Hizi ni Nchi zinazotoa VISA bure, Wabongo tunafeli wapi kusongamana ughaibuni kama Wanaijeria

Hizi ni Nchi zinazotoa VISA bure, Wabongo tunafeli wapi kusongamana ughaibuni kama Wanaijeria

Nchi zenyewe zimechoka hizo hapo yenye ahuweni ni Singapore 🇸🇬 tu hapo ila zungine bora kubaki zako Bahi chimendel huko
Ushawai kufika Malaysia wewe
 
Wabongo nyoso ni wananchi ambao hawana desturi ya kusafiri nje ya nchi. Wote tumesongamana hapa Nchini utafikiri watoto wanaosubiria nyumba ya urithi.

Nchi zinazotoa VISA ya bure kwa Watanzania.


View: https://www.instagram.com/p/CxC5PRyuwra/?igshid=MzRlODBiNWFlZA==

Japokuwa Nchi yetu inashika orodha ya idadi kubwa ya Raia ambao ni zaidi ya milion 60, na kwa Afrika mashariki ndio vinara wa idadi kubwa ya raia, ila hatuna watu wengi wanaotoka nje ya nchi.

Moja wapo ya sababu nchi yetu sio maarufu Duniani kote kama Wanaijeria, wasauzi na Wakenya, ni kuwà Nchi yetu Raia wake sio wengi ughaibuni.

Ukienda nchi za wenzetu Wabongo unaweza kuwatafuta kwa Tochi na usiwapate. Hizo hapo juu ni nchi ambazo huitaji kibali cha Visa kuingia kwao, Yani ni wewe na nauli yako na passport yako basi.

Sasa unakuta na Nchi ni ya Free VISA ila Wabongo bado huwakuti. Hii ni shida sana, na hizi fursa za free VISA watu kama Wanaijeria uwa hawazichezei kabisa.

Ndio maana naijeria ni nchi maarufu duniani kwa sababu Raia wake wametapakaa na kuitangaza nchi hivyo hivyo kwa wasauzi na Wakenya.

Kama una taaluma nchi ambayo naona upo vizuri kwa hizo hapo ni Botswana na Namibia. Ila kama hauna taaluma nakushauri baki nyumbani.
 
Tanzania yetu bado ina opportunities nyingi sana, kwenda kwenye nchi kama hizo kwa lengo la kusaka maisha ni ujinga mkubwa.
 
Sababu kubwa ni kwamba kupata MKOBA napo ni kipengele ,bureaucracy kama yote ,kijana ambaye nayetafuta maisha kwenda kutoa laki 3 ya passport ,halafu 1.5m ya nauli then hajui anaenda kufanya mishe gani ,anaona hiyo 2m ni bora apambane hapa hapa Bongo.
Passport ni 150,000.
Issue inakuja unaenda kufanya mishe gani huko. Inabidi kwanza mtu ujue sio kwenda tu
 
Huitaji kwenda uhamiaji kupata Passport,. passport unaweza kuomba online na kila kitu kufanyia online siku ya kwenda unapeleka tu Documents ambazo ukizoziweka online.
Umefungua uzi na kuanza mjadala ukiwa huna taarifa zitakazo pelekea uzi wako kuwa potential kama title inavyosomeka.
Kwa taarifa yako tu ni kwanlmba, hzo taarifa za kuomba passport online ni za kusadikika.
Ingawa ni lazima ujaze online, ukifika uhamiaji unaanza upya na utatakiwa ku dubmt upya documents zote ulizo submt online pia utaombwa documents zaidi
 
Passport ni 150,000.
Issue inakuja unaenda kufanya mishe gani huko. Inabidi kwanza mtu ujue sio kwenda tu
Si hata kutalii... Ukienda kutalii ndio unajifunza na fursa zilizopo... Sasa wewe huko Tanzania unataka kujua ukafanye mishe gani wakati hujawai kupaona... Hata wenzako wanaofata vitu nje ya nchi, mara ya kwanza wanaenda kama watalii
 
Si hata kutalii... Ukienda kutalii ndio unajifunza na fursa zilizopo... Sasa wewe huko Tanzania unataka kujua ukafanye mishe gani wakati hujawai kupaona... Hata wenzako wanaofata vitu nje ya nchi, mara ya kwanza wanaenda kama watalii
Ndugu yangu..wabongo na kutalii wapi na wapi? Utalii wa ndani tu umetushinda..ni wenye pesa zao tu ndo wanaweza kuwaza kwenda kutalii huko.

Mfano mimi hapa sina mapesa zaidi ya kuweza kujitafutia passport, nataka kwenda kutafuta maisha nje ya nchi , naanzia wapi?
Nipo serious nataka kuondoka hapa...
 
Ndugu yangu..wabongo na kutalii wapi na wapi? Utalii wa ndani tu umetushinda..ni wenye pesa zao tu ndo wanaweza kuwaza kwenda kutalii huko.

Mfano mimi hapa sina mapesa zaidi ya kuweza kujitafutia passport, nataka kwenda kutafuta maisha nje ya nchi , naanzia wapi?
Nipo serious nataka kuondoka hapa...
Omba Green Lotary ya Marekani kwenye mtandao wao, ukishinda unapewa Visa... sema hizi nchi zinazohitaji Visa zina complications sana na kupata mpaka uwe mtalii, mwanafunzi au uwe na kazi maalumu iliyokupeleka huko... Unless ujue jinsi ya kudili na hizi viza, Canada nasikia ndio pa kwenda
 
Omba Green Lotary ya Marekani kwenye mtandao wao, ukishinda unapewa Visa... sema hizi nchi zinazohitaji Visa zina complications sana na kupata mpaka uwe mtalii, mwanafunzi au uwe na kazi maalumu iliyokupeleka huko... Unless ujue jinsi ya kudili na hizi viza, Canada nasikia ndio pa kwenda
Hiyo bahati nasibu hapana, nataka hizi visa free countries hata burundi, sema sina pa kuanzia
 
Wabongo nyoso ni wananchi ambao hawana desturi ya kusafiri nje ya nchi. Wote tumesongamana hapa Nchini utafikiri watoto wanaosubiria nyumba ya urithi.

Nchi zinazotoa VISA ya bure kwa Watanzania.


View: https://www.instagram.com/p/CxC5PRyuwra/?igshid=MzRlODBiNWFlZA==

Japokuwa Nchi yetu inashika orodha ya idadi kubwa ya Raia ambao ni zaidi ya milion 60, na kwa Afrika mashariki ndio vinara wa idadi kubwa ya raia, ila hatuna watu wengi wanaotoka nje ya nchi.

Moja wapo ya sababu nchi yetu sio maarufu Duniani kote kama Wanaijeria, wasauzi na Wakenya, ni kuwà Nchi yetu Raia wake sio wengi ughaibuni.

Ukienda nchi za wenzetu Wabongo unaweza kuwatafuta kwa Tochi na usiwapate. Hizo hapo juu ni nchi ambazo huitaji kibali cha Visa kuingia kwao, Yani ni wewe na nauli yako na passport yako basi.

Sasa unakuta na Nchi ni ya Free VISA ila Wabongo bado huwakuti. Hii ni shida sana, na hizi fursa za free VISA watu kama Wanaijeria uwa hawazichezei kabisa.

Ndio maana naijeria ni nchi maarufu duniani kwa sababu Raia wake wametapakaa na kuitangaza nchi hivyo hivyo kwa wasauzi na Wakenya.

Mimi mkenya hapa. Mjadala wako ni wa tija mno ila ukifuatilia vile wenzako wanachangia unapigwa na butwaa hadi huruma tuu. Kwa hizi akili na vile tunahamasisha biashara baina ya waafrika (intra-african trade), kuna kila sababu ya kukiri bado waafrika tuko na safari ndefu sana. Kama kuna mtu anatoka nchi kama Nigeria ama Ghana n.k na bado anaona fursa Tanzania licha ya kuwa anatoka nchi zilizoizidi Tanzania kiuchumi. Bado utaona mtanzania akidharau eti Tanzania yake bado iko bora. Haya kila la heri mandugu zetu, sisi kama wenye shida vile mnavyodai tutatinga tuu hapo bongo na tukipata fursa bila shaka tutaidandia bila kusita.
 
Hiyo bahati nasibu hapana, nataka hizi visa free countries hata burundi, sema sina pa kuanzia
Unataka kwenda kuishi moja kwa moja au kufanya nini... Tuanzie hapa
 
Back
Top Bottom