Hiyo fedha unayoihangahikia na kuitolea macho kila ipo siku utagundua kuwa fedha si lolote, si chochote, ni suala la muda tu

Mwamuzi wa Tanzania

JF-Expert Member
Joined
Apr 7, 2020
Posts
15,486
Reaction score
45,256
Nimeona watu wenye fedha waliotumia zaidi ya milioni 100 kujitibu lakini fedha haikufua dafu wakafa.

Nimeona matajiri ambao kila mtu angetamani kuwa kama wao lakini hao Matajiri hawajawahi kupumzika hata wiki moja kuitafuta fedha.

Hii maana yake zile fedha zao mamilioni na mabilioni bado hayajaweza kuwapa jawabu la maisha. Wanaendelea kutafuta pesa na hawatapata jawabu na utulivu mpaka kifo kiwakute
 
Mawazo ya kimaskini...
 
Fedha inarahisisha maisha sana sehemu yeyote duniani. Ukiwa na fedha ukipata shida unatumia akili kidogo tu unatoboa.
 
Nimeona Maskini waliovaa nguo zilizochakaa sababu hawana PESA ya kununua nguo mpya.

Nimeona watu waliokufaa njaa sababu ya kukosa pesa ya kununulia chakula.

Nimeona wagonjwa waliokosa matibabu sababu hawana pesa ya kulipia.


Tatizo si Pesa.
tatizo ni pale unapohitaji huduma au kitu na hauna Pesa ya kulipia hicho kitu.(maskini)

Au una pesa ila unachokihitaji hakipo.(Tajiri)
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…