Hongera CCM: Umelijenga Taifa imara Kwa vizazi vijavyo

Hongera CCM: Umelijenga Taifa imara Kwa vizazi vijavyo

Usisahau pia viongozi wa kidini na kimila wamekua na mchango mkubwa katika makuzi ya viongozi wengi wamelelewa vyema asante Mwenyezi Mungu.
 
Ni nchi ngapi zisizo na amani duniani Hadi uone Tanzania ina bahati sana? Nchi zenye vita hazifiki hata 10% ya nchi zote duniani, Sasa what so special kwa Tanzania kuwa na amani?
Ila kwa sisi Tanzania Mungu yupo nasi zaidi kwani anatuepusha na majanga ya njaa na tsunam bila kusahau vita na Mafuriko
 
Ndio akili za wengi zilipoishia, badala ya kuheshimu Katiba tunaheshimu mtu
Katiba sio Msahafu au Biblia kwamba yaliyoandikwa humo hayabadilishwi. Katiba bora ni Ile inayochochea kasi ya mabadiliko hivyo hata iwe katiba ya namna gani kama itadumaza maendeleo itabadilishwa.

Lakini katiba yetu hii iwe ni 1977 au 1984 ni bora Kwa sababu:

1. 1978 iliisaidia Taifa kuwa wamoja kupambana na Nduli amini Kwa umoja. Ndio maana wataalamu wa katiba wanasema hii ni katiba bora na imesaidia kuvuka vipindi vigumu vya kisiasa ,mojawapo ni Hilo la Vita ya Kagera na lingine Lile la joto la kisiasa zanzibar la 1984.

2. Imesaidia kuleta umoja wa kitaifa Kwa kuunganisha dini, kabila na vyama vyote bila ubaguzi. Leo hii nchi yenye makabila zaidi ya 120 hakuna chokochoko za ukabila na wingi wa watu wanaokaribia milioni 70 na Bado imetamalaki ni jambo la kushangaza.

Hoja hizo mbili zinatosha kuelezea ubora wa katiba tuliyonayo lakini haimaanishi toka mwaka 1977 au 1984 hakuna mabadiliko yaliyowahi kufanywa kwenye katiba, yamefanyika mengi na yanaendelea kufanyika Kwa sababu katiba sio Msahafu au Biblia.

Tukimaliza kujadili ubora wa katiba yetu basi Kwa wasaa mdogo tukipongeze chama kulichotuletea katiba hii, HONGERA CHAMA CHA MAPINDUZI Kwa kutupatia katiba bora.
 
Tukimaliza kujadili ubora wa katiba yetu basi Kwa wasaa mdogo tukipongeze chama kulichotuletea katiba hii, HONGERA CHAMA CHA MAPINDUZI Kwa kutupatia katiba bora.
Katiba inayomwabudu Mtu, halafu unajichanganya sana, jifunze kujenga hoja
 
Ni nchi ngapi zisizo na amani duniani Hadi uone Tanzania ina bahati sana? Nchi zenye vita hazifiki hata 10% ya nchi zote duniani, Sasa what so special kwa Tanzania kuwa na amani?
Kwa hiyo unataka kusema hata kama ni 10% nchi zote sio lazima ziwe amani? Kwa kuwa Kuna nyingine hazina amani , basi hata Tanzania isipokuwa lisiwe jambo la kushangaza? Kwamba jitihada zinazofanywa za kutafuta amani ya kudumu kwenye hizo nchi hazina maana maana Kwa mtazamo wako Kuna kanuni na ulazima amani ikosekane kwenye baadhi ya nchi ili Maisha yasonge?
 
Katiba inayomwabudu Mtu, halafu unajichanganya sana, jifunze kujenga hoja
Kijana nimekuacha mbali sana kwenye kujenga hoja na Hilo kubali sio kurukaruka kama maharagwe.

Uwezo nilionao ni huu ,Nina uwezo mkubwa wa kujua unachofikiri na kuwaza ndio maana nakuacha kwenye masuala mengi.

Narudia Tena kusisitiza ,katiba sio Msahafu au Biblia na hapa duniani hakuna vitabu vikamilifu zaidi ya hivyo ni Kwa sababu vitabu hivyo vimeabdikwa nje ya upeo wa akili na ufahamu wa mwanadamu lakini kitabu chochote kinachoandikwa Kwa upeo wa akili na ufahamu wa mwanadamu vinabadilika. Kwa hoja hiyo tunakubaliana kwamba haijalishi uzuri wa katiba ,uzuri huo ni Kwa mahitaji ya Sasa , matumizi ya Sasa lakini Kwa baadaye katiba hiyo inaweza kuonekana ni mbovu Kwa sababu ya mahitaji ya wakati huo.

Kama unakubaliana na Mimi katika hoja hiyo ya kwanza ,hivyo utakubaliana na Mimi pia kwamba hakuna katiba bora ya wakati wote na hata tukisema Kila baada ya miaka 50 tuwe tunabadili katiba mpya ni Bure. Hivyo badala ya kubadili katiba mpya ni bora irekebishwe ili kukidhi mahitaji ya wakati.

Pia, kama umekubaliana na Mimi kwenye hizo hoja za juu pia utakubaliana na Mimi katiba kuwa na nguvu kuliko mtu ni dhana Kwa sababu katiba ni nyenzo tu ya kumsaidia mtu au kusaidia watu kufanya kazi. Hivyo katika hoja hii unakubaliana na Mimi kwamba katiba haiwezi kuleta maendeleo kama hakuna watu wa kufanikisha Hilo. Tofauti ya Biblia au Msahafu na katiba ni kwamba Biblia ni Mungu mwenyewe ila katiba sio Rais au yeyote hivyo yeyoto anayekuwepo ndio anaifanya katiba iwe yeye.

Ukinielewa nitashukuru ila usipoelewa pia nitashukuru zaidi maana ujumbe umefika
 
Kijana nimekuacha mbali sana kwenye kujenga hoja na Hilo kubali sio kurukaruka kama maharagwe.
Hahahaha sijawahi kuona CCM mwenye uwezo WA kujenga hoja, kuandika para nyingi doesn't mean unajenga hoja, labda hio hoja uwe unaandikia wale wanyonge wenu. Unajenga hoja kwa kuishukuru CCM eti ku-revise Katiba?? Unamshukuru Samia? Are you okay upstairs kweli??
 
Kijana nimekuacha mbali sana kwenye kujenga hoja na Hilo kubali sio kurukaruka kama maharagwe.

Uwezo nilionao ni huu ,Nina uwezo mkubwa wa kujua unachofikiri na kuwaza ndio maana nakuacha kwenye masuala mengi.

Narudia Tena kusisitiza ,katiba sio Msahafu au Biblia na hapa duniani hakuna vitabu vikamilifu zaidi ya hivyo ni Kwa sababu vitabu hivyo vimeabdikwa nje ya upeo wa akili na ufahamu wa mwanadamu lakini kitabu chochote kinachoandikwa Kwa upeo wa akili na ufahamu wa mwanadamu vinabadilika. Kwa hoja hiyo tunakubaliana kwamba haijalishi uzuri wa katiba ,uzuri huo ni Kwa mahitaji ya Sasa , matumizi ya Sasa lakini Kwa baadaye katiba hiyo inaweza kuonekana ni mbovu Kwa sababu ya mahitaji ya wakati huo.

Kama unakubaliana na Mimi katika hoja hiyo ya kwanza ,hivyo utakubaliana na Mimi pia kwamba hakuna katiba bora ya wakati wote na hata tukisema Kila baada ya miaka 50 tuwe tunabadili katiba mpya ni Bure. Hivyo badala ya kubadili katiba mpya ni bora irekebishwe ili kukidhi mahitaji ya wakati.

Pia, kama umekubaliana na Mimi kwenye hizo hoja za juu pia utakubaliana na Mimi katiba kuwa na nguvu kuliko mtu ni dhana Kwa sababu katiba ni nyenzo tu ya kumsaidia mtu au kusaidia watu kufanya kazi. Hivyo katika hoja hii unakubaliana na Mimi kwamba katiba haiwezi kuleta maendeleo kama hakuna watu wa kufanikisha Hilo. Tofauti ya Biblia au Msahafu na katiba ni kwamba Biblia ni Mungu mwenyewe ila katiba sio Rais au yeyote hivyo yeyoto anayekuwepo ndio anaifanya katiba iwe yeye.

Ukinielewa nitashukuru ila usipoelewa pia nitashukuru zaidi maana ujumbe umefika
Next time ukiwa unaandika utumbo kama huu, toka nje ya mawazo yako jiweke kwenye nafasi ya Watu wengine, Una akili Kabisa useme Katiba haiwezi kuleta maendeleo? Wewe ndio WA kujenga hoja? Hoja ndio hizi?? Au tafsiri ya Maendeleo kwako ni ipi?
 
Kwa hiyo unataka kusema hata kama ni 10% nchi zote sio lazima ziwe amani? Kwa kuwa Kuna nyingine hazina amani , basi hata Tanzania isipokuwa lisiwe jambo la kushangaza? Kwamba jitihada zinazofanywa za kutafuta amani ya kudumu kwenye hizo nchi hazina maana maana Kwa mtazamo wako Kuna kanuni na ulazima amani ikosekane kwenye baadhi ya nchi ili Maisha yasonge?
Hakuna siku mambo hayo yataisha duniani, yapo toka kuanza kwa Dunia hii, na yataendelea kuwepo. Na amani ni jambo lililo sehemu kubwa kwenye Dunia hii, hivyo sio jambo la kushangaza amani ikiwemo hapa Tanzania.
 
Next time ukiwa unaandika utumbo kama huu, toka nje ya mawazo yako jiweke kwenye nafasi ya Watu wengine, Una akili Kabisa useme Katiba haiwezi kuleta maendeleo? Wewe ndio WA kujenga hoja? Hoja ndio hizi?? Au tafsiri ya Maendeleo kwako ni ipi?
Nakuacha Kwa muda upunguze munkari maana naona nilivyokupeleka puta sana ,unaishia kuuliza maswali ya kitoto. Siku nyingine usivamie hoja bila kushibisha akili yako Kwa zana na dhana
 
Hakuna siku mambo hayo yataisha duniani, yapo toka kuanza kwa Dunia hii, na yataendelea kuwepo. Na amani ni jambo lililo sehemu kubwa kwenye Dunia hii, hivyo sio jambo la kushangaza amani ikiwemo hapa Tanzania.
Nilikuwa najua nimekuuliza maswali magumu mno na Hili jibu nilitegemea. Kwa nini? Upinzani unaamini muafaka wa kisiasa unaletwa na machafuko ,mawazo hayo unayo na wewe pia.
 
chama cha mapinduzi kimezidi kuwa mlezi wa taifa la tanzania mara baada ya kulikomboa toka mikononi mwa mabeberu
 
Next time ukiwa unaandika utumbo kama huu, toka nje ya mawazo yako jiweke kwenye nafasi ya Watu wengine, Una akili Kabisa useme Katiba haiwezi kuleta maendeleo? Wewe ndio WA kujenga hoja? Hoja ndio hizi?? Au tafsiri ya Maendeleo kwako ni ipi?
Narudia kusisitiza Tena na Tena , inawezekana una tatizo kubwa la uelewa. Katiba sio Msahafu au Biblia, ni kitabu kilichoandikwa Kwa upeo wa akili na ufahamu wa kibinadamu nimeona una muelekeo na mtazamo wa kuamini katiba ni kitabu kikamilifu na kilichopo mule ni ukamilifu tupu.

Maendeleo ni hali ya kutoka hali Fulani kwenda hali nyingine au kutoka hatua Fulani kwenda hatua nyingine. Katika somo la historia ,tunajifunza Kuna maendeleo katika zama tofauti na katika zama hizo maendeleo yaliletwa na utashi wa watu na hakukuwa na katiba.

Tuje kwenye swali la maendeleo yanaletwa na katiba. Kwangu nitasema hapana , Kwa sababu maendeleo ni mchakato na katiba sio mchakato. Mchakato wa maendeleo ndio unapelekea mabadiliko ya katiba na sio katiba kuleta maendeleo. Kama ingekuwa katiba inaleta maendeleo basi kusingekuwa na haja ya kufanya mabadiliko ya katiba ,ikiandikwa imeandikwa. Nadhani nimeeleweka bandugu
 
Nilikuwa najua nimekuuliza maswali magumu mno na Hili jibu nilitegemea. Kwa nini? Upinzani unaamini muafaka wa kisiasa unaletwa na machafuko ,mawazo hayo unayo na wewe pia.
Kabisa, kama mtaendelea kukaa madarakani kwa shuruti, sioni ni kwa jinsi gani kusitokee machafuko. Naona mnategemea mtaendelea kukaa madarakani kwa muda mrefu bila ridhaa ya walio wengi, hivyo uoga ambao mmeupa jina amani ndio nguzo yenu, mnajua siku uoga ukiondoka ndio mwisho wenu.

Hivyo mnang'ang'ania neno amani kama kichaka, lakini kiuhalisia mnataka uoga utamalaki Ili muendelee kukaa madarakani kwa shuruti. Machafuko tu, ama mapinduzi ya kijeshi ndio yataleta mabadiliko ya kweli ndani ya nchi hii.
 
Next time ukiwa unaandika utumbo kama huu, toka nje ya mawazo yako jiweke kwenye nafasi ya Watu wengine, Una akili Kabisa useme Katiba haiwezi kuleta maendeleo? Wewe ndio WA kujenga hoja? Hoja ndio hizi?? Au tafsiri ya Maendeleo kwako ni ipi?
Labda nizungumze Kwa mifano labda nitaeleweka zaidi. Mfano, kusingekuwa na nchi nyingine duniani na Tanzania ingekuwa ni nchi pekee, unafikiri maendeleo yangeletwa na katiba au utashi wa watu?

Nimekuuliza swali Hilo Kwa maana ya kwamba nimekusoma katikati na mstari na nimebaini tatizo lako. Unaamini bila katiba hakuna maendeleo na utashi bila katiba ni Bure.
 
Back
Top Bottom