Hongera Waziri wa Kilimo Hussein Bashe kwa kutetea soko la wakulima, wanaokupinga ni wanafiki

Hongera Waziri wa Kilimo Hussein Bashe kwa kutetea soko la wakulima, wanaokupinga ni wanafiki

Hamna serikali imewahi kutoboa wakati wananchi wake wana njaa. Soon, tutajua kama hizo bei tunaweza kuzihimili au la.
Serikali inayojielewa haiwezi kutatua tatizo la mkate kwa kuharibu uwezo wa wazalishaji wa malighafi za mkate , itakuwa imetengeneza tatizo kubwa zaidi.

Kumbuka mazao yanapokuwa adimu pia gharama za uzalishaji zinaenda juu.

Serikali makini itatengeneza mazingira mazuri kwa wazalishaji ili kuongeza production na supply then demand itapungua na price itashuka
 
Wakuu nampongeza mh Bashe waziri wa kilimo kwa mengi aliyoyafanya kilimo, isipokuwa Kwa Leo nampongeza kwa msimamo wake wa kutetea wakulima juu kuuza mazao...
Na Mwaka huu wakulima itakuwa full neema ,soma hapa [emoji116]

Bodi ya Nafaka na Mazao Mchanganyiko (CPB) imesema imeongeza bajeti yake katika mwaka wa fedha 2022/2023 hadi kufikia shilingi billioni 100 ili kuwezesha ununuzi wa mazao na kuongeza uhifadhi wa nafaka kwenye maghala nchini.

Mwenyekiti wa CPB, Salum Awadhi amesema hayo katika kikao cha bodi ya nafaka kilichowakutanisha wadau mbalimbali ambapo licha ya changamoto za mfumuko wa bei ya mazao na nafaka kujadiliwa fursa mpya za mwaka 2023, pamoja na kilimo cha mkataba kwenye mazao ya ngano na alizeti.

Pamoja na mambo mengine mwenyekiti huyo ameweka wazi namna bodi hiyo ilivyojipanga kuwa sehemu ya kuwasadia wakulima kupata mbolea kwa wakati unaofaa baada ya serikali kuipa bodi hiyo jukumu hilo.

"Tunaamini msimu huu wakulima wengi watapata mbolea kwa wakati kwa sababu tumepewa jukumu hilo na mpaka sasa tumeshasambaza mbolea maeneo mengine ambayo mawakala wengi hawajafika," amesema mwenyekiti huyo.

Baadhi ya wafanyabiashara wakiwemo mawakala wa mazao na nafaka mchanganyiko waliohudhuria mikutano huo wameiomba bodi hiyo kutambua mchango wa mawakala katika usambazaji wa mazao ya nafaka sokoni nakupunguza adha kwa walaji.
 
Kama tusipokuwa na sera za kisasa za kilimo tutaendelea kufanya wakulima ambao ndio kubwa kuwa maskini
Na hatimaye kuendelea kuwa taifa maskini. Naamini kama taifa tukiweza kuwekeza kwenye kilimo kwa kuongeza uzalishaji kwenye killmo tunaweza kutoka kabisa kwenye umaskini.
Hili ndiko swali hata Waziri wa Fedha aliuza bungeni kwamba mnaelewa Kwa nini wakulima wengi Bado ni maskini? Sera mbovu
 
Anatetea wakulima au anatetea madalali?
Km hujawahi kua mkulima huwezi elewa kwa upana haya mambo.
Madalali hawawezi Toka Sokoni,dalali ukimfungia mipaka anatoa bei kiduchu Kwa mkulima ukimruhusu auze popote anatoa bei kubwa Kwa mkulima.

You can't eliminate intermediary kwenye biashara ya Kilimo na hao ndio distributors wa mazao
 
Mazao kama pamba,kahawa,korosho na yenyewe Bashe atasimama kidete wakulima wauze wanapotaka?

kahawa ya Bukoba wakulima walikua wakizuiwa wasipeleke Uganda, hivyohivyo na korosho pia ilikua inazuiwa isiuzwe nchi za jirani.
Nadhani ndivyo itakuwa maana nilimsikia hata Bashungwa kule kwao akisema wakulima wa kahawa Waachwe Wauze wanakotaka , Halmashauri ichukue ushuru.
 
Sasa sisi consumers tonao-feel the pinch ya hilo soko huria nani anatutetea?

Kama hiyo ndiyo sera nzuri, basi na sisi consumers turuhusiwe kununua mazao toka soko huria duniani bila vikwazo. Wapo wafanyabiashara wanaoweza...
Jiteteeni wenyewe au kalimeni na nyie mlete msawazo wa bei..

Wakati wenzenu wako maskini si mlikuwa mnawanyonya na kuwaona wajinga,Sasa ngoja muone joto la jiwe
 
Jambo zuri lakini tatizo anayoongea yatabaki kuwa kauli tuu, akija waziri mwingine naye atalipuka na sera zake na hata kuzuia wakulima wasiuze nje mazao yao, apigane alete muswada upitishwe bungeni ili anayoongea ndio yawe sera na sheria za kumwongoza mkulima, tuache blah blah kama mambo muhimu Bashe anajua cha kufanya sio kauli za majukwaani tu.
Itategemea na Rais husika au reaction ya Wakulima, wakulima wanatakiwa kuwa na chama Chao Ili akija mpuuzi kama huyo wakiamshe na kutishia kutolima kama kule India,hii ni muhimu Sana kwao.
 
Huu ni ujinga unaokaribia upumbavu.

Ni "kiwanda" gani ambacho serikali haihusiki nacho kwa njia moja au nyingine...
Sie wajinga tunaolima ndio tunanufaikaje Sasa wewe unatakaje labda? Naona mnajificha kwenye kichaka Cha walanguzi,lugha za wale failures
 
Sasa Bashe mwenyewe hatambui hilo.

Kwamba kama anataka serikali ijiondoe kabisa katika maswala ya wakulima, basi serikali hiyo hiyo itapashwa ijiondoe katika nyanja zingine zinazohusu maeneo mengine yanayowahusu wananchi kwa ujula (walaji/wanunuzi)...
Serikali inajiondoa kwenye kupangia wakulima bei au sehemu ya kuuza..

Inabakia na.jukumu la kuhakikisha uzalishaji unakuwa wa kutosha Ili kuleta msawazo wa bei.

Na wako clear kabisa kwamba Wao wataiwezesha bodi ya mazao Mchanganyiko na wakala wa Serikali kununua mazao ya kutosha Ili ikitokea bei kubwa sana sababu ya soko wao wataingiza bidhaa Sokoni kuleta unafuu,full stop simple and clear
 
Inawezekana mkulima akashindwa kushindana na waagizaji lakini sio lazima iwe hivyo, hata hao waagizaji wana gharama kubwa pia, mkulima akipewa masoko yote free ya ndani na nje pamoja na ruzuku lakini waagizaji wakamzidi acha ashindwe tuu, atatafuta shughuli nyingine ya kufanya au atalima mazao yanayoleta faida, free market haijawahi kumwangusha mtu na inajua kubalance kila kitu
Mtu mmja mjinga amekalia tuu ooh walanguzi mara wafanyabiashara na upuuzi kama huo.

Huyu mnaemuita mlanguzi/Mfanyabiashara ana incur costs kibao mfano usafiri,storage,Kodi za serikali eg TRA,Tozo za Halmashauri na Vijijini na wakala wa vipimo nk Sasa unategemea mkulima ndio atalipa hizo gharama?

Ndio maana Mbeya Ina GDP ya 3 Kwa Tanzania ila kwenye mapato ambayo TRA wanapata haipo hata top 10 Kwa sababu watu wake wengi wako kwenye shughuli za Kilimo ambazo sehemu kubwa hawalipi chochote wanauzia shambani
 
Wakuu nampongeza mh Bashe waziri wa kilimo kwa mengi aliyoyafanya kilimo, isipokuwa Kwa Leo nampongeza kwa msimamo wake wa kutetea wakulima juu kuuza mazao ....
Hakuna kitu hapo, ni siasa na blabla tu, Nilipata kufanya kazi wizara ya kilimo kwenye serikali ya awamu ya nne, ile document ya kilimo kwanza ulikuwa ukiisoma unaona sasa wakulima wanaenda kuneemeka.

Kilichotokea imebaki historia. tatizo nci hii kila Raisi akiingia anataka afanye kitu ili apite tena uchaguzi unafuata, baada ya hapo anayekuja naye anakuja na ya kwake na hakuna kinachokamilika na kuleta tija kwa wananchi.

Nchi hii siasa inavuruga kila kitu, mpaka wasomi na wataalamu wameamua kuwa wanasiasa maisha yaende.
 
Anatetea wakulima au anatetea madalali?
Km hujawahi kua mkulima huwezi elewa kwa upana haya mambo.
Kiufupi wanaoneemeka ni madalali na wafanyabiashara, na kwa uchache wakulima wakubwa wanaoweza tunza mazao yao.

Kwa wakulima wadogo (wa kujikimu), hata mahindi ya kula tu hawana, wengine wanauza yakiwa shambani. Wanaosema anatetea wakulima, wameamua tu kujitoa ufahamu kwa sababu wazijuazo wenyewe
 
Ku export mahindi kwa Karne hii kama taifa tukubali tuna tatizo kubwa.

Nchi inayojielewa ingekuwa Ina export bidhaa zitokanaxo na mahindi na bei kwa mkulima ingekuwa kubwa zaidi. Leo unauza mahindi Kenya halafu Kenya wanatengeneza unga wanakuja kukuuzia kwa bei kubwaaa.
 
Mkuu nimejibu kwamba sera nzuri ya serikali ni ile inayoangalia maslahi ya watu wengi katika nchi, Leo wakulima ni zaidi ya asilimia sitini ya watanzania achilia mbali wale wafanyakazi wanaotegemea kilimo pia kama njia nyingine ya kuongeza kipato chao

Pili suala la kuagiza nje hiyo ni sera nyingine ya mambo ya nje

kwa serikali ya taifa lolote lazima lilinde wazalishaji wake wa ndani kwanza kabla kuagiza bidhaa nje maana wazalishaji wa ndani ndio wanaoshikilia uchumi kuliko wachuuzi wa wanaogiza bidhaa nje ,
Swali je walaji wangapi wenye uwezo wa kuagiza nje kama sio kutegemea wachuuzi wachache wa kimataifa waongeze import kwa taifa

Hii ni sera ya kimapinduzi itawafanya vijana wengi wakinbilie kwenye kilimo kwa sababu wana uhakika wa soko
hivyo kilimo kuajiri mamillion ya vijana
Kuna pull and push attractive factor
serikali zilizopita zilitumia push attractive factor, mgambo na kuwafokea vijana waende kwenye kilimo kisicho na uhakika wa soko,

But akili kubwa imetumia pull attractive factor ya kutengeneza mazingira ya soko zuri hivyo vijana wengi watakimbilia fursa wenyewe ya kilimo
Unachokosea ni kufikiri kilimo kimeajiri watanzania wengi kwa sababu kina faida.
Kilimo kimeajiri watanzania wengi kwa sababu hakuna jinsi.
Matokeo yake watu inabidi tu walime Ili wajikimu. Unakuwa na agrarian economy.

Hakuna nchi tajiri duniani ambayo ina wakulima 60% hata ikiwa na wakulima 10% hiyo nchi lazima itakuwa masikini.

Tunataka kila mwaka tuambiwe ni jinsi gani productions costs za kilimo zimepungua.
Pia tujue mashamba makubwa mangapi yameanzishwa. Mashamba at least size ya ASAS.

Ukishusha gharama za uzalishaji utavutia wawekezaji wakubwa, kuwekeza kwenye mashamba makubwa. Hii itashusha Bei au itaongeza kipato cha mwananchi kwa sababu kilimo kutakuwa kama sehemu ya viwanda.

Mashamba makubwa ni viwanda.
Haya Mambo ya kuacha biashara ya kilimo iwe holela haitatufikisha popote.
Kilimo Ili kiimarike inabidi kifanywe na watu wachache. Siyo umvute kila mtu aanze kujilimia mihogo.

Watu wanahitaji nyama, samaki, maziwa, legumes etc... Vitu hivi Bei yake ni holela siku zote na vikipanda Bei zaidi tutazidi kudumaa, maana hata wakulima wengi hununua vitu hivi. Ndiyo maana tupo 10% ya nchi zinazoongoza kwa kudumaa duniani. People can't afford better nutrition kwa sababu ni Bei ghali.
 
Hakika hii inahamaisisha watu wengi kufikia kwenda kulima kwaajili ya chakula na biashara.

Jembe halimtupi mtu!
 
Back
Top Bottom