Hongera Waziri wa Kilimo Hussein Bashe kwa kutetea soko la wakulima, wanaokupinga ni wanafiki

Hongera Waziri wa Kilimo Hussein Bashe kwa kutetea soko la wakulima, wanaokupinga ni wanafiki

Mkuu ni kweli Waziri ameamua kwa dhati kabisa kuwaona wakulima wanapata sahihi kutokana na kazi zao. Aidha nadhani Waziri angeangalia pia suala la vipimo (kilo) katika soko wakati wa mauzoya mazao yao. Leo vile vipimo rasmi (mizani) havitumiki kabisa huko vijijini, hawa watu wanao itwa wanunuzi (madalalI)wa mazao ya wakulima wanatumia vipimo (ndoo ndogo/kubwa, mabeseni, magunia ya plastiki n.k) katika manunuzi, vitu ambavyo sio vipimo halali. Tunaomba Mh Waziri uliangalie hili, maana vipimo hivi Kilo 1 ya hawa madalali ni sawa na kilo 1. 5 hadi kilo 2. Lumbesa (kujaza mazao kwenye gunia na kuongeza kilemba juu) mara nyingi hufikia kilo 130 hadi 150 na mkulima anaaminishwa ni kilo 100, kwa kweli wakulima wananyonywa. Tunakuomba Mh. Tutatulie na hili, japo kuwa kwa sasa jambo hili ni kama donda ndugu.
Kukiwa na sehemu nyingi za kuuza hivi vipimo vya kinyonyaji vitajifia vyenyewe.
 
Soko huria siyo huria kama unayodhani. Nchi inalinda kwanza wazalishaji wake wa ndani na kuhakikisha ina export zaidi. Si rahisi kupunguza production cost sababu serikali italazimika kutumia pesa nyingi kwenye subsidizing. Njia nzuri ni kuhakikisha soko na bei nzuri. Hili halitavutia tu wawekezaji wakubwa kwenye kilimo, litafanya hata wale wadogo kuwa wakulima wakubwa.

Hao US kila siku wanawezesha wakulima wao kwenda kuuza mahindi na mazoa mengine ya kilimo Mexico huku wakifanya hila matunda ya Mexico(Maparachichi ya Mexico) yasifurike US ili kulinda wakulima wao.
Kupunguza production cost siyo lazima ufanye subsidy. Kwa mfano, unafahamu irrigation kwa mipaka 5 iliyopita imeongezeka kiasi gani? Na imechangia kiasi gani kwenye kilimo?
Hujui, Sasa utamuwajibisha vipi waziri wa kilimo ambaye hakuelezi hayo, anakwambia tumeanzisha mradi so and so wa umwagiliaji.
How many Hectares? Producing what?

How much money was spent on R&D? And what are the results?
Why there's no major agricultural investment?
Siyo lazima tu kutoa fedha za pembejeo.
 
Ndiyo ujiulize hilo swali Sasa.
Ukiwapa wakulima soko huria, basi wape consumers soko huria. Kuwapa consumers soko huria ni kuruhusu imports.

Otherwise, restrict wakulima na restrict consumers. Sasa hivi consumers wapo restricted, hiyo haisaidii taifa, wote tutakula chakula kidogo au kisicho bora.
Punguza production cost na uchochee uwekezaji wa mashamba makubwa.

United States Farm bill iliweka hela kwa wakulima(subsidy) na pia ikatoa food stamps kwa consumers ili waweze kununua vyakula.
You don't just allow food exports, utajimaliza.
Mkuu kimsingi sioni tatizo kwa Serikali kuruhusu wafanyabiashara kuagiza mazao (nafaka) nje ya Nchi ili mradi tu sheria za kodi zifuatwe. Mfanyabiashara alipe kodi stahiki. Kama kodi ya importation italipwa sawa sawa bado mkulima wa ndani atauza mazao yake bila shida yeyote na hata huyo importer hatamudu ku-import. NI suala la kujipanga na UZALENDO tu katika kumjengea mkulima uwezo. Mh Rais na Waziri waameanza wengine mfuate
 
Ndiyo ujiulize hilo swali Sasa.
Ukiwapa wakulima soko huria, basi wape consumers soko huria. Kuwapa consumers soko huria ni kuruhusu imports.

Otherwise, restrict wakulima na restrict consumers. Sasa hivi consumers wapo restricted, hiyo haisaidii taifa, wote tutakula chakula kidogo au kisicho bora.
Punguza production cost na uchochee uwekezaji wa mashamba makubwa.

United States Farm bill iliweka hela kwa wakulima(subsidy) na pia ikatoa food stamps kwa consumers ili waweze kununua vyakula.
You don't just allow food exports, utajimaliza.
Mkuu kimsingi sioni tatizo kwa Serikali kuruhusu wafanyabiashara kuagiza mazao (nafaka) nje ya Nchi ili mradi tu sheria za kodi zifuatwe. Mfanyabiashara alipe kodi stahiki. Kama kodi ya importation italipwa sawa sawa bado mkulima wa ndani atauza mazao yake bila shida yeyote na hata huyo importer hatamudu ku-import. NI suala la kujipanga na UZALENDO tu katika kumjengea mkulima uwezo. Mh Rais na Waziri waameanza wengine mfuate
 
Kupunguza production cost siyo lazima ufanye subsidy. Kwa mfano, unafahamu irrigation kwa mipaka 5 iliyopita imeongezeka kiasi gani? Na imechangia kiasi gani kwenye kilimo?
Hujui, Sasa utamuwajibisha vipi waziri wa kilimo ambaye hakuelezi hayo, anakwambia tumeanzisha mradi so and so wa umwagiliaji.
How many Hectares? Producing what?

How much money was spent on R&D? And what are the results?
Why there's no major agricultural investment?
Siyo lazima tu kutoa fedha za pembejeo.
Ubaya gharama nyingi hazipo kwenye kujenga irrigation schemes na research. gharama nyingi zipo kwenye input wakati wa kilimo. Mafuta ya kuendeshea mashine, madawa na mbolea. Njia bora ya kukabiliana na haya ni kuhakikisha mkulima anapata bei nzuri itayoendana na gharama za uzalishaji. Hapo ndipo utaweza kuvutia wakulima wakubwa na kukuza hawa wadogo.

Sisemi kuwa serikali haipaswi kujenga irrigation schemes na kufanya research za kilimo.
 
Huu ni ujinga unaokaribia upumbavu.

Ni "kiwanda" gani ambacho serikali haihusiki nacho kwa njia moja au nyingine!

Ni shughuli ipi yoyote inayofanywa ndani ya taifa lolote serikali isihusike na shughuli hiyo.

Ni mkulima gani mwenye uwezo wa kusimamia uuzaji wa mazao yake popote duniani bila ya ushiriki wa serikali kwa njia moja au nyingine?
Walanguzi wa mazao ya wakulima leo Bashe anawavisha jina la wakulima?

Bashe anatafuta sifa za kijinga kwa wajinga kama nyinyi.
Polepole wewe na hakuna haja ya kuitana wajinga na wapumbavu, naamini Bashe ana nia nzuri labda kama una ushahidi anatafauta sifa utuambie, na hakuna mtu ambaye hajui serikali ina mkono wake kila sekta, watu wengi wasichotaka humu ni serikali kupangiana bei na kuondoa freedom ya watu wauze wapi, waache market ijiendeshe sio kutafuta mshindi
 
Polepole wewe na hakuna haja ya kuitana wajinga na wapumbavu, naamini Bashe ana nia nzuri labda kama una ushahidi anatafauta sifa utuambie, na hakuna mtu ambaye hajui serikali ina mkono wake kila sekta, watu wengi wasichotaka humu ni serikali kupangiana bei na kuondoa freedom ya watu wauze wapi, waache market ijiendeshe sio kutafuta mshindi
"...market haijiendeshi" kiholela kama anayoizungumzia mheshimiwa wako Bashe, kwa serikali yake ijiondoe kabisa katika shughuli hiyo. Hilo haliwezekani. Lugha anayotumia ni lugha ya kilaghai, kutafuta sifa kwa wasiojua kinachozungumziwa.
 
Bashe ni mjanja sana mnamsifia anawatetea wakulima ni kweli lakini na yeye anajitetea humohumo, ana hundreds oh hectors huko Ikungi sijui anataka kulima zao gani, kama siyo alizeti basi korosho kwahiyo lazima ajiandalie mazingira mapema
Huyo ndo anafaa kuwa waziri wa kilimo sasa,
Kwa sababu anaply kilimo practically na anafahamu uhalisia sio hao wa kwenye makaratasi wamekaririshwa bei ikizidi unabana wakulima
Shabash !??
 
Wakuu nampongeza mh Bashe waziri wa kilimo kwa mengi aliyoyafanya kilimo, isipokuwa Kwa Leo nampongeza kwa msimamo wake wa kutetea wakulima juu kuuza mazao Yao waliyolima kwa gharama zao kuuza kwenye soko lolote Le ye tija kwao ndani na nje ya nchi.

Wakuu, lazima tutambue kwamba kwa sasa kilimo ni biashara na ni kiwanda ambacho kinahitaji gharama kubwa sana za uendeshaji pia kina kuwa na risk kubwa sana ya kupata hasara kwenye mchakato wake so ukimpa mkulima tena risk ya kupata soko unammaliza na kuua kilimo ambayo ni back bone ya uchumi wetu.

Kwa hiyo naona sera mh Bashe inaenda kuinua sekta ya kilimo ambayo ni Uti wa mgongo wa uchumi wa taifa hili, kwa sababu wakulima wana uhakika wa soko.

Pili Inakadiriwa sekta ya kilimo imeajiri zaidi ya watanzania asilimia sitini , Kwa hiyo watanzania asilimia sitini wamehakikishiwa uhakika wa ajira zao Tatu inaweza kuongeza mapato ya nje kwa sababu watanani wengi wenye akili hawataishia kulalamika ila wataona hiyo fursa na kwenda kuzalisha Kwa wingi ili kuuza kwa nje
Kwa uchache sana hizo ni faida za sera kilimo za Mh Bashe.

Wajinga ni wale ambao hawajui faida za hiyo sera wamebaki na fikra za kilimo cha miaka ya sabini. Wanafiki ni wale wanaotambua hizo faida ila wanapindisha ukwell kwa maslahi yao Wakiwemo baadhi ya wabunge waropokaji wasiopenda kupima ukweli wa mambo, mmoja nimemsikia nikashangaa sana.
Soko la wakulima wapi? Bashe anajua jinsi ya kucheza na akili za vilaza kama wewe, Wakulimawaliuza nafaka tangu mwaka jana mwezi wa 7 bei ikiwa chini gunia la mahindi lilikuwa sh 50, 000/ ahdi 40, 000/ Wakulimwa kwa sasa ndio wanao pelekewa mahindi ya msaaada
 
"...market haijiendeshi" kiholela kama anayoizungumzia mheshimiwa wako Bashe, kwa serikali yake ijiondoe kabisa katika shughuli hiyo. Hilo haliwezekani. Lugha anayotumia ni lugha ya kilaghai, kutafuta sifa kwa wasiojua kinachozungumziwa.
Inajiendeahaje mkuu ?
Serikali haiwezi kujiondoa kwa asilimia mia moja iaipokuwa inaweza kubaki TU kama referee wa mchezo sio kuamua mshindi

Lakini serikali ina wajibu wa kulinda timu yake ya ndani huo ndo uzalendo
 
Kwa mfumo wetu wa biashara wa sasa ,
Kuna product chain of supply,

Hii huwezi kuikwepa kirahisi kutoka Kwa mzalishaji mnunuzi wa jumla ,msafirishaji ,store muuzaji wa rejareja then mlaji. Hizo zote zinahitaji kugharama.

Hakuna namna mkulima ataweza kupeleka Moja kwa Moja kwa mlaji bila hiyo chain, either amue mwenyewe kutumia hizo gharama.

Kinachoathiri bei za hao wote mpaka kwa mkulima ni soko zuri I mean bei nzuri ya mazao. Soko linapokuwa baya linathiri chain nzima mpaka kwa mzalishaji /mkulima.
Soko lipi?
 
Soko la wakulima wapi? Bashe anajua jinsi ya kucheza na akili za vilaza kama wewe, Wakulimawaliuza nafaka tangu mwaka jana mwezi wa 7 bei ikiwa chini gunia la mahindi lilikuwa sh 50, 000/ ahdi 40, 000/ Wakulimwa kwa sasa ndio wanao pelekewa mahindi ya msaaada
Acha uongo mkuu kwa mwaka Jana Bei ya mahindi mpaka sasa iko juu sana hizo bei sijui umezitoa wapi
Hizo data kawadanganye wapambavu wenzako huko,
Kabla kuchangia hili jukwaa jitahidi akili ziwe zimetulia
 

Attachments

  • Screenshot_20230212-214525.png
    Screenshot_20230212-214525.png
    33 KB · Views: 3
Ubaya gharama nyingi hazipo kwenye kujenga irrigation schemes na research. gharama nyingi zipo kwenye input wakati wa kilimo. Mafuta ya kuendeshea mashine, madawa na mbolea. Njia bora ya kukabiliana na haya ni kuhakikisha mkulima anapata bei nzuri itayoendana na gharama za uzalishaji. Hapo ndipo utaweza kuvutia wakulima wakubwa na kukuza hawa wadogo.

Sisemi kuwa serikali haipaswi kujenga irrigation schemes na kufanya research za kilimo.
Hivyo vitu ulivyotaja ni constant na havina tofauti kubwa kati ya nchi na nchi. Lazima uangalie vitu ambayo vinakupa faida kubwa kulingana na nchi nyingine.
Proximity to large water sources Tanzania inazipiku nchi nyingi duniani. The challenge is on tapping that advantage.
Kuhusu madawa na mbolea, they can easily be reduced by R&D. Hapo ndipo tunapokwana.
R&D is the backbone of agriculture. Nchi zinazowekeza kwenye R&D ndizo zinazozalisha kwa Bei nafuu.
Kwa mfano tu, kutumia GIS kupulizia madawa na kumwaga mbolea, it's very effective na ni very easy but it needs massive soil sampling which is not that complicated. A lot of simple techniques can make a big difference in saving costs. Mafuta Bei yake hiyo hatuna sana nguvu ya kudhubiti bali kwa kuimarisha tafiti ambazo ni local.
Kumpa mkulima hela hakusaidii kwa sababu kama consumers hawatamudu, basi hakuna cha maana. Hapa nazungumzia mazao ya chakula
 
Mkuu kimsingi sioni tatizo kwa Serikali kuruhusu wafanyabiashara kuagiza mazao (nafaka) nje ya Nchi ili mradi tu sheria za kodi zifuatwe. Mfanyabiashara alipe kodi stahiki. Kama kodi ya importation italipwa sawa sawa bado mkulima wa ndani atauza mazao yake bila shida yeyote na hata huyo importer hatamudu ku-import. NI suala la kujipanga na UZALENDO tu katika kumjengea mkulima uwezo. Mh Rais na Waziri waameanza wengine mfuate
Hapana mkuu, mkulima wa Tanzania won't stand a chance. Kutaletwa Michele hapa labda uitoze Kodi 100% ambayo ni sawa na kuzuia importation.
 
Mleta maada ni kilaza na hao ndio Bashe anawapenda
Wewe ni miongoni either wajinga wasiojua faida ya free market, au mpambavu unajua lakini hutaki kubadilika anataka sera za sabini zitumike kutatua challenge za Karne ya 21,
Au mnafiki anayeping kila kitu hata ukweli for your own interest
 
Back
Top Bottom