Mpenzi, hivi umeshawahi jiuliza sehemu kubwa ya bajeti ya mwanamke kimatumizi huwa inaenda wapi?!Hiyo ni sababu ya mgawanyo wa majukumu yaani pesa tutafute wote ila kazi za nyumbani nifanye mimi peke yangu inakuja kweli hiyo? Ukielewa hilo utaelewa kwanini bado wanawake tunawategemea wanaume kiuchumi
Uongo uko wapi hapo mkuu? Kwani siku hizi wanaume si ndo mnawaita wanawake majina ya ajabu mara sijui wadangaji sijui wauzaji eti kwa sababu wanapenda pesa hivyo mnataka wajitafutie wenyewe siyo nyie?Uwongo hadi aliyekuumba anakushangaa unavyohalalisha unafki kuwa ukweli
Hivi akatokea kaka jambazi ghafla hapo unadhani nani atacheza nae twist?!Kama mwanamke ni mama wa nyumbani hatafuti pesa basi hastahili kusaidiwa majukumu yake na mumewe ila kama anatafuta pesa kwanini mumewe asimsaidie? Hivi wanaume mmeshajaribu kuvaa viatu vyetu na kujiuliza kuwa kama mngekuwa nyie mngeweza?
Imagine wote mnatoka alfajiri mnaenda kazini halafu wote mnarudi usiku lakini mume akirudi anakaa sebuleni miguu juu halafu mke anapitiliza moja kwa moja jikoni anaandaa chakula akimaliza anaosha vyombo halafu ndo mnaenda kulala hivi hiyo ni sawa kweli?
Binadamu tumeshawekewa sheria na amri na Mungu aliyetuumba tuzifuate rejea maandiko usitake kuanza kutolea mifano ya wanyama kwa sababu tu inawafaidisha wanaume hilo siyo lengo la Mungu binadamu na wanyama ni aina mbili tofauti ya viumbeHaki saw inawezekn kwa wazungu especially Western counties lkin huku Africa asia icho kitu n ngum Sana
Pia nahic tamaduni tu tulizo zikuta mwanamke yupo responsible San n Kaz za nyumbn kulea watto n kadharika
Pia hi sio kwa binadamu t hata wanyama females animals are the ones provide foods for their children male are created to rule
Hiyo hali imehatarisha sana ndoa za Watu hadi kufikia hatua Wanaume tunaogopa sana Ke wenye kazi zao, elimu 7bu hujawa na viburi na hata hawajali Waume zaidi ya kuangalia mahitaji yao wenyewe.Dearest one. Movement ya kudai haki sawa haikusababishwa na mtu yoyote kutokutimiza majibu yake Bali ni ile Hali ya kunyanyapaliwa au kunyimwa fursa kutokana na jinsia ya muhusika.
Wanawake zamani hawakupewa fursa ya elimu, umiliki wa mali Kama ardhi au hata Haki ya kurithi mirathi ya waume zao . Pia kulikuwa na mifumo ambayo inahalalisha kunyanyasa wanawake Kama mifumo ya sheria na physical abuse. Hivi ndivyo vitu vya mwanzo kabisaa kupiganiwa
Mliokidaka hiki kitu juu juu bila kuielewa ndio mnaona Ni movement ya kutaka usawa na wanaume badala ya FURSA NA HAKI SAWA.
Kwahiyo wewe ulitaka tuweje mkuu? Mbona wanawake tukitafuta pesa hamlalamiki ila tukifanya mambo mengine ndo mnalalamika?Ndiyomaana kila kukicha yanabaki kulia lia kuachika ktk ndoa 7bu yameiga utamaduni wa kipumbavu toka nchi za magharibi nakati Bibi na Mama zetu hawakuwa hivyo ndiyomaana wadumu sana ktk mahusiano ya mapenzi na ndoa.
Mmmmmmhmn hapa sasa utakuwa unalenga kuachieve nini zaidi yaani?! Kama ni kuelemewa na kazi tafuta msaidizi mzee atalipia mshahara wake.Mkuu sijui kama umenielewa nimesema mwanaume amsaidie mke wake kufanya kazi za ndani ikiwa huyo mwanamke anamsaidia mumewe kutafuta pesa ila kama hamsaidii basi na yeye asimsaidie? Hivi kwani wanaume ni kipi kinachowawia vigumu kufanya hizo kazi? Mtabadilika jinsia?
Ndiyo na kwa maana hiyo mfanye juu chini muhakikishe wake zenu hawafanyi majukumu mengi kuliko nyie yaani eti wewe utafute pesa tu ila mke wako atafute pesa na bado afanye kazi za ndani ni haki hiyo kweli?Katika maelezo yako nahisi umeshatambua kwamba wanawake waliumbwa "kua wasaidizi" vice versa is never true
π...Nahisi nipo nje ya mada kidogo lakini sometimes wanawake tunajichanganya
Tunataka haki sawa kwa wote wakati huo huo tuna ile kauli mbiu yetu eti wanawake tukiwezeshwa tunaweza...SMH!ππ
Kwanini tuhitaji kuwezeshwa wakati tuko na mikono na miguu miwili mixer ubongo kama wanaume
Balimi mkuu
Hahahaha uko sawa mkuu hatupungukiwi kitu ila kwani na wanaume nao wakitafuta pesa na bado wakasaidia wake zao kazi za nyumbani wanapungukiwa kitu gani?Me naomba niwaulizeni nyote. Kwani mwanamke ukapata elimu yako, ukamaliza na kutafuta kazi na ukatapata,ukasave mshahara kwenye account yako, ukafanya usafi wa nyumba kila wakati, ukafua nguo za mume wako weekend, ukamheshimu mume wako kwa kusikilizana nae na kuongea nae kwa adabu na heshima na kumpa moyo wa kutafuta na hata akikwama ukatumia pesa yako uliyosave kulipia utility za familia, na ukawa muaminifu bila kujihusisha na mtu mwingine yoyote nje ya mume wako, hivi ukafanya yote haya unapungukiwa kitu gani....
Ndiyo na kwa maana hiyo mfanye juu chini muhakikishe wake zenu hawafanyi majukumu mengi kuliko nyie yaani eti wewe utafute pesa tu ila mke wako atafute pesa na bado afanye kazi za ndani ni haki hiyo kweli?
Kwani hauwezi? Unaweza ila kwanini unataka ufanyiwe? Basi kama hautaki kuyafanya tafuta pesa hudumia mkeo hata kama yeye anaweza kutafuta pesa na anatafuta pesa wewe achana na pesa zake mhudumie kama jukumu lako na uache kulalamika kuwa wanawake wanapenda pesa wewe hudumia tuKwa hyo mkuu unataka tushinde jikoni, tufue, tudeki si ndio?
Daah wanawake mnaanza kutupanda vichwani
But at the same time you want us to take care of you especially in the financial matters. hapa ndo nliposhindwaga kuwaelewa ni 50/50 gani mnayoitaka!Tatizo ni mgawanyo wa majukumu wanaume hawataki kufanya majukumu yetu ila wanataka wanawake tufanye majukumu yao na matokeo yake wanawake tunajikuta tunafanya majukumu mengi kuliko wanaume something which is not fair I think.
Unajua mimi sidhani kama kuna wanaume waliokamilika wanatafuta wanawake kwaajiri ya kutafuta nao pesa. Bali wanaume waliokamili wanataka wanawake wenye uelewa na hali ya maisha aidha awe na kipato ama la.Sawa kwahiyo mwanamke kukusaidia wewe kutafuta pesa ndo sawa?
Hao wachache ndiyo wanaokula mema ya wake sasa.Unajua kwanini wanasema hivyo? Kwa sababu wameshaaminishwa kuwa wanaume hamtakiwi kufanya hayo majukumu ila wanaume mngeonyesha nia ya kuyabeba hayo majukumu na kuyafanya kama ya kwenu hakika jamii ingezoea tu
Take this from me hakuna mwanamke asiyependa kusaidiwa ikiwa yeye anasaidia hao wanaosema mume bwege sijui kawekwa kiganjani ni exceptions chache tu ni sawa na uwepo wa wanaume ambao hawataki kabisa wake zao watafute pesa (ambapo wanaume wa hivyo siku hizi wapo wachache ukilinganisha na wanaotaka)