Kwa mujibu wa ripoti ya mwenyekiti wa tume ya kuaandaa rasimu ya katiba aliyoitoa mnamo tarehe 30/12/2013 inaonyesha kuwa takribani 61% kutoka Tanzania bara waliunga mkono hoja ya serikali tatu na 60% kutoka Zanzibar walipendekeza Muungano wa mkataba; ni wazi kuwa ripoti hiyo haionyeshi kiuhalisia wa jumla ya watanzania waliohojiwa na kutamka kwa vinywa vyao kuwa wanataka muundo wa serikali tatu.
Kwa mfano ripoti inasema "kwa Tanzania Bara wananchi zaidi ya 39,000 walitoa maoni yao kuhusu Muungano na karibu 27,000 walizungumzia Muundo (Hawakusema kama wanataka serikali tatu).
Kwa Zanzibar karibu wananchi wote waliotoa maoni walijikita kwnye suala Muungano. Kati ya wananchi karibu 38000 waliotoa maoni, wananchi 19,000walitoa maoni kuhusu muundo wa Muungano (hawakusema kama wanataka serikali tatu)".
Sasa swali linalojitokeza ni je, hizi aslilimia zinzoonyesha kuwa idadi kubwa ya watanzania wanataka muundo wa serikali tautu inatoka wapi? Ukweli wa mambo unaonyesha kuwa, kimsingi ni kweli kamati teule iliwahoji watanzania takribani 333,516; kati hao watanzania 16,470 walipendekeza muundo wa serikali tatu, kwa Tanzania Bara, wananchi zaidi ya 39,000 walitoa maoni yao kuhusu Muungano, 27,000 walizungumzia Muundo.
Kwa Zanzibar wananchi 19,000 walitoa maoni kuhusu muundo wa Muungano na wengi wakipendekeza muungano wa mkataba. Takribani wananchi 287537 hawakuzungumzia suala la muungano au muundo wa serikali tatu.
Sasa je, asilimia 61% inatoaka wapi amabyo inaunga mkono hoja ya muundo wa serikali tatu? Ni watanzania wapi wengi ambao wameonyesha nia ya kuwa na muundo wa serikali tatu?