Hizi milioni 700 za Rais Samia kwa Taifa Stars, zinawahusu wachezaji walioitwa mara ya mwisho kufuzu AFCON 2025 au mgao ukoje?

Hizi milioni 700 za Rais Samia kwa Taifa Stars, zinawahusu wachezaji walioitwa mara ya mwisho kufuzu AFCON 2025 au mgao ukoje?

Waufukweni

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2024
Posts
2,060
Reaction score
5,648
Wakuu

Jana Rais Samia kutoa milioni 700 kwa Taifa Stars baada ya kufuzu AFCON 2025 kama pongezi kwa kuliheshimisha taifa kufuzi mara ya nne katika fainali hizo. Je, zawadi hii inawahusu wachezaji waliocheza mechi za mwisho dhidi ya Ethiopia na Guinea pekee, au inajumuisha wachezaji wote waliowahi kushiriki hatua ya makundi?

Pia, Soma:
+ Rais Samia aipa Taifa Stars Milioni 700 kufuzu AFCON
+ Full Time: Tanzania 1 - 0 Guinea | 2025 AFCON Qualifier | Estadio Benjamin Mkapa | 19.11.2024

Tunakumbuka mwaka 2019, Taifa Stars ilifanikisha kufuzu kwa AFCON baada ya kuifunga Uganda 3-0. Kama sehemu ya pongezi kwa mafanikio hayo, Rais wa wakati huo, hayati John Magufuli, aliwazawadia wachezaji viwanja huko Dodoma. Aidha, Mwenyekiti wa Kamati ya Uhamasishaji ya Taifa Stars, Paul Makonda, pia aliahidi Tsh milioni 10 kwa kila mchezaji wakati huo.

Hata hivyo, Nahodha Mbwana Samatta alisimama kidete kuwakumbusha Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) kuhusu mchango wa wachezaji walioumia katika majukumu ya kitaifa. Alitoa mfano wa Shomari Kapombe, ambaye aliumia wakati akiitumikia Stars lakini alionekana kusahaulika wakati wa mgao huo wa zawadi.
1732084949830.png
Sasa, tunapozungumzia zawadi ya milioni 700 kutoka kwa Rais Samia, mgao wake ukoje. Je, wapate Wachezaji wa kikosi cha mwisho kuitwa na kupambana dhidi ya Ethiopia na Guinea nakuvuna alama 6 muhimu ambazo zimechangia kufuzu kwa AFCON 2025?. Lakini je, wachezaji waliokuwa sehemu ya hatua ya makundi, hata kama hawakuitwa kwenye mechi za mwisho, hawastahili kutambuliwa?.
 
Inapaswa wachezaji wote wahusike, kila ambae kashiriki hatua hii ya kufuzu apate mgao.
 
unaacha kusaidia startups, kuwapa motisha vipanga wanaopiga GPAs kali vyuoni, kumotivate watoto wanaopiga division kali katika mitihani yao ya form 4 na form 6, kujenga labs na center za utafiti za maana, kujenga libraries kila wilaya,. Wewe unapeleka mihela kununua goli za Simba na Yanga.

Bora mzee Lowasa ambaye yeye sera yake ilikuwa ni ELIMU, ELIMU, ELIMU
 
Watafute njia iliyo Bora kugawana izo pesa, Hivyo ni vitu vidogo visije vika wavunjia heshima na Morali ya timu katika mashindano yanayo fuata.
 
Wakuu

Jana Rais Samia kutoa milioni 700 kwa Taifa Stars baada ya kufuzu AFCON 2025 kama pongezi kwa kuliheshimisha taifa kufuzi mara ya nne katika fainali hizo. Je, zawadi hii inawahusu wachezaji waliocheza mechi za mwisho dhidi ya Ethiopia na Guinea pekee, au inajumuisha wachezaji wote waliowahi kushiriki hatua ya makundi?

Pia, Soma:
+
Rais Samia aipa Taifa Stars Milioni 700 kufuzu AFCON
+ Full Time: Tanzania 1 - 0 Guinea | 2025 AFCON Qualifier | Estadio Benjamin Mkapa | 19.11.2024

Tunakumbuka mwaka 2019, Taifa Stars ilifanikisha kufuzu kwa AFCON baada ya kuifunga Uganda 3-0. Kama sehemu ya pongezi kwa mafanikio hayo, Rais wa wakati huo, hayati John Magufuli, aliwazawadia wachezaji viwanja huko Dodoma. Aidha, Mwenyekiti wa Kamati ya Uhamasishaji ya Taifa Stars, Paul Makonda, pia aliahidi Tsh milioni 10 kwa kila mchezaji wakati huo.

Hata hivyo, Nahodha Mbwana Samatta alisimama kidete kuwakumbusha Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) kuhusu mchango wa wachezaji walioumia katika majukumu ya kitaifa. Alitoa mfano wa Shomari Kapombe, ambaye aliumia wakati akiitumikia Stars lakini alionekana kusahaulika wakati wa mgao huo wa zawadi.
Sasa, tunapozungumzia zawadi ya milioni 700 kutoka kwa Rais Samia, mgao wake ukoje. Je, wapate Wachezaji wa kikosi cha mwisho kuitwa na kupambana dhidi ya Ethiopia na Guinea nakuvuna alama 6 muhimu ambazo zimechangia kufuzu kwa AFCON 2025?. Lakini je, wachezaji waliokuwa sehemu ya hatua ya makundi, hata kama hawakuitwa kwenye mechi za mwisho, hawastahili kutambuliwa?.

Kwangu mie. Ningekuwa Samatta kama captain wa team.. kwa kuonyesha uzalendo kwa
Nchi na kuwakumbusha viongoz wa serikali kuwa kuna mahitaji mengi ya msingi yanahitaji hiyo pesa kuliko team
Ya taifa..ningewaomba wachezaji na benchi la ufundi hiyo pesa kama timu tuitoe kwa wahitaj wa matibabu mahospitalini.. kununua vitanda na madawa. Au vifaa kujenga vyumba vya operation

Isitoshe wachezaji wote wa taifa stars na benchi lao la ufundi wana kazi zinazowapa mishahara na posho so pesa kama hii ambayo inakuja kama bonus ni sadaka nzuri ya kuitoa kwa wahitaj sababu haiwapunguzii chochote
 
unaacha kusaidia startups, kuwapa motisha vipanga wanaopiga GPAs kali vyuoni, kumotivate watoto wanaopiga division kali katika mitihani yao ya form 4 na form 6, kujenga labs na center za utafiti za maana, kujenga libraries kila wilaya,. Wewe unapeleka mihela kununua goli za Simba na Yanga.

Bora mzee Lowasa ambaye yeye sera yake ilikuwa ni ELIMU, ELIMU, ELIMU
Wanasema hizo mambo hazilipi kisiasa kibongbongo. Watanzania wanapenda vitu vyepesi.
 
Mimi nasema kama.kuna mtu kwenye timu/kempu atapata chini ya milioni 20 basi hizo.hela zitakua zimepigwa na genge la ndumbaro ama karia.
 
Back
Top Bottom