Hoja ya Spika Ndugai: Nitawafukuzaje wabunge ambao Rufaa zao hazijasikilizwa na Baraza kuu kwa mujibu wa Katiba ya CHADEMA?

Kwamba huelewi vyama vyote vya siasa vinafuata muongozo uliowekwa na katiba kwa mujibu wa sheria ya demokrasia ya vyama vingi? Unaposema katiba za vyama vya siasa hazifanani unamaanisha rangi za cover zake sio?[emoji116][emoji116]
Katiba za vyama vya siasa hazifanani bwashee!
Ni kweli ni la kisheria, mbona hauhoji hizo kauli anazo bwatuka 'Jobo' ni kwa mujibu wa sheria zipi? Au hizi sheria zetu ni msumeno wenye makali upande mmoja?[emoji116][emoji116]
Hili swala ni la kisheria zaidi bwashee!
 
Reactions: SMU
Chadema walipaswa ama kuiripoti hiyo jinai kwa DCI au kwenda moja kwa moja mahakamani kuishtaki Tume ya uchaguzi.

Spika amepelekewa tu majina kwahiyo anacheza ngoma isiyo yake!
 
CCM huwezi kufukuzwa uanachama bila kujitetea.

Lakini Chadema wanatimuana tu ila Shibuda ndio walimshindwa!
 
Chadema walipaswa ama kuiripoti hiyo jinai kwa DCI au kwenda moja kwa moja mahakamani kuishtaki Tume ya uchaguzi.

Spika amepelekewa tu majina kwahiyo anacheza ngoma isiyo yake!
CHADEMA should just do their part na kuachana na hii tendecy ya kuplay victim,

Itisha Baraza Kuu na ratify maamuzi ya kuwatimua wale, andikia barua NEC kuikana ile barua na teua wengine 19, report police ile jinai kubwa iliyofanyika then sit back and relax. Bila hivyo Ndugai ataendelea kuwalinda wale watu na hakuna kitu CHADEMA itafanya

BTW CHADEMA inapaswa kupeleka wabunge wa viti maalumu Bungeni. Wao ni zao la uchaguzi ule "haramu" uliompa ushindi Aidah na kumpa Lissu kura ambazo zimesaidia kucalculate ile ruzuku. Kama tunakubali ushindi wa Aidah na ruzuku ile, hatuna grounds za kukataa viti 19
 
Spika wa bunge mh Job Ndugai hana tatizo na wabunge wa viti maalumu wa Chadema akina Halima Mdee na wenzake bali anachotaka ni utaratibu wa natural justice kufuatwa.....
Mnajitahidi sana lakini hoja ni aliwaapishaje watu ambao hawakupendekezwa na chama chao? Yeye ndie anayetakiwa kuweka ushahidi kuwa alifuata taratibu zote wakati anawaapisha. Je, alipata barua ya uteuzi kutoka NEC ambayo iliambatishwa na barua ya Katibu wa CDM na minutes za vikao vya uteuzi wa majina hayo.

Chadema walipolalamika kuwa hawajawateua wakina Halima alifanya juhudi gani kuyafuta ukweli NEC. Akumbuke kuwa NEC waliishasema hadharani kuwa hawajapokea barua yeyote ya uteuzi kutoka Chadema. Hawa hata kama rufaa yao ya kufukuzwa kwenye chama itakubalika lakini bado uapishwaji wao utabaki wenye dosari.

Yeye angependa sana rufaa isikilizwe ili mchezo uhamie Mahakamani ambako wao watazuia mabadiliko yeyote kufanyika wakati wanasikiliza kesi ya msingi.

Amandla...
 
Hii issue ina complications flani. Chama hakijawateua na kuna mtu/watu/kikundi kimefoji barua na kuipeleka NEC then NEC wakaact accordingly na kumjulisha speaker...
Let's assume unacho kisema kiko sawa ingawa nashindwa kukiamini, bado kuna mashaka makubwa sana:

1. Chadema kulijulisha bunge kuwa hawajafanya uteuzi ilikuwa sababu tosha kwa nchi zenye kutii sheria kuhoji hao covid-19 uhalali wao kabla ya kuwaapisha wakati tayari kuna barua toka Chadema.

2. Kufoji ni jinai, kwa nini vyombo vyote ikiwemo polisi viko silent hawa act kwa chochote wakati kodi za wananchi zinatumiwa kulipa 'vibaka' tena waziwazi?

3. Unataka Chadema wafungue kesi wapi, wakati unaona dhahiri kuna consipiracy kati ya bunge, covid-19, serikali na tume juu ya huo uhuni. Kwenye hiyo kesi wanamshitaki nani kati ya hao 'wahuni'?
 
CCM huwezi kufukuzwa uanachama bila kujitetea.

Lakini Chadema wanatimuana tu ila Shibuda ndio walimshindwa!
Hivi ukimuita mtu na asitokee bado haki yake ya kusikilizwa inakuwa reserved?

Hawa wako 19, how comes wote kwa pamoja wakawa na dharura na kushindwa kuitikia wito wa chama? Don't you smell anything fishy?!
 
Nimemsikiliza Spika wa Bunge. Amemuombea mh. Nape msamaha kwa kuwasema wabunge 19 waliofukuzwa Chadema maarufu kama covid 19.

Spika amesema wanawake hawataki kushuhulikiwa kwa nguvu na ukali(wanaume amewashauri wawe soft).

Ila nimejiuliza kipindi kile alipotoa amri Halima Mdee akatiwe pingu popote alipo alikua ndio anatoka Mirembe? Kule alikosema anafaili lake huko

Spika ameiita barua ya Chadema kipeperushi na akatoa sababu zake kwamba hakuna viambatanisho kama vile katiba ya chama,muhtasari wa kikao,majina ya wajumbe nk

Kwanukta hizo,Ndugai atawafukuza covid19 ila barua ya Chadema irekebishwe kama alivyoeleza spika.

Nadhani spika amekubaliana na Chadema bali Chadema wafanye marekebisho hayo
 
Chadema walipaswa ama kuiripoti hiyo jinai kwa DCI au kwenda moja kwa moja mahakamani kuishtaki Tume ya uchaguzi.

Spika amepelekewa tu majina kwahiyo anacheza ngoma isiyo yake!
Ukishasema jinai, mlalamikaji ni jamuhuri. Kitendo cha cdm kusema hadharani tu kuwa hakija wateua, kwa nchi yenye utawala bora kilitosha kuistua NEC, Bunge na Polisi kufanya uchunguzi. Au pia kuichukulia hatua CDM kwa kusema uongo/kuichafua NEC na Bunge. Maana hizo ni serious allegations....zisingeachwa zipite hivyo.

Lakini sote tunajua ni kwa nini yote hayo yanatokea sasa. Kwa hivyo hata kubishana hapa pengine ni kupotea muda tu kwa jambo lililo wazi kabisa.

Unakumbuka wakati Nyalandu anatoka ccm, spika alisemaje?

Suala la vikao vya chama ni factual....halina utata wala ugumu kuchunguza.

But karma is a bitch......nafikiri (w)ameshapata malipo!
 
Tatizo lipo na linapaswa kumalizwa!
Anayetakiwa kulimaliza ni Spika. Pamoja na maneno yote anayosema anajua kuwa wale wakina dada hawana legitimacy na hivyo wanatia dosari Bunge lake. Nnauye hayuko peke yake anayekerwa na hiyo hali.

Na hali inavyozidi ndivyo inavyozidi kuharibu. Chadema hawana wanachopoteza kwa wakina Halima kubaki Bungeni. Wanavyozidi kubaki kunawaondolea haja ya wao kufanya maamuzi kuhusu viti hivyo 19.

Amandla...
 
Hao mlitakiwa muombe wafukuzwe bungeni wakiwa bado wanachama wenu.
sio sasa hamna MADARAKA nao.
 
Chadema inapokea ruzuku baada ya uchaguzi wa 2020?

Unasemaje wameukubali ushindi wa Aida wakati wamedeclare kutoutambua uchaguzi wote?

Usitumie issue ya Aida kujustify hao covid-19, hizo ni scenario mbili tofauti. Aida amepatikana kwa uchaguzi ambapo kama alishinda/kushindishwa amefata mchakato wote kupata hati ya ushindi na kula kiapo hata kama ametofautiana msimamo na chama wa kukataa kutambua uchaguzi, ndio maana CDM hawamzunguzii kwa lolote.

Issue ya covid-19 kuingia bungeni ilihitaji majina yao kuidhinishwa na chama na kisha kupelekwa tume ambapo yangewasilishwa bungeni jambo ambalo Chadema haikulifanya.

Jambo la kujiuliza ni kama CDM haikufanya huo mchakato ni nani yupo nyuma ya hilo sakata? Hapa hauhitaji hata calculator kujua kinacho endelea.

Kuwalaumu Chadema kwenye hili ni ama kwa makusudi kutaka kuhalalisha huu 'upumbavu' uliofanywa au kutokuelewa unacho kiongea.
 
2. Kufoji ni jinai, kwa nini vyombo vyote ikiwemo polisi viko silent hawa act kwa chochote wakati kodi za wananchi zinatumiwa kulipa 'vibaka' tena waziwazi?
Nadhani shida ipo sasa. Nani anapaswa kuinitiate hii kitu? Madai kwamba ile barua ni forged nadhani yalitolewa kwenye media. Kuna msemo unasema hivi "He who alleges must also prove". Wapi, how, when labda ndipo kwenye shida
3. Unataka Chadema wafungue kesi wapi, wakati unaona dhahiri kuna consipiracy kati ya bunge, covid-19, serikali na tume juu ya huo uhuni. Kwenye hiyo kesi wanamshitaki nani kati ya hao 'wahuni'?
Sasa hii ndio tendency yenyewe ya kuplay victim. Kushindwa kuchukua hatua stahiki kwa sababu tu unahisi/unaogopa/umeshaconclude kuwa hutotendewa haki ni udhaifu.
 
Ndio maana nikasema CHADEMA wao waendelee na mchakato wa kuteua wabunge 19 na kupeleka majina yao NEC maana hawawatambui wale waliofoji barua. Process ya kuteua wabunge halali iende sambamba na zoezi la kuratify maamuzi ya Kamati Kuu kwa kuitisha Baraza Kuu.

Vitu vingine tunapaswa kurudi kwenye basics tu na wala havihitaji kuviintegrate
 
Hoja za Ndugai ni za kipuuzi na kipumbavu kwa 100%.

Ndugai anasema hao Covid 19 wanaandamwa na CHADEMA kwa sababu ni wanawake, anasahau kuwa hivyo ni viti maalum vya wanawake, na mwisho wa siku vitakaliwa na wanawake wa Chadema. Hoja ya kuonewa kijinsia ni ya kipumbavu.

Ndugai amekuwa akiimba kuwa hana taarifa ya kuvuliwa uanachama hao Covid 19, na hapo hapo anakiri kuwa wamehukumiwa bila kusikilizwa na kuimba kuwa wamekata rufaa na jana akahitimisha kuwa taarifa za kuvuliwa uanachama anazo lakini hazikubali. Huu nao ni upumbavu.

Ndugai anasema barua ya katibu mkuu wa Chadema hawezi kukurupuka kuifanyia kazi kwa sababu haina viambatanisho, lakini anasahau kuwa katiba inamtaka kupewa tu taarifa kutoka kwa katibu mkuu wa chama, na kama kuna ufafanuzi husika anaweza kuomba kutoka kwa katibu mkuu wa CHADEMA. Kama Ndugai hana dhamira hata Chadema wangefanya nini bado hatakubali. Ni ulevi mbaya wa madaraka unaofanywa na Ndugai.

Mwisho kabisa Ndugai anamaliza kwa kusema Chadema ni taasisi ya wahuni na kuikashifu vibaya, lakini hapo hapo anajitamba kuwakumbatia wabunge wa viti maalum wa wanaotokana na CHADEMA! Huu nao ni upuuzi wa kiwango cha juu.
 
Fundi Mchundo pia amegusia hili hapo juu kuwa kufoji ni jinai, kitendo tu cha Chadema kutoa allegations vyombo husika vilipaswa ku-act hata tu kuwataka Chadema wapeleke formal allegations. Tena basi allegations hizi zina 'national interest' ndani yake, kwa nini wako kimya?
Nadhani shida ipo sasa. Nani anapaswa kuinitiate hii kitu? Madai kwamba ile barua ni forged nadhani yalitolewa kwenye media. Kuna msemo unasema hivi "He who alleges must also prove". Wapi, how, when labda ndipo kwenye shida
Simaanishi kwamba wasishtaki kwa kuwa wanahisi kutotendewa haki bali namaanisha unamshitaki nani hapo? Kwa sababu obvious mahakama itarudi kwa vyombo husika (bunge na tume) kutafuta justification, kwa ujinga unaoendelea vipi mahakama ikiridhia kuwa hizo 'forged documents' ni genuine, si ndio mchezo unakuwa umeishia hapo.
Sasa hii ndio tendency yenyewe ya kuplay victim. Kushindwa kuchukua hatua stahiki kwa sababu tu unahisi/unaogopa/umeshaconclude kuwa hutotendewa haki ni udhaifu.
 

Sasa wakiteua hao 19 si ndicho CCM wanakihitaji ili kujustify uchaguzi usio free and fair?

Yaani in short shida ya CCM ni kuwe na representation ya opposition especially ya CDM ili kuihadaa dunia kuwa 'things are okay' ndiyo maana wame-conspire na hao covid-19 ili mambo yaende.

Meko ali-engineer wizi wa uchaguzi bila hata kujua kwa zama hizi unahitaji wapinzani ili kuwashawishi wahisani 'wakupe' chochote, alipogundua kabugi ndio haya ya covid-19 yakafatia.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…