Hotuba ya Warioba Bungeni Dodoma: Jumanne, Tarehe 18 Machi 2014 na Hoja ya Muungano wa Serikali Tatu

Hotuba ya Warioba Bungeni Dodoma: Jumanne, Tarehe 18 Machi 2014 na Hoja ya Muungano wa Serikali Tatu

Kasuku ni kasuku tu hawezi kugeuka binadamu. Mzee wetu Joseph Sinde Warioba kaonesha dunia umahiri aliokuwa nayo yeye na wajumbe wa tume ya katiba kwa ufafanuzi fasaha mno. Wasomi wetu wa siku hizi (hasa wafundishwao na akina Bashiru Ali) hawawezi kujenga na kuitetea hoja nzito kama hii ya muundo wa muungano wetu, wao wamebaki kumnukuu baba wa taifa tu wakati ule ilhali sasa mambo yamebadilika mno. Huu ni ujumbe tosha kwa mtangazaji Makwaia & co wa Channel TEN katika kipindi chake cha Je tutafika?
 
Lissu anahusika vipi na hotuba ya Warioba, lini wazenji walimchukia Warioba.
huwezi jua wewe kima.....Mchakato mzima ulifikkishia Lissu kuonekana ni mbaya kwa zenj aliposema Zenj wamevunja katiba ya muungano...na hii ilikuwa ktk sekeseke la kuunda tume na nini kiwepo ktk tume....
 
Mkuu umewahi kuona wapi mtu anatoka nchi nyingine na kwenda kupiga kura nchi nyingine au kugombea uongozi nchi nyingine.

Simiyu Yetu, hebu usibadilishe maneno. Tulianza na neno Serikali sasa unasema nchi! Kwa kuwa Z'Bar inapenda sana kujitambulisha kama nchi basi na iwe hivyo na ndiyo maana tunasema Tanganyika lazima iwe nchi. Tunatumia majina anonymous lakini nimeona wanaokufahamu wakisema uko Bungeni. kama ni kweli naomba uamini kwamba mimi nimeelimika. Mimi ni mwanchama wa CCM lakini siamini kabisa uozo ulioko ndani ya CCM unaopandikizwa uwe ni wa Taifa. Taifa haliwezi kuwaza uozo eti tu akina Nape wameoza! Nitawasifu CHADEMA, CUF, TLP, etc. wanapofanya vizuri. Sitapiga makofi kwa kuwa mbele yangu kuna Kikwete hata kama kaishiwa. Afrika hii ina marais vichaa.

Kama Warioba kakosea hebu sahihisha lakini isiwe kama Sendeka wa Bungeni anayeamua kupiga kelele tu! Anaonyeshwa njia anakataa wakati hajui apite wapi.
 
Sijui ccm ya akina Pinda na ole Sendeka itakuja na gia gani ya serikali mbili.Sanasana wanaweza kuja kulivuruga bunge la katiba.
CCM is commiting suicide for obesities retantion of such hypocratic leaders of Sendeka kind
 
Kasuku ni kasuku tu hawezi kugeuka binadamu. Mzee wetu Joseph Sinde Warioba kaonesha dunia umahiri aliokuwa nayo yeye na wajumbe wa tume ya katiba kwa ufafanuzi fasaha mno. Wasomi wetu wa siku hizi (hasa wafundishwao na akina Bashiru Ali) hawawezi kujenga na kuitetea hoja nzito kama hii ya muundo wa muungano wetu, wao wamebaki kumnukuu baba wa taifa tu wakati ule ilhali sasa mambo yamebadilika mno. Huu ni ujumbe tosha kwa mtangazaji Makwaia & co wa Channel TEN katika kipindi chake cha Je tutafika?

Kiukweli kile kipindi cha Je Tutafika kwenye mada hii ya Rasimu, upotoshaji ni mkubwa mno, halafu kipindi kiko Biased, waalikwa wake ni wa mrengo mmoja, kazi yao ni mapovu tu, hawajengi hoja zaidi ya kukariri tu!
 
Sijui ni nani ataweza kupangua hoja za Mh. Jaji Warioba?

Aje Wasira, Aje sijui nani. Serikali 3 is a must
 
Kwani chalinze ilikuwaje, kwani bwanamdogo aliuliwa au unamaanisha nini?

Hiyo ya kusema chama watapendekeza jina mimi sikubaliani nalo kabisa, coz chama kitaleta mtu ambaye wananchi hawamjui wala hawatakuwa na uhahika kama atawaletea maendeleo, bora ya mshindi wa pili kwa sababu wananchi wanakuwa na idea na mtu huyo coz walimuona kwenye kampeni na walimsikia pia

Hiyo unayopendekeza italeta watu kuuana sana. Mtu akijua yeye ameshika nafasi ya pili, kumuua aliyeshika nafasi ya kwanza inakuwa ni mojawapo ya options za yeye kujitwalia ubunge. Au unalionaje hilo?

Btw, mimi natazama haya yaliyojiri chalinze kwa "macho manne manne"...dont quote me please:A S embarassed:!
 
Hata hivyo sita kaona ccm wanakizunguzungu akawaokoa semina isifanyike kumi na moja ili wakapigwe upepo kidogo wangeweza zimia kwa nondo za jaji
Haaaa haaaa! wakale mbuzi, bia na michepuko wakiitafakari lecture ya His Excellence JUDGE Warioba
Werema mchepuko utamshinda leo..
 
Kwa mujibu wa ripoti ya mwenyekiti wa tume ya kuaandaa rasimu ya katiba aliyoitoa mnamo tarehe 30/12/2013 inaonyesha kuwa takribani 61% kutoka Tanzania bara waliunga mkono hoja ya serikali tatu na 60% kutoka Zanzibar walipendekeza Muungano wa mkataba; ni wazi kuwa ripoti hiyo haionyeshi kiuhalisia wa jumla ya watanzania waliohojiwa na kutamka kwa vinywa vyao kuwa wanataka muundo wa serikali tatu.
Kwa mfano ripoti inasema "kwa Tanzania Bara wananchi zaidi ya 39,000 walitoa maoni yao kuhusu Muungano na karibu 27,000 walizungumzia Muundo (Hawakusema kama wanataka serikali tatu).
Kwa Zanzibar karibu wananchi wote waliotoa maoni walijikita kwnye suala Muungano. Kati ya wananchi karibu 38000 waliotoa maoni, wananchi 19,000walitoa maoni kuhusu muundo wa Muungano (hawakusema kama wanataka serikali tatu)".
Sasa swali linalojitokeza ni je, hizi aslilimia zinzoonyesha kuwa idadi kubwa ya watanzania wanataka muundo wa serikali tautu inatoka wapi? Ukweli wa mambo unaonyesha kuwa, kimsingi ni kweli kamati teule iliwahoji watanzania takribani 333,516; kati hao watanzania 16,470 walipendekeza muundo wa serikali tatu, kwa Tanzania Bara, wananchi zaidi ya 39,000 walitoa maoni yao kuhusu Muungano, 27,000 walizungumzia Muundo.
Kwa Zanzibar wananchi 19,000 walitoa maoni kuhusu muundo wa Muungano na wengi wakipendekeza muungano wa mkataba. Takribani wananchi 287537 hawakuzungumzia suala la muungano au muundo wa serikali tatu.
Sasa je, asilimia 61% inatoaka wapi amabyo inaunga mkono hoja ya muundo wa serikali tatu? Ni watanzania wapi wengi ambao wameonyesha nia ya kuwa na muundo wa serikali tatu?
 
Kuwa na passport tofauti ni kwajili issue muhimu..haswa kwa watu wenye uraia mara mbili wawe na passport ambayo hawataweza gombea nafasi km urais.Na bado wakwa raia.
 
Mkuu Wazanzibar wanataka serikali tatu na ndio maana kura ya siri ni mwiba mchungu kwa wapenda serikali mbili. Believe me wakifika kwenye kipengele cha muundo wa muungano Wazenj wote bila kujali vyama vyao watawatosa wapenda serikali mbili ilimradi tu kura iwe ya siri.

Hivi katika bunge hili Wazanzibar ni wangapi kwa ujumla wao?
 
Tatizo akina mwafulani wakiona haina maslahi kwao, utaona timbwili lake...
 
Warioba na maoni sahihi ya wananchi wa Tanzania, JK na msimamo wa kulazimisha (batili) wa chama. Haya sasa.
 
kajitahidi sana.kipengele cha haki za raia kitaleta tabu znz. kuhusu watanganyika kumiliki ardhi znz.hilo naona gumu kwa wazanzibar
 
Azimio la arusha halina tatizo wewe ndiye unalijofia sijui kwa mantiki gani.
Mkuu, palikuwa na hoja kuwa watu wanakazania serikali tatu na kuacha mambo kama ya elimu, afya n.k.. Mie nikahoji kuwa CCM wanatumia nguvu mno kutaka kuteka maoni ya wananchi waliopendekeza muundo wa serikali tatu na wao wanang'ang'ania mbili badala ya nguvu hizo hizo kuelekeza kurejeshwa kwa Azimio la Arusha.
 
Back
Top Bottom