Hotuba ya Rais Rais Bunge la 12 ni nzuri lakini sikuipenda

Hotuba ya Rais Rais Bunge la 12 ni nzuri lakini sikuipenda

Mkuu 'kavulata', wewe ni GT (Great Thinker) wachache tuliojaliwa kubaki nao hapa JF.

Ni watu kama wewe mnaofanya hata tuliokata tamaa na jamvi hili, tunapokutana na mada kama hii yako, tuzidi kuendelea kuchungulia hapa hata kama ni kwa mara moja moja, tukitegemea tutakuta vito ya thamani kama hii yako.

Umeandika kifupi sana, lakini ni andiko linalojitosheleza kabisa; na kama pangekuwepo na vuguvugu linalopaswa kuwepo kwa mambo mazito kama haya, uzi huu ungechukua nafasi ya kipekee kabisa ndani ya jukwaa hili.

Sasa sijui mjadala huu kweli utafika wapi! Hii ndiyo JF ya sasa.

Umetaja mambo muhimu sana, na kama hotuba iliyabeba yote hayo, hiyo ni ishara mojawapo kwamba hata aliyeiwasilisha hotuba hiyo hakuwa makini. Haya siyo mambo ya kuyazungumzia kiujumla jumla, na juu juu tu. Hiyo ni agenda ya miongo kadhaa sio mambo ya miaka mitano au kumi.

Hiyo pekee ni ishara ya kuonyesha kwamba, hata anayenuia kuyafanya mambo hayo, hajui uzito wa mambo yenyewe upoje.

Sasa mimi ngoja nami nitoe matamanio yangu, kama ningekuwa kwenye nafasi ya kushauri au kusimamia mambo machache kabisa ambayo pengine ndio ungekuwa msingi imara wa kuyatimiza hayo matamanio yaliyotajwa hapo juu kwa ufanisi zaidi.

Katika miaka hii mitano, ningerudi kwenye 'basics' kabisa za kuimarisha ELIMU yetu na KILIMO chetu viwe vya ufanisi mkubwa kabisa.

Kilimo chetu ndio tegemeo kubwa la kuwaondoa waTanzania wengi katika rindi la umaskini. Imarisha kilimo kiwe cha tija, wakati huo huo ukijenga viwanda vya kusindika mazao ya wakulima na kuimarisha soko.

ELIMU yetu imeporomoka sana katika ngazi zote. Tunahitaji kuimarisha elimu isiwe ya kukaririsha tu watu ili waweze kwenda Bungeni kwenda kupiga stori. Tunahitaji elimu wezeshi, ya kuwafanya waTanzania kuitumia elimu katika kutatua matatizo yanayowakabili. Tunataka watafiti wanaoweza kufanya tafiti za nyanja zinazoinukia. Hatuhitaji watafiti kwenda kutafiti dawa za kienyeji, kuloweka mizizi kwenye maji na kutegemea kua dawa humo. Huu ni utafiti uliokwishapitwa na wakati wake. Hili nilinuia kulianzishia mada kabla sijasoma hii ya kwako, na pengine nitalitolea ufafanuzi zaidi kama mjadala huu utakuwa wa mvuto kwa wengi.

Wakati wataalam wanakuna vichwa kuhakikisha mgonjwa atibiwe kwa mahitaji yake na ugonjwa wake (individualized medicine) sisi kwanza ndio tunakumbuka mizizi/magome na majani? Hata Kitengo cha Dawa Asili kilichopo Muhimbili ambacho sasa kina umri wa zaidi ya miaka 30, tafiti kama hizi tayari hazina mvuto tena. Na sio swala la mvuto tu, ni kwamba hakuna kitu cha ziada huko! Nitakueleza kinachotakiwa kufanywa huko, ambacho bila shaka sio alichokusudia mtoa hotuba alipozungumzia swala hili.

ELIMU na KILIMO, hivi viwili vilitakiwa viwe vipaumbele vyetu vya kudumu tokea tupate uhuru wetu. Ingetokea ikawa hivyo, wakati huu, haya mengine yote muhimu uliyoorodhesha hapo kwenye mada na mengine yangekuwa yanatekelezwa vizuri sana hatua kwa hatua wakati huu.

Angalizo hapa ni kwamba sijaandika hapa hayo yasitekelezwe wakati tukiimarisha vipaumbele vyetu. Yatakuwa yanatekelezwa hatua kwa hatua. Kiongozi mmoja hawezi kamwe kutekeleza mahitaji yote muhimu katika ngwe yake, hata kama anayomipango ya kujiongezea miaka ya kudumu kwenye utawala wake.
Mkuu uko vizuri. Hayati Rais Mandela alisemaga huko nyuma kuwa Elimu ndio kitu kinachomkutanisha mtoto wa masikini na wa tajiri kwenye meza na ofisi moja. Kama kuna mtu mwenye uchungu sana na walala hoi basi awasomeshee watoto wao na sio kuwapa bodaboda ili wavunje miguu yao. Elimu lazima iwe ile inayoweza kumkutanisha mtoto wa tajiri na maskini sehemu moja darasani na kazini. Sasa hivi mtoto wa maskini hawezi kushindana na mtoto wa tajiri kupata nafasi ya kusoma chuo kikuu. Watoto wanaopata alama za juu za ufaulu kwenye mitihani hawatoki kwenye shule za kata. Watoto wengi wa maskini wanasoma vyuo binafsi vyenye ada kubwa kwasababu ya kushindwa kushindana kupata nafasi kwenye vyuo kama Muhimbili na UDSM.

Hata elimu inayotolewa haitoi wahitimu wanaoweza kushindana kwenye free market ya ajira. Hata maprofessor wetu ni wepesi sana kiviwango na hata kupambanua mambo. 99.1% ya maprofessor wetu wako kwenye payroll za serikali na wale waliostaafu wako kwenye payroll za taasisi binafsi wameajiliwa tena. Professor anashindwa kutoa ajira kwa watu japo 20. Elimu yetu lazina itazamwe upya.
 
Basi ujue, karibu kila mhadhiri na wasomi wengine wote ndoto zao zimeelekezwa huko! Wengi wa hawa watu ;aspirations' zao kubwa ni kuwa kama Kabudi. Ni wachache, kama wapo wana-'commitment' ya kweli na kazi zao.
👍👍👍
 
Mkuu 'marxlup', hali iko hivyo kwa sababu zinazojulikana na ndilo tatizo letu kubwa.

Unawaona akina Kabudi na ma-profesa wengi wengine waliposasa?

Basi ujue, karibu kila mhadhiri na wasomi wengine wote ndoto zao zimeelekezwa huko! Wengi wa hawa watu ;aspirations' zao kubwa ni kuwa kama Kabudi. Ni wachache, kama wapo wana-'commitment' ya kweli na kazi zao.

Na sio hao tu, hata mwalimu wa shule toka ya msingi na kwenye vyuo mbalimbali, ni wachache sana wenye kujitoa na kufanya kazi zao kwa kujituma zaidi na kwa ufanisi. Wengi wao wapo ili kutimiza wajibu na mradi mshahara unaingia.
Hata tafiti wanazofanya vyuoni ni kwaajili ya kupata hela za utafiti lakini hawamaanishi hasa kutatua tatizo kwenye jamii. wanapika matokeo yatakayosaidia wahisani wampe pesa. Tafiti zao zinazingatia kwenye kupata pesa za wafadhaili na kutokuwaudhi watawala
 
Mkuu uko vizuri. Hayati Rais Mandela alisemaga huko nyuma kuwa Elimu ndio kitu kinachomkutanisha mtoto wa masikini na wa tajiri kwenye meza na ofisi moja
Ni vizuria kabisa kumkumbuka Mandela kwa msimamo huo; lakini usisahau sisi wenyewe hapa Tanzania tulikuwa na kiongozi aliyeamini hivyo na akatimiza aliyaoyaamini juu ya hali hiyo.

Mwalimu Nyerere alihakikisha ufukara wa mzazi kamwe usingekuwa kikwazo cha mtoto kutofaidika na elimu kwa kadri ya uwezo wake, bila ya kuwepo tofauti na yule anayetumia utajiri wake.

Matokeo yake ndio hao akina Kabudi wengi waliopata elimu kutokana na juhudi hizo. Kwa bahati mbaya hawa vijana wa wakati huo waliopewa "akiba ya mwisho ya chakula kijijini kwao ili kukinusuru kijiji na janga la njaa", leo hii ndio wanawakandamiza wanakijiji waliotakiwa kuwasaidia kuleta neema ya kijiji. Leo hii wanawanyima haki zao kwa visingizio vya 'kuwaletea maendeleo'. Wanasahau kuwa maendeleo hayaletwi na wao, bali wananchi wenyewe ndio watakaojiletea maendeleo.
 
Hata elimu inayotolewa haitoi wahitimu wanaoweza kushindana kwenye free market ya ajira.
Unaongelea fani zipi za arts ? kama ni hizo hata mtu asome kenya au ulaya akija Tanzania hawezi compete

Fani za sayansi aliyesoma aweza compete popote mfano daktari ,engineer ,mwalimu wa hisabati,fizikia ,kemia,biologia nk ni moto wa kuotea mbali ila kama ni hayo masomo ya porojo hata usome ulaya ukija Tanzania kwenye free makert kibarua unacho kwenye competition
 
Unaongelea fani zipi za arts ? kama ni hizo hata mtu asome kenya au ulaya akija Tanzania hawezi compete

Fani za sayansi aliyesoma aweza compete popote mfano daktari ,engineer ,mwalimu wa hisabati,fizikia ,kemia,biologia nk ni moto wa kuotea mbali ila kama ni hayo masomo ya porojo hata usome ulaya ukija Tanzania kwenye free makert kibarua unacho kwenye competition
Hata usome nini hapa Tanzania kwenye vyuo vyetu utapata tabu sana kwenye competition, lazima utahitaji msasa. Tulikuwa na dk pekee wa moyo tanzania lakini akakubali kwenda kuwa katibu mkuu wizara ya maji.
 
Sijawahi kuona nchi imeendelea bila elimu na teknolojia yahali yajuu. Kwakweli hajaeleza ataiboreshaje elimu, hajaweka wazi serikali itainuaje kilimo chakisasa chaumwagiliaji kwa nguvu,haongei mbegu na mifugo yakisasa.

Hataji atavyosapoti tafiti na taasisi za tafiti mbalimbali nchini, anaeleza ataitunza amani bila kueleza haki zitakavyotimilizwa,haelezi gesi yetu itatusaidiaje,hasemi mbinu kuzuia magonjwa Bali kujenga Hosp. na kununua madawa,hajaweka wazi atavyoboresha maisha ya watu,ajira zitavyopatikana hasemi anataja tuu idadi yakusadikika.

Anaongea kujenga mameli,mabarabara kununua madege treni namavituvitu mmmno vinavyotoa hela kwenda nje ya mzungukk nchini bila kueleza tutajizatiti kuexport kitugani!

Binafsi sijaisapoti hotuba ile kwenye mia ningeipa 35 yaani D (dhaifu)
Hapo kwenye elimu, amefanya yafuatayo miaka 5 iliyopita:
1) Utoaji elimu bila malipo, elimu isiyo na viwango, msingi hadi form 4
2) madawati kwa kiasi fulani, lakini upungufu mkubwa wa majengo, na idadi kubwa ya watoto wanaketi chini
3) Uvurugaji mkubwa wa elimu ya chuo kikuu:
i) Wenzetu profesa anaendelea kutumika mpaka atakapochoka kabisa. Magu kaleta utaratibu unaowakatisha tamaa kabisa.
ii) Magu anadai vyuo vikuu vitoe gawio kwa serikali badala ya fedha hiyo kidogo kuelekezwa kwenye tafiti.
iii) Serikali ya Magu haiajiri, na amevuruga sekta binafsi. Mikopo anayotoa kapandisha riba, ajira hakuna. Atakuja nyonga watu kwa msononeko

4) Maslahi kwa walimu na wafanyakazi wote ni sifuri.

Sasa miaka 5 ijayo hakuna dalili ya maboresho yoyote. Hajui alipokosea, hakuna wa kumwambia atakapokosea sasa maana hakuna upinzani, vyombo vya habari kavididimiza, nchi nzima sasa ni kumwimbia mapambio. Atajenga mabarabara ba kununua madege kwa kasi na nguvu zaidi, bila kujali ulinganifu wa uchumi
 
Hapo kwenye elimu, amefanya yafuatayo miaka 5 iliyopita:
1) Utoaji elimu bila malipo, elimu isiyo na viwango, msingi hadi form 4
2) madawati kwa kiasi fulani, lakini upungufu mkubwa wa majengo, na idadi kubwa ya watoto wanaketi chini
3) Uvurugaji mkubwa wa elimu ya chuo kikuu:
i) Wenzetu profesa anaendelea kutumika mpaka atakapochoka kabisa. Magu kaleta utaratibu unaowakatisha tamaa kabisa.
ii) Magu anadai vyuo vikuu vitoe gawio kwa serikali badala ya fedha hiyo kidogo kuelekezwa kwenye tafiti.
iii) Serikali ya Magu haiajiri, na amevuruga sekta binafsi. Mikopo anayotoa kapandisha riba, ajira hakuna. Atakuja nyonga watu kwa msononeko

4) Maslahi kwa walimu na wafanyakazi wote ni sifuri.

Sasa miaka 5 ijayo hakuna dalili ya maboresho yoyote. Hajui alipokosea, hakuna wa kumwambia atakapokosea sasa maana hakuna upinzani, vyombo vya habari kavididimiza, nchi nzima sasa ni kumwimbia mapambio. Atajenga mabarabara ba kununua madege kwa kasi na nguvu zaidi, bila kujali ulinganifu wa uchumi
Hali vyuo vikuu ni mbaya sana, walimu na wanafunzi wote hawajui kiingereza wala kiswahili. Mitaala ya vyuo vikuu ina somo la English course (eti wanaita communication skills), vijana wanaotoka shule za umma hawajiwezi kabisa katika lugha ya kufundishia na wale wanaotoka shule za private wamekaririshwa majibu ya maswali hawawezi kujisomea wenyewe na kudadavua walichokisoma wanapofika vyuoni.
 
Imejaa mambo mengi sana ya kutimiza kwa miaka 5. Inatia mashaka kuwa huenda akaanzisha miradi mingi sana itakayolazimu aongezwe muda ili aikamilishe mwenyewe vizuri na kwa ubora kama alivyokusudia.

Ningetamani kama angejikita kwenye umalizaji wa reli, bwawa la umeme, uchimbaji wa chuma na makaa ya mawe na ununuzi wa meli za uvuvi kina kirefu tu.

Ningetamani kama angesema kwa miaka 5 ijayo Gesi yetu itatumika kuendesha magari yooote madogo ya majiji makubwa ili kuokoa pesa tunazonunulia mafuta.

Ningetamani kusikia watu wa Nyumbu kwa kushirikiana na UDSM, VETA, TIRDO, COSTECH wanashirikiana kutegeneza/kuunda mashine za kilimo kama matrekta ya bei nafuu kwa wakulima.

Anamaliza kaabiisa shida ya umeme na maji vijiji vyooote nchini 100% iliyodumu tangu wakati wa mkoloni.

Twende kidogokidogo bila kuumiza sana sehemu nyingine.
Kavulata hayo yooooote uliyotaja yatafanyika na kukamilishwa kwa umakini na usahihi wa AJABU. Hayo yote yamo kwenye ILANI YA CCM, tena in very detailed notes na kwa kila mkoa. Pata muda uisome baada ya kui - download kutoka tovuti ya CCM. Kila kitu kiko HADHARANI ndugu yangu. Halafu, utekelezaji wa ILANI hiyo ndiyo TEKE JINGINE LA MAUAJI litakalotumika dhidi ya wapinzani come 2025 elections kwa sababu haitaacha kufukua kila jiwe, yaani itafukua kila jiwe la kiutekelezaji.
 
Hapo kwenye elimu, amefanya yafuatayo miaka 5 iliyopita:
1) Utoaji elimu bila malipo, elimu isiyo na viwango, msingi hadi form 4
2) madawati kwa kiasi fulani, lakini upungufu mkubwa wa majengo, na idadi kubwa ya watoto wanaketi chini
3) Uvurugaji mkubwa wa elimu ya chuo kikuu:
i) Wenzetu profesa anaendelea kutumika mpaka atakapochoka kabisa. Magu kaleta utaratibu unaowakatisha tamaa kabisa.
ii) Magu anadai vyuo vikuu vitoe gawio kwa serikali badala ya fedha hiyo kidogo kuelekezwa kwenye tafiti.
iii) Serikali ya Magu haiajiri, na amevuruga sekta binafsi. Mikopo anayotoa kapandisha riba, ajira hakuna. Atakuja nyonga watu kwa msononeko

4) Maslahi kwa walimu na wafanyakazi wote ni sifuri.

Sasa miaka 5 ijayo hakuna dalili ya maboresho yoyote. Hajui alipokosea, hakuna wa kumwambia atakapokosea sasa maana hakuna upinzani, vyombo vya habari kavididimiza, nchi nzima sasa ni kumwimbia mapambio. Atajenga mabarabara ba kununua madege kwa kasi na nguvu zaidi, bila kujali ulinganifu wa uchumi
Hizo details nyingine wanazotaka, ZIMO KWENYE ILANI JAMANI! Nendeni mkayasome huko.
 
Imejaa mambo mengi sana ya kutimiza kwa miaka 5. Inatia mashaka kuwa huenda akaanzisha miradi mingi sana itakayolazimu aongezwe muda ili aikamilishe mwenyewe vizuri na kwa ubora kama alivyokusudia.

Ningetamani kama angejikita kwenye umalizaji wa reli, bwawa la umeme, uchimbaji wa chuma na makaa ya mawe na ununuzi wa meli za uvuvi kina kirefu tu.

Ningetamani kama angesema kwa miaka 5 ijayo Gesi yetu itatumika kuendesha magari yooote madogo ya majiji makubwa ili kuokoa pesa tunazonunulia mafuta.

Ningetamani kusikia watu wa Nyumbu kwa kushirikiana na UDSM, VETA, TIRDO, COSTECH wanashirikiana kutegeneza/kuunda mashine za kilimo kama matrekta ya bei nafuu kwa wakulima.

Anamaliza kaabiisa shida ya umeme na maji vijiji vyooote nchini 100% iliyodumu tangu wakati wa mkoloni.

Twende kidogokidogo bila kuumiza sana sehemu nyingine.
Mimi sikuelewa kauli hii aliyeielewa anieleze: "Uhuru na haki bila wajibu ni bure. Nahisi wamenielewa".
 
Unaongelea fani zipi za arts ? kama ni hizo hata mtu asome kenya au ulaya akija Tanzania hawezi compete

Fani za sayansi aliyesoma aweza compete popote mfano daktari ,engineer ,mwalimu wa hisabati,fizikia ,kemia,biologia nk ni moto wa kuotea mbali ila kama ni hayo masomo ya porojo hata usome ulaya ukija Tanzania kwenye free makert kibarua unacho kwenye competition
Nenda pale UDSM, maabara ya kemia ya wanafunzi 40 sasa wanahudhuria 200, utazania wapo kwenye mkutano wa ccm.

Kule Engineering, wataalamu mafundi wa kuongoza practicals za wanafunzi wanastaafu hakuna watu wa kuwaachia ujuzi walionao, ambao utausomea wapi? Maana hawa wapo toka enzi mjerumani amezifunga na kuwafundisha, na wakaenda ujerumani kwa mafunzo zaidi. Leo Magu haajiri technicians wapya, waliopo wanaondoka na ujuzi wao. Hakuna anayejali.
 
Sijawahi kuona nchi imeendelea bila elimu na teknolojia yahali yajuu. Kwakweli hajaeleza ataiboreshaje elimu, hajaweka wazi serikali itainuaje kilimo chakisasa chaumwagiliaji kwa nguvu,haongei mbegu na mifugo yakisasa.

Hataji atavyosapoti tafiti na taasisi za tafiti mbalimbali nchini, anaeleza ataitunza amani bila kueleza haki zitakavyotimilizwa,haelezi gesi yetu itatusaidiaje,hasemi mbinu kuzuia magonjwa Bali kujenga Hosp. na kununua madawa,hajaweka wazi atavyoboresha maisha ya watu,ajira zitavyopatikana hasemi anataja tuu idadi yakusadikika.

Anaongea kujenga mameli,mabarabara kununua madege treni namavituvitu mmmno vinavyotoa hela kwenda nje ya mzungukk nchini bila kueleza tutajizatiti kuexport kitugani!

Binafsi sijaisapoti hotuba ile kwenye mia ningeipa 35 yaani D (dhaifu)
Hajazungumzia katiba mpya ambayo itatoa dira ya jinsi ya mfumo wa utawala utakao endana na karne hii ya tehama. Bila mfumo wa kiutawala unaoendana na matakwa ya karne hii ya tehama yote aliyotaja kutekeleza ni kusadikika.
 
Kavulata hayo yooooote uliyotaja yatafanyika na kukamilishwa kwa umakini na usahihi wa AJABU. Hayo yote yamo kwenye ILANI YA CCM, tena in very detailed notes na kwa kila mkoa. Pata muda uisome baada ya kui - download kutoka tovuti ya CCM. Kila kitu kiko HADHARANI ndugu yangu. Halafu, utekelezaji wa ILANI hiyo ndiyo TEKE JINGINE LA MAUAJI litakalotumika dhidi ya wapinzani come 2025 elections kwa sababu haitaacha kufukua kila jiwe, yaani itafukua kila jiwe la kiutekelezaji.
We need a full and comprehensive Constitutional Reform to ensure freedom and justice prevails to all. Not "Mateke ya mauwaji" to the opposition.
 
Kavulata hayo yooooote uliyotaja yatafanyika na kukamilishwa kwa umakini na usahihi wa AJABU. Hayo yote yamo kwenye ILANI YA CCM, tena in very detailed notes na kwa kila mkoa. Pata muda uisome baada ya kui - download kutoka tovuti ya CCM. Kila kitu kiko HADHARANI ndugu yangu. Halafu, utekelezaji wa ILANI hiyo ndiyo TEKE JINGINE LA MAUAJI litakalotumika dhidi ya wapinzani come 2025 elections kwa sababu haitaacha kufukua kila jiwe, yaani itafukua kila jiwe la kiutekelezaji.
Mnapomsifu mkiambiaji usisahau kumsifu na anaemkimbiza. Kama CCM itafanya vizuri kwaajili ya 2025 basi sisi wananchi hatunabudi kuisifu CCM lakini bila kusahau kuisifu Chadema. Huu ni ushahidi kuwa upinzani umekomaa nchini kiasi cha kuisukuma ccm itende yale ya wananchi. Na hii ndiyo sababu ya baba wa Taifa kupigania uwepo wa vyama vingi vya siasa hata baada ya 80% ya wananchi kuvikataa. Bila ya chadema imara 2015 CCM isingempendekeza Rais JPM kuwa mgombea wake. Hivyo hata JPM atalazimika kuishukuru chadema na Lowassa waliosababisha yeye apewe nafasi hiyo kukabiliana na Lowassa.

Pamoja na hayo ni heri kufanya vitu vichache kwa ubora wa hali ya juu kuliko vitu vingi vya juujuu. Mfano, tulijenga vituo vya afya vingi lakini hakuna dawa, vifaa tiba, watumishi, maji na fedha za uendeshaji. Tumejenga shule nyingi lakini hakuna walimu, viti, maabara, mabweni, na ukaguzi
 
Hana Mpya unapata wapi muda wa kumsikiliza mtu ambaye hakuchaguliwa kihalali.
 
Hali vyuo vikuu ni mbaya sana, walimu na wanafunzi wote hawajui kiingereza wala kiswahili. Mitaala ya vyuo vikuu ina somo la English course (eti wanaita communication skills), vijana wanaotoka shule za umma hawajiwezi kabisa katika lugha ya kufundishia na wale wanaotoka shule za private wamekaririshwa majibu ya maswali hawawezi kujisomea wenyewe na kudadavua walichokisoma wanapofika vyuoni.
Walimu vijana wa vyuo vikuu kwa kweli wanatisha. Ni Doti Komu ya kufa mtu. Ni kweli wazuri wapo, lakini wabovu ni asilimia kubwa zaidi.

Ni vicious circle inayoteremka chini. Hili ni Bomu la Nuclear
 
Walimu vijana wa vyuo vikuu kwa kweli wanatisha. Ni Doti Komu ya kufa mtu. Ni kweli wazuri wapo, lakini wabovu ni asilimia kubwa zaidi.

Ni vicious circle inayoteremka chini. Hili ni Bomu la Nuclear
Eti kigezo cha kuwa mwalimu chuo kikuu ni GPA, kigezo hiki pekee sio halisia hasa katika katika kuwapata walimu hasa katika mataifa maskini ambayo rushwa za aina zote zipo. Waweza kuta MTU ana GPA kubwa lakini hajui kitu.
 
Back
Top Bottom