Hoja zangu za Kisiasa, Katiba, Sheria na Haki humu JF zina mashiko? Zimesaidia kitu? The Consequences ya baadhi ya hoja zangu! Kazi inaendelea!

Huyu jamaa Kwa uandishi wake wa kuuma na kupuliza Ili asiwaudhi wanasiasa ulinifanya nianze kumpuuza, huenda huyu ndo chanzo Cha tatizo la uchawa liko Kila secta na linalotusumbua Kwa sasa
 
Kabla haujabadili kutoka Pasco na kuwa pascal nyuma ya 2015 ulikua na mabandiko makini sana, lakini sahivi!!!!!
 
Wanabodi

Hili ni bandiko la kufanya assessment ya baadhi ya mabandiko yaliyoleta impact kama hoja zangu zina mashiko?, zimesaidia kitu au ninaandika for nothing kupoteza tuu muda?

Paskali
Angalia bandiko hili Amri Kuu Kuliko Zote ni Upendo! Mpende Mungu, Ipende Nchi, Wapende Viongozi, Mpende Jirani Yako Kama Nafsi Yako!. Jirani yako ni Nani?, Unampenda?
Hili ni bandiko la Krismasi ya mwaka jana, angalia nilishauri nini na nini kilitokea
Wanabodi,
Hili ni bandiko la salaams zangu za Krismasi ya mwaka jana ambayo nilisisitiza upendo. Kwenye medani za siasa za vyama, nilisema "CCM kama chama tawala, jirani zake ni Chadema, ACT Wazalendo, CUF, NCCR etc, wana CCM wanawajibu wa kuwapenda vyama vingine kama wanavyojipenda wenyewe!, haiwezekani wao wawe huru kufanya mikutano, lakini wanawazuia wengine!".

Hoja hii ilijibiwa kwa vitendo kwa mikutano ya siasa kuruhusiwa, hivyo haya tunayoandika, sio tunajiandikia kupoteza muda, tunayo yaandika yanafanyiwa kazi.

Ukiandika kuomba kitu fulani, siku ukipewa hicho ulichokiomba, una wajibu wa kumrejelea yule uliyemuomba na kumshukuru kupokea ombi lako na kulitekeleza, hivyo nami baada ya mikutano ya siasa kuruhusiwa, kwanza niliandika makala ya kushukuru, Asante Rais kuruhusu mikutano, tunakuomba uruhusu haki nyingine ambayo imeporwa ya Watanzania wote kuchagua na kuchaguliwa kisha nikaomba ile haki nyingine iliyoporwa irudishwe.

Kikao cha Bunge lijalo, kitapitisha mabadiliko ya sheria ya uchaguzi, vyama vya siasa na Tume ya Uchaguzi, mabadiliko yote hayo ni superficial tuu kama hakuna mabadiliko ya katiba, hivyo mwaka huu ujao wa 2024, let's press for mabadiliko ya katiba ili tufanye uchaguzi mkuu wa 2025 uwe uchaguzi huru na wa haki.
Mungu Ibariki Tanzania
I wish you a erry Christmas and Prosperous New Year!.
P
 
Nimekuwa nikikufuatilia tangu enzi za kipindi chako cha KITIMOTO na hata mabandiko yako yalikuwa Yana msaada mkubwa na makini mpaka hapo ulipompiga swali zuri mwendazake na aka-panick akakuita kuwa ' Mayala' Ina maana ya 'njaa' na wewe ku-demonstrate Hilo ukaenda kugombea Ubunge Kawe na kuambulia kura 2,.
Baafa ya episode ya Kawe,ulikuwa DISTRACTED na hata hate reasoning yako ikabadilika na kuwa ya ki- chawa zaidi haswaa mabandiko yako ya kutetea COVID- 19 hayana msaada wowote Kwa jamii
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…