Hongera Waziri wa Kilimo Hussein Bashe kwa kutetea soko la wakulima, wanaokupinga ni wanafiki

Hongera Waziri wa Kilimo Hussein Bashe kwa kutetea soko la wakulima, wanaokupinga ni wanafiki

Wakuu nampongeza mh Bashe waziri wa kilimo kwa mengi aliyoyafanya kilimo, isipokuwa Kwa Leo nampongeza kwa msimamo wake wa kutetea wakulima juu kuuza mazao Yao waliyolima kwa gharama zao kuuza kwenye soko lolote Le ye tija kwao ndani na nje ya nchi.

Wakuu, lazima tutambue kwamba kwa sasa kilimo ni biashara na ni kiwanda ambacho kinahitaji gharama kubwa sana za uendeshaji pia kina kuwa na risk kubwa sana ya kupata hasara kwenye mchakato wake so ukimpa mkulima tena risk ya kupata soko unammaliza na kuua kilimo ambayo ni back bone ya uchumi wetu.

Kwa hiyo naona sera mh Bashe inaenda kuinua sekta ya kilimo ambayo ni Uti wa mgongo wa uchumi wa taifa hili, kwa sababu wakulima wana uhakika wa soko.

Pili Inakadiriwa sekta ya kilimo imeajiri zaidi ya watanzania asilimia sitini , Kwa hiyo watanzania asilimia sitini wamehakikishiwa uhakika wa ajira zao Tatu inaweza kuongeza mapato ya nje kwa sababu watanani wengi wenye akili hawataishia kulalamika ila wataona hiyo fursa na kwenda kuzalisha Kwa wingi ili kuuza kwa nje
Kwa uchache sana hizo ni faida za sera kilimo za Mh Bashe.

Wajinga ni wale ambao hawajui faida za hiyo sera wamebaki na fikra za kilimo cha miaka ya sabini. Wanafiki ni wale wanaotambua hizo faida ila wanapindisha ukwell kwa maslahi yao Wakiwemo baadhi ya wabunge waropokaji wasiopenda kupima ukweli wa mambo, mmoja nimemsikia nikashangaa sana.
Huna akili
 
Inawezekana mkulima akashindwa kushindana na waagizaji lakini sio lazima iwe hivyo, hata hao waagizaji wana gharama kubwa pia, mkulima akipewa masoko yote free ya ndani na nje pamoja na ruzuku lakini waagizaji wakamzidi acha ashindwe tuu, atatafuta shughuli nyingine ya kufanya au atalima mazao yanayoleta faida, free market haijawahi kumwangusha mtu na inajua kubalance kila kitu
Unazungumzia 'Free market" na humo humo bado unaweka "ruzuku"?

Mkuu, hakuna soko huria la aina hiyo..
Na nikujidanganya na hizi nadharia zisizo na maana, kwamba kuna soko huria halafu katika jamii hiyo hiyo kuna makundi yanayofaidika kwa aina moja au nyingine kwa msaada wa ziada zaidi ya wengine.

Hizi ni nyimbo tunazoimbishwa tu toka vitabuni nasi tunaimba kama ma'robot' bila kuweka akili juu yake kuhusu uhalisia wake upoje.
 
Naungana na Bashe, kufunga mipaka ni kupunguza hali ya kulima, Acha watu wauze popote, Ili kesho wengi waingie kwenye kilimo KWA sababu jirani zao wamelima wamepata.
Tunataka tuone magari ya plate number za Kenya yakizurura hadi mashambani vijijini yakimwaga noti kwa wakulima kama zamani.
Kabla ya Magu gari za friji za Kenya unazikuta zimepaki shambani bagamoyo zinapakia tikiti, nanasi, matango nk mkulima unalambwa cash. Ndio unaoziona hizi nyumba za mabati zilizochipuka kama uyoga vijijini, hali ingeendelea kisingekuwepo kwa nyumba za nyasi vijijini.
 
Ujinga ni kutokujua jambo katika eneo Fulani ,
Nilitegemea baada ya kuelezea hapo juu mfumo WA supply unavyogusa maeneo mengi ungesoma na kulewa hivyo kupunguza ujinga lakini umeamua TU kujibu bila kuelewa mada

Kwenye suala la uchumi sera na aina mrengo wa kiuchumi wa serikali ndo inayoamua nafasi na majukumu ya serikali

Kwenye sera soko huria serikali haipaswi kuingilia soko kwa njia ya kidikteta Bali huacha soko liamue lenyewe , yenyewe hukusanya Kodi na ushuru TU,
Kwenye sera hii serikali Ina njia Moja TU ya kuingilia kwa kununua bidhaa kwa Bei ya soko na kuziuza kwa Bei inayotaka


Unaonyesha kweli una mawazo ya miaka ya sabini ndo maana unaita kwa hasira wafanyabiashara wa kati walanguzi
Suala la middle man kwenye biashara yoyote nimelezea halikwepeki , maana hakuna mkulima anaweza kusimamia gharama na michakato yote kutoka shambani mpaka kwa mlaji peke yake , Endapo atafanya hivyo utaingia kwenye risk kubwa zaidi maana Kila mchakato unahitaji mtaji na maarifa zaidi ya kuusimamia na serikali inahitaji vibali vyake

Hivyo soko lenye bei nzuri ndilo linaamua kiwango Cha faida kwanzia muuzaji wa reja reja jumla na mkulima,
Unapoharibu soko anayeumia zaidi ni mkulima ambaye ni mzalishaji

Mfano Lini serikali ilitangaza bei elekezi kwenye viwanda vya bahresa

Achana na fikra za kizamani za kijinga na za kijamaa zilizokandamiz uchumi wa wakulima na kuua uchumi wa nchi yetu,
Kama unaona wakulima wanafaidi kuchukue hiyo fursa sio kulalamikia serikali iwapangie wakulima bei ya mazao waliyolima wenyewe kwa gharama zao Tena Kwa mitaji ya kuungaunga
Mkuu 'Gift', kwa kawaida sina muda wa kupoteza kusoma magazeti kama haya unayoweka hapa. Hizi nadharia ni nadharia tu na common sense au intuition basi.
 
Sie wajinga tunaolima ndio tunanufaikaje Sasa wewe unatakaje labda? Naona mnajificha kwenye kichaka Cha walanguzi,lugha za wale failures
Toka kwenye ukulima, nenda kawe 'mlanguzi', bado huelewi?
Anayefaidika ni huyo anayenunua mazao yako siyo wewe mkulima.
 
Serikali inajiondoa kwenye kupangia wakulima bei au sehemu ya kuuza..

Inabakia na.jukumu la kuhakikisha uzalishaji unakuwa wa kutosha Ili kuleta msawazo wa bei.

Na wako clear kabisa kwamba Wao wataiwezesha bodi ya mazao Mchanganyiko na wakala wa Serikali kununua mazao ya kutosha Ili ikitokea bei kubwa sana sababu ya soko wao wataingiza bidhaa Sokoni kuleta unafuu,full stop simple and clear
Hapa bado unaiingiza serikali kwenye biashara, ambayo Bashe anataka serikali isijiingize kabisa..

Kwa maana hiyo, acha wanaoingiza bidhaa toka nje nao wawe huru kuingiza chochote wakati wowote.
 
Kama tutaanza kuangalia pain kwa mlaji bila kuangalia mzalishaji,
Tutakuwa hatujatumia akili zetu vizuri , Cha kwanza ni mzalishaji alindwe na atengenezewa mazingira ya kuendelea kuzalisha kwa wingi na kwa faida nzuri ili kumuongezea motisha ili kuhakikisha costastant supply.

Kumbuka sera nzuri ni ile inayobeba watu wengi na kumbuka asilimia sitini ni wakulima, ambao kwa wakati mmoja ni wazalishaji na walaji pia.

Kila taifa linaangalia uzalendo kwanza, tunaangalia sera ipi yenye manufaaa Kwa majority sio minority, ingawa minority nao wanaweza kutafutiwa unafuu pia lakini sio kuumiza majority.
Alichofanya ni kama kubeba maji kwenye ndoo yenye matobo akitegemea itajaa...Akifungua mipaka huku watanzania ambao ndiyo walaji ndiyo wanaotengeneza cash economy watapata wapi power ya kununua mazao ya mkulima? Huoni kawatengenezea quater wale wa nje na hivyo watakuja kuichukua na kwenda ku enjoy kwao huku wakiiacha nchi hoi?

Uki calculate welfare effects hiyo quater ime enda nje na both consumer na producer wamekuwa impacted negatively...Hesabu za uchumi siyo absolute kama mathematics au calculus lazima ujue conditionalities na physical nature ya transactions unayo deal nayo kuanzia levels mbalimbali...
 
Sasa Bashe mwenyewe hatambui hilo.

Kwamba kama anataka serikali ijiondoe kabisa katika maswala ya wakulima, basi serikali hiyo hiyo itapashwa ijiondoe katika nyanja zingine zinazohusu maeneo mengine yanayowahusu wananchi kwa ujula (walaji/wanunuzi).

Maana yake ni kwamba serikali isiingilie wafanya biashara wanaoingiza nfaka (mahindi) toka nje, na wao wauze kwa bei ambayo wananchi/walaji wataimudu.

Lakini hapa ni lazima ujue kwamba ikiwa kama unavyosema wewe"watu waachwe wafanye watakavyo"; maana yake huyo mkulima wa ndani hana kazi. Habari yake itakuwa ni historia.
Hakuna nchi kichaa ya kufanya hivyo. Nchi zote kwanza zinalinda wakulima wao kwa kuhakikisha wanapata bei nzuri za ndani na hata kuexport. Jambo la pili wanazuia na kubana import ya mazoa ambayo yanaweza kuzalishwa na wakulima wao. Kuingiza mazao kutoka nje ni pale imepatwa na uhaba au haiwei kuzalisha bidhaa hiyo. Biashara huria si ya kwenda kichwakichwa.
 
Mkuu hujajibu swali lake. Soko huria maana yake ni kuruhusu pia consumers wawe na bargaining power kwa kuangalia masoko mengine duniani. Kwa mfano mchele wa Pakistan. Au mahindi ya Mexico. Unafikiri mkulima wa Tanzania ata-survive?

Watumiaji wa mazao hasa ya chakula ni watanzania pia na inabidi walindwe. Tanzania ni moja ya nchi inayoongoza kwa udumavu wa watoto duniani. Watoto wengi Tanzania hawali chakula cha kutosha.

Njaa siyo mpaka watu wafe, that's the lowest bar ever na kiongozi kuwaambia hamfi njaa ni kiongozi ambaye ame-set standards ndogo sana, he's not revolutionary. Not good enough.
Hakunaga soko huria la namna hiyo. Serikali zote zinamanipulate hili soko huria kwa faida ya nchi zao. Kanuni ya kwanza ni kuhakikisha unafanya export kubwa kuliko import. Serikali inaweza hata ruhusu mahindi kutoka USA, sukari kutoka Brazil na mchele kutoka SEA, lakini ni akili hiyo kwa uchumi wa nchi?
 
Hakuna nchi kichaa ya kufanya hivyo. Nchi zote kwanza zinalinda wakulima wao kwa kuhakikisha wanapata bei nzuri za ndani na hata kuexport. Jambo la pili wanazuia na kubana import ya mazoa ambayo yanaweza kuzalishwa na wakulima wao. Kuingiza mazao kutoka nje ni pale imepatwa na uhaba au haiwei kuzalisha bidhaa hiyo. Biashara huria si ya kwenda kichwakichwa.
Naona wewe na Bashe hamuelewani.
Bashe yupo kwenye wizara ambayo wanunuzi toka nchi jirani wanakwenda shambani kwa mkulima na kununua mazao yangali shambani, na yeye Bashe hajui hilo kuwa linatokea nchini mwake.
Malori toka nje yanaingia ndani yanachukua mizigo Bashe hana habari, anasikia tu wakulima wameuza mazao yao wanakotaka wao!
 
Wakuu nampongeza mh Bashe waziri wa kilimo kwa mengi aliyoyafanya kilimo, isipokuwa Kwa Leo nampongeza kwa msimamo wake wa kutetea wakulima juu kuuza mazao Yao waliyolima kwa gharama zao kuuza kwenye soko lolote Le ye tija kwao ndani na nje ya nchi.

Wakuu, lazima tutambue kwamba kwa sasa kilimo ni biashara na ni kiwanda ambacho kinahitaji gharama kubwa sana za uendeshaji pia kina kuwa na risk kubwa sana ya kupata hasara kwenye mchakato wake so ukimpa mkulima tena risk ya kupata soko unammaliza na kuua kilimo ambayo ni back bone ya uchumi wetu.

Kwa hiyo naona sera mh Bashe inaenda kuinua sekta ya kilimo ambayo ni Uti wa mgongo wa uchumi wa taifa hili, kwa sababu wakulima wana uhakika wa soko.

Pili Inakadiriwa sekta ya kilimo imeajiri zaidi ya watanzania asilimia sitini , Kwa hiyo watanzania asilimia sitini wamehakikishiwa uhakika wa ajira zao Tatu inaweza kuongeza mapato ya nje kwa sababu watanani wengi wenye akili hawataishia kulalamika ila wataona hiyo fursa na kwenda kuzalisha Kwa wingi ili kuuza kwa nje
Kwa uchache sana hizo ni faida za sera kilimo za Mh Bashe.

Wajinga ni wale ambao hawajui faida za hiyo sera wamebaki na fikra za kilimo cha miaka ya sabini. Wanafiki ni wale wanaotambua hizo faida ila wanapindisha ukwell kwa maslahi yao Wakiwemo baadhi ya wabunge waropokaji wasiopenda kupima ukweli wa mambo, mmoja nimemsikia nikashangaa sana.
Bashe ni mjanja sana mnamsifia anawatetea wakulima ni kweli lakini na yeye anajitetea humohumo, ana hundreds oh hectors huko Ikungi sijui anataka kulima zao gani, kama siyo alizeti basi korosho kwahiyo lazima ajiandalie mazingira mapema
 
Naona wewe na Bashe hamuelewani.
Bashe yupo kwenye wizara ambayo wanunuzi toka nchi jirani wanakwenda shambani kwa mkulima na kununua mazao yangali shambani, na yeye Bashe hajui hilo kuwa linatokea nchini mwake.
Malori toka nje yanaingia ndani yanachukua mizigo Bashe hana habari, anasikia tu wakulima wameuza mazao yao wanakotaka wao!
Sasa hilo linashida gani? Serikali inachotakiwa ni kuhakikisha imenunua chakula cha kutosha kwa bei ya soko kufidia wakati wa njaa. Hii waliifanya wachina baada ya kupigwa na njaa na umasikini wakati wa Mao. baada ya Mao wakaja na Household responsibility. Unaiuzia serikali kiasi kadhaa cha mazao yako na mengine yote ni uu yako na jukumu lako kuyafanya utakavyo. Ukiuza , ukilisha wanyama ni wewe.
 
Serikali inajiondoa kwenye kupangia wakulima bei au sehemu ya kuuza..

Inabakia na.jukumu la kuhakikisha uzalishaji unakuwa wa kutosha Ili kuleta msawazo wa bei.

Na wako clear kabisa kwamba Wao wataiwezesha bodi ya mazao Mchanganyiko na wakala wa Serikali kununua mazao ya kutosha Ili ikitokea bei kubwa sana sababu ya soko wao wataingiza bidhaa Sokoni kuleta unafuu,full stop simple and clear
Kama ingekuwa hivi ingekuwa sahihi kwamba anaend akununua kwa mkulima na mkulima akishauza mazao yao yapo sehemu, yakiwa yameisha huko kwao serikali inaya rudisha sokoni na ndiyo hivyo nchi inakuwa haijapoteza, kinyume na hapo watu wa nje wananunua ama walanguzi (ambao ni wachache kwahiyo wanafanya monopsony kwakua hakuna masoko ya uhakika zaidi yao) na kwa bei ya chini kwa mkilima kisha wakisha ya toa mikononi mwa wakulima wanayarudisha kwa bei ya juu sokoni (Monopoly) kama ingekuwa ni wao tu boader imefungwa angalau tungekuwa na watanzania ambao watawekeza humu je ipo guaranteed? Kuna sera zipi za kuhakikisha hao wanunuzi walanguzi hawataenda kuwekeza nje ya nchi? Mbaya zaidi wanafungua mipaka na hivyo mazao yetu ambayo hayajawa processed yanaondoka na kwenda kuwa value added kisha yanarudishwa kwa walaji ambao unawakamua kodi kwa bei ya juu....Fungueni macho na masikio, uchumi haujengwi na mtu mmoja na wala si model moja unayoijua ndiyo infanya kazi, uchumi ni art na inahitaji magination and creativity ili kiweza kuujenga ndiyo sababu lazima saa nyingine utumie subjectivity na saa nyingine uwe objective....Tofaut na science zenye frames ambazo zipo absolute
 
Kiufupi wanaoneemeka ni madalali na wafanyabiashara, na kwa uchache wakulima wakubwa wanaoweza tunza mazao yao.

Kwa wakulima wadogo (wa kujikimu), hata mahindi ya kula tu hawana, wengine wanauza yakiwa shambani. Wanaosema anatetea wakulima, wameamua tu kujitoa ufahamu kwa sababu wazijuazo wenyewe
Sera mbovu ndizo zilizalisha madalali wanyonyaji. Mkulima hana options za pa kuuza hivyo anampa dalali kwa bei ya hasara. Leo hii kama wafanyabiashara wa nje wanafuata mizigo mashambani huyo dalali hatakuwa na nguvu. Cha muhimu ni sera hii kuwa endelevu tu. inatatua hata hiyo shida ya dalali mnyonyaji.
 
Hakunaga soko huria la namna hiyo. Serikali zote zinamanipulate hili soko huria kwa faida ya nchi zao. Kanuni ya kwanza ni kuhakikisha unafanya export kubwa kuliko import. Serikali inaweza hata ruhusu mahindi kutoka USA, sukari kutoka Brazil na mchele kutoka SEA, lakini ni akili hiyo kwa uchumi wa nchi?
Ndiyo ujiulize hilo swali Sasa.
Ukiwapa wakulima soko huria, basi wape consumers soko huria. Kuwapa consumers soko huria ni kuruhusu imports.

Otherwise, restrict wakulima na restrict consumers. Sasa hivi consumers wapo restricted, hiyo haisaidii taifa, wote tutakula chakula kidogo au kisicho bora.
Punguza production cost na uchochee uwekezaji wa mashamba makubwa.

United States Farm bill iliweka hela kwa wakulima(subsidy) na pia ikatoa food stamps kwa consumers ili waweze kununua vyakula.
You don't just allow food exports, utajimaliza.
 
Mkuu ni kweli Waziri ameamua kwa dhati kabisa kuwaona wakulima wanapata sahihi kutokana na kazi zao. Aidha nadhani Waziri angeangalia pia suala la vipimo (kilo) katika soko wakati wa mauzoya mazao yao. Leo vile vipimo rasmi (mizani) havitumiki kabisa huko vijijini, hawa watu wanao itwa wanunuzi (madalalI)wa mazao ya wakulima wanatumia vipimo (ndoo ndogo/kubwa, mabeseni, magunia ya plastiki n.k) katika manunuzi, vitu ambavyo sio vipimo halali. Tunaomba Mh Waziri uliangalie hili, maana vipimo hivi Kilo 1 ya hawa madalali ni sawa na kilo 1. 5 hadi kilo 2. Lumbesa (kujaza mazao kwenye gunia na kuongeza kilemba juu) mara nyingi hufikia kilo 130 hadi 150 na mkulima anaaminishwa ni kilo 100, kwa kweli wakulima wananyonywa. Tunakuomba Mh. Tutatulie na hili, japo kuwa kwa sasa jambo hili ni kama donda ndugu.
 
Ndiyo ujiulize hilo swali Sasa. Ukiwapa wakulima soko huria, basi wape consumers soko huria. Kuwapa consumers soko huria ni kuruhusu imports.
Otherwise, restrict wakulima na restrict consumers. Sasa hivi consumers wapo restricted, hiyo haisaidii taifa, wote tutakula chakula kidogo au kisicho bora.
Punguza production cost na uchochee uwekezaji wa mashamba makubwa.
United States Farm bill iliweka hela kwa wakulima(subsidy) na pia ikatoa food stamps kwa consumers ili waweze kununua vyakula.
You don't just allow food exports, utajimaliza.
Soko huria siyo huria kama unayodhani. Nchi inalinda kwanza wazalishaji wake wa ndani na kuhakikisha ina export zaidi. Si rahisi kupunguza production cost sababu serikali italazimika kutumia pesa nyingi kwenye subsidizing. Njia nzuri ni kuhakikisha soko na bei nzuri. Hili halitavutia tu wawekezaji wakubwa kwenye kilimo, litafanya hata wale wadogo kuwa wakulima wakubwa.

Hao US kila siku wanawezesha wakulima wao kwenda kuuza mahindi na mazoa mengine ya kilimo Mexico huku wakifanya hila matunda ya Mexico(Maparachichi ya Mexico) yasifurike US ili kulinda wakulima wao.
 
Back
Top Bottom