Hivi, wanaume mnaposema kuwa wanawake wa siku hizi tunapenda usawa huwa mnamaanisha nini?

Hivi, wanaume mnaposema kuwa wanawake wa siku hizi tunapenda usawa huwa mnamaanisha nini?

basi kumbe hapo ndo huwa mnakosea mwanaume sio kwamba akisema akili ya maisha ni kutafuat pesa akisema akili ya maisha ni mwamke anayelewa kwamba kuna kupata kuna kukosa na kuna mihangaiko mingi katika maisha na pengine kutokupata kabisa na uwezo wa kukubaliana na hali hiyo ndio akili ya maisha anayitaja mwanaume kwa sababu kwa mwanaume anayejielewa mwanamke kwake ni investment katika familia...japokua sikatai kuna wanaume ambao wanajifany awao ndio wanaolewa lia sio kwamba hawajui kutunza familoa ni jukumu lao ila ni ujinga tuu walionao...kuhusu kuosha vyombo ni kwamba hebu assume wewe ni ma awa nyumbani kazi yako ni kuweka mji safi na watoto waonekane ni wenye afya halafu unakaa mpaka jioni hujaosha vyombo mtu kaja amechoka kaleta pesa ya kula unamuambia aodhhe vyombo we unaona hiyo ni haki....ukija hoj y apili system ya maisha huku africa imabedilika sana unakuta wadada pia wanaenda shule wanasoma masters degree sasa mtu keshasoma je nikimuambia akae home aache kazi alee familia atakubal jibu ni hapana ...kwa au hata wewe assume mama kawapikia halafu kaondoka anakuta hamjaosha vyombo je alikua anaachekea?
Kama mwanamke ni mama wa nyumbani hatafuti pesa basi hastahili kusaidiwa majukumu yake na mumewe ila kama anatafuta pesa kwanini mumewe asimsaidie? Hivi wanaume mmeshajaribu kuvaa viatu vyetu na kujiuliza kuwa kama mngekuwa nyie mngeweza?

Imagine wote mnatoka alfajiri mnaenda kazini halafu wote mnarudi usiku lakini mume akirudi anakaa sebuleni miguu juu halafu mke anapitiliza moja kwa moja jikoni anaandaa chakula akimaliza anaosha vyombo halafu ndo mnaenda kulala hivi hiyo ni sawa kweli?
 
Haki saw inawezekn kwa wazungu especially Western counties lkin huku Africa asia icho kitu n ngum Sana
Pia nahic tamaduni tu tulizo zikuta mwanamke yupo responsible San n Kaz za nyumbn kulea watto n kadharika

Pia hi sio kwa binadamu t hata wanyama females animals are the ones provide foods for their children male are created to rule
 
Wanaume wa leo mnataka mpate wanawake wenye akili ya maisha na wanaojua kutafuta pesa ili wawasaidie katika kuhudumia watoto na mahitaji ya nyumbani lakini ninyi hamko tayari kusaidia kufanya kazi za ndani na kulea watoto sasa hapo hamuoni kuwa wanawake ndo wanakuwa wanafanya majukumu mengi kuliko wanaume? Kitu ambacho hakitakiwi maana mwanamke aliumbwa kama msaidizi tu kwa mwanaume
Katika maelezo yako nahisi umeshatambua kwamba wanawake waliumbwa "kua wasaidizi" vice versa is never true
 
Mnadai isawa wakati huo mnatutegemea tuwawezeshe na kuwahudumia.

Mmekuwa na katabia cha kupenda kushindana. Yaani nikifanya hivi na wewe ufanye vile.
Hiyo ni sababu ya mgawanyo wa majukumu yaani pesa tutafute wote ila kazi za nyumbani nifanye mimi peke yangu inakuja kweli hiyo? Ukielewa hilo utaelewa kwanini bado wanawake tunawategemea wanaume kiuchumi
 
Wanawake wanaopenda haki sawa ndo wanaotaka kuwa na wao wanakoroma kwenye familia.

Familia ambayo mwanamke anakoroma hiyo sio familia bora
Sasa kama mwanamke ndo anafanya majukumu ya mwanaume kwanini asikorome?
 
Katika maelezo yako nahisi umeshatambua kwamba wanawake waliumbwa "kua wasaidizi" vice versa is never true
Kwaio mama, kua msaidizi mzuri & enjoy the duty! Ndo mungu alikusudia iwe ivo,

Dont put much struggles kma vle kna mtu amekuonea. Thats nature.
 
Unaweza kuchimba kaburi?[emoji3]
[emoji2][emoji2][emoji2][emoji2]mkuu hapa tunaongelea majukumu ya kwenye familia kati ya baba na mama hata hivyo ndiyo wapo wanawake wanaochimba makaburi na hata kujenga nyumba pia japo mimi siwezi
 
Me naomba niwaulizeni nyote. Kwani mwanamke ukapata elimu yako, ukamaliza na kutafuta kazi na ukatapata,ukasave mshahara kwenye account yako, ukafanya usafi wa nyumba kila wakati, ukafua nguo za mume wako weekend, ukamheshimu mume wako kwa kusikilizana nae na kuongea nae kwa adabu na heshima na kumpa moyo wa kutafuta na hata akikwama ukatumia pesa yako uliyosave kulipia utility za familia, na ukawa muaminifu bila kujihusisha na mtu mwingine yoyote nje ya mume wako, hivi ukafanya yote haya unapungukiwa kitu gani....
 
Hiyo ni sababu ya mgawanyo wa majukumu yaani pesa tutafute wote ila kazi za nyumbani nifanye mimi peke yangu inakuja kweli hiyo? Ukielewa hilo utaelewa kwanini bado wanawake tunawategemea wanaume kiuchumi
Kwa hyo mkuu unataka tushinde jikoni, tufue, tudeki si ndio?


Daah wanawake mnaanza kutupanda vichwani
 
Nahisi nipo nje ya mada kidogo lakini sometimes wanawake tunajichanganya

Tunataka haki sawa kwa wote wakati huo huo tuna ile kauli mbiu yetu eti wanawake tukiwezeshwa tunaweza...SMH!😔😔

Kwanini tuhitaji kuwezeshwa wakati tuko na mikono na miguu miwili mixer ubongo kama wanaume
I normally say you’re very smart and wise..
 
Me naomba niwaulizeni nyote. Kwani mwanamke ukapata elimu yako, ukamaliza na kutafuta kazi na ukatapata,ukasave mshahara kwenye account yako, ukafanya usafi wa nyumba kila wakati, ukafua nguo za mume wako weekend, ukamheshimu mume wako kwa kusikilizana nae na kuongea nae kwa adabu na heshima na kumpa moyo wa kutafuta na hata akikwama ukatumia pesa yako uliyosave kulipia utility za familia, na ukawa muaminifu bila kujihusisha na mtu mwingine yoyote nje ya mume wako, hivi ukafanya yote haya unapungukiwa kitu gani....
hawezi kukuelewa hapa mkuu akili zao zimejaa mashindano wanataka kila kitu tufanye sawa
 
Hiyo ni sababu ya mgawanyo wa majukumu yaani pesa tutafute wote ila kazi za nyumbani nifanye mimi peke yangu inakuja kweli hiyo? Ukielewa hilo utaelewa kwanini bado wanawake tunawategemea wanaume kiuchumi
Kwa mwanamke kufanya kazi si lazima. Naweza kukustopisha na maswali sitaki.
Ila hali za sasa ndio kwa kiasi kikubwa huchangia haya yote.
Wote mna degree, pesa wote mnazo. Yaani automatically kuna ile akili huwaijia kuwa hanibabaishi(mwanamke ni chombo dhaifu). Hata kama haikuwa dhamira yako. Hapo ndipo kiburi huzaliwa na kujikuta unataka umpande.
 
Mimi siyo mjuzi ila ninaeleza kile ninacho elewa mimi.

Tunapoongelea usawa tunamaanisha tuondoe ule mnaouita mfumo dume kwamba binadamu wote ni sawa kitu ambacho si kweli. Mnaouita mfumo dume ni ule unaom favor mwanaume zaidi katika nafasi mbalimbali. Lakini kiukweli huo usawa mnaoulilia hauwezi kuja kutokea kwa sababu hata mkipewa nafasi bado hamtaweza kufanya vitu ambavyo mwanaume anafanya.

Mwanaume kaumbiwa roho ya ukakamavu, uvumilivu, na kujitoa muhanga katika hatari wakati huo mwanamke ana hali ya unyonge, kulia lia kila kitu na mwepesi kukata tamaa. Sasa mtu kama huyu anataka usawa na mwanaume.

Usawa tunaoulalamikia sisi ni ule wa kuingilia mipaka yetu achana hiyo uliyoongelea hapo.
I hail you my dude for this.
 
Umeongea simple Sana mkuu. Nilikuwa na mawazo light Sana kabla sijapata chance ya kulea ujauzito na mtoto mchanga. Nilipata kuona Kila step anayopitia mwanamke bro. Hicho kitu kina mkono wa Mungu na usishangae mtoto akipatwa na tatizo bhasi tumbo la uzazi humshika mwanamke ilhali MWANAUME unaeza kuwa unakula ulabu tu na wana.

Wanaume ni bread winners ila usicheze na life keeper.
So ulitakaje ss ikiwa Mungu alishawaumba Wanawake hivyo na kuwathibitishia watazaa kwa uchungu na watatawaliwa na Me daima na tamaa za Ke zitakuwa juu ya Me ilihali sisi Me tuliambiwa tule kwa jasho [emoji848]
 
But Edelyn, me sidhani kama hao wanaume wa kuachia mwanamke majukumu wapo wengi kiasi hicho. Na asilimia kubwa wanawake wanaopitia scenario za kulipia gharama za maisha bila msaada wa mwanamke huwa ni wale wanaochagua wanaume wa kuishi nao.

Ni mara chache sana mwanaume atakaye kufuata na kukutaka na kukuomba uwe wake atakutegemea wengi wanakuwa wapo tayari kukuhudumia na hata kama alikuwa hajiwezi ni rahisi sana kwake kuniongeza ili akufurahishe.

Golden rule ni mwanaume akuchague uwe wake, ila naona wadada wengi leo mnachagua wanaume wa kuwa nao az if mnachagua magari na mind you ukichagua mwanaume nakupa guarantee ni mara chache sana atakupambania maana wewe si chaguo lake ila ulikuwa available kwake na wanaume huwa hatuchagui chakula tunakula chochote kinachokatiza na kuzagaa mbele ya macho.
Kama hayo majukumu ni mepesi mbona wanaume wengi huwa mnayachukia? Tunasema umsaidie mkeo hayo majukumu endapo na yeye anakusaidia majukumu yako ila kama yeye hakusaidii majukumu yako basi haina haja ya wewe kumsaidia majukumu yake
 
Hakuna cha kupungukiwa..kiburi tu wakati mwingine

Ila tuseme tu ukweli kwa dunia ya sasa hakuna mwanamke wa kufanya yote hayo
Me naomba niwaulizeni nyote. Kwani mwanamke ukapata elimu yako, ukamaliza na kutafuta kazi na ukatapata,ukasave mshahara kwenye account yako, ukafanya usafi wa nyumba kila wakati, ukafua nguo za mume wako weekend, ukamheshimu mume wako kwa kusikilizana nae na kuongea nae kwa adabu na heshima na kumpa moyo wa kutafuta na hata akikwama ukatumia pesa yako uliyosave kulipia utility za familia, na ukawa muaminifu bila kujihusisha na mtu mwingine yoyote nje ya mume wako, hivi ukafanya yote haya unapungukiwa kitu gani....
 
Mimi naona hii haki sawa ilitokana na baadhi ya wanaume kutokutimiza majukumu yao kwa wake zao maana majukumu ya mwanaume ni kutafuta pesa na kuhudumia mke na watoto na majukumu ya mwanamke ni kufanya kazi za ndani na kulea mume na watoto ila kuna wanaume waliwanyanyasa wake zao kwa sababu walijua kuwa wake zao waliwategemea wao kwa kila kitu

Ndipo sasa wanawake wakaona kwanini wanyanyaswe wakati sisi wote ni binadamu basi na wao wakaona waanze kujitafutia pesa zao wenyewe ili wasinyanyaswe tena na ndipo haki sawa ilipoanzia sasa hii ni kwa upande wa kiuchumi

Haki sawa nyingine inayoongelewa ni ile ya kupendana, kuvumiliana, kusameheana na kuheshimiana na hii ilitokana na kwamba wanaume wengi hasa wa kiafrika wanataka wao tu ndo wapendwe, wavumiliwe, wasamehewe na waheshimiwe na wake zao ila wao hawana muda wa kufanya hayo kwa wake zao

Na wake zao wakikosea basi hao hao wanaume aidha watawapiga watawasaliti watawapa talaka au watawaongezea wake kwa kisingizio cha kuwa wao ndo wanatoa mahari kwahiyo wanaona wakishatoa tu hizo mahari kazi yao imekwisha kazi inabaki kwa mwanamke sasa kuhakikisha anafanya mengine yote kulinda ndoa je hiyo ni sawa?
Africa hatuna huo upumbavu bali yote hayo yameratibiwa na shetani kupitia Mawakala wake ughaibuni, ndiyomaana ss hv pamebakiwa na mvunjiko wa ndoa kwa kila mwaka ni zaidi ya 45%-67% hadi kuunda upya ndoa za mikataba.
 
Hakuna cha kupungukiwa..kiburi tu wakati mwingine
Me huwa nashangaa sana. Sababu hizi kelele zote huwa zinakuja kama watu wanaendekeza mashindano ya kitoto. Katika maisha ya ndoa kuna mambo mengi sana ya muhimu ya kufanya. Ukiona mwanamke unapata muda wa kurumbana na mume wako, na kufanya vituko, hebu jiulize ni nani anasimamia majukumu ya familia yaani household operations.... Na hilo ni jukumu kuu la mama.....

Ni sawa leo waziri mkuu atake kuwa sawa na raisi.... Haiwezekani in practicing ingawa ukiweka kinadharia inakuwa kama kweli.
 
Back
Top Bottom