Hivi, wanaume mnaposema kuwa wanawake wa siku hizi tunapenda usawa huwa mnamaanisha nini?

Hivi, wanaume mnaposema kuwa wanawake wa siku hizi tunapenda usawa huwa mnamaanisha nini?

Mkuu kuwa realistic sawa anauwezo mkubwa sana na mm nakubali kama kubeba kiumbe mieezi tisa....... lakini jiulize hicho kiumbe anachobeba kajipa mwenyewe? Mind you Kuna aliesababisha kiingie na kukaa tumboni mwake.

Kikubwa nadhani tunapaswa kuelewa/kuelewani kuna suala muhimu sana la haki na wajibu kwa mke na mume. Hivi vitu ni nature ya muumba na hata ukipingana navyo ni kama kushindana na ukuta. Mume ana wajibu kwa mkewe na mke nae vivyohivyo. Sitaki kusema haki ya nani inamzidi yupi hilo linataegemeana na misingi mbalimbali ikiwemo ya imani za dini ambapo jamii husika ipo. Kuna jamii kabisa mke yupo juu ya mume mfano wao ndiyo walipa mahari na wanaolewa na wanaume zaidi ya mmoja. Mwanamke kwa maana rahisi anakuwa na mitala.... yaani anapanga lini nikalale na mume yupi.

Hivyo ndiyo maana tangu awali nilisema haya mambo kuyajadili na kuyapatia jibu la uhakika ni ngumu sana. nilitoa mfano wa ukristo ukifundisha kuwa wajibu wa mume ni kumpenda mkewe na mke ni kumtii....sasa tafuta kwa kina maana ya KUPEND na maana ya KUTII kuna baadhi ya watu wanaweza kuikana imani kabisa. Lakini pia nikasema baadhi ya jamii/makundi Ulaya na America wao wana ndoa za mikataba yenye makubaliano ya lini ndoa itaisha, itaishaje na hata namna ya kuishi ndani ya hiyo ndoa ikiwa ni pamija na mtu kuja na mchepuko wake nyumbani siku akijisikia bila kubughudhiwa na mwezake.

Kwa ujumla haya mabo yanahitaji mtizamo mpana sana ili kujua hiyo 50/50 inaweza apply kwa kundi gani na wakati gani.
Suala la nani awe nani katika suala la uzazi liliwekwa na Mungu na kila jinsia ikapewa quality maalumu kwa ajili ya kutekeleza jukumu lake; mwanamke amepewa role yake ambayo huwezi kuilinganisha na mwanaume katika hili ukilifikiria kwa kina lakini

Suala la balance ni la kinadharia sana haswa katika nchi zetu za kiafrika ambazo zinaishi kwa misingi ya kidesturi na kidini ambayo kwa kiasi fulani ipo kinyume na hiyo concept
 
Sawa ila kama yeye anakusaidia kutafuta pesa basi na wewe ni wajibu wako kumsaidia kufanya kazi za ndani
Tatizo mke akishakuwa provider tu shida inaanzia hapo

mimi laziama nitoe zaidi yake
 
Mkuu huyo kwenye avatar ni wewe? [emoji470][emoji470][emoji470][emoji470][emoji470][emoji470]
Siyo yeye. Labda ni shangazi au mama wa ubatizo. Yeye ni chuma hatari. Trust me. Kuna avatar yake ya kweli bado naitafuta nitakupa nikiipata [emoji16][emoji16][emoji16]
 
Na wewe za kwako huwa unampa??

Yes madam ninampa na hata akiniambia bana sikiliza this time hela yangu nafanyia hiki naomba uniongezee pesa kadhaa kiroho safi anachuku

Anajua exactly role zake na anajua ana deal na mtu mwenye mind set ya kibabu anafuata mule mule
 
Sawa ila kama yeye anakusaidia kutafuta pesa basi na wewe ni wajibu wako kumsaidia kufanya kazi za ndani

Mama narudia tena kazi za ndani sina wajibu nazo na ndo maana siwezi kuhangaika na nyinyi wanaharakati

Ninyi wa haki sawa ni wa kuweka tu na kusepa
 
Kwa namna moja ama nyingine mkuu unasisitiza mwanamke amtii mwanaume

Utii maana yake lazima mke awe chini ya mume

hapa unamaanisha mwanaume ndo muamuzi sio

Yaani hata kama majadiliano yakishindkana inabidi wazo la mwanaume lifuatwe si ndio mkuu ee

Yaani ni hivi Baba abaki kuwa baba na awe provider si ndio

Mama yeye afanye kazi zake za kuwa mwangalizi wa familia hata kama ana kazi si ndio

nimekuelewa mwanangu

sorry pale juu nilikuletea noma mzee

najua umenisamehe mkuu
Unajua mkuu kuna watu wengi sana hata bible hawaielewi vyema. Ni kweli kwa upande mmoja inasema Mume ni kichwa cha nyumba. Na tafsri ya wengi hapa inaangukia kwenye supremacy...kwa maana ya mwenye nguvu na mabavu juu ya mke....kitu ambacho kiuhalisia si kweli. Kuna jukumu ambalo mwanaume amepewa la upendo kwa mke... kama watu wakilielewa hili vizuri lenyewe tayari linaweka usawa katika mahusiano ya ndoa na wala si kumuweka mwanaume kama mtawala wa mwanamke. Wakorintho wa kwanza 13:4-8 inasisitiza kabisa kuwa upendo huvumilia, upendo hufadhili, upendo hauna wivu au majivuno. Upendo hauna kiburi na haukosi kuwa na adabu. Upendo hau tafuti kujipendeza nafsi, haukasiriki upesi, hauweki orodha ya mabaya, upendo haufurahii mabaya, bali hufurahia kweli. Upendo huvumilia yote, huamini yote, hutumaini yote, hustahim ili yote. hivyo basi wanaume kujiinua kuwa juu ya wanawake kinyume na haya maandiko wanataka utukufu wao tu si wa kimungu.

Hivyo basi kwa wana ndoa mume anapokuwa na upendo wa dhati kama andiko linavyosema ukachanganya na andiko la utii analotakiwa kuwa nalo mke kwa mume....ndugu yangu raha inayopatikana kwenye couple hiyo ni kama paradiso. Maana kila mmoja anawajibu kwa mwenzake....mume akigawiwa pipi na rafiki zake huko njiani ni lazima ifike nayo kwa mkewe ili wakamege kwa pamoja. Mke hawezi fikia maamuzi ya jambo lolote lile lazima akamshirikishe mume na mume kwa sababu ya upendo lazima amshauri kwa busara na hata kama hakubaliani nalo sana kwa ajili ya upendo atamkubalia mkewe ili tu kutoikwaza nafsi na furaha yake. kosa hutokea pale tu mmoja anapotaka ku abuse nafasi na jukumu lake alilopewa.

Ku declare interest tu mm ni muumini wa usawa wa jinsia. lakini kuna baadhi ya mambo nayaunga mkono na mengine nayapinga. kwa mfano mila potofu dhidi ya wanawake ziwanyimazo fulsa ya elimu, ukeketaji, kuwapora wajane mirathi, kurithi wajane, kuwapa wanawake kazi kwa rushwa ya ngono n.k haya mimi sikubaliani nayo kabisa. Lakini pia sikubaliani na propaganda za wanaharakati wa jinsia wasio na maelezo ya kina wao wameshikilia tu kwa mfano mwanamke ana haki ya kuamua mambo yake ikiwa pamoja na lini ampe mumewe unyumba. Au kulazimisha tu nafasi zote ktk jamii zigawanywe kwa 50/50 bila kuzingatia uwezo na taaluma.

Lakini narudia tena hili masuala ya usawa wa jinsia ni yana mjadala mpana sana kulingana na imani tofauti za dini, mila na utamaduni wa jamii husika hali kadharika maeneo ya kijographia katika ulimwengu huu.
 
MMMH MAMBO HAYA NI MAGUMU SANA DADA YANGU....

KWA KWELI DUNIA YA LEO LINAPOKUJA SWALA NA USAWA KATI YA MKE NA MUME NI MJADALA MPANA SANA NA WAKATI MWINGINE UNAKOSA MUAFAKA KUTOKANA NA MAKUNDI AMBAYO NI WAHUSIKA KATIKA HILI.

KWA UFUPI TU MAKUNDI KAMA YA IMANI ZA DINI, WANAHARAKATI WA MASUALA YA JENDA NA MAKUNDI YASIYOSOMA NA YALIYOSOMO WANATOFAUTIANA SANA KIMITIZAMO NA KUNA NAMNA TOFAUTI TOFAUTI ZA UFANYAJI WA MAKOSA UYASEMAYO NA HATA KAMA YAKIFANYIKA UTATUZI WAKE PIA HUTOFAUTIANA.

MFANO KATIKA UKRISTO KUNA BAADHI YA MAKOSA HAYARUHUSIWI KUFANYWA KABISA..... MAKOSA KAMA UZIZI, ULEVI NA UGOMVI HAYARUHUSIWI KABISA. NA MSISITIZO NI MUME KUMPENDA MKE NA MKE KUMTII MUME. MTU AKIMPENDA MKEWE KATIKA MAPANA YAKE NA KWA MAANA YAKE HATAWEZA KUZINI, KULEWA, KUMPIGA NA KUTOMSHIRIKISHA KWENYE JAMBO LOLOTE LILE. VILE VILE NA MKE AKIMTII MUME HATAWEZEKANA KUDAI KIITWACHO HAMSINI KWA HAMSINI KATIKA NYUMBA WALA KUINUA MDOMO MREFU KAMA SAMAKI CHUCHUNGE NA KUMSONYA MUMEWE HATA KAMA KAMKOSEA. MAMBO YAO HUMALIZWA KATINA NAMNA YA KIMUNGU KWA HOFU NA UTII.

NA UKIKUTANA NA KUNDI LISILOMJUA MUNGU NALO LINA NAMNA YAKE WANAVYOCHUKULIANA KATIKA NDOA NA MAHUSIANO HALIKADHARIKA MIFUMA YA KISOMI HUSUSANI YA KIMAGHARIBI AMBOA WANA HADI NDOA ZA MIKATABA AMBAPO MKATABA UNAWEZA SEMA SIKU UKINIKUTA NA MCHEPUKO WANGU USINIGUSE WALA KUNINYOOSHEA KIDOLE. KTK ULIMWENGU WA UISLAM MWANAMKE HAWEZI KULALAMIKA KUHUSU KUTOFANYA KAZI NA KUKAA NDANI TU NA WALA KUTOENDESHA MAGARI (KAMA VILE SAUDIA....JAPO SASA HIVU KUNA MSUKUMO USIO NA NGUVU WA KUTAKA KUWAPA WANAWAKE FURSA MAGARI YA KUENDESHA NA KUSHIRIKI MCHAKATO WA UCHAGUZI ILI WAPIGIWE KURA) KAMA ILIVYO KWA WANAUME. IMANI NA MAFUNDISHO YAKE YANASEMA HIVYO NA HALIWEZI KUHOJIWA. UCHAGANI MTOTO WA KIKE HAKUWA NA NAFASI TANGU DAHARI KURITHISHWA KIHAMBA KAMA WARITHISHWAVYO WANAUME.

HIVYO BASI USAWA HUO UUZUNGUMZIAO UNATEGEMEANA SANA NA MAKUNDI NA SALSAFA HUSIKA ZA MAKUNDI HAYO KUHUSIANA NA SUALA LA NDOA. USIPOYAELEWA HAYA MAMBO NA KUKUELEKEZA KUWA UNAINGIA KWENYE NDOA AU MAHUSIANO NA KUNDI LIPI UTAYUMBA SANA KTK MAHUSIANO YAKO.
Ni kweli sio kweli pia. Kwa kifupi tu, hata mtazamo wa kale wa jamii nyingi ulifanana na mtazamo wa kiimani. Mfano mjane kurithiwa, mwanamke kutorithi mali wala kuajiriwa, majukumu ya mtoto wa kike vs wa kiume n.k. Tatizo lililopenyezwa ni mfumo wa kimagharibi. Tunatumikia matakwa ya wageni ndio maana tumepotea kama taifa. Tumeukana utamaduni wetu
 
Back
Top Bottom