Hivi zile Scania benz za kampuni ya Azam (approximately) zinauzwa shs ngapi?

Hivi zile Scania benz za kampuni ya Azam (approximately) zinauzwa shs ngapi?

Zile ni gari za Azam nyingi ni International bwana si Benz ama Scania kama mtoa mada alivyosema. International ni gari ya kimarekani hiyo inakimbia sana hata ikiwa kwenye mzigo. Ukiwa na basi huwezi kuacha mbali na ikikutangulia ufanye kazi kuiovertake
 
Zile ni gari za Azam nyingi ni International bwana si Benz ama Scania kama mtoa mada alivyosema. International ni gari ya kimarekani hiyo inakimbia sana hata ikiwa kwenye mzigo. Ukiwa na basi huwezi kuacha mbali na ikikutangulia ufanye kazi kuiovertake

Mkubwa nenda kacheki tena hana international hata moja. Ile unayoiona ni Volvo VNL 12 470 mpaka 500 Horse power from america convetional cabin.
 
Mkubwa nenda kacheki tena hana international hata moja. Ile unayoiona ni Volvo VNL 12 470 mpaka 500 Horse power from america convetional cabin.

International anazo yule jamaa wa TRH tena mpya.. Na za kutosha.. Biashara hii inahitaji moyo.. Ni pasua kichwa hasa kama pesa zako za mawazo
 
ushauri wa bure tafuta kiwanja maeneo ya kibaigwa,ubaruku,mtwara,mkuranga,mafia jenga hotel ka vyumba 10 self,kuwe na restaurant bed & breakfast kuwe na parking hutajutia!!!ipo siku utanikumbuka

hahahaha umenivunja mbavu:becky:
 
International anazo yule jamaa wa TRH tena mpya.. Na za kutosha.. Biashara hii inahitaji moyo.. Ni pasua kichwa hasa kama pesa zako za mawazo

Yeah yataka moyo. TRH anazo international nyingi ila ndo wamejikita mizizi miaka mingi wale wahindi enzi hizo Biashara ilikua rahisi siku hizi Biashara hiyo imeingia mkono labda uwe na pesa za Escrow
 
Kama umeamua kuwekeza kwenye biashara ya magari makubwa usiwe na presha wala haraka. Usitaraji makubwa sana kwenye biashara hii,utasifiwa tuu kwamba una mende mbili tatu ila itakuwa siri yako. Kila la kheri.
 
Asante sana mkuu...naona leo ulikuwa na hamu ya kutukana na kweli umefanikiwa.....
Ninachokukumbusha ni kwamba aliyekujaalia wewe mgao wa escrow ndio katunyima sisi....wakati wewe unawaza ule chakula cha aina gani ,wengine tunawaza tutakula nini maana tumakula tunachopata na sio tunachotaka....
Wakati wewe unatupa chakula kilicho lala.....
Kuna mtu mwingine anakufa na njaa....
Wakati wewe unamnunulia kimada wako zawadi ya gari, kuna mtu anakaribia kukata roho kwa kukosa hela kwa ajili ya matibabu......wakati wewe unamwagilia maua maji safi na salama kwa kunywa ,kuna mtu anakunywa maji ya mtaroni.....
Ninachokukumbusha ni kwamba duniani hatulingani........hayo maneno uliyoyaandika ni ya mtu aliyevimbiwa na shibe na kamwe hatamkumbuka mwenye njaa.....wakati wewe unanishangaa kumaliza mwaka wa tatu kudunduliza hela ya baiskeli kuna watu wanamaliza mwaka wa nne wanatafuta hela ya kandamabili.......hii ndio dunia....

such a wise comment, kudos
 
Japo sina hata baiskeli ila haya mambo ni muhimu kuyajua just for knowledge, naweza nikajua wenzangu waishio dunia ya kwanza ndani ya Tanzania wanaishi vipi
 
bandarini kwenu pamejaa wezi sana! rushwa bado tra wanakupiga za kutosha ndiyo maana tumewahama
Asante kwa taarifa maana kuna mzigo natarajia kuuagiza toka Japan hivyo nitaku pm kwa msaada zaidi.
 
Kama umeamua kuwekeza kwenye biashara ya magari makubwa usiwe na presha wala haraka. Usitaraji makubwa sana kwenye biashara hii,utasifiwa tuu kwamba una mende mbili tatu ila itakuwa siri yako. Kila la kheri.

Kweli kabisa labda utumie gari hizo kupakia mizigo yako binafsi au company yako lakini ni pasua kichwa
 
Sikushauri ujiingize kwenye haya matruck mm nina track mbili mende nilinunulie uingereza na moja niliinua kwenye mradi fulani bressuls zote zilikuwa zina km 70000 ni scania ila biashara kwa huu upande wa bagamoyo hamna kitu kabisa springi kila siku tanroads ndio usisema najikuta gharama za uendeshaji ni kubwa kuliko kinachoingizwa na haya magari
 
Bora uuze tofali kuliko kununua haya matruck ndio hata st abri aliamua kumuachia ndugu yake aendele yy kajikita kwenye spea
 
We mavi kweli ..scania benz ndio nini? Kwenda huko na akili zako za kupoga vidufu unashindwa hata kujua scania na benz ni brands mbili tofauti....

Hakukuwa na sababu ya kumtukana mleta mada kias hicho.
Kukosea si jambo baya
 
Back
Top Bottom