Hoteli na Migahawa ya siku hizi imekaa kimchongo sana yaani hawataki kuandika menyu kabisa!

Hoteli na Migahawa ya siku hizi imekaa kimchongo sana yaani hawataki kuandika menyu kabisa!

Trainee

JF-Expert Member
Joined
Sep 22, 2018
Posts
2,660
Reaction score
3,501
Kwanza enzi hizo tulizoea jina moja tu la hoteli. Hili neno mgahawa lilikuja kama jipya/geni hivi na tukazoea taratibu kwahiyo hapa nitatumia neno mgahawa au hoteli kumaanisha kitu kimoja.

Sizungumzii makitu makubwa makubwa hapa nazungumzia vimigahawa vya kawaida vinavyopatikana uswahilini. Zamani tulizoea ukienda hotelini unaona ukutani MENU ya vyakula na bei zake hivyo kwa ajuaye kusoma kama ni mgeni wala hatapata tabu wala kuwapa taabu wahudumu kwa kuwauliza maswali mengi

Ajabu ya siku hizi ni kwamba wahudumu (hasa wanawake) wanaamini midomo yao kuliko maandishi, umefika mgahawani kimama kinajieleza mpaka kinaboa. Unakuta wateja kibao huku apike, huku aandalie wateja huku atafute chenji huku tena bado ajibu maswali ya wateja kuhusu vyakula alivyonavyo na bei zake. Matokeo yake nini sasa?

Ujue wabongo tulio wengi siyo mara zote tunakula tulichokipanga bali tunakula tulichokitamani. Wengine wana aibu kuuliza uliza maswali hawawezi au hawapendi kwahiyo unakuta umeagiza chakula fulani mara paap mwenzako mwingine kaagiza chakula kingine ambacho hukutarajia kabisa kama kipo. Unajikuta umeingia kwenye self conflict isiyo na maana

Halafu kumezuka mtindo mwingine tena mteja ukisema kwa mfano nipe supu utasikia ya ng'ombe au kuku, ukisema ya ng'ombe utasikia tena ya buku au buku mbili, ukisema ya kuku utasikia paja, shingo, bawa, kidali au paja ya juu nk mara chapati ngapi, ubwabwa wa sh ngapi..!? Maswali siyapendi haya! Kungekuwa na menu kwani tungesumbuana hivyo? Na of course mara nyingine haya makitu ndio yanaleta ugumu kuandika menyu maana orodha itakuwa ni kitini kizima

Miaka ya nyuma kule nyumbani ukisema supu ilikuwa ni tatu tu na hakuna maswali mengi (Kulikuwa kuna supu kama supu kisha kuna supu ya utumbo inayojumuisha mapupu na vitu vingine vya ndani kisha kulikuwa na supu ya kongoro, kuku enzi zile haikuwa ikipikwa supu- kuku ni mboga 🤣)

Tukirudi kwenye mada hebu andikeni menyu ya vyakula bana mturahisishie na mjirahisishie kazi. Binafsi nikifika hotelini huwa kama ni mgeni eneo hilo napata tabu sana maana kwanza sipendi maswali maswali lakini pia sijiandaagi kwamba naenda kula chakula fulani

#rudisheni menu migahawani#
 
Moderator pelekeni huu uzi jukwaa la mapishi huku hoja mchanganyikio tumeshachanganyikiwa na uchaguzi mbili haikai wala tatu... JamiiForums
Ila hao viongozi wana kazi kweli, ujue mimi kila nikiandika uzi huwa naupakia kwenye hoja mchanganyiko sijisumbuagi kutafuta jukwaa sahihi
 
Tukirudi kwenye mada hebu andikeni menyu ya vyakula bana mturahisishie na mjirahisishie kazi. Binafsi nikifika hotelini huwa kama ni mgeni eneo hilo napata tabu sana maana kwanza sipendi maswali maswali lakini pia sijiandaagi kwamba naenda kula chakula fulani
 
Ila hao viongozi wana kazi kweli, ujue mimi kila nikiandika uzi huwa naupakia kwenye hoja mchanganyiko sijisumbuagi kutafuta jukwaa sahihi
itakuwa sahivi wameenda mgahawani wanahangaika na menu ambayo haipo wakirudi watauweka jukwaa husika
 
Ajabu ya siku hizi ni kwamba wahudumu (hasa wanawake) wanaamini midomo yao kuliko maandishi, umefika mgahawani kimama kinajieleza mpaka kinaboa. Unakuta wateja kibao huku apike, huku aandalie wateja huku atafute chenji huku tena bado ajibu maswali ya wateja kuhusu vyakula alivyonavyo na bei zake. Matokeo yake nini sasa?
Ni kama vinyozi, wanaficha bei ili kuwaibia wasiouliza bei kabla ya kunyolewa, tulikuwa pale Mawasiliano kwenye mgahawa mmoja maarufu, jamaa kaja na mchepuko (nahisi alikuwa mwanachuo) maana walitokea bondeni kwenye lodge moja imejificha hivi, wakaagiza vyakula na vinywaji bila kuuliza bei, ulipofika muda wa kulipa jamaa hana hela ya kutosha mfukoni, akamuacha yule binti akaaga anakwenda kutoa fedha pale jirani na geti la kutokea mabasi kuna ATM, hakurudi jumla, yule binti alinyanyasika na kudhalilika kwa mambo aliyofanyiwa maana ilibidi apokonywe simu yake na baadhi ya wahudumu wakamwambia inawezekana hata huduma aliyotoa huko walikotoka haijalipiwa
 
Bongo kila sehemu ni janja janja hata trafiki akikukamata hakuambii kosa lako anakuuliza unajua kosa lako ukijichanganya tu imekula kwako
 
Back
Top Bottom