Hizi ndio sababu kwanini ni rahisi kwenda mbinguni kuliko motoni

Hizi ndio sababu kwanini ni rahisi kwenda mbinguni kuliko motoni

Mimi ninachoona hapa kwenye hoja zako ni ukosaji wa mtiririko au mpangilio.

Maandiko yanasema vitu vyote viwili wewe unataka kuvimerge ili kukubwisha hoja yako kitu ambacho ni kosa la kimakusudi.

Tukizingatia biblia inasema kwa neno la mashahidi wawili shauri ninathibitika. Kuhusu watu wote kwenda mbinguni limesisitizwa kwa waandishi wa vitabu vya biblia zaidi ya kimoja akiwemo na Yesu mwenyewe atakayesimamia mchakato huo.

Pili Maandiko yamezungumzia jambo la pili katika mchakato wa kwenda mbinguni utafuatiwa na tukio la kuubwa upya maskani ya mwanadamu baada ya uteketezwaji wa huu uchafu dunia.

Mungu mmiliki wa dunia na sayari zaidi ya decillion katika ulimwengu kwa hiyari yake mwenyewe ataamua kuuunganisha maskani yake mbinguni na yale atakayowatengenezea wanadamu. Hii ni baada ya kuwachukua wote na makaburi kupasuliwa na watu wasiohesabika kwenda mbinguni aliko sasa Mungu.

Tena hawendi tu mbinguni wanaenda kukaa mahali pa hadhi ya juu sana ambapo hata malaika wa mbinguni hawajawahi kupaona hata kupafikia labda wale makerubi.
Kwenye kiti cha enzi na Baba yao.

Ufunuo wa Yohana 3:21
Yeye ashindaye, nitampa kuketi pamoja nami katika kiti changu cha enzi, kama mimi nilivyoshinda nikaketi pamoja na Baba yangu katika kiti chake cha enzi.

Hoja yako imejengwa katika kuyafarakanisha maandiko na sio kuyaunganisha. Tukio ulilosimamishia hoja lako ni sehemu ya tukio la shamlashamla ya baada ya kuchukuliwa hapa duniani sio jumla kuu.


Yaani ni sawa na kipofu aliyeletewa tembo akashika sikio akaanza kubishia watu kuwa tembo anafanana na jani la gimbi au sinia. Kumbe anazungumzia sehemu ya tembo sio stori yote kuhusu mofolojia ya tembo. Mimi ninaposema mbinguni najumuisha package yote.

Kwa sasa huyu Mungu ikulu yake iko mbinguni na anaikulu ndogo katika subconscious mind yangu akitawala kutokea huko.
Yohana 14:23
Yesu akajibu, akamwambia, Mtu akinipenda, atalishika neno langu; na Baba yangu atampenda; nasi tutakuja kwake, na kufanya makao kwake.

Kama mtu mwenye majini anavyoitwa kiti na Mkristo ni kiti cha Serikali ya Mungu. Hivyo hizo raha za kuingia mbinguni na makao mapya tutakayoishi naye zimeshaanza sasa kwa jinsi ya rohoni kwa kutembea ukiwa na convoy ya serikali ya mbinguni duniani. Kama ni mkristo na hauamini haya ni afadhali uwe atheist au mason maana utakuwa ni ukristo wa shida na taabu sana. Dini itakuwa ni mzigo mkubwa
Bro, Mungu akubariki sana na Mungu azidi kukubariki sana sana sana
 
Kwahio hatujui.., sababu ukisema furaha isiyo kifani (je furaha inafanana kwa kila mtu) unless tuseme ni kama vile mtu anapotumia kilevi (drugs) yaani zile chemicals zinamfanya awe na furaha no matter nini kinamzunguka....

Haijalishi kama mtu atakiri au vipi ndio maana hata wale wabakaji na majangari kule mahakamani bado wana ndugu wanaowatembelea na kuwaonea huruma..., Sasa kama mimi nakula bata na mke wangu kipenzi na watoto wote wanachomwa moto mimi kuendelea na furaha lazima ubinadamu wangu (huruma na upendo) utakuwa umeondoka na nimekuwa kama roboti

Mimi tuseme nimekwenda mbinguni na wadau wangu wote marafiki zangu wapo motoni kwahio company yangu ipo motoni ila mbinguni kuna wadau kama nyie ambao hata huku kitaa zilikuwa haziivi (uoni hapo ni vigumu kuniambia takuwa nina furaha)

Siongelei kulalamika au Haki naongelea uhalisia binafsi siwezi nikala bata wala kufurahia kama kuna wadau wangu wanahangaika..., Kwangu mimi raha ni kula na wenzangu..., Kwahio if that is the case ninaomba Wasabato Imani yao iwe ya kweli kwamba wakosaji tusiamshwe tulale usingizi wa maisha sababu ni heri kulala kuliko kuwa macho kushuhudia watu wanahangaika na kupata shida za hatari
Broo, kuhusu kula bata na wenye dhambi, na wote waende motoni alafu wewe uende Mbinguni...

Hili ni ngumu sana kutokea..

Soma Wagalatia 5:25 SUV‬
[25] Tukiishi kwa Roho, na tuenende kwa Roho.

Ukienenda kwa Roho, hadi marafiki wako watachujika, maana Roho ni Mungu mwenyewe, na Mungu hafungamani na mwenye dhambi.
 
Broo, kuhusu kula bata na wenye dhambi, na wote waende motoni alafu wewe uende Mbinguni...

Hili ni ngumu sana kutokea..

Soma Wagalatia 5:25 SUV‬
[25] Tukiishi kwa Roho, na tuenende kwa Roho.

Ukienenda kwa Roho, hadi marafiki wako watachujika, maana Roho ni Mungu mwenyewe, na Mungu hafungamani na mwenye dhambi.
Hata kama ni maadui zangu kama nikibadilika na kuwa mtu wa furaha wakati nakula na kusaza wakati hapo chini kuna wadau wanakufa njaa watoto kwa wazee na mimi ninachekelea na kufurahia..., huyo mimi wa kesho nadhani nitakuwa duni kuliko mimi wa leo ambaye sifurahishwi na suffering....
 
Dr. Nimesahau kidogo, labda ningeona nikakumbuka. Ila ulieleza concept ya mama wa Yesu kutokuwa bikra.
Nop Hapana..
Nilisema kuhusu Lile Fungu la Isaya Linalosema Bikra kuchukua Mimba..
Neno Lililotumiwa ni Ha'Almah "Msichana mdogo" na sio Betulah " Bikra"
 
  • Thanks
Reactions: 511
Back
Top Bottom