Hivi walioanzisha utaratibu wa mwanamke kulipiwa mahari walikuwa na sababu gani za msingi?

Hivi walioanzisha utaratibu wa mwanamke kulipiwa mahari walikuwa na sababu gani za msingi?

Ni sababu za kitumwa, kijima na ubinafsi.

Mahari ni Pesa ya kumnunua Mwanamke ili ummiliki Kwa jina la MKE.

Ni mfume dume hasi(katili) ambao umefanywa Kwa lengo la kumkandamiza Mwanamke.

Mwanamke yeyote mwenye Akili timamu, huru, hawezi kukubali kutolewa Mahari.

Na Mwanaume yeyote huru, timamu, hawezi kumnunua Mwanamke anayempenda ili awe Mkewe.

Watibeli hatufanyi hivyo na kamwe hatutakuja kufanya hayo.
Binti zetu hawatolewi Mahari wala Vijana wetu hawatoi Mahari.
HV wee ulivyo oa hujatoa mahari ,mahari ni heshima bhna
 
Atakae dislike hii post ni bwabwa.. mngeserema labisa
Screenshot_20230922-102411_Chrome.jpg
 
HV wee ulivyo oa hujatoa mahari ,mahari ni heshima bhna

Safari yako ni ndefu Sana.
Nawajua maelfu Kwa maelfu ya wanaume waliotoa hizo Mahari(walionunua Wanawake) ambao hawana heshima yoyote,
Kutwa kunyanyasa Wanawake, ubinafsi uliopitiliza, usaliti na kuchepuka hovyohovyo Watu wasioweza kuzuia tamaa zao, ulevi, kupiga wake zao, n.k
Hizo ndio heshima.

Mahari haijawahi kuwa heshima popote pale. Ile ni biashara kama biashara zingine.

Unaposikia ndoa ndoano ziangalie nyingi Mahari zimetolewa.
 
Unasema tu hata wewe hiyo 50/50 hutaiweza. Mwanamke akijikomboa kiuchumi basi hiyo 50/50 ni rahisi sana kwake.

Na wanawake wengi wamejikomboa na wengine wana mawazo ya kujikomboa ni suala la muda tu.

Sasa wewe upangiwe zamu ya kuosha vyombo kelele utakazopiga nchi jirani watasikia
ndio mkuu mtu anaona kazi kuosha vyombo kwa sababu anajua kazi ya mahari aliyolipia kuoa mwanamke,iwapo 50/50 itakuwepo itakuwa njema zaidi kwasababu mwanamke na mwanaume watakuwa huru zaidi mfano hakuta kuwa na kuoa wala kuolewa hivyo mtu ataamue azae tu.kuhusu kufua,kuosha vyombo na kupika hivyo ni vitu vya kawaida tu,jalibu kuchunguza katika hotel nying za nyota tano wapishi na wahudumu wengi ni wanaume kama kupika kuosha vyombo ni kazi kwa mwanaume, isingekuwa dhana labda yakuoa ili kupata watoto wengi wasingeoa. kwa sababu utelezi usio na masharti upo tena wakutosha.
 
HV wee ulivyo oa hujatoa mahari ,mahari ni heshima bhna
Hakuna heshima yoyote kama aliyekutolea mahari hakuheshimu.

Ndoa nyingi mke na mume hawaheshimiani kwani mahari haikuhusika? Heshima kivipi yaani

Hata wanaosema ukioa au kuolewa unapata heshima, heshima ipi? Heshima inaanza na nyinyi wenyewe kuheshimiana, sidhani kama heshima ya watu baki ina maana yoyote kama nyie wenyewe mpo mpo tu vita ni vita kila siku.
 
Wanawachimba ninyi mnaoendekeza ujingaujinga na mawazo yasiyo na kichwa na miguu. Sijui laana, sijui baraka, sijui radhi, blah! Blah! Blah! Tuu.

Waambie huwaoi wao, kama mtoto wao anataka kutolewa Mahari na wewe hautaki muache, kwani ni lazima umuoe yeye au aolewe na wewe..
Duuu! Moto unawaka nakubali mtibeli
 
Utaratibu ambao vijana wa sasa mnatakiwa muufute ni wa michango ya harusi.
Mahari ni kama token ya appreciation kwa wazazi kwa kumtunza na kumkuza binti yao halafu huwa hata haimalizwi kama huna unatoa kiasi tu.
Mahari sioni shida yake sababu utazaliwa watoto, watabeba jina lako, watatunzwa, mke atakuhudumia n.k. na pia ni kama inarasimisha nafasi ya mwanaume katika familia sababu anayeolewa ndo analipiwa mahari.
Wahindi mwaume ndie anaye lipiwa mahari tuachane na hilo la wahindi.

Kwani mtoto wa kiume hajatunzwa na wazazi wake ?
 
Wahindi mwaume ndie anaye lipiwa mahari tuachane na hilo la wahindi.
Ni utaratibu pia, Je mtoto anabeba jina la ukoo wa mwanamke au mwanaume kwa wahindi?
Kwani mtoto wa kiume hajatunzwa na wazazi wake ?
Katunzwa ila nafasi yake katika jamii inamweka hapo kuwa alipe mahari, atoe ulinzi, malazi, afya na chakula kisha yeye azaliwe watoto, wabebe jina lake, mke amtunze na kulea watoto wake.

Wewe ulitaka utaratibu uweje? Usilipe mahari halafu mwanamke asifanyaje? Maana ni suala la nafasi ya mwanaume na mwanamke katika jamii na utaratibu sahihi wa kuhakikisha hizo nafasi zinaheshimiwa.

Sasa kama hutaki hiyo nafasi uliyopewa upo tayari kubadilishana na nafasi ipi kutoka kwa nafasi alizopewa mwanamke?
 
Back
Top Bottom