Hotuba Ya Rais Samia Yapongezwa kila Kona Mitaani, Yawakosha na kuungwa Mkono na Watanzania

Uongo na unafiki ni mbaya kuliongoza taifa kubwa kama Tanzania , hotuba ya jana ilijaza watanzania wengi hofu nakupoteza imani dhidi ya serikali yake ,serikali yenye uwezo wakulinda usalama wa raia na mali zake , lakini usalama unakosekana anasema jeshi lisilaumiwa hata nchi nyingine yanatokea , alipaswa atoe tamko lakukabiliana na machafuko haya ,, lakini chaajabu kaishia kulisify Jeshi kwa kazi nzuri, ambalo kwa sasa wanaharakati wengi wanaopotea na Jeshi limehusishwa kwa tuhuma hizo , Taifa linahitaji kiongozi mwenye kulipenda Taifa lake na watu wake wote .haijalishi anakosolewa au hakosolewi.
 
Nasikia mnalipwa elfu 8 kwa sasa kutoka elfu 7 hapo awali.

Wahi Lumumba ukapate mgawo wako.
 
Hotuba ya Rais Samia imewapa matumaini makubwa sana watanzania juu ya kuendelea kutamalaki kwa amani na utulivu kwa Taifa letu ,huku likiwa limejaa upendo na mshikamano. Jeshi letu lipo imara na ndio maana wetu wanaendelea kufanya shughuli na biashara zao hadi usiku wa manane. Matukio hayo machache ambayo hutokea hata kwingineko Duniani yataendelea kudhibitiwa vizuri.
 
Nasikia mnalipwa elfu 8 kwa sasa kutoka elfu 7 hapo awali.

Wahi Lumumba ukapate mgawo wako.
Sipo hapa kwa ajili ya kulipwa.nipo hapa kwa ajili ya Taifa langu linaloongozwa vyema kabisa na Rais wetu mpendwa Daktari Mama Samia Suluhu Hasssan
 
Safi sana Kada wa chama
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…