Hotuba ya Warioba Bungeni Dodoma: Jumanne, Tarehe 18 Machi 2014 na Hoja ya Muungano wa Serikali Tatu


moja ya sababu ya ujio wa vyama vingi ndo hiyo,tunagombana mpaka ngaz ya familia kwa tofaut za kisiasa,mtu wa chama fulan hata akiongea ponit as long mpo tofaut basi watu wanampinga
 
Jaji amesema hatua hii inamuondoa Rais kwenye bunge kwani kwa kuwa na Mawaziri ndani ya bunge Hilo kunalifanya bunge kushindwa kuisimamia serikali ipasavyo kwa kuwa serikali ni sehemu ya bunge Hilo.

Amesema Mawaziri watateuliwa na Rais NA kuthibitishwa na bunge . Aidha , rasimu ya Katiba inapendekeza kuwa Rais achaguliwe kwa kupata kura zaidi ya asilimia 50 ya kura zote .

Rais Mara baada ya uchaguzi na kutangazwa na Tume ya uchaguzi anaweza kufikishwa mahakama ya rufaa kuhoji uhalali wake na mgombea yeyote wa kiti hicho aliyeshindwa na Shauri hilo kuamuliwa ndani ya mwezi mmoja.

Jaji Warioba amesema Rasimu ya Katiba inapendekeza kuwepo NA ukomo wa wabunge wa miaka 15 ya kukalia kiti hicho mfululizo ili kuondoa dhana ya umiliki wa ubunge na kuimarisha uwajibikaji.

Hakutakuwepo na uchaguzi mdogo endapo Mbunge atafariki badala yake nafasi hiyo itazibwa na jina litakalokuwa kwenye orodha zilizoandaliwa NA vyama vya siasa vyenye wabunge husika na kuwasilishwa kwa Tume ya Uchaguzi.

Aidha, Spika na Naibu Spika hawatatokana na Mawaziri, Naibu Waziri NA wabunge ili kupata viongozi ambao hawataelemea upande wowote.
 

Sijui ni hisia sijui nini, kwa kweli sijui, Mtanzania mimi leo nimesisimkwa na mwili kwa nondo ambazo mzee Warioba alikuwa anazitoa! Kuna wakati nilikuwa nasisimkwa na presentation hadi natokwa na machozi. Mwenzangu niliyekuwa nae akasema kaka unahisia, nikamwambia unajua hamna kitu bora kama facts. Unajua kwa sie wengine tuliosomea hesabu hamna jibu la kubahatisha, ni straight, na ndicho alichofanya leo mzee Warioba!
 
Lissu anahusika vipi na hotuba ya Warioba, lini wazenji walimchukia Warioba.
 

Pamoja na mawazo yako kumbuka hoja ya serikali mbili au tatu haiepukiki kuijadili, kwani hayo uliyosema utayafanikisha katika serikali ipi 'fikiria tena'
 
haya ndiyo mawazo mgando sasa tunayosema. warioba hajaongea maneno kutoka kichwani kwake ww mbwiga hayo ni matokeo ya utafiti na mawazo ya wananchi waliosoma na wanaojua historia ya nchi na c washamba kama wewe
 
ndo kusema wameelewa wamechanganyikiwa or.......... malizia mengine........
 

Attachments

  • 1904051_609078335837488_469303939_n.jpg
    6.8 KB · Views: 260
Warioba akzidi nifurahisha alipotoa mifano ya makundi yaliyosuggest serikali 3..akasema hadi taasisi za serikali na mihimili km Bunge....akasema na baraza la mawaziri la Zenj wote walikuwa ktk serikali ama 3 ama muungano wa mkataba ambao ujumla wake ni serikali zilezile 3... Maccm bado ulevi unawasumbua.
 
Mungu akubariki Ritz kwa kuutambua na ujasiri wa kuukiri ukweli.by the way vyama na sera zinapita lakini umoja na nchi yetu vitabaki milele. aidha hapa hakuna mshindi kama kalenga bali watanzania ndio tumeshinda kwa ujumla wetu

Hata mimi nawaomba wanaopost sasa wasiseme nani kashinda nani kashindwa ila tuiunge mkono Rasim tu ili ipite! Kwa dhati kabisa tume haikuwa na nia mbaya, na hayo yalikuwa maoni ya Wananchi!
 
Msalani siyo lazima uchangie kila thread. "Solid Food for Matured People Only, not for Babies". Unafahamu umafia wa Mahakama zetu? Sometimes zinaendeshwa kama "Kangaroo Courts" kwenye "Banana Republics"
 
JK atakacha majungu kesho kutwa km alivyowatosa CCM ktk maoni ya CDM ..CCM walikuja juu sana CDM walipoingia Ikulu na k umwacha JK akiwa na mawazo yao..CCM wakaishia kudai kuwa CDM wali enjoy juice ya ikulu...eti waliona wivu
 
Nimependa busara ya Tume ya Warioba. BMLK liige busara hizo:
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…