Hotuba ya masaa 7 mfululizo ya Luhaga Mpina ina ujumbe gani kwa watanzania?

Hotuba ya masaa 7 mfululizo ya Luhaga Mpina ina ujumbe gani kwa watanzania?

saidoo25

JF-Expert Member
Joined
Jul 4, 2022
Posts
624
Reaction score
1,456
LUHAGA MPINA, Mbunge wa Kisesa ametumia takribani masaa 7 mfululizo kuanzia saa 11 jioni hadi saa 6 na nusu usiku akizungumza na watanzania juu ya matatizo mbalimbali yanayolikabili taifa letu ikiwemo maonevu wanayofanyiwa wachimbaji wadogo wa madini kufukuzwa na maeneo yao kupewa raia wa kichina kinyume na sheria za nchi.

Amezungumzia makato makubwa waliyowekewa wakulima wa mazao kama pamba, choroko, mbaazi na kusababisha kunufaisha walanguzi na wakulima kubaki masikini, Amezungumia suala la viongozi ambao siyo raia wa Tanzania hali inayochangia kushamiri kwa rushwa, wizi, ufisadi wa mali za umma na kuwaonea wananchi wakiamini kuwa hii sio nchi yao na siku yoyote wataondoka kurudi makwao. KWA KIREFU Hotuba ya masaa saba imewafumbua macho watanzania wengi ambao wako gizani wakishabikia mipira ya simba na yanga huku taifa lao likizidi kutafunwa na kikundi cha watu huku watanzania wengi wakilia umasikini wa kutupwa.

Pia nilipomsikiliza anasema hotuba yake hiyo wakati akiiandaa amezingatia pia ushauri uliotolewa na Mzee Warioba, Mzee Butiku, Mbunge Kishimba, Mzee Kasori, Rostam Aziz, Mzee Charles Gishuli, Mzee Christopher Liundi, Padri Kitima na watanzania wengine wa kada mbalimbali.

Swali la muhimu Hotuba ya Masaa 7 ya Luhaga Mpina ina ujumbe gani kwa watanzania?
 
LUHAGA MPINA, Mbunge wa Kisesa ametumia takribani masaa 7 mfululizo kuanzia saa 11 jioni hadi saa 6 na nusu usiku akizungumza na watanzania juu ya matatizo mbalimbali yanayolikabili taifa letu ikiwemo maonevu wanayofanyiwa wachimbaji wadogo wa madini kufukuzwa na maeneo yao kupewa raia wa kichina kinyume na sheria za nchi.

Amezungumzia makato makubwa waliyowekewa wakulima wa mazao kama pamba, choroko, mbaazi na kusababisha kunufaisha walanguzi na wakulima kubaki masikini, Amezungumia suala la viongozi ambao siyo raia wa Tanzania hali inayochangia kushamiri kwa rushwa, wizi, ufisadi wa mali za umma na kuwaonea wananchi wakiamini kuwa hii sio nchi yao na siku yoyote wataondoka kurudi makwao. KWA KIREFU Hotuba ya masaa saba imewafumbua macho watanzania wengi ambao wako gizani wakishabikia mipira ya simba na yanga huku taifa lao likizidi kutafunwa na kikundi cha watu huku watanzania wengi wakilia umasikini wa kutupwa.

Swali la muhimu Hotuba ya Masaa 7 ya Luhaga Mpina ina ujumbe gani kwa watanzania?
Labda amewajulisha Watanzania kuwa, mna tabia ya kupenda zaidi hotuba za viongozi kuliko uwajibikaji wao kwenye shida zenu.

Ova
 
LUHAGA MPINA, Mbunge wa Kisesa ametumia takribani masaa 7 mfululizo kuanzia saa 11 jioni hadi saa 6 na nusu usiku akizungumza na watanzania juu ya matatizo mbalimbali yanayolikabili taifa letu ikiwemo maonevu wanayofanyiwa wachimbaji wadogo wa madini kufukuzwa na maeneo yao kupewa raia wa kichina kinyume na sheria za nchi.

Amezungumzia makato makubwa waliyowekewa wakulima wa mazao kama pamba, choroko, mbaazi na kusababisha kunufaisha walanguzi na wakulima kubaki masikini, Amezungumia suala la viongozi ambao siyo raia wa Tanzania hali inayochangia kushamiri kwa rushwa, wizi, ufisadi wa mali za umma na kuwaonea wananchi wakiamini kuwa hii sio nchi yao na siku yoyote wataondoka kurudi makwao. KWA KIREFU Hotuba ya masaa saba imewafumbua macho watanzania wengi ambao wako gizani wakishabikia mipira ya simba na yanga huku taifa lao likizidi kutafunwa na kikundi cha watu huku watanzania wengi wakilia umasikini wa kutupwa.

Swali la muhimu Hotuba ya Masaa 7 ya Luhaga Mpina ina ujumbe gani kwa watanzania?
Mbona unatuchanganya? Umeishasema "imewafumbua macho Watanzania" halafu inauliza eti ina ujumbe gani!!
 
Mbona unatuchanganya? Umeishasema "imewafumbua macho Watanzania" halafu inauliza eti ina ujumbe gani!!
mimi mwenyewe imenifumbua nilikua sijui kama migodi ya wachimbaji wadogo wamepewa wachina, samaki ziwa victoria wanavua hadi wachina, kariakoo wamachinga wanafanya wachina ndio maana nikasema imetufumbua ila je ina ujumbe gani kwa watanzania?
 
Back
Top Bottom