Hizi hotuba za kisiasa za Rais Magufuli zitatuponza. Tuchague mambo ya kusema hadharani

Hizi hotuba za kisiasa za Rais Magufuli zitatuponza. Tuchague mambo ya kusema hadharani

Kwani huyu Jamaa yetu wazungu walimfanyaje na kwanini anataka kutuaminisha watu wote kuwa wazungu ni maadui zetu?
Niliwahi kuandika na ninarudia tena. Wazungu si rafiki zetu hata siku moja. Kila wanachotupatia wana malengo nacho na ni kwa manufaa yao 99%.

Kama wangekuwa na nia njema wasingeua wataalamu wa Afrika wanaojaribu kuweka tafiti zao zenye matokeo mazuri kama vile madawa ya tiba za binadamu.

Wasingebuni chanjo kama zile za kikanda kama za saratani ya shingo ya kizazi, amabazo baadhi ya nchi wamegundua zina kemikali za kuzuia uzazi kwa wasichana au kusababisha mimba kuharibika. Tnapewa chanjo hizo kimyakimya ili iweje.
 
Wewe mbona hujielewi? Nimetoa fact ya kwa Nini vaccine ya covid inatia mashaka lakini naona hiyo hujaiona.
Unauliza viongozi wa Afrika kuunga mkono kaulli ya Magufuli? Nani ana ubavu wa kuwachallenge mabeberu zaidi ya Magufuli, viongozi wengi wa Afrika ni wanafiki.

Mimi nimepitia comments za waafrika kwenye mitandao ya kijamii, wengi wameunga mkono kauli ya JPM.
Yeye mwenyewe ni mnafki. Mabeberu hao hao almost technologia.. madawa..mfumo wa elimu yetu ni modified copy cat na rip off kutoka ya uingereza.

Bidhaa kibao tunachukua kutoka kwao?
Hivi unadhani hawa jamaa wakitaka kutumaliza serious unadhani wanashindwa?
Halaf baadae tena tunaanza kupiga sera ya kuwavutia wawekezaji.. wawekezaji wenyewe wa nje ndio hao mabeberu.

Yaani sitaki nataka zinakuwa nyingi.
Kama kweli hawapendi mabeberu. Aondoe wawekezaji wakigeni..
Akatae dawa zote zinazotoka nje.. bidhaa yoyote inayotoka nje ipigwe marufuku.
Sio kuoiga porojo majukwaani
 
Aweke akiba ya maneno
1. Hiyo korona ikichachamaa mtaani kwelikweli na kuanza kukwangua hadi wateule wake na familia zao na yake hiyo lockdown anayoikataa ataiweka tu.

2. Korona ikipiga haswaa, hiyo chanjo ataikubali tu

Ukiwa raisi chagua na pima maneno, na uweke akiba ya maneno!, maana ukiwaaminisha watu kitu fulani halafu baadae ukafanya opposite hakuna atakayekuchukulia serious tena!
 
Tunaweza tukasikilizwa au hapana, ukweli ni kwamba rais anatakiwa kusaidiwa jinsi ya kuchagua maneno ktk majukwaa ya kisiasa. Tunaona jinsi Rais anavyotumia jukwaa na kujisahau kwamba maneno ya rais hutafsiriwa na ofisi zote nchini na kuvuka mipaka....
Uwezo wa Magufuli wa kuelewa na kupambanua mambo ni mdogo mno; Korona nayo imemsamehe sana, Inatakiwa imchape ili tuone kama ataendeleza mzaha wake huu wa kijinga
 
Urais sio cheo cha kuonyeshea mapenzi na mapungufu ya mtu, labda hujui unaongea nini.
Nyie mnaojua kuongea mbona bado mnaishia kuwa na maisha mabaya Tu......kuongea kote na mkeo anafanana na Bibi yako......kuongea kote bado wewe ni punguani.......kuongea kote bado upo upo Tu kujifanya mjuaji akati ujui unacho kijua.......nyie ndio ambao kinga tunawachoma matakoni Kwa kihere here
 
Niliwahi kuandika na ninarudia tena. Wazungu si rafiki zetu hata siku moja. Kila wanachotupatia wana malengo nacho na ni kwa manufaa yao 99%. Kama wangekuwa na nia njema wasingeua wataalamu wa Afrika wanaojaribu kuweka tafiti zao zenye matokeo mazuri kama vile madawa ya tiba za binadamu. Wasingebuni chanjo kama zile za kikanda kama za saratani ya shingo ya kizazi, amabazo baadhi ya nchi wamegundua zina kemikali za kuzuia uzazi kwa wasichana au kusababisha mimba kuharibika. Tnapewa chanjo hizo kimyakimya ili iweje.
Umasikini wa akili na kipato unawatesa sana
 
Nyie mnaojua kuongea mbona bado mnaishia kuwa na maisha mabaya Tu......kuongea kote na mkeo anafanana na Bibi yako......kuongea kote bado wewe ni punguani.......kuongea kote bado upo upo Tu kujifanya mjuaji akati ujui unacho kijua.......nyie ndio ambao kinga tunawachoma matakoni Kwa kihere here

Kwamba tuna maisha mabaya! Duuu, basi kazi ipo.
 
Hizi chanjo mpya mpya utakiwi uziamini kwa % 100, lakini haifai kuzibeza hata kidogo, mana chanjo za wazungu kama ya polio pepopunda tumezitumia tangu tukiwa wadogo na tumeona matokeo yake.

Ila kwa sababu papa le nambari wan mukubwa ya kijani, mkemia mkuu, mbeba maono, kaoteswa kwamba chanjo ni mbaya sasa sisi ni nani hata tupinge.
 
Maneno ya Lissu yanaendelea kila kukicha kwamba tuna Rais......."
 
Magufuli ni Raisi wa aina yake, siyo mtu wa kumumunya maneno kuogopa mabeberu watamfikiriaje. Kwa Africa hadi sasa sijaona Rais mwenye uthubutu Kama huo, maraisi wengi wa Africa ni wanafiki wanaojipendekeza kwa mabeberu wakiogopa kusitishiwa misaada...
Fungua Aljazeerah uone jinsi walivyomshangaa na kumwona kuwa ni mwendawazimu mmoja amekaa ikulu huko Africa. Acheni ujinga hiyo misimamo yake aipeleke nyumbani kwake awaache wananchi wajipiganie afya zao. Ebo
 
Kwa taarifa yako huu msimamo wa leo wa Magufuli umekuwa gumzo Afrika in a positive way, watu wengi wamekubaliana na msimamo wa Magufuli.
Nimependa hadithi yako. Lakini pia usipende sana kusema watu wengi. Hao wengi ni watu wa aina gani? Tatizo siyo wingi, ni ubora wa hao wengi.

Mi napenda sana ukweli wa Magufuli na ukweli huo ubaki hivyo hivyo! Tukumbuke pia siku za mwanzo, Kuna mfaransa alitaka majaribio ya chanjo yafanyike Africa hadi kufikia Mkurugenzi wa WHO kufoka.

Majaribio kwa waafirka yamefanyika mara nyingi sana tena kwa bei nafuu sana kwa baadhi ya watendaji wa serikali. Ni ktk kila nyanja! Hata ktk vyakula. Kilimo cha GMO nasikia kumbe kuna mbegu kibao zinaingizwa kinyemela kwa msaada wa watendaji wa serikali.
 
Ukiwa na akili za kitumwa ndio utakua muoga kuzungumza unachokiamini.
 
Kuna hatari wayanzania kwa uzuzu wao wakaacha kuwapeleka watoto wao kupata chanjo...sababu zipo feki

Taifa kitapukutika kama upupu!!
 
Hivi kwa nini huwa haruhusu maswali kama wenzake kina Biden?

Sent from my moto g power using JamiiForums mobile app

atajibu nini ndugu yangu ? ye anajua kukaripia na kutoa amri za kipuuz imagine jana kamwona mtu anasukumana na watu kwenye umati wa watu waloenda kumsikiliza akaamuru akamatwe apelekwe jela eti anafanya fujo, alivyosema ivyo watu wengine wakaona nasisi tusije tukakamatwa wakaanza kuondoka akaona noma akasema huyo mlomkamata mumsamehe , ndio rais wa kwanza naona anafanya hivi, hii hata sijui imekaaje , ni standard procedure kweli hii ?
 
Labda Jamaa walimfanya kitu wakati alipopita ujerumani,maana chuki zake kwa mzungu hazina tofauti na chuki za Hitra kwa wayahudi,sema tu hana uwezo ila wazungu wangekoma

Dah hatari sana
 
Huyu mzee angeweka msisitizo labda kwenye hizo tiba mbadala kama mambo ya lishe na hayo ya kujifukiza mivuke

Lakini kuwaponda Wazungu na chanjo zao ni kutaka na kutuingiza ktk uhasama na spotlight ambazo hazina umuhimu wowote zaidi ya kutengenezeana mizwenge tu kujihusisha na Dunia baadae hapa rejea katazo la kuingia UK ( yatakuja mengi tu haya)

Kingine nashangaa kusema Mungu wetu yupo na ni hai ni kama wengine wame msahau na hawana kabisa huyo Mungu na mbaya hata yeye kumjua huyo Mungu alie hai ni huyo huyo Mzungu kasababisha hapo ndo tunaonekana Waafrika tuna shida kiasi, angeweka mkazo labda kwenye tiba mbadala kumuingiza Mungu tena naona kama ni kujichanganya tu

( Huko Roma/Vatican wanahenyeshwa na huyu mdudu hivi yeye ndo mtakatifu zaidi ya viongozi wake kina Papa) mantiki ya Mungu alie hai haina mashiko

Kama anataka kuutetea u Afrika akomae na dawa asilia aachane na issue ya Mungu alie hai sijui
 
Back
Top Bottom