Hizi shule za English Medium zimetugeuza Wazazi kuwa Walimu?

Hizi shule za English Medium zimetugeuza Wazazi kuwa Walimu?

Niliwahi kumfanyia dogo homework akaenda akakosa yote
Hebu kila mtu afanye kazi yake wasee mi na stress zangu za pesa na kujipiga na nyundo kwenye vidole badala mwalimu ufanye kaz yako unaniongezea mzigo na mm tena?
[emoji1] [emoji1] [emoji1] halagu ukikosea tu mtoto anaanza kusema hujui,kesho yake anatafuta mwingine wa kumsaidia
 
Acha kabisa mkuu, binafsi pia inaniboa mnoo. Hapa dogo kaniletea maswali,nmejibu lakini kuna maswali mawili nmechemka.wajuzi wanisaidie please.

1.Farming involving permanent settlement is called...........
2.Farming with no permanent settlement is called.............

Nmemuambia akalale,namtafutia majibu atajaza alfajiri..nmejaribu ku Google lakini wapi
1. Zero grazing 2. Non zero grazing
 
Nilidhani tatizo liko kwangu tu, kumbe hata kwa wengine? Mtoto wangu ameanza darasa la kwanza 'medium school'. Mbali na ada kuna tuition. Halafu naona kwamba watoto wanafundishwa kwa kukaririshwa na siyo kuelewa. Nijuavyo mimi tuition inahitajika labda kwa mtoto mwenye mahitaji maalumu na siyo kwamba ni aina ya ku'catch up' kwa mwanafunzi darasani. Ada tunalipa kubwa, mtoto haelewi na hata anayofundishwa tuition haelewi na tuition iko kwenye Sh25,000 kwa mwanafunzi. Watoto wanapewa diary kuleta nyumbani, halafu unakuta mtoto ndiye anayeambiwa aandike kwenye diary. Sasa kama mtoto hajaelewa anachotakiwa kufanya, mzazi hajui mwalimu anachohitaji. Watoto pia wanafundishwa na walimu ambao wako trained kufundisha madarasa ya juu, lakini hawana skills za kuwafundisha watoto wadogo. Ni shida na inanipa hasira sana maana naona kama ada ninayolipa inakufa bure!
Nilikataa kbs habari za tution
Wanatafuta pesa tu kiujanja
 
[emoji3][emoji3][emoji3][emoji3][emoji3][emoji3][emoji3]
Mtoto wangu Homework ya Kiswahili alikosa methali na nahau, mtoto akaulizwa nani kakusaidia akajibu baba... Mwalimu akamwambia babaako na wewe wote akili hamna....

Taarifa ikanifikia, nikaona isiwe tabu, kwakuwa ni class VII nimemhamisha mkoa yupo boarding na homework hainihusu tena.
[emoji1] [emoji1] [emoji1] [emoji1] [emoji1]
 
Niliwahi kumfanyia dogo homework akaenda akakosa yote
Hebu kila mtu afanye kazi yake wasee mi na stress zangu za pesa na kujipiga na nyundo kwenye vidole badala mwalimu ufanye kaz yako unaniongezea mzigo na mm tena?
Sipati picha..ulivyomdisappoint dogo
 
Nyie ndo wazazi mtoto atakuja kukuambia nimevunja photosynthesis ya shule tunadaiwa afu ulivyo boya unampa pesa kulipia fidia! Jitaidi ujue hata Yes and no!
 
Watoto kila siku wanarudi na homework mpya mzazi uwasaidie. Ukimuuliza anakuambia mwalimu hajamuelekeza akaelewa.

Sasa nalipia ada zaidi ya milioni ili watoto wapewe homework niwe mwalimu wao?
Kwa nini hawawafundishi wanafunzi wakaelewa ndipo wawape hizo home work wakazifanye!?

Wazazi wengine hatuna hulka ya kufundisha na wengine ndio tuliishia la sababa.

Tunatafuta hela na kulipa ada ili walimu wawafundishe sio watuletee homework kuja kutupima ujinga wetu..!! Walimu fanyeni kazi yenu ya kufundisha msihamishe goli.

Mbona kwenye ada hatupunguziwi kwamba tumeshiriki kufundisha watoto hivyo tulipwe stahiki zetu!?
Mtoto anapewa "Homework" ili aushughulishe ubongo wake na siyo akuulize wewe mzazi umsaidie. Siyo jukumu lako wewe mzazi kumsaidia mtoto wako kufanya "homework" , ukimsaidia unamfanya kuwa tegemezi.

Lengo la homework ni kumfanya mtoto atumie akili zake mwenyewe kupata majibu kwa kufikiri zaidi na siyo kuuliza majibu kwako wewe mzazi.
Na hata kama mtoto atakuuliza umsaidie homework yake, kama wewe mzazi una uwezo kielimu basi usimpe majibu ya moja kwa moja, mpe majibu yatakayomfanya aushughulishe ubongo wake yeye mwenyewe kupata majibu sahihi.
Mtoa mada usilalamike, inaonekana wewe ndiyo hujui lengo la mtoto wako kupewa homework. Akija kwako na homework mwambie anapaswa kutafuta majibu yeye mwenyewe na ni lazima aifanye. Tena mwanao akikwambia eti hawajafundishwa huyo ni mwongo, ni lazima wamefundishwa, sema yeye hakuwa makini darasani wakati Mwalimu anaelekeza. Kikawaida Mwalimu hawezi kuwapa watoto homework kwa mambo ambayo hajawafundisha.
 
Acha kabisa mkuu, binafsi pia inaniboa mnoo. Hapa dogo kaniletea maswali,nmejibu lakini kuna maswali mawili nmechemka.wajuzi wanisaidie please.

1.Farming involving permanent settlement is called...........
2.Farming with no permanent settlement is called.............

Nmemuambia akalale,namtafutia majibu atajaza alfajiri..nmejaribu ku Google lakini wapi
Hivi kuna kilimo cha kuhamahama 🤣🤣🤣🤣
 
Nasoma koment nacheka jamani ...

Ngoja nmpe mwanangu swalehe simu na yeye acheke
 
Acha kabisa mkuu, binafsi pia inaniboa mnoo. Hapa dogo kaniletea maswali,nmejibu lakini kuna maswali mawili nmechemka.wajuzi wanisaidie please.

1.Farming involving permanent settlement is called...........
2.Farming with no permanent settlement is called.............

Nmemuambia akalale,namtafutia majibu atajaza alfajiri..nmejaribu ku Google lakini wapi
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Mleta mada upo sahii sana. Home work si kitu cha kujifunza upya ni kitu cha kujikumbusha.

Mimi haiwezekani nimfundishe mtoto.

[emoji117]Jinsi ya kuanza sentensi na herufi kubwa
[emoji117]Kupiga mistari
[emoji117]Kuachanisha sentensi.

Huu ni ujinga nafundisha jinsi hata ya kusoma yani mzazi niligundua mtoto hajui kusoma anakariri halafu mwalimu hajui hilo. Siku nitawaibukia shule watajua hawajui.....

Hizi shule ni bomu sana...
 
Nilikataa kbs habari za tution
Wanatafuta pesa tu kiujanja
Of course, hata mimi nimekataa. Ila tatizo mtoto wangu hajaelewa vizuri. Mfano, kwenye maths mtoto naona amefundishwa kujua missing number in an ascending order. Mfano, akipewa swali kama: fill in the missing numbers: 1, 2,--, --, 5,--, --, ---, 9, etc anajua. Lakini akipewa swali kama: fill in the missing numbers: 11, --,--, --, 7, --, --, --, 3, mtoto ataandika 12, 13, 14, 15, 16, 17. Kwa hiyo, inawezekana mwalimu hajawahi kuwaonyesha hizi njia mbili kwamba kwenye ascending order unaanza na namba ndogo kwenda kubwa na kwenye descending order unaanza na namba kubwa kwenda ndogo. Sasa hivi nimeamua nitenge muda wangu angalau kila siku kwa nusu saa nipitiea vitabu wanavyotumia na ni'formulate' maswali kwa muda kadhaa mpaka nitakapojiridhisha kwamba ame'catch up'. Otherwise, akienda darasa la 2 akiwa tabula rasa hivi, hatakuwa amepta background nzuri kwa mambo ya msingi.
 
Ili mtoto aweze kufanya vizuri kimasomo kuna factor mbili ambazo huwa za msingi sana,external na internal!external ni mazingira yanayomzunguka kuanzia nyumbani mpaka shuleni,na internal ni yeye mwenyewe mtoto!
Ukielewa hili kama mzazi wala hutapata shida na hizo homework za mwanao
Kwenye internal pia watoto wanatofautiana kuna ambao wanajiweza wenyewe wakiwa nyumbani bila kuwa pushed kuanzia kwenye masomo mpaka activitiez zingine,lakini wengine ni mpaka mzazi utoe msaada haswa akiwa home
Wewe kama mzazi lazima uelewe hili as hiyo ni future ya mwanao na huo mzigo huko mbele unaubeba wewe na wala sio mwalimu
 
Hakika umesema kweli yani kwa sasa na mm najiona nipo grade 3 A hahaha maana leo uataulizwa what is th process of changing liquid to gas mara draw coat of arm yan kwa kwel inachosha.

Huwa nawaza vipi kwa wale wazazi ambao hawajafika hata form four hawa watoto wanawasidiaje home work
Bado asubuhi hujakumbushwa kusign diary
[emoji1787] wanachosha na huwa hawakubali kirahisi ukiwaambia ntasaini kesho...ninao wawili basi kila siku ni kusoma...!
 
Masomo kama SOCIAL STUDIES ni magumu kweli kweli. Mtoto darasa la tano anapewa swali la homework utadhani ni A level- "Explain in details the benefits and challenges of Regional integration by siting examples in economic, social and other aspects "!! [emoji86][emoji86][emoji86]

Mimi mzazi, I am like...seriously? [emoji56].

Sijui elimu siku hizi ipoje?
Acha tu, kijana wangu kaisha kabaki kichwa tu...! Akirudi ana homework zaidi ya 1 anafanya kisha analala anaamka tena alfajiri kumalizia namuhurumia lakini simuoneshi...ajikaze tu si kwa ubaya [emoji5]
 
Back
Top Bottom