Hoja binafsi: Vyama vya siasa viwe makini sana kwenye uteuzi wa wagombea wenza katika chaguzi zijazo ama sivyo Katiba imulikwe

Hoja binafsi: Vyama vya siasa viwe makini sana kwenye uteuzi wa wagombea wenza katika chaguzi zijazo ama sivyo Katiba imulikwe

Dam55

JF-Expert Member
Joined
Oct 8, 2015
Posts
5,641
Reaction score
11,958
Wasalaam wakuu,

Hili ni wazo langu tu kwaajili ya kuleta afya ya kiuongozi kwa Tanzania yetu ili kupunguza hatari za kiuongozi zinazoweza kutokea na nchi kujikuta ikiangukia kwenye mikono ya watu ambao hawakujiandaa kuwa kwenye nafasi fulani fulani za kiuongozi.

Katiba yetu iko wazi jinsi madaraka yanavyoweza kubadilika ikiwa kitatokea chochote wakati wowote.

Hivyo basi ni muhimu sasa kwa vyama vya siasa viweke umakini mkubwa kwenye uteuzi wa wagombea wenza ili tuhakikishe watu wanao patikana tuwe na uhakika na uwezo wao kwenye nafasi kubwa kama hiyo pindi itakapotokea dharura yoyote ile tusiteteleke kiutawala.

Ni ukweli ulio wazi kuwa vyama vya siasa mara nyingi sana vimekuwa vikifanya mizaha kwenye uteuzi wa wagombea wenza bila ya kuangalia kwa makini takwa la kikatiba kuwa watu hao wanaweza kuja kuwa wakuu wa nchi siku moja.

Wagombea wenza limeonekana Kama suala dogo sana lisilo na uzito wowote na maranyingi limechukiliwa kirafiki na kishikaji sana bila kujali madhara yake.

Rejea uchaguzi wa 2020 angalia wagombea wenza wote kwenye vyama vyote kisha angalia katiba yetu inasemaje ndipo utagundua mzaha tunao ufanya Watanzania.

Mungu tusaidie waja wako, kama ugombea wenza ni ushkaji basi tuimulike Katiba kwenye vipengele fulani.
 
Kweli..na sio mgombea mwenza tu hata na rais pia
Kwa mfano chadema walituwekea lowasa na yule makamu wake sijui walikuwa wanatuchukuliaje
Mlisema Lowasa hawezi, akina Marehemu Samweli Sita na JPM wakimkejeli kwamba Ikulu siyo wodi ya wagonjwa, leo Lowasa yupo anadunda, lakini walio wazima wapo?

Nataka nimwambie, jambo usilolijua ni kama usiku wa kiza. Hivi kama Hayati JPM asingetutupa mkono, uwezo wa Mama Samia tungeujua wapi? Umdhaniaye ndiye siye!! Au labda naye unasema anapwaya!
 
Mleta mada hebu funguka, mbona kama kuna kitu wataka andika lakini wajificha nyuma ya maneno 'mgombea mwenza'
Hapo ndio nisha funguka tayari mkuu, tuwe makini na wagombea wenza nyakati nyingine ili kuepuka mabalaa yanayoweza kutokea.
 
Ni kweli; hata mimi nimeshaona tatizo la kikatiba hata. Ile katiba ya zamani ilikuwa inasema rais akifa, basi uchaguzi mwingine mdogo wa rais unafanyika kujaza nafasi yake kama ambavyo anapokufa mbunge nafasi yake inajazwa kwa uchaguzi mdogo wa bunge.

Mabadiliko ya kusema makamu wa rais anakuwa automatic rais na akishachukua madaraka anafanya lolote atakalo ikiwa ni pamoja na kupangua serikali aliyokuta linaweza kuwa na unintended consequences kwa mustkhabali wa nchi. Inabidi katiba ingaliwe upya namna ya kurithisha kiti cha uraisi aliyefariki na kuongeza checks and balances zaidi kwa mrithi wa kiti hicho. Njia rahisi sana ni ile ya kuundwa kwa kamati ya urais itakaokuwa inaongozwa na aliyekuwa Makamu wa rais kabla ya kifo cha rais; kamati hii uhai wake utakwisha baada ya uchaguzi mkuu unaofuata. Halafu rais aliyerithi asiwe na power zote za rais aliyechaguliwa; sehemu ya powers za rais aliyechaguliwa ziwe mikononi mwa kamati hii. Utaratibu huu utapunguiza kidogo tamaa ya madaraka kwa makamu wa rais.

Kusema tu kuwa waliaminiana wakati wa uchaguzi siyo hoja kabisa, binadamu huamini wenzao walio hai tu, baada ya vifo husahauliana kabisa. Kesi hii ya kifo cha Magufuli imeonyesha tafsiri hiyo kwa uwazi sana tena kwa muda mfupi sana. Ndani ya mwezi mmoja tu wa kifo chake, mkataba wa bandari ya Bagamoyo uliopingwa na magufuli unaaza kujadiliwa tena!
 
Sheria hazitungwi hivyo! Sheria zinaangalia long term na inabidi ziheshimiwe, siyo ikifika wakati wa kutekeleza sheria husika mnaona ni inconvenience. Ndiyo maana mmebadili sheria nyingi kwa sababu mliona zinazuia kutekeleza matamanio yenu!

Ila unachosema kina ukweli kwa upande mwingine. Kutokana na mfumo wa Muungano, Zanzibar imependelewa sana. Imagine kama wagombea wa Rais wa JMT wakiwa 20, kinchi kama Zanzibar nacho kinajihakikishia at least wagombea (wa Urais au Makamu) 20 kati ya hao! Matokeo yake, vyama vingi havipati wagombea wenza makini au wale wanaoonekana wana hadhi ya kuwa Marais.
 
Ni kweli; hata mimi nimeshaona tatizo la kikatiba hata. Ile katiba ya zamani ilikuwa inasema rais akifa, basi uchaguzi mwingine unafanyika kujaza nafasi yake kama ambavyo anapokufa mbunge nafasi yake inajazwa kwa uchaguzi mdogo. Mabadiliko ya kusema makamu wa rais anakuwa automatic na akishachukua madaraka anafanya lolote atakalo ikiwa ni pamoja na kupangua serikali aliyokuta, linaweza kuwa unintended consequences kwa mustkhabali wa nchi.
Mkuu hili ni tatizo kubwa sana
 
Ndg Yangu Kubaliana na Khali tu Rais wa JMT ni Mama SSH, Hauna Namna. Mama SSH anatosha na ametuonyesha ni Jinsi gani anatosha. Je ulishawahi Kujua tangu Ndege ya Kwanza hadi ya Nane ni Hasara kila Mwaka kwa Kwenda Mbele. Je angekuwepo Mwendazake ungejua hizi hasara BIl.150 only kwa Midege tena Mibovu.

Serikali halali ni seriali ya watu na kuna transparency, sasa ya Mwendazake iligubikwa na usiri mkubwa kwani ni serikali iliyokwishakujua ina Makandokando Mengi na ya Kutisha. Wenye Hakili Tuliliona hili Mapema ya Mwaka wake wa Mwanzo wa Utawala wake.. Karagabaoo.
 
Kweli..na sio mgombea mwenza tu hata na rais pia
Kwa mfano chadema walituwekea lowasa na yule makamu wake sijui walikuwa wanatuchukuliaje
Chama changu kilikosea jambo moja kuu kutuwekea mgombe ambaye kwanza walijua ni mgonjwa lakini pua walizijua tabia zake
 
Back
Top Bottom