Zanzibar 2020 Hongera ZEC kwa maamuzi ya akili. NEC ni tatizo katika Uchaguzi wa Bara

Zanzibar 2020 Hongera ZEC kwa maamuzi ya akili. NEC ni tatizo katika Uchaguzi wa Bara

Zygot

JF-Expert Member
Joined
Apr 14, 2016
Posts
2,265
Reaction score
2,919
Nilisikiliza maamuzi ya ZEC juu ya pingamizi la mgombea wa ACT, Maalim Seif. ZEC iliona makosa ya ujazaji fomu lakini haikuona kama makosa hayo ni sababu ya kuharibu Uchaguzi. Kwa maana kwamba, kosa la ujazaji halikuwa na lengo la kunufaisha mgombea au kuufanya Uchaguzi usiwe wa haki n.k.

Tatizo liko kwa NEC, NEC imeonesha ubwege wa aina fulani na kuufanya mchakato mzima kuwa kama zoezi la watoto wadogo.

Ni aibu kwa chombo kama NEC kubariki mapingamizi yanayotokana na mgombea kutoweka nukta katika majina yake, kusahau kuweka sahihi, au kuweka sahihi kabla ya kuwasilisha fomu, nk. Mapingamizi mengi yaliyowekwa kuwazuia wagombea udiwani na ubunge kwa vyama vya upinzani yameonesha udhaifu mkubwa wa Tume.

Ni Tume isiyo na umahiri wa kisheria au inayofany kazi kujipendekeza na kupewa heko kwa idadi ya kuwazuia wagombea wa vyama vya upinzani.
 
Hizi ni Tume Mbili tofauti na kila TUME ina sheria, Kanuni na Miongozo yake! Kwahiyo Usitake NEC ifanye kazi kwa kufuata Taratibu za ZEC.

Kina Prof. Lipumba walipowekewa PINGAMIZI. NEC ilijibu kwa utaratibu huu ambao ZEC imetumia, Hilo hujaliona yani!

Tambua Kuna Mambo ya Muungano na yasiyo ya MUUNGANO!

Tusiwasikie Mkilalamika ZEC itakapoanza kushughulikia Rufaa, maana mmekuwa Vigeugeu kama bata mdondo!
 
Maamuzi ya kuzuiliwa wagombea wa upinzani yaliyopitishwa na NEC, yalinifanya nitafute video za maafisa wa NEC ili nione nyusoi zao zikoje. Wengine ukiwaangalia usoni unasoma ishara za udhaifu wa akili.

Yaani eti mgombea anazuiliwa kwa kuwa tu kuna sehemu aliweka sahihi kabla hajaruhusiwa na msimamizi. Bahati mbaya sana kwa madiwani na wabunge waamuzi ni wakurugenzi wa halmashauri; tuliowashuhudia ktk video wakiharibu fomu za wagombea kwa makusudi. NEC nao wakakaa kimya!
 
Hizi ni Tume Mbili tofauti na kila TUME ina sheria, Kanuni na Miongozo yake! Kwahiyo Usitake NEC ifanye kazi kwa kufuata Taratibu za ZEC.

Kina Prof. Lipumba walipowekewa PINGAMIZI. NEC ilijibu kwa utaratibu huu ambao ZEC imetumia, Hilo hujaliona yani!

Tambua Kuna Mambo ya Muungano na yasiyo ya MUUNGANO!

Tusiwasikie Mkilalamika ZEC itakapoanza kushughulikia Rufaa, maana mmekuwa Vigeugeu kama bata mdondo!
Nawe bonge la kimeo! Uko ndani ya Tume nini! Hujasikia wagombea udiwani na ubunge wakiambiwa waliweka sahihi kabla ya wakati?
 
Shida kubwa ni ule muhimili wa CHATO umejawa na uongo na dhuruma.

Taifa limehama kutoka utawala wa kisheria amani na upendo hadi kufikia taifa la dhuruma uongo mababe na Udikteta.

Heko Think tank
Heko PENTAGON.
 
Mimi tofauti ninayoiona ni kwamba huku NEC inaonekana wagombea wengi walioxhukua fomu ni mabwege na walilazimisha kuwa na sifa za kugombea wakati hawana, sasa NEC imelazimika kuwakata kwa sababu kama mgombea hajui kusoma na kuandika alafu analazimisha kupitishwa, mi naona NEC ilikuwa makini zaidi kwa kuzingatia matakwa ya kisheria.
 
ZEC na NEC ni vyombo huru kabisa na vinamfanya kazi kwa mujibu wa katiba.

Ndio maana unaona wametupilia mbali pingamizi lisilo na tija alilowekewa Maalim Self kama walivyotupilia mbali lile alilowekewa Lipumba na Magufuli.
 
Mimi tofauti ninayoiona ni kwamba huku NEC inaonekana wagombea wengi walioxhukua fomu ni mabwege na walilazimisha kuwa na sifa za kugombea wakati hawana, sasa NEC imelazimika kuwakata kwa sababu kama mgombea hajui kusoma na kuandika alafu analazimisha kupitishwa, mi naona NEC ilikuwa makini zaidi kwa kuzingatia matakwa ya kisheria.
Kwa maana hiyo ubwege uko vyma vya upinzani tu! Mbona CCM wamejaa?
 
Wagombea wa CCM walifanya kama fasheni kuwaondoa vyama vya upinzani kwa kutumia wakurugenzi wa halmashauri ambao wote ni makada wa CCM. KUwa kada siyo kosa, kosa ni kuchukuwa maamuzi ya kijinga kwa kushirikiana na mjinga.
 
]Kimsingi NEC na ZEC ni vyombo vya kusimamia na kuratibu chaguzi lakini kila moja inafanya kazi zake kwa mujibu wa Sheria, kanuni na taratibu sasa nakushangaa wewe unaejiita zygot kuleta hoja ya hovyo kabisa kuhusu mapingamizi ya kisheria wewe unaleta humu Kama story za vijiweni kwanza mlitakiwa mjitathimini kwanza kwamba kwanini wagombea wa upinzani wanashindwa kujaza forms? Je ni uelewa mdogo au uwezo mdogo wa kiungozi?

Kwa kuwa NEC inaendeshwa kisheria tuambie ni Sheria ipi TUME imevunja?. Imagine unaenda kumkabidhi kata,jimbo au nchi ambaye hata fomu tu ya kawaida sana Tena kwa maslahi yake inakuaje mbona uwezo wa hawa watu unatia shaka?. Mpaka muda huu NEC imewarudisha wagombea wengi kwenye nafasi zao mbona hizo husemi?
 
Wagombea wa CCM walifanya kama fasheni kuwaondoa vyama vya upinzani kwa kutumia wakurugenzi wa halmashauri ambao wote ni makada wa CCM. KUwa kada siyo kosa, kosa ni kuchukuwa maamuzi ya kijinga kwa kushirikiana na mjinga.
Ndio maana ya kuwa na NEC, wakurugenzi wanafanya walichoweza kwa level yao na mwenye mamlaka ambae ni NEC ameenda kutimilisha. Kwani bado kuna shida hapo?
 
[emoji3][emoji3][emoji1666] Kila siku ni kulalamika tuuu tena kwa kila kitu. Tatizo sana!!
 
Ndio maana ya kuwa na NEC, wakurugenzi wanafanya walichoweza kwa level yao na mwenye mamlaka ambae ni NEC ameenda kutimilisha. Kwani bado kuna shida hapo?
Shida ni moja tu waliopita bila kupingwa ni watu wenye nguvu zao kimwili na kifedha siyo walemavu!
 
Sawa uko sahihi. Kimantiki ZEC wana akili zaidi ya NEC. Wanatumia busara zaidi na wanatoa hoja za msingi kabisa.
 
Lissu anaposema mfumo wetu wa Elimu unapaswa kufumuliwa anamaanisha.

Fikiria kama waziri wa Elimu hawezi kujieleza vizuri kwa kutumia lugha aliyokuwa anafundishiwa kuanzia kidato cha kwanza hadi kwenye hiyo phd yake, watoto wa mlalahoi watakuwa na hali gani
 
Lissu anaposema mfumo wetu wa Elimu unapaswa kufumuliwa anamaanisha.

Fikiria kama waziri wa Elimu hawezi kujieleza vizuri kwa kutumia lugha aliyokuwa anafundishiwa kuanzia kidato cha kwanza hadi kwenye hiyo phd yake, watoto wa mlalahoi watakuwa na hali gani
Kuna watu wamezaliwa na kilema ambacho huwezi kiondoa kwa elimu.
 
Back
Top Bottom