisi tusiowaislam kuufurahi uislam.

Mimi sitaki kueleza mambo ya kuletewa Tende, Kualikwa Kula Futari msije sema Taikon anapenda Kula, lakini hata mkisema ni Sawa kwani Kupenda Kula ni kosa! ama Kwa hakika uislam wa kipindi kile ulikuwa ni Neema kubwa katika jamii zetu.

Labda maisha yamebadilika kutokana utandawazi lakini haiondoi ukweli kuwa uislam wa sasa umezidiwa na uislam wa Enzi ninakua.

Labda kilichobaki ni Adhana ya kukumbushana Sala!

Au je Waislam wasasa wanaona aibu kuwa Waislam?

Mungu awabariki waislam wote wa Zama hizo walioufurahisha moyo wangu, waliojitahidi kuutangaza uislam kwa namna njema.
Walioleta neema ndani ya jamii.

Pia awabariki wanaoendelea kufurukuta katika Zama hizi mbaya za utandawazi.
Kwa kweli Zama hizi ukiona Muislam anayejitahidi kufuata miiko na Mila za kiislam mpe hongera hata Kama sio dini yako.

Wako wapi wale Waislam wa Zama zile?

Taikon nimemaliza, Leo sitaki maswali.

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa sasa Kibiti, Pwani.
 
Kwa hiyo kumbe Wale ndio waliokuwa wanakosea Mkuu?

Kwamba uislam wa sasa ni Bora kuliko wa Kale?
Elimu haikufikishwa kwa usahihi Kuna mambo yaliongezwa ili kuuharibu uislam halisi kutembea na kupiga ngoma kwenye majumba ya watu usiku hayo siyo mafundisho ya uislam
Uislam mafundisho yake yamejaa ustaarabu na aman

Ukitaka kustaarabika soma Quran na Sunnah za mtume huko ndo ulipo uislam halisi
 
Elimu haikufikishwa kwa usahihi Kuna mambo yaliongezwa ili kuuharibu uislam halisi kutembea na kupiga ngoma kwenye majumba ya watu usiku hayo siyo mafundisho ya uislam
Uislam mafundisho yake yamejaa ustaarabu na aman

Ukitaka kustaarabika soma Quran na Sunnah za mtume huko ndo ulipo uislam halisi

Kwa hiyo wale kumbe ndio waliokuwa wanakosea?

Sasa sikukuu inasheherekewa vipi Kama sio Kwa muziki na nyimbo?

Embu nijuze ni sikukuu gani hiyo bila ya mambo hayo!
 
Taikoni umesahau na mwezi wa ramadhani ikifika usiku hua kuna vigoma vya daku vinapita mtaa kwa mtaa kuwasisitiza waislamu waamke kula daku.
Utandawazi umechangia kwa kiasi kikubwa kuwafanya watu kuwa wabinafsi, zamani futari zilikua zinaliwa kwenye kibaraza cha nje ya nyumba na kila mpita njia alikua anakaribishwa ajumuike kwenye futari ya pamoja, siku hizi watu futari wanalia vyumbani mwao, hata ule mshikamano na mapenzi hayapo tena.
 
Kwa hiyo wale kumbe ndio waliokuwa wanakosea?

Sasa sikukuu inasheherekewa vipi Kama sio Kwa muziki na nyimbo?

Embu nijuze ni sikukuu gani hiyo bila ya mambo hayo!
Nyimbo/muziki katika uislam ni Haram kabisa.
Waislam wanasherehekea kwa kula na kunywa vilivyo halali na kushiriki mashindano mbali mbali Kama kusoma Quran na kucheza michezo mbali mbali ya kujenga afya ambayo ipo katika maadili sahihi ya ubinadam ambayo hailazimishi kuwa uchi ili ushiriki
 
Elimu haikufikishwa kwa usahihi Kuna mambo yaliongezwa ili kuuharibu uislam halisi kutembea na kupiga ngoma kwenye majumba ya watu usiku hayo siyo mafundisho ya uislam
Uislam mafundisho yake yamejaa ustaarabu na aman

Ukitaka kustaarabika soma Quran na Sunnah za mtume huko ndo ulipo uislam halisi
Jazzakallahu khairan umemjibu kiuhalisia Sana Kama hajaelewa atakuwa mbishi tu
 
Nyimbo/muziki katika uislam ni Haram kabisa.
Waislam wanasherehekea kwa kula na kunywa vilivyo halali na kushiriki mashindano mbali mbali Kama kusoma Quran na kucheza michezo mbali mbali ya kujenga afya ambayo ipo katika maadili sahihi ya ubinadam ambayo hailazimishi kuwa uchi ili ushiriki


Hiyo mashindano ya kusoma Quran imeandikwa kwenye Quran?

Muziki sio haramu, Ila Inategemea na ain ya Muziki unaotumika.
Ndio maana kuna Kawaida, au hujui kaswida pia ni nyimbo/muziki?

Hakuna sherehe pasipo Nyimbo, muziki, vinywaji na chakula. Hakunaga sherehe ya hivyo.

Kuhusu chakula Hilo lipo wazi, Waislam sheria zinawaongoza vyakula vya kutumia.
Sikukuu si wanapika Pilau, wali, nyama, nqvyakula vingine vinavyoruhusiwa.

Hiyo kucheza michezo yenye Afya imeandikwa kwenye Quran, nani michezo gani hiyo?

Kumbuka kwenye dini yoyote Ile kuna mambo yaliyoagizwa na Mungu ambayo ndio yamsingi lakini pia kuna mambo ya kibinadamu.
 
Sipo hapa kubishana.

Kwa hiyo Elimu ya sasa iliyowafikia Waislam wengi na zamani, wapi waislam wenye unafuu?

Kwa muono wangu Waislam wa zamani wamewaacha mbali Sana Waislam wa sasa. Mbali sana
Tulia bwana Taikon uislamu hauendeshwi kibubusa na Rai za ajabu ajabu ...Muislam safi Ni Yule anaefuata Quran na Sunnah ,,,kataa wahuni na Wazushi ktk dini...
 
Hiyo mashindano ya kusoma Quran imeandikwa kwenye Quran?

Muziki sio haramu, Ila Inategemea na ain ya Muziki unaotumika.
Ndio maana kuna Kawaida, au hujui kaswida pia ni nyimbo/muziki?

Hakuna sherehe pasipo Nyimbo, muziki, vinywaji na chakula. Hakunaga sherehe ya hivyo.

Kuhusu chakula Hilo lipo wazi, Waislam sheria zinawaongoza vyakula vya kutumia.
Sikukuu si wanapika Pilau, wali, nyama, nqvyakula vingine vinavyoruhusiwa.

Hiyo kucheza michezo yenye Afya imeandikwa kwenye Quran, nani michezo gani hiyo?

Kumbuka kwenye dini yoyote Ile kuna mambo yaliyoagizwa na Mungu ambayo ndio yamsingi lakini pia kuna mambo ya kibinadamu.
Haya Ni maoni yako na sio ya uislamu kwahiyo ...baki nayo mwenyewe...
 
Hiyo mashindano ya kusoma Quran imeandikwa kwenye Quran?

Muziki sio haramu, Ila Inategemea na ain ya Muziki unaotumika.
Ndio maana kuna Kawaida, au hujui kaswida pia ni nyimbo/muziki?

Hakuna sherehe pasipo Nyimbo, muziki, vinywaji na chakula. Hakunaga sherehe ya hivyo.

Kuhusu chakula Hilo lipo wazi, Waislam sheria zinawaongoza vyakula vya kutumia.
Sikukuu si wanapika Pilau, wali, nyama, nqvyakula vingine vinavyoruhusiwa.

Hiyo kucheza michezo yenye Afya imeandikwa kwenye Quran, nani michezo gani hiyo?

Kumbuka kwenye dini yoyote Ile kuna mambo yaliyoagizwa na Mungu ambayo ndio yamsingi lakini pia kuna mambo ya kibinadamu.
Muongozo wa uislam ni Quran na sunna Na siyo hisia zako braza.

Yeyote atakaefanya matendo ambayo hayakuamrishwa/ kufundishwa na hayako katika muongozo wa uislam mtu huyo atarudishiwa matendo yake.
 
Muongozo wa uislam ni Quran na sunna Na siyo hisia zako braza.

Yeyote atakaefanya matendo ambayo hayakuamrishwa/ kufundishwa na hayako katika muongozo wa uislam mtu huyo atarudishiwa matendo yake.

Ndio maana nikasema nipe Aya basi inayosema kuwe na mashindano ya Quran Kama uislam hauna hisia na maoni ya watu.

Nasubiri Aya MKUU
 
Back
Top Bottom