Hongera Spika Dkt. Tulia Ackson. Kuna haja MaSpika wetu iwe lazima kuwa Wanasheria?

Pascal Mayalla

Platinum Member
Joined
Sep 22, 2008
Posts
53,857
Reaction score
121,995
Wanabodi,

Kama kawaida yangu kila nipatapo fursa, huja na makala za Kwa Maslahi ya Taifa, makala ya leo ni kuhusu umuhimu wa viongozi wetu na haswa wakuu wa Mihimili lazima sio tuu wawe wasomi, weledi na wachapakazi, bali lazima wawe Bright, brilliant na wabobezi wa fani husika.

Niko mahali nafuatilia Bunge Live, kiukweli kabisa nimekuwa very impressed na jinsi Madam Spika Dr. Tulia Akson anavyoliongoza Bunge.

Juzi aliifanua vizuri Ripoti ya CAG na kuifafanua ile kauli ya hasira ya Mama ya stupid na "Watupishe", ni walioongeza "cha juu" kwenye ununuzi wa ndege ya mizigo, na sio wote waliotajwa kwenye ripoti ya CAG.

Leo Mbunge wa Liwale kaibua kubwa kuliko Bungeni kuwa Bwawa la Mwalimu Nyerere, JNHPP japo liko Rufiji, bwawa hilo liko wilaya ya Liwale mkoani Lindi, na sio Mikoa ya Pwani na Morogoro, hivyo wilaya ya Liwale inastahili asilimia 60% ya mgao wa fedha za CSR ya JNHPP, lakini Liwale haikupata hata senti 5!.

Spika Tulia akaingilia kati kwa kumuuliza Mhe. Mbunge athibitishe Bwawa la JNHPP liko Liwale, Mbunge akasema lipo Liwale!.

Dr. Tulia akafafanua tofauti ya mahali Bwawa lilipo na the catchment area maji ya kulijaza bwawa yanakotoka!. Mhe. Mbunge akang'ang'ana bwawa liko Liwale!.

Dr. Tulia akamwambia Mhe Mbunge kuwa yeye na wabunge wamekwenda lilipo na hadi kubonyeza kitufe kukajaza maji, bwawa liko Rufiji na sio Liwale, hivyo akamwambia mbunge akae kwanza.

Kisha akauliza wahusika kama wapo waeleze Bunge bwawa la JNHPP liko wapi, ndipo akasimama Naibu Waziri wa Nishati, Byabato, akasema kwa mujibu wa ramani zao, bwawa la JNHPP liko Rufiji na Morogoro, ila kama Mbunge anayo ramani yake inayoonyesha bwawa liko Liwale, ailete na kuwaelimisha wengine tuko tayari kujifunza!.

Mbunge mwingine akasimama kuchangia kuwa bwawa liko Rufiji ila the catchment area ya maji ya bwawa hilo yanatoka Liwale.

Ndipo Spika Tulia akampiga darasa Mbunge huyo kuwa bwawa la JNHPP liko Rufiji ila maji ya kulijaza yanaweza kutiririka kutoka popote na kumruhusu kumalizia kuchangia.

Hii ndio faida ya kuwa na Spika msomi wa sheria, natumaini wengi unakumbuka uendeshaji wa Bunge enzi za Spika Sitta pia alikuwa ni msomi wa sheria.

Kwa vile mimi ni mtu wa mastori mastori
Ngoja niwape mastori ya Mimi na Dr. Tulia Akson, kwa msiopenda mastori jump kule chini
Tanzania tunakwama baadhi ya maeneo kwasababu tuna viongozi vilaza!. We can afford kuwa na wabunge vilaza, ndani ya Bunge la JMT but we can't afford kuwa na wabunge vilaza kwenye Bunge la EALA! Ubunge EALA, Wito Kwa CCM, Msiangalie Ukwasi, Tuteulieni, Wazalendo wa Kweli wa Taifa Hili, Wenye Uwezo na Uzoefu wa Kimataifa Kutuwakilisha Ipasavyo

Ili Tanzania tuweze kupata viongozi bora,, the best of the best, hatuwezi kuuendeleza ule ujinga uliochomekewa ndani ya katiba yetu kiubatili, kuwaachia kakikundi ka watu wachache kuamua huyu ni wenzetu mpe uongozi, hata kama ni vilaza!, na huyu sii wenzetu kata jina tupa kule, hatumuhitaji, hata kama ni the best bright and Brilliant

Kwa maoni yangu, nashauri Spika asitokane na ukanda wa chama cha siasa, Spika Dr. Tulia huyu, tunayemsifu leo, kuwa anakwenda kuwa Spika bora ndio Dr. Tulia yule yule aliye naibu Spika chini ya bora Spika, na alinyamaza kimya wakati katiba yetu ikikanyagwa Je, Bunge letu linaendeshwa kikada? Ili tuwe na Bunge la haki, lenye uwezo wa kuisimamia Serikali Kikamilifu, kuna haja Spika asitokane na vyama?

Hitimisho,
Nahitimisha kwa lile swali, la msingi la makala hii, kufuatia Spika Sitta na Spika Dr. Tulia Akson, ambao ni wanasheria, kuwa so good kwenye uendeshaji wa Bunge la JMT, kwasababu, they are smart, bright & brilliant! kuna haja sasa, kuanzia sasa kuhakikisha MaSpika wetu wote lazima wawe wanasheria?.

Wasalaam

Paskali
 
Spika ni mwasheria kwa kiwango cha shahada ya uzamivu, it was too low kwake kujadili hoja dhaifu kama hizo. Tunataka tuone mchango wake wakati sheria zinletwa bungeni.

 
Nini kazi ya Spika? Na Spika ni Jeshi la mtu mmoja au ana timu ya wabobebezi kwenye ofisi yake kwa ushauri wowote anaotaka na hata asioutaka, Binafsi naona she is just a rubber stamper na hilo lina-dilute kazi yoyote nzuri anayoweza kuifanya ukizingatia tunaamini kwenye illusion ya Separation of Powers

Nimeongelea part ya uzi wako pekee hayo mengine nimeachana nayo sababu naona siku hizi kuongelea issue kumekuwa diluted na sifa, kusifia na uchawa
 
Uchawa uchawa uchawa
 
Ofcourse pasipo mashaka yo yote ni aibu mkuu wa mhimili wa kutunga sheria asiwe mwanasheria au mtu mwenye uelewa wa sheria.....

lakini kipengele cha mbunge kuhamisha bwawa kwa fikra zake kimenichekesha sana. Nikawaza hata Jafo angedai kuwa lipo kisarawe
 
Uchawa uchawa uchawa
Hivi mtu akifanya jambo lolote zuri, no matter how big or small, mtu huwezi kumsifia mtu bila kuitwa chawa?. Huyu ni Mwalimu wangu wa 1st Year, nikamtabiria atakuwa spika, amekuwa Spika!. Kuna ubaya kumsifu?.
Hivyo ilipotokea wewe ni Mwanafunzi umekutana na Mwalimu wako mambo yanakuwa hivi Kuna ubaya?.
P
 
Suala sio kuwa tu na spika msomi bali ni kuwa na mtu mwenye utulivu wa akili kuongoza Bunge.

Bunge lenye watu zaidi ya 300 wenye hulka, sifa, Elimu na tabia tofauti unatakiwa uwe mtulivu sana na wakati wote akili inatakiwa ifanye kazi vizuri.

Sina shaka na uwezo Wa Spika wetu Dr.Tulia.

nadiriki kusema kuwa baada ya Spika mstaafu Mzee Msekwa, Spika mwengine atakaye ongoza Bunge kwa muda mrefu zaidi ni Dr. Tulia, tunamuombea uzima na uhai.
 
Sasa hapo kwenye maneno ya Tulia mbona sijaona hata neno moja la kisheria?

Naona umejisikia kumsifia huyo Tulia tu na ni haki yako kufanya hivyo ila siyo kisa ni mwana sheria.
 
Pascal, brilliance hapo iko wapi? Mtoto wa darasa la Saba au sekondari aliyefundishwa vema regional geography mbona atajibu tu vizuri?
Hapo excellence ya Sheria Iko wapi? Watu ilipotumika Sheria?

Bado una fight for uteuzi. Kazana more and more
 
hana lolote ashukuru tu pale anasimamia bunge la ng`ombez ccm bila upinzani smart
 
Hivi kumsifia mtu bila kuitwa chawa?. Huyu ni Mwalimu wangu wa 1st Year, nikamtabiria atakuwa spika, amekuwa Spika!. Kuna ubaya kumsifu?.
Hivyo ilipotokea wewe ni Mwanafunzi umekutana na Mwalimu wako mambo yanakuwa hivi Kuna ubaya?.
P
Hakuna ubaya maana hiyo ni haki yako ndugu Mayala.

Ila labda ungerekebisha kichwa cha habari uondoe sifa za uana sheria
 
Kwa aina ya wabunge waliopo bungeni kwa sasa hata mwanafunzi wa darasa la saba anaweza kuliongoza maana hakuna mwenye kutumia akili zake zaidi ya kufuata maelezo kutoka ndani ya chama ccm
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…