Hizi shule za English Medium zimetugeuza Wazazi kuwa Walimu?

Sisi wakati tuko primary in the 90's tulikua hatupewi homework kila siku especially below darasa la 5. Watoto waachwe wawe watoto kwa kupata muda wa kucheza na kujifunza kwa vitendo,sioni sababu ya homework za kila siku kwa watoto wadogo.
 
Wako sahihi kwa asilimia fulani kwa sababu mzazi unapata nafasi ya kukagua kidogo madaftari ya mwanao na kujua mwenendo wake shuleni

Wazazi wa kitanzania wana asili ya uvivu sana na wamejawa na unafiki.

Mwanafunzi akifeli utasikia waalimu wenu wajinga na hawafundishi, je wewe kama mzazi ulitenga muda wa kukagua mwanao anafanya nini shuleni?

Elimu sio shule tu, hata nyumbani nako kunapaswa kuwa na ufuatiliaji.

Endapo mtindo huu utaigwa na shule za serikali nina imani tutafika mbali sana.
 
Waalimu wananikera hata mimi,kuna siku nimegoogle majibu nikampa dogo kufika akapigwa mikasi kibao sasa dogo ananiaminije tena?Au waalimu nao hawajui majibu?Cha ziada wawafundishe basi kama hawajaelewa lakini notes zipo tunaweza na sisi wazazi tukasoma ili tupate majibu humuhumo.
 
... citing ... actually neno "citing/citation" sikumbuki kukutana nalo sekondari. Kama primary za siku hizi ni common word basi kuna mabadiliko makubwa!
Citing form four lipo..mitihani ya miaka hii ya karibuni
 
Daa Kaka we kama hizo coat of arms na gas ndio maswali Kila siku

Sent using Jamii Forums mobile app
 

Hujslazimishwa kumpeleka huko medium mkuu! Kama unaona ada ni kubwa na kwamba wewe kama mzazi unashiriki kufundisha kwamba kwako ni mzigo, basi mpeleke huko kayumba!

Wazazi wengine wamesha adopt huu mfumo, wala hawaoni tabu watoto kupewa hizo homework! Wewe kalia kulalamika utabaki mwenyewe!
 
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]Aisee elimu ya tz ni upumbavu mtupu,

Sasa hapo hiyo homework atakuwa kafanya mwanafunzi au mzazi?

Lengo la homework ni kumpima mwanafunzi kama kaelewa alichofundishwa au la!
Yani unampa kazi akafanyie nyumbani kulingana na kile alichofundishwa!

Sasa mzazi ukimfanyia akaenda kupata vema atajiona na akili lakini kiuhalisia anakuwa hajaelewa chochote.

Hizi shule kumbe bora mtoto umpeleke kayumba tu.
 
Hili umeongea ukweli kabisa, wanamtindo wa kutoa homework tena kwa topic za mbele ili wazazi wawasaidie kufundisha. Unakuta umerudi umtoka kwenye mihangaiko yako ya siku nzima Unakuta mtoto anakusubiri na maswali kama 150 hivi kwa masomo matatu, ili umsaidie homework, kwa kuwa umechoka na hautaki kumdisappoint mtoto unaamua kumfanyia homework, siyo kumfundisha narudia tena kumfanyia anacopy anaenda shule. Hizi shule ni mzigo na tunaibiwa sana. Mtoto akifika darasa la nne boarding lazima kwa kisingizio cha mtihani wa taifa, hivi watoto wakiwa day hawawezi kufundishika?
Anaachiwa kidogo la sita nako boarding lazima kisingizio maandalizi ya mtihani wa darasa la saba. Mwisho wa siku matokeo yanalingana tu na wale waliosoma shule za serikali. Nina mtoto wa ndugu yangu kasoma majita huko vijijini, matokeo ya darasa la saba alipata A katika masomo yote matano na kwenda boading.
Narudia kusema tunaibiwa tu, Ushahidi mwingine kijana wangu alisoma hizi shule darasa la saba kafaulu vizuri sana kapelekwa Kibaha Sec, kufika kule alitaka kulia, kule siku ya kwanza alionyesha library ajitafutie material mwenyewe aliona kama amepotea na kutaka kunishawishi nimtafutie uhamisho au nimpeleke tena private school, nikakomaa huko kakutana na vijana waliotoka shule za kata huko vijijini. Mtihani wa kwanza kawa wa themanini ( 80) kati ya watoto 120. Nikajua hapa lazima akili imkae sawa.
Nashukuru mtihani wa mwisho taifa alitoka na two ya point 19, sasa hivi anamalizia paper ya Alevel.

Hitimisho hizi shule za private zaidi ya kiingereza tunaibiwa tu, tunatumikishwa kama walimu na tunalipa ada ambazo haziendani na huduma. Shule msingi unalipa ada sawa na mwanafunzi wa Medicla Muhas.
 
Hizi shule wanachukua walimu wabovu tena form four ya kufeli na yote hii ni ubahili anaona kuliko amlipe mwalimu wa digrii sh laki 8 anachukua wa form 4 ya kufeli anamlipa laki 2 na nusu kwa mwezi.

Ni ujinga mtupu
 
[emoji1787] wanachosha na huwa hawakubali kirahisi ukiwaambia ntasaini kesho...ninao wawili basi kila siku ni kusoma...!
Hahahhaha mimi pia yani nasoma haswa nipo grade 1 na 3 A hatari. Ila pia jifunze kumtengeneza ajue kua anatakiwa asome mwenyewe. Mimj nampa page tatu asome kisha namuuliza maswal kdg inaanza kunipunguzia kazi
 
NA ADA ELEKEZI IMEONDOLEWA JIANDAE NA ONGEZEKO
 
WANAPIMA MZAZI KAMA ALIPATA DEGREE KIHALALI AMA KWA KUDESA
HAHAHAHAAAAAAAAA
 

Kuna point kwenye hili....
 
1. Permanent crop cultivation /Permanent Agriculture
2. Shifting cultivation
 
Kwa kweli ni kero na udharirishaji kwa sisi wazazi tusiosoma yani mwanangu daily homework ngumu lugha ndio sielewi basi inabidi nimsukume kwa jirani akamsaidie uko, Sasa sijui jirani ananifikiriaje😄
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…